Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,346
- 9,846
- Thread starter
- #81
Tuendelee....
UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD
Sehemu ya tatu.
Reuven Shiloah, miaka arobaini(40), mpole na mstaarabu, msiri, alikuwa ni mtu aliyejaa mafumbo. Alitokea kwenye tamaduni tajiri, akiwa na ubongo mwepesi kwa uchambuzi, mwenye uelewa mpana wa Uarabuni ya mashariki ya kati, mila zake za kikabila, koo zinazoongoza, ushirikiano wa mashaka na ugomvi uliopelekea umwagaji wa damu.
Moja kati ya watu waliomhusudu sana alimwita "malkia katika mchezo wa chess wa Ben- Gurion" wakati akifanya kazi kama mshauri wa kisiasa wa David Ben- Gurion. Baadhi walimfananisha na Kadrinali Richelieu wa Ufaransa; wengine walimuona kama mtu 'mjanja mjanja', 'mpiga pupa' mzamivu, mtu aliyejua namna ya kuendesha matukio nyuma ya pazia bila kujihusisha moja kwa moja. Shiloah alikuwa akijihusisha moja kwa moja, katika maisha yake yote, katika misheni za siri na kazi za uaskari kanzu.
Akiwa mchangamfu, aliyejiamini, muadilifu na mtoto wa mwalimu wa sheria za kiyahudi (rabbi), Shiloah alizaliwa katika iliyokuwa Jerusalem ya zamani. Kila wakati akiwa amevalia nadhifu na kunyoa ndevu vizuri, akinyemelewa na upaa - Shiloah alikuwa amejiwekea misheni huko Baghdad, muda mrefu nyuma kabla ya kuzaliwa kwa taifa la Israel.
Alishakaa kwa miaka mitatu ndani ya Iraq, akijifanya kama mwandishi wa habari na mwalimu huku akijifunza siasa za nchi hiyo.
Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia (wwii) alifanya makubaliano na Uingereza ili kuanzisha kikosi cha makomandoo cha wayahudi ili kuhujumu operesheni za wa-Nazi waliokua wakiitawala Ulaya.Alisaidia katika kutengeneza vikosi viwili vya makomandoo: Kimoja kikiwa ni Battaliani ya wajerumani, waliokua na silaha na sare za Ujerumani, ambao walitekeleza operesheni za hatari nyuma ya maadui huko Ulaya; Kingine kilikuwa ni Battaliani ya waarabu, ambao washiriki wake waliongea kiarabu, walivalia kiarabu, na walipewa mafunzo kwa misheni ndani kabisa Uarabuni. Aliwashawishi pia waingereza kuwaingiza kwa miavuli ya upepo - parachute, wayahudi waliojitolea kutokea Palestina ili kuingia Ulaya, ili kupangilia upinzani wa ndani wa wayahudi dhidi ya wa-Nazi.
Shiloah alikua wa kwanza kuanzisha mawasiliano na OSS (Office of Strategic Service), taasisi iliyokwuwepo kabla ya CIA. Wakati wa vita ya uhuru wa Israel, alisafiri kwenda makao makuu ya nchi jirani ya Kiarabu kwa siri na akarudi na 'kombe la thamani kubwa': mkakati wa uvamizi wa majeshi ya kiarabu. Uhitaji wa Shiloah kufanya kazi chini ya wingu kubwa la usiri ulikuwa chanzo cha shujaha huyu wa ajabu.
Marafiki zake waliwahi kutania kuwa, wakati alipokodi teksi na kuulizwa,"unaelekea wapi?". Shiloah alijibu: "Hiyo ni siri ya serikali".
Itaendelea......
UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD
Sehemu ya tatu.
Reuven Shiloah, miaka arobaini(40), mpole na mstaarabu, msiri, alikuwa ni mtu aliyejaa mafumbo. Alitokea kwenye tamaduni tajiri, akiwa na ubongo mwepesi kwa uchambuzi, mwenye uelewa mpana wa Uarabuni ya mashariki ya kati, mila zake za kikabila, koo zinazoongoza, ushirikiano wa mashaka na ugomvi uliopelekea umwagaji wa damu.
Moja kati ya watu waliomhusudu sana alimwita "malkia katika mchezo wa chess wa Ben- Gurion" wakati akifanya kazi kama mshauri wa kisiasa wa David Ben- Gurion. Baadhi walimfananisha na Kadrinali Richelieu wa Ufaransa; wengine walimuona kama mtu 'mjanja mjanja', 'mpiga pupa' mzamivu, mtu aliyejua namna ya kuendesha matukio nyuma ya pazia bila kujihusisha moja kwa moja. Shiloah alikuwa akijihusisha moja kwa moja, katika maisha yake yote, katika misheni za siri na kazi za uaskari kanzu.
Akiwa mchangamfu, aliyejiamini, muadilifu na mtoto wa mwalimu wa sheria za kiyahudi (rabbi), Shiloah alizaliwa katika iliyokuwa Jerusalem ya zamani. Kila wakati akiwa amevalia nadhifu na kunyoa ndevu vizuri, akinyemelewa na upaa - Shiloah alikuwa amejiwekea misheni huko Baghdad, muda mrefu nyuma kabla ya kuzaliwa kwa taifa la Israel.
Alishakaa kwa miaka mitatu ndani ya Iraq, akijifanya kama mwandishi wa habari na mwalimu huku akijifunza siasa za nchi hiyo.
Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia (wwii) alifanya makubaliano na Uingereza ili kuanzisha kikosi cha makomandoo cha wayahudi ili kuhujumu operesheni za wa-Nazi waliokua wakiitawala Ulaya.Alisaidia katika kutengeneza vikosi viwili vya makomandoo: Kimoja kikiwa ni Battaliani ya wajerumani, waliokua na silaha na sare za Ujerumani, ambao walitekeleza operesheni za hatari nyuma ya maadui huko Ulaya; Kingine kilikuwa ni Battaliani ya waarabu, ambao washiriki wake waliongea kiarabu, walivalia kiarabu, na walipewa mafunzo kwa misheni ndani kabisa Uarabuni. Aliwashawishi pia waingereza kuwaingiza kwa miavuli ya upepo - parachute, wayahudi waliojitolea kutokea Palestina ili kuingia Ulaya, ili kupangilia upinzani wa ndani wa wayahudi dhidi ya wa-Nazi.
Shiloah alikua wa kwanza kuanzisha mawasiliano na OSS (Office of Strategic Service), taasisi iliyokwuwepo kabla ya CIA. Wakati wa vita ya uhuru wa Israel, alisafiri kwenda makao makuu ya nchi jirani ya Kiarabu kwa siri na akarudi na 'kombe la thamani kubwa': mkakati wa uvamizi wa majeshi ya kiarabu. Uhitaji wa Shiloah kufanya kazi chini ya wingu kubwa la usiri ulikuwa chanzo cha shujaha huyu wa ajabu.
Marafiki zake waliwahi kutania kuwa, wakati alipokodi teksi na kuulizwa,"unaelekea wapi?". Shiloah alijibu: "Hiyo ni siri ya serikali".
Itaendelea......