Mitandao isitumike kumchafua Rais

Mitandao isitumike kumchafua Rais

Rais anahusika vipi na matokeo ya mtoto wake? uzumbukuku huu.
Baadhi ya binaadamu(tena wachache) ni wepesi kusahau kuwa unapoishia uhuru wa mtu mmoja ndipo unapoanzia uhuru wa mtu mwingine. Tukiacha kufikiri kwa kwa matumbo tutajikomboa!
 
Bwana yesu apewe sifa, wote sema amen!. Jamani binafsi nampongeza rais kwa kuwa mzalendo kwa nchi anayoiongoza, kama binti yake mwenyewe anasoma hapa nyumban. Jamani tujaribu basi kuwaheshimu hata wanaotuongoza! Kwan yeye rais kasema nin kuhusu watoto wetu/dada zetu walio fail? Kwan yeye alie fail hatakiw ku fail kisa ni mtoto wa rais? Ama yeye ni malaika? Au huu mtandao watoto wamezidi? Au wengi hawana shule? No, tubadilike, na tuache tabia ya kusakama maisha binafsi ya mtu!

FEZA ni shule ya Private; ningemuona ni mzalendo kweli kama angelimpeleka katika shule za KATA zilizotapakaa kila kata. na ambazo anazisimamia MKULU AU HATA SHULE YA MSINGI ALIFELI HIVYO HAKUCHAGULIWA HATA KWENDA SHULE YA KATA??


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Editorial page ya Tanzania Daima haiwezi kumtetea Kikwete hata siku moja, hili ni dongo kwa Rais na mwanae lililojificha, veiled attack. Mwandishi ni mtu mahiri sana, very shrewd critic.


The Editorial page of a newspaper is always the stand of that news paper organisation on a particular issue.

 
Rais anahusika vipi na matokeo ya mtoto wake? uzumbukuku huu.

Kama huwezi kuhusisha U-Rais na matokeo ya mtoto wake, basi coginitive yako is below 0. RAIS sio tu anahusika na matokeo ya mtoto wake bali pia ana uhusiano wa moja kwa moja na matokeo ya watoto wa nchi hii.

Mnakumbuka yule Waziri wa Elimu wa England aliyefukuzwa U-waziri simply alimuhamisha mtoto wake kutoka kwenye government school kwenda kwenye private school? Mwanaasha alitakiwa asome shule za kata kwanza in the first place. Acha u.j.i..n.ga wa kutuambia mambo ya kusoma Ulaya. Hiyo Stereotype ndiyo imetufanya tuwe nchi ya tatu kwa ombaomba duniani.
 
Rais anahusika vipi na matokeo ya mtoto wake? uzumbukuku huu.
kwa kidhungu wanasema like faza like mwanaasha.

na kama raisi ameshindwa kumsimama mtoto wake mmoja je ataweza kulisimamia taifa. kama unaona mtu kuongoza familia yake tu kunamshinda nafikiri huyu ukimpa mtaa ushuhudie tu haya tunayoyashuhudia kwenye taifa.

Au ndio atakapoenda tena nje ya nchi na kukutana na vyombo vya habari akaulizwa vipi kuhusu ubora wa elimu tanzania na kama kiongozi mkuu wa nchi una mpango gani wa kuahakikisha kuwa unaboresha na kuweka mazingira mazuri ya elimu kwa watanzania na kuhakikisha kuwa wanasoma, kuelewa na kufaulu na hivyo kuja kukabiliana na soko la ajira haswa ikizingatiwa kuwa sasahivi kuna ushindani wa ajira kutokana na kuingia kwa umoja wa afrika ya mashariki.

Ndio atajibu kwanza swali lenyewe refu sana lakini nieleze tu kuwa watanzania wanatakiwa wajue mimi sio Mungu kuweza kuwawekea hali nzuri ya masomo, na kwanini wanafeli hata mimi sijui ndio nashanga hata wanaasha kila siku namwona akijisomea lakini kwamba hajui anachokisoma hata mimi sijui.

Na mfano mzuri ni kwamba kama mtoto wangu amesomea ikulu na amefeli sasa sijui mjukuu wa mtoto wa mtoto wa mkulima ambaye pia ni waziri mkuu aliyeko kule sumbawanga vijijini anayesomea kwenye kibatari ambacho nacho tulipandisha mafuta ya taa ili ashindwe kabisa kujisome lakini nashaa anazidi kusoma kwa kutumia mbalamwezi na kumshinda hata huyu wa kwangu, pale ikulu pale nifunga mpaka taa maalumu za kusome sasa ukiniuliza kwanini mtoto kafeli hata mimi ntakushanaa.
 
  • Thanks
Reactions: ral
Tanzania daima imefanya vizuri kutueleza wengine kwamba hata mtoto wa Rais ameshindwa mtihani ni dalili mbaya ya kushindwa kuongoza familia je atawezaje kuongoza nchi ?
 
Kweli watu wana hang-over ya kuperembwa....

Wewe mtu hau perform...Matatizo ya kimsingi unakaa kimya as if haupo....Unatoa ahadi mwenyewe unashindwa kuzitekeleza mwenyewe...Unaendesha nchi kiajabu-ajabu mfano kuwaamuru wezi warudishe walichoiba then wanakuwa free..unajaza mahawara na washkaji ktk utendaji tena hadi kwenye pozishoo muhimu ambazo zinahitaji vetting...unaulizwa kiini cha umasikini wa nchi yako unadai hujui...

Anataka aelezwe fairly kiasi gani...?
 
Magazeti ya bongo nayakubari yanauma na kupuliza ili mradi maisha yanaendelea. Mtoto kufeli haki ya mungu si kitu ya kawaida, manake kufeli kayumba ni sawa ila mtoto wa kishua anakila kitu cha kumfanya apasue jamani hata average jamani.

Asichafuke raisi katika mikashfa ya rushwa na uzembe kama anavyoandikwa na magazeti akachafuke kwa binti yake kufeli kama wanamitandao wanavyotoa michango yao. Tanzania Daima please zipo tahariri ambazo zingekuwa na tija kuliko hii inayoonekana ni kujikomba na kujipendekeza.
 
Hakuna anayekulazimisha umusifu, tunachozungumzia hapa ni kwa nini atukanwe hata kwa mambo yasiyo na tija kwa taifa na hayahusiani? Kasome Tanzania Daima la leo unaweza kupata mantiki ya hii thread!

Aisee wewe unasahau kale kamsemo "as you climb the ladder you expose your bottom"
 
lakini tunapaswa kuelewa kuwa mtoto wa Rais ameshindwa kama walivyoshindwa wanafunzi wengine pasipo kujali amesoma shule gani au mzazi ana wadhifa gani
Ni kigezo tosha kwani kushindwa kwa mwanae jambo ambalo liinaonesha ni kwa kiasi gani hali ngumu ya maisha imesababisha uwezo wake mdogo wa kuiongoza nchi. Kama kwenye familia yake kuna failure wa form four katika mitihani atawezaje kuwaongoza wananchi kuelekea kwenye maisha vizuri. Napita tu nitarudi baadayel
 
Sijapata kuona mtu ambaye anachafuliwa na mtu mwingine halafu akachafuka. Kama mimi sio mwizi, au mzinzi au mbakaji, itasaidia nini kuniita mwizi,mbakaji na mzinzi? Haitanisumbua kichwa maana kwenye ukweli uongo unajitenga. Issue inakuwa nyingine pale unaponiita mzinzi halafu kweli niwe mzinzi...walahi tutapigana.
 
Nani kasema ubongo wa watoto wa Marais uko tofauti na watoto wengine?
mtoto hana shida ya umeme
hana shida ya nauli wala usafiri
hana shida ya hela ya matumizi
hana shida ya ada
hana shida ya vitabu
hana shida ya walimu
shule sio ya kata
 
Huyu mtoto angepata div1 ya point saba nina uhakika kingeandaliwa kipindi maalumu kwa ajli yake ili awasihi wanafunzi wengine namna alivyokuwa anasoma ili na wao wafaulu.....lakini kwa kuwa amefeli na kupata four ya point 27 watu wakiuliza imekuwaje mtoto mwenye kila kitu nyumbani akapata daraja hilo wanaonekana ni wachochezi....tena ilifaa waandishi wamfate huyo mtoto na wamuulze imekuwaje akapata hivyo....nini kilipungua?

Lakini ukweli utabaki pale pale juu ya mwanaasha......huyu mtoto alikuwa mzito na wazazi wake hawakujua mapungufu yake toka alipotimuliwa kifungiro baada ya kushindwa kufikisha wastani na wakamuhamishia hapo Feza.... Wazazi walishindwa kujua kuwa binti ni mzito wa kuelewa na walikuwa hawafuatilii maendeleo yake ya shule...kama wote mjuavyo wazazi wa huyu binti wanashinda angani na kwenye bembea na wakirudi nyumbani badala ya kufatilia maendelea ya mtoto wao wao...wenyewe wazazi wanamchukua mtoto na kumpeleka kwenye shows kama inavyoonekana hapa chini...

Sasa hivi mama Salma na Kikwete waongeze nguvu na ufatiliaa kwa watoto wao wengine..kuna huyo mmoja anaitwa Ali nae ni mzito wa kuelewa tena sana.....kwa kuwa wako Botswana najua matokeo yao hayataonekana kama ya huyu Mwanaasha...ila ukweli utabaki kusemwa kuwa juu ya Mwanaasha, ni uzembe wake na uzembe wa wazazi wake...

Siku zote huwa nasema hivi:

Anayepata div one na anaepata div.iv wote msuli wao uko sawa ila in opposite direction.....wakati huyu anakomaa kupata div one huyu mwingine nae yuko bize na shows kama hizi :

LIONS%2BPRESIDENT%2BFRANK%2BGOYAYI%2B%2C%2BFIRST%2BLADY%2BSALMA%2BKIKWETE%2BAND%2BMWANAASHA%2BKIKWETE%2BFOLLOWING%2BTHE%2BEVNT%2BATTENTIVELY.JPG
 
Maoni ya Mhariri hayawezi kuwa maoni ya watanzania wote ana haki yake ya kufikiria nasi pia..lakini kwa hili la Mwanasha ambaye anapata malazi bora, chakula bora,kasoma shule bora na ghali kabisa Tanzania ambako wengi wa wanafunzi wake wamefaulu kwa viwango vya juu lazima tujiulize wapi tatizo, je ni yeye binafsi au wazazi?
 
..kuna huyo mmoja anaitwa ali nae ni mzito wa kuelewa tena sana.....kwa kuwa wako botswana

Mkuu, Mhariri kampongeza eti anasomesha watoto hapa nchini...hapo tuna jiuliza umakini wa mhariri..
 
angekuwa amepata division 4 ktk shule ya kata kama wanazosoma wengine rais angekuwa anaonewa lakini kwa shule kana FEZA, naamini hata wenye shule wanalaani kuwa na mtoto kama mwanaasha sababu kawaletea division 4, nilitegemea rais ajiuzulu kwa kashfa hii.
 
Back
Top Bottom