Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 71
- Thread starter
- #181
ukiona watu wenye akili na taaluma zao wanatumia mda wao kujadili maisha binafsi ya viongozi ujue wanatakiwa kulazwa I.C.U MIREMBE
kama kweli wote tulipitia posts baada ya tukio matokeo ya mwanaasha tunakubaliana kwamba mjadala ulihama kutoka kwa mtoto kwenda kwa baba.
wenze2 wazungu wenye akili mara nyingi kabla hawajagombea nafac hizi za kisiasa.. wanakaa na familia zao kwanza.. wanaelewa unapoingia kwenye siasa ni sawa na kuamua kuvua nguo hadharani.. so hauwi uamuzi wa wake binafc.. ila unakuwa ni uamuzi wa baba na mama na watoto.. Jenerali Collin Powell alishawishiwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kugombea urais marekani.. lakini baada ya kukaa na familia yake.. alikataa kabisa kujiingiza.. ukishakuwa mwanasiasa unakuwa sawa na taulo..
kikwete ni kiongozi anaeishi maisha ya wananchi wake.yeye mwnyw amesoma shule za humu humu,kazi ameanzia vijijini tena singida watoto wake ndio hao wanasoma ktk shule hizi hizi za yebo yebo.hawa wenye gubu wanaoropoka humu hawana uzalendo.
Hapo kwenye red Safari_ni_Safari sijui kama umetumia kiswahili vizuri.... nilifuatilia sana na kuchangia hoja unayoisema, lakini ni watoto wangapi wa wakubwa na wenye fedha wanafeli mitihani huku wakiishi katika mazingira bora na shule wanazosoma ni nzuri? Unataka kuniambia mwanaasha ndiyo wa kwanza? Na pengine tu unieleze, kufeli kwa huyu binti kuna uhusiano gani na urais wa baba yake?
Baba anapimwa kwa mafanikio ya familia yake. haya sasa Riz 1 kashakuwa fisadi, Mwanaasha kalamba IV. tuna baba kweli hapa?? Je ataweza kulea watoto wa wenzie kweli (akina Kayumba)???
ndiyo uhuru wa maoni !!!
FEZA Academy shule ya yebo yebo? Kamuzu Academy shule ya yebo yebo?
bata ni bata huwa hachafuliwh bali anachafua mwenyewe
huna hoja..watoto wa nyerere akina makongoro walikuwa walevi wa gongo arusha lakini nyerere alibaki na msimamo na uzalendo wake adi leo tunamkumbuka kwa mazuri yake,hatuangalii watoto.
Mkuu sikubaliani na wewe kuhusu matokeo katika level ya sekondary. Ingekuwa level ya higher education tungekuwa ukurasa mmoja. Unachotakiwa kujua kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya wanafunzi wa sekondary kurudi chini na vyuo vya juu.
Wanafunzi wa sekondary wengi wao ni dependants na walezi wana haki ya kuyajua matokeo ya vijana wao bila kuficha. Tunaficha nini?, tena kwangu mimi hii ni motivating factor ya kuwafanya watoto wajitume sana kusoma kwani wasipofanya hivyo matokeo yao yatawaumbua. Mimi nina kijana wangu ninamlipia pesa nyingi sana, kila nikimuuliza matokeo ananiambia jina lake halipo. Kabla sijaenda kufuatilia nikaingia mtandaoni na kukuta amepata Div iv. Je si nimeepuka usumbufu?.
Hawa watoto ni wajanja sana. Hawasomi na kutudanganya wazazi. Mimi ninakubaliana kabisa na utaratibu huu wa kuanika majina public. Huko nyuma baraza walikuwa wanaweka namba tu, na matatizo waliyokutana nayo nafikiri ndiyo yamewafanya kuweka majina. Kuna wakati namba zinakosewa na kufanana ila kama kuna jina pembeni unaondoa utata.
Kuhusu mtoto wa JK kuwekwa mtandaoni that was unfortunate. Nilikemea sana kumshambulia mtoto kama mtoto kwa sababu tu baba yake ni mkuu wa nchi. Tupo wazazi wengi sana watoto wetu wamefanya vibaya sana. Uzembe hauna 'genes'. Ila kwa upande mwingine sioni kama kufanya hivi ni kumchafua rais, unamchafua kwa lipi?. Nafikiri nature ya kazi aliyo nayo Jakaya Kikwete, inamuweka kwenye spot light, hivyo kumzungumza vibaya au vizuri yote ni matokeo ya kazi aliyo nayo. Kama hutaki kuzungumwa vizuri au vibaya usijiweke kwenye Public spotlight (Ie usi-contest for public office)
Ukiingia katika mitandao ukaona jinsi Obama anavyoongelewa vibaya utachanganyikiwa. Ila kinachofanya hivyo si yeye bali ni ofisi aliyoishika. The only thing kujiweka kwenye good mood kama wewe si mvumilivu ni kutokuingia mitandaoni na kusoma criticism dhidi yako. Fanya kazi tu, waache watu waongee. Huwezi kuzuia watu kuongea/kuandika kwenye mitandao. Na ukifuatilia utakuwa mwendawazimu. Ndiyo maana mimi huwa nikiwasikia maafisa usalama wakitolea ufafanuzi maandishi ya kwenye internet huwa nawaona kama wamechanganyikiwa. Kazi yao ingekuwa ni ku-monitor maandishi yanayoweza kuhatarisha usalama wa mtu na kuyaangalia ukweli wake. Ila siyo kuangalia mipasho dhidi ya rais.
FEZA Academy shule ya yebo yebo? Kamuzu Academy shule ya yebo yebo?
ukiona watu wenye akili na taaluma zao wanatumia mda wao kujadili maisha binafsi ya viongozi ujue wanatakiwa kulazwa I.C.U MIREMBE
ukiona watu wenye akili na taaluma zao wanatumia mda wao kujadili maisha binafsi ya viongozi ujue wanatakiwa kulazwa I.C.U MIREMBE
Mkuu, nakubaliana kwa kiasi kikubwa na hoja ulizotoa. Ila baraza/wizara waangalie na upande wa pili wa trauma these children are going through (nina maana watoto waliofeli). Kuna wengine wanafikiria hata kujitundika, etc.