Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Tuendelee...

SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI

Sehemu ya nne

Akiwa mkali, mbishi asiyekubali kushundwa na mwenye uthubutu, alihama Kibbutz kwa sababu zisizofahamika akiwa na mke, mtoto, na shati moja tu alilokuwa amevaa. Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia -WW II, alijiunga na Haganah na mara akawa kiongozi wa kitengo cha kiyahudi cha Shai, kilichokua kikiwatafuta waasi na wapinzani. 'Wapinzani' walikua wanachama wa Irgun na kundi la Stern - vyama viwili vya siri vyenye kuegemea mrengo wa kulia vilivyopinga madaraka na siasa za David Ben- Gurion na jamii ya kiyahudi iliyojipanga pamoja.

Baada ya kuanguka kwa 'Big Isser', 'Dogo Isser' akawa kiongozi wa taasisi ya ulinzi wa ndani, Shabak. Mossad ni kama ilikuwa haijaanza kufa kazi wakati Ben- Gurion, katika hatua za haraka, alipokubali kujiuzulu kwa Reuven Shiloah na kumteua Isser kama kiongozi wa Mossad. Sababu rasmi za mabadiliko hayo ilikuwa ajali ya gari iliyomtia Shiloah ukilema; Ila minong'ono ndani ya Mossad ilisema kama Isser alimuandama Shiloah mpaka akatolewa, baada ya kumshawishi Ben- Gurion kuwa huyo 'ramsad' alikuwa msomi sana a mtu mwema, ila hakuweza kuwaongoza majasusi wakorofi na kutekeleza operesheni za siri.

Chini ya Isser, jamii ya kijasusi ilipata iliyoitwa 'muundo muafaka'. Ilijumuisha vitengo vitano : Mossad, Shabak, Aman ( majasusi wa jeshi), tawi maalum la polisi, kitengo cha utafiti cha wizara ya mambo ya nje. Kati ya hivi, ni Mossad, Aman, na Shabak vilikuwa na umuhimu; hivi vingine viwili havikuchukuliwa kwa umuhimu kivilee. Wakurugenzi wa hivi vitengo vitano na wasaidizi wao waliunda 'kamati ya viongozi wa vitengo'. Isser aliteuliwa kama mwenyekiti wa kamati hii. Ben - Gurion pia alijitengenezea jina la kipekee: memunneh - Mkurugenzi mkuu anayesimamia vitengo vya usalama.

Wakati amemteua 'dogo Isser' kwenye hii nafasi mpya, Ben - Gurion alisema : "Hata hivyo utaendelea kuongoza Shabak, pamoja na kuwa sasa una Mossad". Isser akachagua mkurugenzi mwingine wa Shabak, ila uthibiti wa vyote, Mossad na Shabak ulibaki kwenye mikono yake. Hivyo, 'dogo Isser' akawa mtawala - tsar wa ujasusi Israel. Suala la Pygmalion likawa moja kati ya operesheni muhimu Isser alizoongoza katika miaka ya mwanzo ya uwepo wa Israel, zaidi, dhidi ya wapelelezi wa kisovieti, wangi ambao walikamatwa, kufungwa au kufukuzwa Israel.

Ila sio wapelelezi wote waliowatumikia wasovieti - na sio kila hadithi ya kila mpelelezi ilikua na mwisho mzuri.
Siku moja mchana, mapema December 1954, ndege moja ya mizigo iliendelea kuzunguka juu ya Mediterranean ya mashariki. Wakati marubani wake walipokuwa na hakika kuwa hamna chombo chochote kinachotembea baharini kwenye hilo eneo, moja kati ya milango ya ndege ukafunguliwa na 'kitu' kikubwa kikadondoshwa ndani ya bahari - mwili wa mtu.

Itaendelea...
 
Kwenye jamii kuna watu wa hovyo sana nadhani na wewe ukiwemo..
Umewaza nini kuniita tapeli?

Kuna watu wanaweka story watsapp na kuunga watu kwa hela, nao ni matapeli?

Hii elfu mbili mia nne ndio inayokufanya unitukane?

Nimeishiwa maneno ila nimekwazika sana!
Umaniita dogo, hunijui, hujui umri wangu... yani ni pepo mchafu tu umeamua kuniharibia siku!!
Na umeweka biblia kama profile photo ila unatukana tu bila kufikiria kama umetanguliza biblia...
Utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani huwezo kutofautisha kati ya Ukweli na chuki !!

Ulianza mwenyewe kuweka story , ukataka kujua muitikio wa watu juu ya kile unaandika , ukajibiwa kuwa Ni mzuri , ukaona hiyo Ni fursa kuomba hela kwa kisingizio Cha MBs. Sasa kila baada ya post 2 au 3 unaomba hela !!!! As if hukuwa umejipanga kwa bundle la kutosha kuleta content uliyokuwa umekusudia ? Kama ndio hivyo Basi ungekaa kimya kijana huu sio mradi . Usitafute kuwatapeli watu kwa kisingizio Cha mchango wa bundle. Fanya kazi
 
Kwenye jamii kuna watu wa hovyo sana nadhani na wewe ukiwemo..
Umewaza nini kuniita tapeli?

Kuna watu wanaweka story watsapp na kuunga watu kwa hela, nao ni matapeli?

Hii elfu mbili mia nne ndio inayokufanya unitukane?

Nimeishiwa maneno ila nimekwazika sana!
Umaniita dogo, hunijui, hujui umri wangu... yani ni pepo mchafu tu umeamua kuniharibia siku!!
Na umeweka biblia kama profile photo ila unatukana tu bila kufikiria kama umetanguliza biblia...
Mkuu achana nae kwenye jamii watu hao wapo
 
Tuendelee...

SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI

Sehemu ya Tano.

Ile ndege ikageuka na, lisaa limoja baadae ikatua Israel, kuashiria mwisho wa operesheni Injinia ( sio jina lake halisi), operesheni hii ikawa ya usiri wa hali ya juu kwa zaidi ya miaka hamsini. Mwaka 1949, ndugu wa tatu wa kiume kutoka familia moja ya kiyahudi huko Bulgaria waliwasili Haifa. Mkubwa wao, Alexander Israel, alikuwa amehitimu katika chuo cha Uinjinia huko Sofia. Akajiandikisha jeshini, akapewa cheo cha ukapteni, na akapangiwa kwenye jeshi la wanamaji wa Israel.

Kapteni Israel alikuwa ni kijana mwenye mvuto na mchangamfu sana. Alithaminiwa na wakubwa zake na akapangwa katika utafiti wenye usiri wa hali ya juu katika vita vya kielektroniki na utengenezaji wa silaha mpya. Akapewa kibali cha usalama cha hali ya juu na aliweza kushuhudia na kuwa karibu na nyaraka na vitu vingine vingi ambavyo ni vya nyeti sana. Akabadili jina lake lakwanza kuwa Avner, jina la kiebrania, na mwaka 1953 akamuoa Matilda Arditi, msichana mrembo mwenye asili ya Uturuki.

Wawili hawa wakaweka makazi huko Haifa, karibu na ngome kubwa zaidi ya Kijeshi ya Israel. Matilda alimpenda sana huyu mume wake mwenye mvuto, ila hakujua mapungufu yaliyokuwa katika utu wake. Hakujua kama alikuwa na rekodi ndefu na mbovu huko polisi. Avner Israel alituhumiwa kwa kukodishia jengo moja la makazi mara kadhaa kwa mpangaji zaidi ya mmoja; kwa kujifanya kama muwakilishi wa kampuni ya kuuza friji na kukusanya malipo ya awali kwa friji ambazo hazikukabidhiwa kwa waliotoa fedha; na dili nyingine kadhaa za sampuli hiyo.

Kesi moja ilifika mahakamani, na akapewa wito wa kufoka mahakamani kwa kesi November 8, 1955. Matilda akiwa amebanwa na majukumu ya mtoto, hakujua chochote juu ya utapeli wa mume wake, wala mahusiano yake na karani mrembo katika ubalozi wa Italia huko Haifa. Avner hata alimchumbia na kuweka nia ya kumuoa, ila huyu msichana wa kiitalia alikubali kwa sharti moja: lazima kwanza abadili dini na kuwa mkatoliki.

Kwa kijana Avner hili halikuwa tatizo hata kidogo. Alishawahi kubadili dini mara moja kabla, huko Bulgaria, wakati alipolazimika kumuoa msichana mwingine wa kikristu ambaye alimtongoza. Familia yake iliyokuwa imekasirishwa ilimtaka - karibu kwa kumtisha na bunduki - kwamba abadili dini na amuoe huyo msichana.
Mara tu baada ya harusi akakimbia Sofia, mke wake akajiua, na kisha akarudi Sofia na kurudia dini yake ya 'Judaism'. Sasa akarudia tena. Alisafiri kwenda Jerusalem akiwa na 'mpango wa kando', akabatizwa kwenye konventi ya Terra Santa, na akabadili jina lake kuwa Ivor. Kwa kutumia nyaraka alizopatiwa na kanisa, kapteni huyu mchangamfu alijisajili na wizara ya mambo ya ndani na akapatiwa passi ya kusafiria kwa jina lake jipya, Alexander Ivor.

Yeye na 'bi mdogo' wa kitaliano wakapanga November 7, 1954, kama tarehe ya harusi yao. Ile kesi kule Haifa ilipangwa kusikilizwa November 8. Avner Israel, aka Alexander Ivor, hakuwa na nia ya kuhudhuria hayo matukio yote. Muda ulikua umewadia kwa yeye kupotea.
Mwishoni mwa October, kapteni Israel alienda kwenye likizo ya wiki mbili. Alikuwa hana Visa ya kutoka ila Alexander Ivor alikuwa nayo, na nyaraka zinazojitosheleza, nyingine halisi, nyingine zakugushi. Akanunua tiketi ya ndege kwenda Rome, na November 4 aka...

Itaendelea....
 
Tuendelee...

SHUSHUSHU WA KISOVIETI NA MWILI WA MTU BAHARINI

Sehemu ya sita.

...ondoka. Sio mke wake wala "mchumba wake" aliyejua kuondoka kwake. Baada ya mchumba wake kuondoka, huyu mwanamke wa Kiitaliano akaanza msako wa shauku. Mwishowe akawaendea Polisi wa Haifa; kwa msaada wao akapata anwani yake, ambapo alipata mshtuko alipokutana na Mrs. Matilda Israel, akiwa na mimba ya miezi saba. Alipofika Rome Avner Israel akatoweka, ila sio kwa muda mrefu. Afisa mkazi wa Mossad pale alikuwa na vyanzo vizuri vya taarifa ndani ya jamii ya kidiplomasia ya kiarabu. November 17 simu yenye uharaka ikaita makao makuu ya Mossad huko Tel Aviv:" Kuna afisaa wa Israel kwa jina la Alexander Ivor au Ivon au Ivy yuko hapa, na anajaribu kuuza taarifa za kijeshi kwa mjumbe wa kijeshi wa Misri"

'Ramsad' na kiongozi mpya wa Shabak, Amos Manor, wakaunganisha nguvu kujua huyu mtu ni nani. Ndani ya siku chache wakagundua utambulisho wake, na walikatishwa tamaa kujua ni afsa wa jeshi la majini wa Israel. Telegramu nyingine kutoka Rome ilileta shida zaidi: Jasusi wa Mossad alitaarifu kuwa yule Muisrael amemuuzia yule mmisri mkakati wenye taarifa za kutosha wa ngome kubwa ya IDF huko Israel, na alikua amelipwa dola elfu moja na mia tano ($ 1,500/=), ambazo aliweka katika Benki ya Suisse. Ilisemekana alimuahidi yule mmisri taarifa zaidi, na alikubali kusafiri kwenda Misri, kutoa taarifa zote kwenye mahojiano.

Siku chache mbele, simu nyingine : " Ubalozi wa Misri uliweka oda ya tiketi mbili kwenda Cairo mwishoni mwa November, katika wakala wa TWA. Ilifahamika hao abiria wawili wangekuwa mjumbe wa jeshi la Misri na afisa wa Israel". Kengele za tahadhari zikagonga makao makuu ya Mossad. Kwa Isser, kulikuwa na tofauti ya kuhojiwa kwa 'mtoa taarifa' na mjumbe wa jeshi kwenye nchi ya ugenini na kusafirishwa kwa 'mtoa taarifa' yuleyule kwenda mji mkuu wa Misri, ambako atahojiwa na wataalam, ambao wangepata taarifa nyingi zaidi na za hatari kutoka kwake.

Isser alidhamiria kuzuia - kwa gharama yoyote - safari ya Avner Israel kwenda Cairo. Aliamua kutuma timu yake ya operesheni kwenda Rome. Katika hizi siku za mwanzo, Mossad haikuwa na kitengo cha operesheni na kilitumia vikosi vya operesheni vya Shabak. Kamanda wake, moja kati ya majasusi bora kabisa wa Israel, alikuwa shujaa kwa watu wake - Rafi Eitan. Alizaliwa huko Kibbutz, alikuwa mfupi na mnene, aliyevaa miwani, na alipenda utani ila pia alikuwa na uthubutu, mbunifu,na asiye na huruma. Alikuwa mpiganaji wa Palmach miaka kadhaa kabla ya uhuru, na alikuwa amejihusisha kwa undani sana na Aliya Beth, chama cha silicho waingiza wayahudi kinyemela Palestina pamoja na zuio la Uingereza.

Walikua wamekwepa boti za ulaya zilizowakatisha matumaini, wakakwepa Meli za kivita za Uingereza zilizokuwa zikilinda fukwe za Palestina, na kutua katika fukwe zilizotelekezwa, na kisha kujichanganya na jamii ya wayahudi wenyeji.

Tukio maarufu la kimedani la Rafi ilikuwa kulipua kituo cha rada che Uingereza juu ya mlima Carmel, karibu na Haifa, kilichokuwa kikiangalia vyombo vya majini vya Aliya Beth vilivyokua vikisogea.
Kuzifikia Rada, Rafi alitambaa kwenye bomba za maji taka na kujipatia jina la utani "Rafi anayenuka".

Itaendelea....
 
Akiendelea kuzingua NAPANDISHA KITABU HAPA choote page 300...wengi tukaamua kwenda kusoma the book itself
 
Officially nakuachia kijiti, malizia mkuu!
Soon mimi nitaanza kitabu kingine na Richard Flanagan - Njia nyembamba kuelekea ndani kabisa ya Kaskazini " The narrow road to the deep North".

Hicho komaa nacho..

Akiendelea kuzingua NAPANDISHA KITABU HAPA choote page 300...wengi tukaamua kwenda kusoma the book itself
 
Ila huyu ndugu anakwaza, amesoma parts zote fresh, hajanipa hata jero ya MB ila kaamua kunitukana...

Anyway, na yenyewe ni sadaka!
Ungeandika tangu ulipoanza kwamba utahitaji mchango wa MBs tujue sio unakuja kutafuta huruma kwa wadau kila wakati .

Alafu utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani Bado huwezi kutofautisha kuambiwa Ukweli na kutukanwa ?
 
Nachagua kunyamaza this time!
Ungeandika tangu ulipoanza kwamba utahitaji mchango wa MBs tujue sio unakuja kutafuta huruma kwa wadau kila wakati .

Alafu utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani Bado huwezi kutofautisha kuambiwa Ukweli na kutukanwa ?
 
Nachagua kunyamaza this time
Ungeandika tangu ulipoanza kwamba utahitaji mchango wa MBs tujue sio unakuja kutafuta huruma kwa wadau kila wakati .

Alafu utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani Bado huwezi kutofautisha kuambiwa Ukweli na kutukanwa ?
 
Ungeandika tangu ulipoanza kwamba utahitaji mchango wa MBs tujue sio unakuja kutafuta huruma kwa wadau kila wakati .

Alafu utakuwa unashida kwenye uelewa wako yaani Bado huwezi kutofautisha kuambiwa Ukweli na kutukanwa ?
Wewe jamaa una wivu wa kike ka gasho
 
Kitu nachoona mimi, huku mtaani maisha yanawafanya watu vibaya...
Kuna watu wana maumivu makali na wamepata shida kwenye kufikiri na hawajui kama wamepata shida..
Kuna watu wana 'sonona' na hawajashtukia...

Mimi nadhani twendeni taratibu tu tutafika! Tuwasiliane vizuri na kwa staha..
Usigombane na mtu wakati msongo wa mawazo ulionao yeye hajahusika hata nukta nao.
 
Kitu nachoona mimi, huku mtaani maisha yanawafanya watu vibaya...
Kuna watu wana maumivu makali na wamepata shida kwenye kufikiri na hawajui kama wamepata shida..
Kuna watu wana 'sonona' na hawajashtukia...

Mimi nadhani twendeni taratibu tu tutafika! Tuwasiliane vizuri na kwa staha..
Usigombane na mtu wakati msongo wa mawazo ulionao yeye hajahusika hata nukta nao.
Kwa kifupi n kwamba tubalance shobo

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom