Miss JF 2023 FaizaFoxy: Wanaonitongoza waje hapa

Miss JF 2023 FaizaFoxy: Wanaonitongoza waje hapa

Wale wote wanaojidai kunitongoza majukwaa ambayo hayahusiani na mahusiano, waje hapa kwenye jukwaa mahsusi kwa ajili hiyo.

Wacheni kuharibu nyuzi na mada za watu kwenye majukwaa yasiyohusiana na kutongozana

Hii inawahusu na wale wanaokuja kunikera PM... Karibuni hapa, mshindane kunitongoza.
Unataka kutongozwa?
 
Nikinywa maji nakuona kwenye glasi, nikijiangalia kwenye kioo naona sura yako, macho yako mazuri yananiita ita. Rangi yako ya chocolate naipenda sana

Nikilala sipati usingizi mpaka niangalie picha yako, mapigo yangu ya moyo yanadunda kwa kutaja jina lako, unajina zuri sana natamani kila muda nikuite.

Kama ingekuwa naweza kuufungua moyo wangu ningekuonyesha nilivyokuhifadhi moyoni mwangu, uone jinsi gani ninavyokupenda.

Nakupenda sana mrembo.
(Just joking, usije ukanikubalia[emoji23][emoji23][emoji23])

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu katika siku umeanzisha nyuzi ya kitoto ni leo?

Hii nyuzi imekaa kikahaba sana, hua nimekueka group la wanawake wenye ubongo mkubwa sana humu Jf ...but not anymore

Naanza kuamini wengi wa wasichana jf hawana utofauti na wale wa badoo,sema ndo vile baadhi wanajitahidi sana kujificha hadharani ila ukimuotea angle yake utakuta ni walewale...leo mkuu umeteleza sana,au ulikua unapost ktk ID ya matukio bahati mbaya umepost kwa ID yako ya heshima?

Narudia tena...Huu uzi ni wa kitoto mno...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili ni darsa kubwa kuliko unavyofikiria.

Naelewa lakini kwa kaliba ya watu wengi walivyo hapa hawataambulia elimu wala kujifunza kitu.

Ingetosha kufikisha ujumbe wa watu kuheshimu nyuzi za wengine bila kuingiza mambo yao yasiyohusu mjadala.
Wavurugaji wapo wengi na sio wote wanatongozana. Hii haitakua njia bora ya kutatua hilo tatizo.
 
Back
Top Bottom