Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Special mention kwa Asajile Mwaikambo..
Mtandao tu ulikuwa chini, ungekuta tuko mbali.. anyways, ngoja tusogee
 
Tuendelee...

UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD

Sehemu ya tisa.

....aliweka kitanzi kwenye shingo yake na kukamata mshikio wa kudhibiti mtego. Taggar alikataa mfuko mweusi waliojaribu kumvalisha kichwani. Mnyongaji sasa akamtazama afisa anayetoa amri, akiwa amesimama na wengine wachache mbele ya mtu anayeenda kufa.
Taggar aliwaza juu ya familia yake, juu ya nyumbani kwake Jerusalem, na juu ya maisha ambayo angeweza kuwa nayo kama asingechagua hii njia. Hivi, shingo yangu itavunjika? Alitafakari, na kuhisi hofu kuu ikimtafuna.

Na mara, ghafla, maafisa wakaondoka. Taggar akatolewa kwenye mlango wa mtego. Yule mnyongaji akaondoa mifuko ya mchanga kwenye miguu na kitanzi kwenye shingo yake, akilalamika kuwa amekosa malipo yake kwa siku hiyo. Taggar akagundua, kwa mshangao, kuwa hangekufa siku hiyo! Kila kitu, kwa mpangilio wote kilikuwa mtego. Walidhani wangemfanya akiri na kutoa taarifa zaidi juu wa watu alioshirikiana nao. Ila kwa sasa, akijikongoja kurudi kwenye sero yake, akiwa hai, Taggar alikuwa na hakika kuwa asingeweza kufa ndani ya jela ya Iraq. Rafiki zake wangemtoa ije mvua, lije jua.

Wakati kesi ilipoisha, alihukumiwa kifo, ila,mara, hukumu yake ikabadilishwa na kuwa atumikie maisha yote jela. Batzri na Salach walinyongwa. Walitumia siku yao ya mwisho na Taggar, aliyejaribu kuwafanya wawe wenye furaha.

Kisha ikaanza "Yudke - Mungu asifiwe" kama njia ya Yesu kule Jerusalem kuelekea msalabani, ila alifanikiwa kushinda. Katika kampuni ya wauaji, wafungwa wa kisiasa, na mabwana jela wenye roho mbaya katika jela kadhaa ndani ya Iraq, ila Taggar aliamini asingeweza kufa mateka. Siku moja atakuwa huru!

Alikua amesubiri kwa miaka tisa. Mwaka 1958, jenerali Abdul Karim Kassem alikamata madaraka kwa mapinduzi na kumuua waziri mkuu wa Iraq na familia yake yote. Miaka miwili baadae, wasaidizi wake wa karibu wakatengeneza mkakati wa kumuua ( ambao walikuja kufanikiwa miaka michache mbele). Mosad wakapata hizo habaro, na kiongozi wa Mossad mara moja akatengeneza mawasiliano na watu waaminifu wa Kassem, na kukubaliana dili : Angewapatia majina ya wasaliti waliopanga kumuua Kassem - kwa kubadilishana na uhuru wa Yehuda Taggar.

Taggar alikuwa kwenye sero yake iliyochoka na yenye giza, wakati mabwana jela walipomfuata na nguo za Khaki. "Vaa hizi" walimuamuru. "Unaenda Baghdad".
Gari ya Polisi ilimpeleka Taggar mpaka kwenye jengo la ikulu. Wanajeshi kadhaa wakamsindikiza mpaka kwenye ofisi kubwa. Nyuma ya dawati la thamani alikaa mtu aliyemfahamu - rais Kassem mwenyewe. Taggar aligundua mara: anaachwa kuwa huru! Kassem akatumia muda kidogo kumtizama huyu muisrael.
"Niambie", kisha akasema,"kama vita ikitangazwa kati ya Iraq na Israel, utapigana dhidi yetu?"
"Nitakaporudi nchini kwangu", Taggar akajibu, "Nitajitahidi nitakavyoweza kuleta uelewa na amani kati ya Israel na mataifa ya kiarabu. Ila kama vita itatokea, nitapigania Israel, kama ambavyo wewe umepigana mara nyingi kwa nchi yako".

Itaendelea...
 
Tuendelee...

UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD

Sehemu ya kumi.

Kassem alilipenda hili jibu. Alisimama."Utakapofika nyumbani", alisema,"waambie watu wako kwamba Iraq ni taifa linalojitegemea kwa sasa. Sisi sio watwana wa ubepari tena".

Kutoka ikulu, gari ikampeleka Taggar uwanja wa ndege. Bado hakuamini kilochokuwa kikiendelea. Walimpandisha ndege iliyokuwa ikielekea Beirut, halafu akapanda ndege iliyoelekea Nicosia, kisha Cyprus, na mwishowe akatua Israel. Pale uwanjani, marafiki na watumishi wenzake walikua wakimsubiri. Walitegemea kukutana na mtu aliyepigika na nafsi iliyopondeka - ila mtu aliyeshuka kutoka kwenye ndege alikuwa yuleyule shupavu, mchangamfu, mtu mwenye tabasamu ambaye walimuona kwa mara ya mwisho zaidi ya miaka tisa iliyopita.

Uliwezaje kushinda haya, walimuuliza. Uliwezaje kuendelea kuwa timamu, na mwenye matumaini? "Nilijua mngenitoa pale", Yudke alijibu kwa wepesi. Kwa kumrudisha Taggar nyumbani, viongozi wa Mossad walikua wametekeleza moja ya kanuni zilizowekwa kuanzia kutungwa kwa Mossad: Usibakize jitihada zozote, wala uwezo wowote, wala sadaka yeyote, kuwarudisha watu wetu nyumbani.

Akiwa Israel, Taggar alioa, akaanza familia, na baada ya kuhudumu vizuri kama mwana diplomasia nchi za nje, alikuwa profesa wa chuo kikuu. Reuven Shiloah hakujihusisha na 'balaa' la Baghdad kwa namna yeyote ile. Alistaafu mwishoni mwa mwaka 1952. Nafasi yake ikachukuliwa na nyota, aliyekuwa akichomoza kwenye ulimwengu wa vivuli wa taasisi ya kijasusi ya Israel. Dogo Isser (Little Isser)

Huu ni Mwisho wa sura ya tatu ila ni mwanzo wa sura ya nne - SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI.

Usikae mbali...
Tutaendelea...
 
Kazeni buti tuanze sura ya nne kwa speed ya 5G..
In the meantime MB zisisahaulike..
 
4. SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI.

Sehemu ya Kwanza.

Ze'ev Avni alitamaani sana kuwa shushushu wa Mossad. Alipokuja, siku moja yenye mvua, April 1956, makao makuu ya Mossad, alitamaani kwa moyo wake wote kuwa wakati wa kuondoka hapo awe tayari mwajiriwa wa Mossad. Kwa miaka mingi alijaribu kuwa mmoja kati ya wale wachache waliochaguliwa, na hili lilikuwa lengo la muhimu kwake zaidi katika maisha.

Alizaliwa akiitwa Wolf Goldstein ndani ya Riga, Latvia, na alikulia Uswisi, akahudumu katika jeshi la Uswisi katika vita kuu ya pili ya dunia (WW II), na kuhamia Israel mwaka 1948. Alibadili jina lake na kuwa la kiebrania Ze'ev Avni, na baada ya miaka kadhaa akiishi na kufanya kazi huko Kibbutz Hazorea, alijiunga na wizara ya mambo ya nje na akapangwa kufanya kazi Brussels. Akiwa mtu mwenye utu, msomi mzuri, na muongeaji mzuri wa lugha kadhaa, aliwakosha wakubwa wake kwa tabia zake na bidii pamoja na utayari wake kujitolea kwa kila shughuli, hasahasa zile zilizohusika na Mossad. Wakati wowote ambapo mwanadiplomasia alihitajika kwa kazi ya mjumbe wa siri, kwa safari ya haraka kwenda kwenye jiji lingine, kupeleka nyaraka za siri kwa kitengo chochote cha siri cha Mossad popote Ulaya - Avni alikua wakwanza kujitolea.

Ushirika wake wa kila mara na Mossad ukamfanya kuwa 'mtu wao' , ila asiye rasmi ndani ya Ulaya; na ushirika huu ulishika kasi wakati alipohamishiwa katika ubalozi wa Israel huko Belgrade, Yogoslavia. Katika barua kadhaa kwa 'ramsad'- kiongozi wa Mossad, Isser Harel, Avni alishauri kuanzishwa kwa kituo cha Mossad huko Belgrade. Harel alikataa : Mossad haikuwa na uhitaji wa kituo huko Yugoslavia; ila Avni hakukata tamaa.

April 1956, Avni alirudi Israel kwa safari binafsi na akaomba kumuona 'ramsad'. Ombi lake likakubaliwa, na sikuhiyo ndio angekutana na Isser Harel kwa mara ya kwanza. Akiwa mwenye shauku na wasiwasi, aliingia ofisini kwa Harel katika nyumba ya zamani ya lililowahi kuwa Koloni la Ujerumani huko Tel Aviv. Harel alikuwa ameteuliwa kuwa 'ramsad' sio chini ya miaka minne iliyopita, ila tayari alishakuwa Shujaa mahiri.

Watu walimuhusudu na kumuogopa huyu mtu mfupi asiyeisha mafumbo; hadithi za kweli na za uongo kumhusu zilisimuliwa katika viunga vya ofisi za Mossad. Avni alikua amesikia kiasi kuhusu Harel, ambaye alipewa jina la utani "Dogo Isser" - kumtofautisha na "Big Isser" aliyekuwa na sifa mbaya. Avni alikuwa na wasiwasi na huu mkutano, kufuatoa minong'ono ya ukaidi wa "Dogo Isser", tabia zake za paniki na hisia kali.

Itaendelea...
 
Tuendelee...

SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI.

Sehemu ya Pili.

Ila huyu mtu mfupi, mwenye kibihongo cha mbali, na upaa akiwa amevalia suruali ya Khaki na shati la mikono mifupi aliyempokea Avni katika ofisi iliyofanania na ofisi ya mtawa aliongea taratibu na alijawa na upendo. Alikiri kufurahishwa na tabia za Avni na ujuzi wake kwenye siasa.
Akamuuliza Avni sababu za yeye kutembelea Israel kwa sasa, na Avni akaeleza kuwa binti yake kutoka kwenye ndoa yake ya mwanzo alitaka aje kumuona."Binti yako ana miaka mingapi?" Isser aliuliza, huku akitabasamu. "Miaka nane"."Miaka nane?" Isser alionekana kushangaa. Alifikiri sio Kawaida kwa mwanadiplomasia kukimbia toka nchi za nje kuja nyumbani eti kisa binti yake mdogo amemuita.

Kisha Avni akaelezea kwa undani ,kuhusu uhusiano tata aliokuwa nao na mke wake wa kwanza, kuhusu mtoto, na kuhusu mke wake wa sasa. Isser alikosa uvumilivu, akamkatisha maelezo, na kumwambia hakutakuwa na kituo cha Mossad huko Belgrade. Na kuhusu nini Avni angeifanyia Mossad mbeleni, alisema,"Tutaona mara baada ya wewe kumaliza safari yako ya kikazi huko Yugoslavia". Avni akawa amegonga mwamba. Hata hivyo, kabla ya kuondoka, Isser alimpa ofa ya kukutana tena siku kadhaa zijazo,"Ila sio katika jengo hili, watu wengi sana wanaingia na kutoka hapa. Tutakutana kwenye ofisi yangu ya siri katikati ya jiji, dereva wangu atakupeleka hapo".

Bado kuna matumaini, Avni aliwaza. Kama sio - Kwanini Isser atake kumuona tena? Siku chache mbele, Avni aliingia katika majengo ya ofisi ya kawaida kabisa yasiyokuwa na utambulisho wowote wa tofauti katikati ya Tel Aviv. Sasa hakuwa na sababu ya kumhofia Isser tena; hata na hivyo alikuwa mkarimu kwenye mkutano wao wa mwanzo.Isser alikuwa akimsubiri na akamuongoza kuelekea kwenye chumba kikubwa: kuta za kawaida, dawati, viti kadhaa na madirisha yaliyofungwa.

Avni akaketi na Isser ghafla akabadilika na kuwa 'dume la ng'ombe' lenye hasira. Uso wake ulikunjamana, akapiga ngumi yake kwenye dawati na kufoka:" Wewe ni shushushu wa Kisovieti! Kubali! Kubali!" Akarudia tena:"Kubali!"
Akaendelea kupiga ngumi kwenye dawati, na kufoka:" Ninajua umetumwa na wasovieti! Najua wewe ni mpelelezi! Kubali!" Avni alikuwa kama amepigwa na radi, aliganda. Akajisikia kushindwa kutamka neno. "Kubali! Na kama ukinipa ushirikiano, nitajaribu kukusaidia, ila vinginevyo..."Moyo wa Avni ulidunda vibaya kifuani mwake. Alijawa na jasho la baridi na ulimi wake ukawa mzito.

Alikuwa na hakika kuwa siku zake za mwisho zilikuwa zimefika na Isser angemuacha auawe. Mwishowe akakusanya nguvu za kutamka maneno machache. "Nakubali", akasema, "Nafanya kazi na warusi". Isser akafungua mlango uliokuwa umefichwa, na wakaingia majasusi wake wawili mahiri zaidi na afisa wa polisi. Yule afsa akamkamata Avni, na akachukuliwa kwenda kwenye kituo cha mahojiano. Kisha hatua kwa hatua, akaweka wazi utambulisho wake na malengo yake ya kweli. Alikiwa mpenzi wa ujamaa toka utoto wake, alipewa mafunzo na ajira na wasovieti....

Itaendelea....
 
Tuendelee...

SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI.

Sehemu ya tatu.

...kupitia taasisi ya GRU (kitengo cha ujasusi cha Red army) wakati bado akiwa Uswisi, na alitumikia wasovieti katika kazi ya ushushushu katika vita kuu ya pili ya dunia - WW II.
Muda mfupi baadae alishauriwa kuhamia Israel na kusubiria. Alipangiwa kuwa 'fuko -mole) wa muda mrefu. Kwa miaka mingi, alitegemea ujumbe kutoka Moscow, ila viongozi wa ujasusi Urusi walisubiri kuwasiliana nae mpaka atakapopangiwa kituo cha kazi Brussels. Hapo aliwapatia taarifa muhimu juu ya dili za Israel na F.N (kiwanda cha jeshi huko Ubelgiji), aliwapatia pia alama za siri za mawasiliano 'codes' za wizara ya mambo ya nje ya Israel, na hata kuwawekea wazi majina ya wajerumani wawili waliokua wa-Nazi miaka ya nyuma na wanaoisaidia Israel kwenye kazi za kishushushu.

Kwa mshangao wa wathibiti wao, hawa wajerumani wawili ghafla walifukuzwa Misri. Ila hiyo haikutosha kwa maafisa wa Kesi wa Urusi waliokua wakimsimamia Avni. Walitaka mtu wao ajipenyeze ndani ya Mossad. Na hicho ndicho Avni alijitahidi kwa nguvu zote kufanya, mpaka muda Isser alipofoka,"Kubali!" Na alipoungama, hakujua jambo litakalomshtua zaidi: Angeweza kutoka kwenye mtego wa Isser kama mtu huru! Huyu kiongozi wa Mossad- ramsad hakuwa na hata tone la ushahidi dhidi yake, zilikuwa hisia tu, hakuna ushahidi wowote kwamba Avni alikuwa mpelelezi.

Ni kweli, muda mrefu uliopita, kuna mtu alimwambia Isser kuwa Avni alifukuzwa kutoka Kibbutz kwasababu ya mitazamo yake ya kijamaa. Ila shushushu wa Kisovieti?
Isser alichukua hatua kwa kufuata hisia zake tu. Jitihada zisizochoka za Avni kujiunga na Mossad; Safari iliyoonekana kuwa na utata kumtembelea mtoto wake; majaribio yake ya kumshawishi Isser kuanzisha kituo cha Mossad huko Belgrade .... matukio yote haya madogo madogo yalijikusanya pamoja kwenye fikra kali za Isser na kumpelekea kutamatisha: Shushushu, msaliti, alikuwa amekaribia kujipenyeza patakatifu pa watakatifu ( sanctum sanctorum).

Katika kesi yake, Avni alikiri makosa yake yote na kuhukumiwa miaka kumi na nne (14) jela. Aliachiwa kutoka gerezani baada ya miaka tisa, akawa raia wa mfano na mwana saikolojia. Isser aliwaeleza waandishi wa historia yake kuwa Avni alikuwa mpelelezi hatari zaidi kuwahi kukamatwa ndani ya Israel ila pia 'mtu mchangamfu sana' na akamzungumzia vizuri kuwa 'mpelelezi mstaarabu'. Avni mwenyewe alituambia baada ya miaka kupita baadhi ya maafisa wa polisi wa ngazi za juu na wapelelezi wa Shabak (mfano wa FBI ya marekani) walikuja kuwa marafiki zake wazuri.

Operesheni Pygmalion, kama jambo la Avni lilivyoitwa, kwa miaka mingi ilikuwa siri iliyolindwa kwa karibu sana na Mossad. Ila kwa wachache waliofahamu, ilikuwa ushahidi zaidi wa hisia za kushangaza za Isser.
Ila Isser alikuwa nani? Mtu mkimya, mwenye aibu, mbishi kama punda, ilisemekana alizaliwa katika ngome ya zamani ya Dvisk, katika dola ya Urusi; Inasemekana kuwa wakati amehamia Israel akiwa na miaka kumi na nane (18), alikuwa amebeba mfuko wenye mkate ambao ndani yake kulikuwa na bastola -revolver aina ya bakeda. 'Dogo Isser' kwanza alikaa kibbutz Shefayim, ambako alimuoa mwanamke wa wa 'shoka' mwenye furaha, Rivka.

Itaendelea....
 
Mkuu Kama umeamua kuweka story weka usifanye kuwa mradi.

Kumbuka hatukukuomba uanzishe story. Hii Ni dalili ya utapeli na ujanja ujanja kila baada ya vipande viwili unataka hela, kaa nayo Basi ili ije kugeuka kuwa bank upate hizo hela.
 
Duh! Punguza hasira...
Maisha yanaweza kuwa magumu ila mimi sijachangia lolote kwenye huo ugumu.
Usinichukie bure mkuu
Mkuu Kama umeamua kuweka story weka usifanye kuwa mradi.

Kumbuka hatukukuomba uanzishe story. Hii Ni dalili ya utapeli na ujanja ujanja kila baada ya vipande viwili unataka hela, kaa nayo Basi ili ije kugeuka kuwa bank upate hizo hela.
 
Duh! Punguza hasira...
Maisha yanaweza kuwa magumu ila mimi sijachangia lolote kwenye huo ugumu.
Usinichukie bure mkuu
Utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani huwezo kutofautisha kati ya Ukweli na chuki !!

Ulianza mwenyewe kuweka story , ukataka kujua muitikio wa watu juu ya kile unaandika , ukajibiwa kuwa Ni mzuri , ukaona hiyo Ni fursa kuomba hela kwa kisingizio Cha MBs. Sasa kila baada ya post 2 au 3 unaomba hela !!!! As if hukuwa umejipanga kwa bundle la kutosha kuleta content uliyokuwa umekusudia ? Kama ndio hivyo Basi ungekaa kimya kijana huu sio mradi . Usitafute kuwatapeli watu kwa kisingizio Cha mchango wa bundle. Fanya kazi
 
Bosi umekomaa mno na sijui ulichokomalia.
Hapa niko sura ya nne na toka nimeanza nimechangiwa elfu mbili na mia nne (Tsh 2,400/=)

Wewe unasoma story kiroho safi ila unataka kupambana na mimi..
Mkuu kama shem amekuchanganya vumilia tu ndio maisha...
Nilikuwa natiririka ila hata appetite umeniondolea..

Wewe kama huwezi kuchangia MB piga kimya soma mada nyingine zipo kibaooo...
Usigeuke mgomvi bila sababu..
Utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani huwezo kutofautisha kati ya Ukweli na chuki !!

Ulianza mwenyewe kuweka story , ukataka kujua muitikio wa watu juu ya kile unaandika , ukajibiwa kuwa Ni mzuri , ukaona hiyo Ni fursa kuomba hela kwa kisingizio Cha MBs. Sasa kila baada ya post 2 au 3 unaomba hela !!!! As if hukuwa umejipanga kwa bundle la kutosha kuleta content uliyokuwa umekusudia ? Kama ndio hivyo Basi ungekaa kimya kijana huu sio mradi . Usitafute kuwatapeli watu kwa kisingizio Cha mchango wa bundle. Fanya kazi
 
Maandiko
Hivi hata ningepata hela kwa kupitia haya maandiko kuna shida gani??
Maana kuna watu wamenifuata watsapp na kuniuliza kama nauza hii kazi na nikawajibu siuzi ila wachangie MB wakiwa interested. ..

Wewe tatizo lako hasa ni nini?
 
Back
Top Bottom