Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
- Thread starter
- #81
Hivi ni kumchafua au kumjadili?
Mijadala inayohusisha matusi na kejeli siku zote humchafua mtu!
Hivi ni kumchafua au kumjadili?
amkane basi kwamba yule sio mwanae ili ajitenge na 'uchafu' ............kama mwanae kupata Div 4 ni uchafu.
mwanaume mzima kuhongwa nguo unakuwa ushajichafua kabisa mbele ya wanaume wenzako, hata mbele ya wanawake wa maana.
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.
Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-
1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.
Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.
Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.
Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012
Mitandao isitumike kumchafua Rais
Tanzania Daima. 15 Feb, 2012
HIVI karibuni, Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha nne yaliyofanyika nchini mwaka 2011.
Na miongoni mwa wahitimu waliofanya mtihani huo ni mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, aliyemaliza katika moja ya shule za sekondari jijini Dar es Salaam.
Kwa bahati mbaya sana, matokeo ya mtoto huyo hayakuwa mazuri licha ya shule yake kufanya vizuri kitaifa katika mitihani hiyo na kuwa moja ya shule kumi bora.
Hoja yetu si kurejea matokeo hayo, bali tungependa kukemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hasa wakati wa kujadili masuala kadhaa na hata mengine ambayo kimsingi ni ya kibinafsi lakini yanahusishwa moja kwa moja na maslahi kwa umma.
Tunasema hivyo kutokana na baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao hiyo, kuchukulia matokeo mabaya ya mtoto wa Rais kama suala la kitaifa lenye kuhusishwa na uongozi wa baba yake, na hivyo kumshambulia kiongozi huyo bila sababu ya msingi.
Kwanza, lazima tutambue kuwa kufanya vibaya katika mitihani ni jmabo la bahati mbaya ambalo kimsingi linamuumiza mtahiniwa na vile vile wazazi au walezi wake, lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani.
Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.
Ni vyema wakati wa kujadili na kuchangia maoni hasa kuwahusu watawala wetu, tukazingatia majukumu na wajibu wa msingi tunaowapa viongozi ili watekeleze, na hivyo tunapaswa kuwahukumu kwa kuzingatia mipaka hiyo si kuingilia hata mambo yao binafsi na familia zao.
Mtoto wa Rais kushindwa mtihani si jambo la kutufanya tumtukane baba yake, yeye si malaika kwani huo ndiyo uwezo aliopewa na Mungu na walimu wake wakaongezea ujuzi wao.
Kama hoja ni kwamba kila anayeshindwa mtihani wazazi wake wasakamwe kwa matusi, basi hebu tuwatazame kwanza wa kwetu.
Tunaamini umefika wakati kwa wale wamiliki wa mitandao hiyo kuwa makini na hoja zinazoletwa hewani kujadiliwa na kujifanyia uhakiki kabla ya kuzichapisha, vnginevyo tutajikuta tumegeuka taifa linalovunja haki za msingi za binadamu kwa kuingilia masuala binafsi ya watu wengine.
Kama hoja ni kufeli kwa mtoto wa Rais, basi kafeli kama wale wa kwetu ambao tunawasomesha kwenye shule duni au zile za mamilioni lakini mwisho wa siku hawafaulu, sasa iweje tumwandame kiongozi wetu kwa suala lisilohusiana na kazi tuliyompa?
Tundhani kwa hili Rais alipaswa kusifiwa kuwa si mbinafsi kwa kuwa hakumpeleka mtoto wake kusoma Ulaya kama ambavyo viongozi wengi wa nchi hii wafanyavyo hata kwa watoto wao wasiokuwa na uwezo kimasomo.
JK is a public figure ni lazima tumjadili. Nyie magazeti endeleeni kulala tu.Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.
Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-
1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.
Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.
Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.
Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012
Mitandao isitumike kumchafua Rais
Tanzania Daima. 15 Feb, 2012
HIVI karibuni, Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha nne yaliyofanyika nchini mwaka 2011.
Na miongoni mwa wahitimu waliofanya mtihani huo ni mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, aliyemaliza katika moja ya shule za sekondari jijini Dar es Salaam.
Kwa bahati mbaya sana, matokeo ya mtoto huyo hayakuwa mazuri licha ya shule yake kufanya vizuri kitaifa katika mitihani hiyo na kuwa moja ya shule kumi bora.
Hoja yetu si kurejea matokeo hayo, bali tungependa kukemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hasa wakati wa kujadili masuala kadhaa na hata mengine ambayo kimsingi ni ya kibinafsi lakini yanahusishwa moja kwa moja na maslahi kwa umma.
Tunasema hivyo kutokana na baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao hiyo, kuchukulia matokeo mabaya ya mtoto wa Rais kama suala la kitaifa lenye kuhusishwa na uongozi wa baba yake, na hivyo kumshambulia kiongozi huyo bila sababu ya msingi.
Kwanza, lazima tutambue kuwa kufanya vibaya katika mitihani ni jmabo la bahati mbaya ambalo kimsingi linamuumiza mtahiniwa na vile vile wazazi au walezi wake, lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani.
Pili, tunapaswa kulichukulia jambo hili kama funzo na changamoto kwa elimu yetu, kwani ni watoto wachache sana wa viongozi wetu wakuu wanasoma shule za hapa Tanzania, na kwa ubabaishaji uliyopo kwenye usimamizi wa mitihani bado Rais angeweza kutumia nguvu yake kuhakikisha mwanaye anapendelewa lakini haikuwa hivyo.
Ni vyema wakati wa kujadili na kuchangia maoni hasa kuwahusu watawala wetu, tukazingatia majukumu na wajibu wa msingi tunaowapa viongozi ili watekeleze, na hivyo tunapaswa kuwahukumu kwa kuzingatia mipaka hiyo si kuingilia hata mambo yao binafsi na familia zao.
Mtoto wa Rais kushindwa mtihani si jambo la kutufanya tumtukane baba yake, yeye si malaika kwani huo ndiyo uwezo aliopewa na Mungu na walimu wake wakaongezea ujuzi wao.
Kama hoja ni kwamba kila anayeshindwa mtihani wazazi wake wasakamwe kwa matusi, basi hebu tuwatazame kwanza wa kwetu.
Tunaamini umefika wakati kwa wale wamiliki wa mitandao hiyo kuwa makini na hoja zinazoletwa hewani kujadiliwa na kujifanyia uhakiki kabla ya kuzichapisha, vnginevyo tutajikuta tumegeuka taifa linalovunja haki za msingi za binadamu kwa kuingilia masuala binafsi ya watu wengine.
Kama hoja ni kufeli kwa mtoto wa Rais, basi kafeli kama wale wa kwetu ambao tunawasomesha kwenye shule duni au zile za mamilioni lakini mwisho wa siku hawafaulu, sasa iweje tumwandame kiongozi wetu kwa suala lisilohusiana na kazi tuliyompa?
Tundhani kwa hili Rais alipaswa kusifiwa kuwa si mbinafsi kwa kuwa hakumpeleka mtoto wake kusoma Ulaya kama ambavyo viongozi wengi wa nchi hii wafanyavyo hata kwa watoto wao wasiokuwa na uwezo kimasomo.
Huu ni mwanzo wa anguko la cdm kama chama cha upinzani. Hii tahariri ya tanzania daima ilipaswa kuandikwa uhuru na habari leo. Ngoja tuendelee kutazama hii sinema
Huu ni mwanzo wa anguko la cdm kama chama cha upinzani. Hii tahariri ya tanzania daima ilipaswa kuandikwa uhuru na habari leo. Ngoja tuendelee kutazama hii sinema
Nani alikuwa anamlipia Mwanaasha school fees au Mwanaasha alikuwa anauza maandazi kujilipia?Rais anahusika vipi na matokeo ya mtoto wake? uzumbukuku huu.
Kufeli kwa mtoto wake kuna uhusiano gani na urais wake? na je wewe kwenu hakuna waliowahi kufeli mitihani na pengine ukiwemo wewe, je nani alimsema Baba yako?
Sidhani kama kuna mtu kasema Mwanaasha kashindwa maisha, tunachosema ambacho kiko wazi ni kuwa mtoto wa rais kapata DIV IV.mkuu wangu naamini unaelewa kwamba licha ya mazingira bora ya kuishi na shule nzuri siyo waranti ya mtoto kufaulu mtihani. tushukuru kwamba baba yake hakutumia wadhifa wake kuiba mtihani ama kulazimisha apandishwe daraja la juu. inawezekana huyo mtoto ana kipaji cha jambo jingine ambacho kikitumika vizuri atakua msaada kwa familia yake na taifa. kufeli mitihani siyo kushindwa maisha!