Tuendelee....
MAZISHI NDANI YA TEHRAN
Sehemu ya kumi na moja.
...mashinikizo ya kidiplomasia, vikwazo vilivyowekwa na baraza la usalama la umoja wa mataifa; mbinu za kukwamisha kasi - kuwazuia wairan kupata malighafi zilizohitajika kutengeneza bomu; vita vya kiuchumi - Kukataza mabenki katika nchi zinazoendeshwa kidemokrasia kufanya biashara na Iran; Kuchochea mabadiliko ya kiutawala, Kwa kutoa misaada na kuimarisha vurugu za kisiasa na kuchochea mipasuko ya kikabila ndani ya Iran, ambapo wakurd, waazeri, wabeloshi, waarabu na wa-Turkmen walichangia asilimia hamsini (50%) ya idadi yote ya watu; na zaidi sana, hatua za siri, operesheni maalum na za 'giza' dhidi ya mradi wa Iran.
Ila pamoja na ubora wao wote, hawakuweza kuusimamisha mradi moja kwa moja, hata pamoja na ushirikiano wao wote."Dagan ndiye 'James Bond' wa ukweli",mchambuzi wa hadhi ya juu wa Israel alisema, ila kwenye huu mradi, hata James Bond hakuweza kuiokoa dunia. Alifanikiwa tu kuwapunguza kasi wairan. Ni au maamuzi ya serikali ya Iran au shambulio kubwa kutoka nje ya Iran, ambavyo vingeweza kabisa kusitisha ndoto ya Iran ya kuwa taifa lenye nguvu ya nyuklia mahali ambapo, kabla, ilisimama Hima ya Persia.
Hata hivyo, wakati Dagan anachaguliwa kuwa kiongozi wa Mossad (ramsad - kifupi cha rosh hamossad), wataalam walibashiri kuwa Iran itafikia uwezo wa kinyuklia mwaka 2005; tarehe hii ilisogezwa mpaka 2007, baadae 2009, kisha 2011. Na Dagan aliposimama kazi, Januari 6,2011, alikuwa na ujumbe kwa nchi yake: Mradi wa Iran umecheleweshwa angalau mpaka mwaka 2015. Hivyo alishauri muendelezo wa matendo yaleyale, yaliyofanikiwa sana kwa miaka nane iliyopita, na kuachana na shambulio lolote la kijeshi dhidi ya Iran. Ni pale tu makali ya kisu yatakapoanza kutukata, hapo ndipo tutashambulia; makali hayo yamebakiza miaka minne kuanza kutukata.
Dagan alihudumu kama kiongozi wa Mossad (ramsad) kwa miaka nane na nusu - miaka mingi zaidi kuzidi viongozi wengi wa Mossad. Aliachia kiti kwa Tamir Pardo, afsa mkongwe wa Mossad aliyeanza kazi za operesheni kama msaidizi wa karibu wa Yoni Netanyahu, shujaa wa uvamizi wa 1976 wa Israel kule Entebbe, na baadae akajitanabaisha kama jasusi mwenye uthubutu mkubwa, mtaalam wa tekinolojia mpya, na mpanga mikakati mbunifu kwenye operesheni zisizo za kawaida.
Wakati wa kumkabidhi Pardo tochi, Dagan aliongelea mazingira magumu ya upweke ya majasusi wa Mossad wanaofanya operesheni katika nchi maadui, wakati hawana mtu wa kumgeukia, hawana mtu wa kuwaokoa inapohitajika. Kwa unyenyekevu alikubali baadhi ya madhaifu yake; kubwa zaidi ikiwa kushindwa kufahamu sehemu ambayo Hamas walimficha mwanajeshi wa Israel, Gilad Shalit, aliyetekwa miaka mitano iliyopita. Ila hata pamoja na madhaifu hayo, mafanikio ya Dagan yalimheshimisha kama kiongozi bora zaidi wa Mossad kuwahi kutokea.
Waziri mkuu, Benjamin Netanyahu alimshukuru "kwa niaba ya waisraeli wote" na kumkumbatia kwa upendo. Katika tukio la ghafla na lisilotegemewa, baraza la mawaziri lilisimama na kumpigia makofi kiongozi huyu wa Mossad aliyekuwa na miaka sitini na tano (65). George W. Bush alimsalimu katika barua binafsi.
Ila sifa za kipekee kabisa kwa Dagan zilitolewa mwaka mmoja kabla, kutoka kwenye chanzo cha habari cha nje, gazeti la kila siku huko Misri, Al- Ahram, lililofahamika kwa uadui na upingaji mkali wa Israel.
Januari 16, 2010, lilichapisha makala iliyoandikwa na mwandishi aliyefahamika vizuri, Ashraf Abu Al- Haul. "Bila Dagan," Al- Haul aliandika,"mradi wa nyuklia wa Iran ungekuwa umekamilika miaka mingi iliyopita.... wairan wanajua ni nani aliyehusika na mauaji ya mwanasayansi wa nyuklia Masud Ali Mohammadi. Kila kiongozi wa ngazi za juu Iran anajua kuwa neno la msingi ni 'Dagan'.
Ni watu wachache wanaolifahamu jina la mkurugenzi wa Mossad. Anafanya kazi kimyakimya, mbali kabisa na vyombo vya habari. Ila kwa miaka saba iliyopita ametoa mapigo yenye maumivu makali kwa mradi wa nyuklia wa Iran na kuzuia muendelezo wake.
"Mossad inahusika na operesheni kadhaa zilizohitaji uthubutu wa hali ya juu Mashariki ya jati," Al - Haul aliongeza, na kutaja baadhi ya mafanikio ya Dagan dhidi ya Syria, Hizbollah, Hamas, na Islamic Jihad.. (tutaona katika sura ya 18 -20).
"Yote haya," alimalizia," Yamemfanya Dagan kuwa mtu wa kutukuka sana ndani ya taifa la Israel."
Hakukuwa na watu wa kutukuka sana ndani ya shirika la kijasusi la Israel wakati linazaliwa May 1948, ukiacha wakongwe wachache wa 'Shai', waliokua wamepata uzoefu katika operesheni za siri na za kuhujumu kutoka kwenye shirika la kijasusi la Haganah, shirika la jeahi la siri la jamii ya kiisraeli ndani ya Palestina.
Na katika miaka yao ya mwanzo, hawa wapiganaji wa viwango vya kawaida ila waliojituma, wa taasisi changa ya usalama ya kijeshi, walitingishwa na fujo, misuguano ya ndani, ukatili na mauaji ya, iliyokuja kujulikana kama "jambo la Be'eri".
Mwisho wa sura ya pili.. ila ni mwanzo wa sura ya tatu - UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD.
Hivyo usiende mbali...
Tutaendelea...