Mitandao isitumike kumchafua Rais

Kuna haja ya kuwashtaki waandishi wa habari magazetini,ni kwa nini wanaiba habari za JF na kuzifanyia biashara kwenye magazeti yao?hii ruhusa ya ku copy habari za JF nani anawapa?Uongozi wa JF hamulioni hilo,JK HAJACHAFULIWA NA MTU BALI MWANAE NDIO KAMCHAFUA,sasa mlitaka tumsifie Mwanaasha kwa kufeli?
 
Tatizo ni baraza la mitihani na wizara ya elimu. Kama siyo wao hii mitandao ingepata wapi hayo matokeo. Huu ujinga wa kuanika majina ya watoto hadharani ukomeshwe. Matokeo ya mitihani ni private matter. Wanachofanya baraza/wizara ni kama vile upime afya halafu matokeo ya lab yatolewe hadharani. Sioni sababu ya Tz daima kulaumu mitandao
 
Asanteni Tanzania Daima kwa kuwajulisha watanzania woote kuwa mtoto wa JK kilaza!!
Maana mitandao inabagua, si kila mtu anaweza kuipitia kama gazeti,..... big uo!!

Kama ile stori ya kuhongwa suti na mwarabu!
 
amkane basi kwamba yule sio mwanae ili ajitenge na 'uchafu' ............kama mwanae kupata Div 4 ni uchafu.

mwanaume mzima kuhongwa nguo unakuwa ushajichafua kabisa mbele ya wanaume wenzako, hata mbele ya wanawake wa maana.

Amkane kwa lipi? na wewe cha ajabu unachokiona ni kipi? Hapo kwenye red ELIZA na wewe ni mmoja wa hao wanawake wa maana?
 
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.

Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-

1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.

Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.


Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.

Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012

Mitandao isitumike kumchafua Rais


Tanzania Daima. 15 Feb, 2012

HIVI karibuni, Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha nne yaliyofanyika nchini mwaka 2011.

Na miongoni mwa wahitimu waliofanya mtihani huo ni mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, aliyemaliza katika moja ya shule za sekondari jijini Dar es Salaam.

Kwa bahati mbaya sana, matokeo ya mtoto huyo hayakuwa mazuri licha ya shule yake kufanya vizuri kitaifa katika mitihani hiyo na kuwa moja ya shule kumi bora.

Hoja yetu si kurejea matokeo hayo, bali tungependa kukemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hasa wakati wa kujadili masuala kadhaa na hata mengine ambayo kimsingi ni ya kibinafsi lakini yanahusishwa moja kwa moja na maslahi kwa umma.

Tunasema hivyo kutokana na baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao hiyo, kuchukulia matokeo mabaya ya mtoto wa Rais kama suala la kitaifa lenye kuhusishwa na uongozi wa baba yake, na hivyo kumshambulia kiongozi huyo bila sababu ya msingi.

Kwanza, lazima tutambue kuwa kufanya vibaya katika mitihani ni jmabo la bahati mbaya ambalo kimsingi linamuumiza mtahiniwa na vile vile wazazi au walezi wake, lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani.

Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.

Ni vyema wakati wa kujadili na kuchangia maoni hasa kuwahusu watawala wetu, tukazingatia majukumu na wajibu wa msingi tunaowapa viongozi ili watekeleze, na hivyo tunapaswa kuwahukumu kwa kuzingatia mipaka hiyo si kuingilia hata mambo yao binafsi na familia zao.

Mtoto wa Rais kushindwa mtihani si jambo la kutufanya tumtukane baba yake, yeye si malaika kwani huo ndiyo uwezo aliopewa na Mungu na walimu wake wakaongezea ujuzi wao.

Kama hoja ni kwamba kila anayeshindwa mtihani wazazi wake wasakamwe kwa matusi, basi hebu tuwatazame kwanza wa kwetu.

Tunaamini umefika wakati kwa wale wamiliki wa mitandao hiyo kuwa makini na hoja zinazoletwa hewani kujadiliwa na kujifanyia uhakiki kabla ya kuzichapisha, vnginevyo tutajikuta tumegeuka taifa linalovunja haki za msingi za binadamu kwa kuingilia masuala binafsi ya watu wengine.

Kama hoja ni kufeli kwa mtoto wa Rais, basi kafeli kama wale wa kwetu ambao tunawasomesha kwenye shule duni au zile za mamilioni lakini mwisho wa siku hawafaulu, sasa iweje tumwandame kiongozi wetu kwa suala lisilohusiana na kazi tuliyompa?

Tundhani kwa hili Rais alipaswa kusifiwa kuwa si mbinafsi kwa kuwa hakumpeleka mtoto wake kusoma Ulaya kama ambavyo viongozi wengi wa nchi hii wafanyavyo hata kwa watoto wao wasiokuwa na uwezo kimasomo
.

labda unipe maana ya kumchafua mtu kwa mtazamo wako wewe
 
Huu ni mwanzo wa anguko la cdm kama chama cha upinzani. Hii tahariri ya tanzania daima ilipaswa kuandikwa uhuru na habari leo. Ngoja tuendelee kutazama hii sinema
 
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.

Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-

1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.

Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.


Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.

Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012

Mitandao isitumike kumchafua Rais


Tanzania Daima. 15 Feb, 2012

HIVI karibuni, Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha nne yaliyofanyika nchini mwaka 2011.

Na miongoni mwa wahitimu waliofanya mtihani huo ni mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, aliyemaliza katika moja ya shule za sekondari jijini Dar es Salaam.

Kwa bahati mbaya sana, matokeo ya mtoto huyo hayakuwa mazuri licha ya shule yake kufanya vizuri kitaifa katika mitihani hiyo na kuwa moja ya shule kumi bora.

Hoja yetu si kurejea matokeo hayo, bali tungependa kukemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hasa wakati wa kujadili masuala kadhaa na hata mengine ambayo kimsingi ni ya kibinafsi lakini yanahusishwa moja kwa moja na maslahi kwa umma.

Tunasema hivyo kutokana na baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao hiyo, kuchukulia matokeo mabaya ya mtoto wa Rais kama suala la kitaifa lenye kuhusishwa na uongozi wa baba yake, na hivyo kumshambulia kiongozi huyo bila sababu ya msingi.

Kwanza, lazima tutambue kuwa kufanya vibaya katika mitihani ni jmabo la bahati mbaya ambalo kimsingi linamuumiza mtahiniwa na vile vile wazazi au walezi wake, lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani.

Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.

Ni vyema wakati wa kujadili na kuchangia maoni hasa kuwahusu watawala wetu, tukazingatia majukumu na wajibu wa msingi tunaowapa viongozi ili watekeleze, na hivyo tunapaswa kuwahukumu kwa kuzingatia mipaka hiyo si kuingilia hata mambo yao binafsi na familia zao.

Mtoto wa Rais kushindwa mtihani si jambo la kutufanya tumtukane baba yake, yeye si malaika kwani huo ndiyo uwezo aliopewa na Mungu na walimu wake wakaongezea ujuzi wao.

Kama hoja ni kwamba kila anayeshindwa mtihani wazazi wake wasakamwe kwa matusi, basi hebu tuwatazame kwanza wa kwetu.

Tunaamini umefika wakati kwa wale wamiliki wa mitandao hiyo kuwa makini na hoja zinazoletwa hewani kujadiliwa na kujifanyia uhakiki kabla ya kuzichapisha, vnginevyo tutajikuta tumegeuka taifa linalovunja haki za msingi za binadamu kwa kuingilia masuala binafsi ya watu wengine.

Kama hoja ni kufeli kwa mtoto wa Rais, basi kafeli kama wale wa kwetu ambao tunawasomesha kwenye shule duni au zile za mamilioni lakini mwisho wa siku hawafaulu, sasa iweje tumwandame kiongozi wetu kwa suala lisilohusiana na kazi tuliyompa?

Tundhani kwa hili Rais alipaswa kusifiwa kuwa si mbinafsi kwa kuwa hakumpeleka mtoto wake kusoma Ulaya kama ambavyo viongozi wengi wa nchi hii wafanyavyo hata kwa watoto wao wasiokuwa na uwezo kimasomo
.
JK is a public figure ni lazima tumjadili. Nyie magazeti endeleeni kulala tu.
Ninategemea mngetuletea hata mahawara wa JK na wengine na hata mkewe/wakewe. Kioo cha jamii kinatakiwa kiwe kweli kioo hakuna kufichaficha. Kama nyie magazeti mmeamua kurudi ughaibuni rudini siye tutaendelea. Rais Kibaki ilibidi aende kwa waandishi wa habari na kumtangaza Lucy kama mke pekee!! Huyu JK anaishi kwa kodi zetu anakula, anavaa lazima tumchambue kila wakati.
 
Bwana yesu apewe sifa, wote sema amen!. Jamani binafsi nampongeza rais kwa kuwa mzalendo kwa nchi anayoiongoza, kama binti yake mwenyewe anasoma hapa nyumban. Jamani tujaribu basi kuwaheshimu hata wanaotuongoza! Kwan yeye rais kasema nin kuhusu watoto wetu/dada zetu walio fail? Kwan yeye alie fail hatakiw ku fail kisa ni mtoto wa rais? Ama yeye ni malaika? Au huu mtandao watoto wamezidi? Au wengi hawana shule? No, tubadilike, na tuache tabia ya kusakama maisha binafsi ya mtu!
 
kutokana na sayansi mtoto anarithi sehemu kubwa ya akili ya baba na mama. wewe unataka tumsifie kwa lipi? analeta ubishoo shuleni kwa vile baba ni Rais. Hana control na internet ingekuwa gazeti sawa wangelifungia na bado tutamuonyesha uchafu wake ili ajisafishe
 
Huu ni mwanzo wa anguko la cdm kama chama cha upinzani. Hii tahariri ya tanzania daima ilipaswa kuandikwa uhuru na habari leo. Ngoja tuendelee kutazama hii sinema

Utatazama mpaka uchoke hakuna anguko lolote kutoka CDM.
 
Huu ni mwanzo wa anguko la cdm kama chama cha upinzani. Hii tahariri ya tanzania daima ilipaswa kuandikwa uhuru na habari leo. Ngoja tuendelee kutazama hii sinema

Mkuu. Kumbuka pia Tanzania Daima linasomwa na yeyote si wa wenye mlengo wa CDM tu. Kwa mantiki hiyo, TD wamefanya vema kuutahadharisha umma wa Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao.
 
Kufeli kwa mtoto wake kuna uhusiano gani na urais wake? na je wewe kwenu hakuna waliowahi kufeli mitihani na pengine ukiwemo wewe, je nani alimsema Baba yako?

Uhusiano uliopo ni kwamba yeye ndio mwenye dhamana ya elimu hapa nchini.

Kwa muda mrefu elimu imeendelea kushuka bila hatua zozote madhubuti kuchukuliwa.
Walimu wameendelea kudharauliwa na serikali, vitendea kazi shuleni hakuna.
Kufeli kwa halaiki, wizi wa mitihani, ukosefu wa maabara, madawati,vitabu n.k..

Kufeli kwa mtoto wake ni kielelezo kizuri kushindwa kusimamia hata elimu ya mtoto wake.
Kama ameshindwa ya mtoto wake atapata wapi uwezo kuhakikisha Tanzania inatoa elimu bora kwa watoto wote na kuzuia hili tatizo la sasa la kufeli kwa halaiki. Ni lazima kwanza uwe kiongozi bora ndani ya familia yako ndio uweze kuwa kiongozi bora nje ya familia yako.
 
mkuu wangu naamini unaelewa kwamba licha ya mazingira bora ya kuishi na shule nzuri siyo waranti ya mtoto kufaulu mtihani. tushukuru kwamba baba yake hakutumia wadhifa wake kuiba mtihani ama kulazimisha apandishwe daraja la juu. inawezekana huyo mtoto ana kipaji cha jambo jingine ambacho kikitumika vizuri atakua msaada kwa familia yake na taifa. kufeli mitihani siyo kushindwa maisha!
Sidhani kama kuna mtu kasema Mwanaasha kashindwa maisha, tunachosema ambacho kiko wazi ni kuwa mtoto wa rais kapata DIV IV.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom