wanamchafua au wanasema ukweli?
kwa tukio hili tuwe fair mtoto ndiye alaumiwe kwa kumtia aibu baba yake.
Sisi huku vijijini tunaambiwa kuwa ili mtoto aweze kufaulu mzazi lazima afuatilie, asimwachie mwalimu peke yake. Sijui kama nadharia hii inaapply hata huko Feza. Kama inaapply then nani alaumiwe kwa suala hili?
sikubali wala kukataa kinachojadiliwa, ila najaribu tu kuwaza,
Kama Mwanaasha Jakaya Kikwete angepata Division 1 na au angeongoza katika kumi bora ingekuwaje?
Maana lazima watu tungemsifu kuwa mtoto wa raisi kapasua kwenye mitihani yake, je, mngelalamika pia kwamba tuna'mkashifu' mtoto wa raisi?
At the end of the day as long yeye ni raisi hakuna cha maisha binafsi, tutamjadili kwa jema au baya, awe tayari kukubali tu.
Uhusiano uliopo ni kwamba yeye ndio mwenye dhamana ya elimu hapa nchini.
Kwa muda mrefu elimu imeendelea kushuka bila hatua zozote madhubuti kuchukuliwa.
Walimu wameendelea kudharauliwa na serikali, vitendea kazi shuleni hakuna.
Kufeli kwa halaiki, wizi wa mitihani, ukosefu wa maabara, madawati,vitabu n.k..
Kufeli kwa mtoto wake ni kielelezo kizuri kushindwa kusimamia hata elimu ya mtoto wake.
Kama ameshindwa ya mtoto wake atapata wapi uwezo kuhakikisha Tanzania inatoa elimu bora kwa watoto wote na kuzuia hili tatizo la sasa la kufeli kwa halaiki. Ni lazima kwanza uwe kiongozi bora ndani ya familia yako ndio uweze kuwa kiongozi bora nje ya familia yako.
sikubali wala kukataa kinachojadiliwa, ila najaribu tu kuwaza,
Kama Mwanaasha Jakaya Kikwete angepata Division 1 na au angeongoza katika kumi bora ingekuwaje?