Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Wadau naombeni comments zenu! Vipi tupunguze speed au tuongeze..
Mzigo una sura ishirini na moja na ndio kwanzaa sura ya pili...
Na utamu wa hii kitu uko tunakoelekea japo ni muhimu kuwa na hii misingi ya mwanzo.
 
Wadau naombeni comments zenu! Vipi tupunguze speed au tuongeze..
Mzigo una sura ishirini na moja na ndio kwanzaa sura ya pili...
Na utamu wa hii kitu uko tunakoelekea japo ni muhimu kuwa na hii misingi ya mwanzo.
Mkuu shusha nondo sisi wengine tunaenjoy sana hizi story huwezi amini mimi huwa sipati usingizi kama kuna mambo matamu kama haya
 
Wadau naombeni comments zenu! Vipi tupunguze speed au tuongeze..
Mzigo una sura ishirini na moja na ndio kwanzaa sura ya pili...
Na utamu wa hii kitu uko tunakoelekea japo ni muhimu kuwa na hii misingi ya mwanzo.
Weka mzigi
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya nane.

Mwaka 2008 na 2010, gazeti la New York Times liliripoti kuwa 'Tinners', familia ya uswisi ya mainjinia, ilisaidia CIA kuweka hadharani programu ya nyuklia ya Libya na Iran na walilipwa dolla millioni kumi na CIA ($10 million). CIA pia ilisaidia kuwalinda dhidi ya mashtaka ambayo wangeweza kufunguliwa na mamlaka za Uswisi kwa kutorosha vifaa vya ki-nyuklia. Baba yao, Frederic Tinner, na wanawe wawili, Urs na Marco, waliiuzia Iran vifaa feki katika ufungaji wa umeme kuelekea kituo cha Natanz, vilivyowezesha kuharibu vizungushi vya kasi hamsini (50 centrifuges). Kina- Tinner walinunua pampu za presha kutoka, Pfeiffer Vacuum Company, ya Ujerumani? Na wakazifanyia mizengwe huko New Mexico na kisha kuziuza kwa Iran.

Gazeti la Time lilieleza kuwa, Mossad ilihusika katika utekaji wa meli kwenye bahari ya Arctic, ambayo ilisafiri kutoka Finland kwenda Aljeria na mabaharia wa Urusi huku ikipeperusha bendera ya Maltese, ikibeba 'mzigo wa kuni'. Julai 24, 2009, siku mbili baada ya kuanza safari, chombo kilitekwa na watekaji nane. Ilichukua mwezi mzima kwa Urusi kusema kuwa kikosi cha makomandoo wa Urusi kimeikomboa meli hiyo.
Gazeti la Times la London na Daily Telegraph vilidokeza kuwa Mossad ndio waliopiga kengele ya hatari. Watu wa Dagan, walisemekana, waliitaarifu Urusi kuwa meli ilikuwa imebeba mzigo wa Uranium, uliouzwa kwa Iran na afisa wa zamani wa Urusi.Ila admirali Kouts, aloyeongoza mapambano dhidi ya maharamia katika umoja wa Ulaya alitoa mtazamo wa peke yake kwa gazeti la Times. Maelezo pekee yaliyonyooka, alisema, ni kiwa meli ilitekwa na Mossad ili kuzuia Uranium kufika Iran.

Ila pamoja na haya mashambulizi yaliyoendelea, Wa-Iran hawakukaa tu bila kufanya kitu. Kati ya 2005 na 2008, kwa usiri mkubwa,walijenga kituo kipya karibu na Qom. Walipanga kuweka vizungushi vya kasi elfu tatu (3000) kwenye kumbi mpya chini ya ardhi.

Hatahivyo, katikati ya 2009, Iran ilitambua yakua, taasisi za ujasusi za Marekani, Uingereza na Israel walikuwa na taarifa zote kuhusu kituo cha Qom.Iran ikachukua hatua mara moja. Septemba 2009, Tehran ilishangaza dunia kwa kuwahi kuwataarifu waangalizi wa kimataifa wa masuala ya atom (IAEA) juu ya uwepo wa kituo cha Qom.

Baadhi ya vyanzo vya taarifa vilieleza kuwa Iran ilimdaka mpelelezi kutoka magharibi ( ilidokezwa huenda ni mpelelezi wa MI6 ya Uingereza), ambaye alikwishakusanya taarifa za muhimu na za kuaminika juu ya Qom; hivyo waliweka wazi uwepo wa kituo hicho ili kupunguza aibu.

Mwenzi mmoja baadae, mkurugenzi wa CIA, Leon Panetta aliliambia gazeti la Times kuwa taasisi yake ilifahamu juu ya Qom kwa miaka mitatu na Israel ilihusika katika kuigundua. Ugunduzi wa Qom ulionyesha kwa mbali ushirikiano uliotengenezwa kati ya taasisi tatu zilizohusika na mapambano dhidi ya Iran: CIA, MI6, na Mossad.
Kutoka kwenye vyanzo vya taarifa vya Ufaransa, taasisi hizo tatu zilifanya kazi pamoja, ambapo Mossad ilikuwa ikitekeleza operesheni ndani ya Iran, CIA na MI6 wakiwasaidia waisraeli.

Itaendelea.....
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya nane.

Mwaka 2008 na 2010, gazeti la New York Timesa liliripoti kuwa 'Tinners', familia ya uswisi ya mainjinia, ilisaidia CIA kuweka hadharani programu ya nyuklia ya Libya na Iran na walilipwa dolla millioni kumi na CIA ($10 million). CIA pia ilisaidia kuwalinda dhidi ya mashtaka ambayo wangeweza kufunguliwa na mamlaka za Uswisi kwa kutorosha vifaa vya ki-nyuklia. Baba yao, Frederic Tinner, na wanawe wawili, Urs na Marco, waliiuzia Iran vifaa feki katika ufungaji wa umeme kuelekea kituo cha Natanz, vilivyowezesha kuharibu vizungushi vya kasi hamsini (50 centrifuges). Kina- Tinner walinunua pampu za presha kutoka, Pfeiffer Vacuum Company, ya Ujerumani? Na wakazifanyia mizengwe huko New Mexico na kisha kuziuza kwa Iran.

Gazeti la Time lilieleza kuwa, Mossad ilihusika katika utekaji wa meli kwenye bahari ya Arctic, ambayo ilisafiri kutoka Finland kwenda Aljeria na mabaharia wa Urusi huku ikipeperusha bendera ya Maltese, ikibeba 'mzigo wa kuni'. Julai 24, 2009, siku mbili baada ya kuanza safari, chombo kilitekwa na watekaji nane. Ilichukua mwezi mzima kwa Urusi kusema kuwa kikosi cha makomandoo wa Urusi kimeikomboa meli hiyo.
Gazeti la Times la London na Daily Telegraph vilidokeza kuwa Mossad ndio waliopiga kengele ya hatari. Watu wa Dagan, walisemekana, waliitaarifu Urusi kuwa meli ilikuwa imebeba mzigo wa Uranium, uliouzwa kwa Iran na afisa wa zamani wa Urusi.Ila admirali Kouts, aloyeongoza mapambano dhidi ya maharamia katika umoja wa Ulaya alitoa mtazamo wa peke yake kwa gazeti la Times. Maelezo pekee yaliyonyooka, alisema, ni kiwa meli ilitekwa na Mossad ili kuzuia Uranium kufika Iran.

Ila pamoja na haya mashambulizi yaliyoendelea, Wa-Iran hawakukaa tu bila kufanya kitu. Kati ya 2005 na 2008, kwa usiri mkubwa,walijenga kituo kipya karibu na Qom. Walipanga kuweka vizungushi vya kasi elfu tatu (3000) kwenye kumbi mpya chini ya ardhi.

Hatahivyo, katikati ya 2009, Iran ilitambua yakua, taasisi za ujasusi za Marekani, Uingereza na Israel walikuwa na taarifa zote kuhusu kituo cha Qom.Iran ikachukua hatua mara moja. Septemba 2009, Tehran ilishangaza dunia kwa kuwahi kuwataarifu waangalizi wa kimataifa wa masuala ya atom (IAEA) juu ya uwepo wa kituo cha Qom.

Baadhi ya vyanzo vya taarifa vilieleza kuwa Iran ilimdaka mpelelezi kutoka magharibi ( ilidokezwa huenda ni mpelelezi wa MI6 ya Uingereza), ambaye alikwishakusanya taarifa za muhimu na za kuaminika juu ya Qom; hivyo waliweka wazi uwepo wa kituo hicho ili kupunguza aibu.

Mwenzi mmoja baadae, mkurugenzi wa CIA, Leon Panetta aliliambia gazeti la Times kuwa taasisi yake ilifahamu juu ya Qom kwa miaka mitatu na Israel ilihusika katika kuigundua. Ugunduzi wa Qom ulionyesha kwa mbali ushirikiano uliotengenezwa kati ya taasisi tatu zilizohusika na mapambano dhidi ya Iran: CIA, MI6, na Mossad.
Kutoka kwenye vyanzo vya taarifa vya Ufaransa, taasisi hizo tatu zilifanya kazi pamoja, ambapo Mossad ilikuwa ikitekeleza operesheni ndani ya Iran, CIA na MI6 wakiwasaidia waisraeli.

Itaendelea.....
Kiongozi unatoa kidogo sana hebu ongeza mkuu maana dah!
 
Wadau naombeni comments zenu! Vipi tupunguze speed au tuongeze..
Mzigo una sura ishirini na moja na ndio kwanzaa sura ya pili...
Na utamu wa hii kitu uko tunakoelekea japo ni muhimu kuwa na hii misingi ya mwanzo.
ongeza speed mkuu.. uzi wako unafuatiliwa, sanaa..

ushatuoa arosto
 
Tuendelee....

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya tisa.

Mossad ilihusika na milipuko kadhaa ndani ya October 2010, ambapo wataalam 18 wa Iran waliuawa katika kituo kimoja kilichokua katika milima ya Zagros, kikiunganisha makombora aina ya Shehab.
Kwa msaada wa marifiki zake, Uingereza na Marekani, Mossad ilifanikiwa pia kuwaua wanasayansi watano waliojihusisha na nyuklia.

Urafiki huu uliimarishwa kiasi kikubwa kwa juhudi za Meir Dagan. Kuanzia siku amekuwa mkurugenzi wa Mossad, aliongeza presha kwa watu wake kujenga ushirikiano wa karibu na taasisi za nje za kijasusi.
Wasaidizi wake walimshauri kutoanika siri za Mossad kwa wageni, ila alipotezea huo ushauri."Achaneni na huo ujinga", alifoka,"na muende mkafanye nao kazi!"

Ukiacha Uingereza na Marekani, Dagan alikuwa na rafiki mwingine wa muhimu aliyeleta taarifa za thamani kubwa kutoka ndani ya Iran: Kiongozi wa upinzani Iran. Katika mkutano usiokua wa kawaida na vyombo vya habari uliofanyika nje ya Iran,Kiongozi wa baraza la upinzani la kitaifa alitaja jina la mwanasayansi kiongozi katika mradi wa Iran. Mpaka kufikia hapo, utambulisho wake ulikua umefanywa kuwa siri.

Mohsen Fakhri Zadeh, akiwa na miaka harobaini na tisa, alikuwa profesa wa Fizikia katika chuo kikuu cha Tehran. Alisemekana kuwa mtu wa ajabu na aloyeishi kwa kupoteapotea.
Upinzani uliweka hadharani taarifa nyingi kumhusu, ikiwa ni pamoja na uanachama wake kwenye jeshi la ulinzi wa mapinduzi kutokea umri wa miaka kumi na nane (18), anwani yake - mtaa wa ShahidMhallalti, Tehran, namba za paspoti ya kusafiria - 0009228 na 4229533, na hata namba yake ya simu ya nyumbani, 021 - 2448413.

Fakhri Zadeh alikuwa na taaluma iliyojikita katika mchakato wa kugeuza bomu la msingi kuwa na ujazo na uzito wa kutosha kuanzisha mnyororo wa matukio ambao unapelekea mlipuko wa nyuklia. Timu yake pia ilikuwa ikifanya kazi kupunguza ukubwa wa bomu, ili liweze kubebwa katika kichwa cha kombora la shehab.

Kufuatia ufahamu wa mambo haya, Zadeh alikataliwa kuingia Marekani na katika nchi za jumuiya ya Ulaya, na akaunti zake za benki katika nchi za magharibi zikazuiliwa.
Upinzani walieleza hatua kwa hatua matendo yake yote, wakaweka bayana majina ya wanasayansi wengine waliokua wakishirikiana naye na hata sehemu zilipo maabara zake za siri.

Huu wingi wa taarifa na namna zilivyotolewa, zinampelekea mtu yeyote kuamini kuwa, kwa mara nyingine, "taasisi fulani ya ujasusi" iliyowahi kushukiwa na mataifa ya magharibi kwa kuwa na ajenda yake peke yake ya siri, ilikusanya hizi taarifa kwa shida juu ya huyu mwanasayansi wa Iran na kuwapatia Wapinzani ndani ya Iran, ambao waliziwasilisha kwa mataifa ya magharibi.
Kumuweka 'uchi' kulikua na maana ya kumuonya kuwa anaweza kuwa "ndiye anayefuata katika mstari" wa kuuawa na kumchagiza kujificha au kuchagua suluhu bora zaidi: kukimbilia kwenye mataifa ya magharibi.

Jenerali AliReza Asgari, waziri wa ulinzi msaidizi aliyepita wa Iran, alipotea Februari 2007 akisafiri kwenda Istanbul. Alikuwa amehusika kwa undani sana kwenye mradi wa nyuklia. Majasusi wa Iran walimtafuta kila mahali, ulimwengu mzima, ila hawakuweza kumpata.

Kama miaka minne baadae, Januari 2011, waziri wa mambo ya nje wa Iran, AliAkbar Salehi, akamgeukia katibu mkuu wa umoja wa mataifa na kuituhumu Mossa kwa kumteka na kumfunga kwenye magereza ndani ya Israel. Ila kwa mujibu wa gazeti la Sunday Telegraph la London, Asgari alikuwa ameasi na kukimbilia magharibi; Mossad ilipangilia uasi huo na walihusika kumlinda akiwa Uturuki. Vyanzo vingine vilidai kua baadae alihojiwa na CIA na akawapatia taarifa muhimu sana juu ya programu ya nyuklia ya Iran.

Mwezi mmoja baada ya kupotea kwa Asgari - March 2007 - afisa mwingine wa ngazi za juu wa Iran naye alipotea. Amir Shirazi aliyetumikia katika kikosi cha "Al Quds", kikosi mahiri sana ndani ya jeshi la ulinzi wa mapinduzi, kilichojihusisha na operesheni za siri nje ya mipaka ya Iran.
Chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya Iran kililiambia gazeti la London Times kuwa, ukiacha kupotea kwa Asgari na Shirazi, afisa mwingine wa ngazi za juu pia alipotea: kamanda wa jeshi la ulinzi wa mapinduzi kwenye ghuba ya Persia, Mohammad Soltani.

Julai 2009, mwanasayansi wa nyuklia, Shahram Amiri alijiunga kwenye orodha ya wasaliti. Amiri aliyekuwa ameajiriwa Qom, alipotelea Saudi Arabia alipoenda kuhiji Mecca. Iran iliwataka wasaudia kuchunguza kilichompata Shahram. Amiri alijitokeza miezi michache baadae huko Marekani, akahojiwa vyakutosha, akapewa dolla millioni tano ($5 million), kitambulisho kipya, na makazi mapya huko Arizona.

Vyanzo vya CIA vilieleza kuwa Amiri alikuwa mtoa taarifa kwa miaka mingi kwa vyombo vya ujasusi vya magharibi na alikiwa akiwapatia taarifa 'halisi na iliyochakatwa vizuri'.
Amiri alieleza kuwa chuo cha Tecknolojia cha Malek - Ashtar, alipowahi kufundisha, kilikuwa tu kama geresha kwa kutoa elimi. Ila ukweli ni kuwa kilikuwa kituo cha utafiti wa kuunda vichwa vya kubebea mabomu yatakayorushwa na makombora ya masafa marefu ya Iran; Fakhri Zadeh alikuwa mkuu wa hicho chuo.

Itaendelea...
Usikae mbali.
 
Tuendelee....

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya tisa.

Mossad ilihusika na milipuko kadhaa ndani ya October 2010, ambapo wataalam 18 wa Iran waliuawa katika kituo kimoja kilichokua katika milima ya Zagros, kikiunganisha makombora aina ya Shehab.
Kwa msaada wa marifiki zake, Uingereza na Marekani, Mossad ilifanikiwa pia kuwaua wanasayansi watano waliojihusisha na nyuklia.

Urafiki huu uliimarishwa kiasi kikubwa kwa juhudi za Meir Dagan. Kuanzia siku amekuwa mkurugenzi wa Mossad, aliongeza presha kwa watu wake kujenga ushirikiano wa karibu na taasisi za nje za kijasusi.
Wasaidizi wake walimshauri kutoanika siri za Mossad kwa wageni, ila alipotezea huo ushauri."Achaneni na huo ujinga", alifoka,"na muende mkafanye nao kazi!"

Ukiacha Uingereza na Marekani, Dagan alikuwa na rafiki mwingine wa muhimu aliyeleta taarifa za thamani kubwa kutoka ndani ya Iran: Kiongozi wa upinzani Iran. Katika mkutano usiokua wa kawaida na vyombo vya habari uliofanyika nje ya Iran,Kiongozi wa baraza la upinzani la kitaifa alitaja jina la mwanasayansi kiongozi katika mradi wa Iran. Mpaka kufikia hapo, utambulisho wake ulikua umefanywa kuwa siri.

Mohsen Fakhri Zadeh, akiwa na miaka harobaini na tisa, alikuwa profesa wa Fizikia katika chuo kikuu cha Tehran. Alisemekana kuwa mtu wa ajabu na aloyeishi kwa kupoteapotea.
Upinzani uliweka hadharani taarifa nyingi kumhusu, ikiwa ni pamoja na uanachama wake kwenye jeshi la ulinzi wa mapinduzi kutokea umri wa miaka kumi na nane (18), anwani yake - mtaa wa ShahidMhallalti, Tehran, namba za paspoti ya kusafiria - 0009228 na 4229533, na hata namba yake ya simu ya nyumbani, 021 - 2448413.

Fakhri Zadeh alikuwa na taaluma iliyojikita katika mchakato wa kugeuza bomu la msingi kuwa na ujazo na uzito wa kutosha kuanzisha mnyororo wa matukio ambao unapelekea mlipuko wa nyuklia. Timu yake pia ilikuwa ikifanya kazi kupunguza ukubwa wa bomu, ili liweze kubebwa katika kichwa cha kombora la shehab.

Kufuatia ufahamu wa mambo haya, Zadeh alikataliwa kuingia Marekani na katika nchi za jumuiya ya Ulaya, na akaunti zake za benki katika nchi za magharibi zikazuiliwa.
Upinzani walieleza hatua kwa hatua matendo yake yote, wakaweka bayana majina ya wanasayansi wengine waliokua wakishirikiana naye na hata sehemu zilipo maabara zake za siri.

Huu wingi wa taarifa na namna zilivyotolewa, zinampelekea mtu yeyote kuamini kuwa, kwa mara nyingine, "taasisi fulani ya ujasusi" iliyowahi kushukiwa na mataifa ya magharibi kwa kuwa na ajenda yake peke yake ya siri, ilikusanya hizi taarifa kwa shida juu ya huyu mwanasayansi wa Iran na kuwapatia Wapinzani ndani ya Iran, ambao waliziwasilisha kwa mataifa ya magharibi.
Kumuweka 'uchi' kulikua na maana ya kumuonya kuwa anaweza kuwa "ndiye anayefuata katika mstari" wa kuuawa na kumchagiza kujificha au kuchagua suluhu bora zaidi: kukimbilia kwenye mataifa ya magharibi.

Jenerali AliReza Asgari, waziri wa ulinzi msaidizi aliyepita wa Iran, alipotea Februari 2007 akisafiri kwenda Istanbul. Alikuwa amehusika kwa undani sana kwenye mradi wa nyuklia. Majasusi wa Iran walimtafuta kila mahali, ulimwengu mzima, ila hawakuweza kumpata.

Kama miaka minne baadae, Januari 2011, waziri wa mambo ya nje wa Iran, AliAkbar Salehi, akamgeukia katibu mkuu wa umoja wa mataifa na kuituhumu Mossa kwa kumteka na kumfunga kwenye magereza ndani ya Israel. Ila kwa mujibu wa gazeti la Sunday Telegraph la London, Asgari alikuwa ameasi na kukimbilia magharibi; Mossad ilipangilia uasi huo na walihusika kumlinda akiwa Uturuki. Vyanzo vingine vilidai kua baadae alihojiwa na CIA na akawapatia taarifa muhimu sana juu ya programu ya nyuklia ya Iran.

Mwezi mmoja baada ya kupotea kwa Asgari - March 2007 - afisa mwingine wa ngazi za juu wa Iran naye alipotea. Amir Shirazi aliyetumikia katika kikosi cha "Al Quds", kikosi mahiri sana ndani ya jeshi la ulinzi wa mapinduzi, kilichojihusisha na operesheni za siri nje ya mipaka ya Iran.
Chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya Iran kililiambia gazeti la London Times kuwa, ukiacha kupotea kwa Asgari na Shirazi, afisa mwingine wa ngazi za juu pia alipotea: kamanda wa jeshi la ulinzi wa mapinduzi kwenye ghuba ya Persia, Mohammad Soltani.

Julai 2009, mwanasayansi wa nyuklia, Shahram Amiri alijiunga kwenye orodha ya wasaliti. Amiri aliyekuwa ameajiriwa Qom, alipotelea Saudi Arabia alipoenda kuhiji Mecca. Iran iliwataka wasaudia kuchunguza kilichompata Shahram. Amiri alijitokeza miezi michache baadae huko Marekani, akahojiwa vyakutosha, akapewa dolla millioni tano ($5 million), kitambulisho kipya, na makazi mapya huko Arizona.

Vyanzo vya CIA vilieleza kuwa Amiri alikuwa mtoa taarifa kwa miaka mingi kwa vyombo vya ujasusi vya magharibi na alikiwa akiwapatia taarifa 'halisi na iliyochakatwa vizuri'.
Amiri alieleza kuwa chuo cha Tecknolojia cha Malek - Ashtar, alipowahi kufundisha, kilikuwa tu kama geresha kwa kutoa elimi. Ila ukweli ni kuwa kilikuwa kituo cha utafiti wa kuunda vichwa vya kubebea mabomu yatakayorushwa na makombora ya masafa marefu ya Iran; Fakhri Zadeh alikuwa mkuu wa hicho chuo.

Itaendelea...
Usikae mbali.
Mwaga vitu kiongozi wangu mambo matamu sana haya
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya kumi.

Baada ya mwaka mmoja Marekani, Amiri alibadili mawazo na kuamua kurudi Iran. Alidai hakuweza kuhimili 'stress' za maisha hayo mapya. Katika video aliyotengenezea nyumbani kwake na kuonyeshwa kwenye intaneti, alidai alitekwa na CIA; masaa machache baadae, akatuma video nyingine na kukataa video ya kwanza, na kisha akatoa video ya tatu, na kupinga video ya pili. Kisha akawasiliana na ubalozi wa Pakistani, uliokua ukiwakilisha maslahi ya Iran nchini Marekani, na akaomba kurudishwa Iran.
Wapakistani wakamsaidia; Julai 2010, Amiri akatua Tehran.
Akatokea katika mkutano na vyombo vya habari na kuwatuhumu CIA kwa kumteka na kumtesa - kisha akapotea.
Watazamaji waliituhumu CIA kwa kushindwa, ila msemaji wa CIA alifunguka: "Tumepata taarifa muhimu na Iran imempata Amiri; sawa, nani amepata dili nzuri kuliko mwenzie?"

Ila sio kama Wairan hawakuwa na lakufanya dhidi ya Mossad. Desemba 2004, Iran iliwakamata watuhumiwa kumi (10) wa upelelezi kutoka Israel na Marekani; watatu walikuwa wakifanyakazi katika vituo vya nyuklia. Mwaka 2008, Iran ilitangaza ilitangaza kusambaratisha kikundi kingine na mashushushu wa Mossad : raia watatu wa Iran waliopewa mafunzo na Mossad kutumia vifaa vya kisasa vya mawasiliano,silaha na vilipuzi.

Novemba 2008, Iran ilimnyonga Ali Ashtari, miaka harobaini na tatu (43), ambaye alipatikana na hatia ya kuwa shushushu wa Israel. Katika mchakato wa kesi yake, alikubali kuwahi kukutana na majasusi watatu wa Mossad Ulaya. Alisema walimpatia fedha na vifaa vya kielekitroniki."Watu wa Mossad walinitaka mimi niziuzie taasisi za usalama za Iran mzigo wa kompyuta na vifaa vya kielekitroniki nilivyopewa na Mossad na kupandikiza vinasa sauti katika vifaa nitakavyowauzia", Ashtari alishuhudia.

Tarehe 28, Desemba 2010, katika uwanja wa jela ya Evin huko Tehran, maafisa wa Iran walimnyonga mpelelezi mwingine,Ali-Akbar Siadat, aliyepatikana na hatia ya kufanya kazi na Mossad na kuwapatia taarifa juu ya uwezo wa kijeshi wa Iran na programu ya makombora iliyoendeshwa na jeshi la ulinzi wa mapinduzi. Kwa miaka sita iliyopita, Siadat alikuwa akikutana na majasusi wa Israel Uturuki, Thailand, na Netherland, na alijipatia malipo ya kati ya dola elfu tatu na dola elfu saba kwa kila kikao. Maafisa wa Iran waliahidi kwamba ukamataji zaidi na unyongaji vingefuata.

Ila mwaka 2010 ulikua mwaka mbaya zaidi uliorudisha nyuma juhudi za mradi wa nyuklia wa Iran. Je, ilikua ni kwasababu ya kukosa vipuri vyenye ubora wa kiwango cha juu?
Au ni kwasababu ya vipuri feki na chuma ambazo kampuni za kimchongo za Mossad zilivyowauzia Iran?
Au kwasababu ya ajali za ndege, kuungua kwa maabara, milipuko katika vituo vya makombora na nyuklia, uasi wa maafisa wa juu, vifo vya wanasayansi waliotumainiwa, migomo na fujo katika jamii ndogondogo na vikindi - matukio yote hayo na mengine ambayo Iran (kwa usahihi na kwa makosa) waliwatuhumu watu wa Dagan?

Au ni kwasababu ya 'shambulio kubwa' la Dagan, kama ilivyoelezwa na vyombo vya habari vya Ulaya?
Katika majira ya joto mwaka 2010, maelfu ya Kompyuta zilizoendesha mradi wa nyuklia wa Iran ziliathiriwa na kirusi kibaya cha 'Stuxnet'. Hiki kilitambukiwa kama kirusi cha kisasa zaidi ulimwenguni. Stuxnet ilizishambulia kompyuta zilizoendesha vizungushi vya kasi katika kinu cha Natanz na kuleta balaa.

Utata wake haukuacha shaka kuwa lilikuwa ni zao la timu kubwa ya wataalamu na uwekezaji wa kiwango kikubwa. Moja kati ya sifa maalum za kirusi hiki ni kuwa kiliweza kuelekezwa kwenye mfumo fulani na kisiathiri mifumo mingine wakati wa utekelezaji. Uwepo wake kwenye kompyuta pia haukua rahisi kugundua. Kilipoingia kwenye mifumo ya Iran, kiliweza kubadili kasi ya vizungushi vya kasi, na kufanya mazao ya kazi yake yasiwe na maana, bila mtu yeyote kufahamu.

Waangalizi waliongelea nchi mbili ambazo zina uwezo wakufanya shambulio kama hilo la kimtandao: Marekani na Israel.
Rais Ahmadinejad alijaribu kupuuza ukubwa wa madhara ya Stuxnet na kutangaza kuwa hali ni shwari.

Ila ukweli ni kwamba, mwanzoni mwa mwaka 2011, karibu nusu ya vizungushi kasi vya Iran vilikua vimeharibiwa na havikufanya kazi. Inasemekana watu wa Dagan walifanikiwa kuchelewesha programu ya nyuklia ya Iran kwa mashambulizi kama hayo kutoka kila upande kwa miaka mingi

Itaendelea....
 
Sehemu inayofuata - sehemu ya kumi na moja itakuwa ndio ya mwisho katika sura ya pili..

Baada ya hapo tutaanza sura ya tatu...
UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD!

Baada ya Mechi ya Simba tumalizie sura ya pili.. kisha kesho ikikaa poa, mdogomdogo tutembee na sura ya tatu!
 
Sehemu inayofuata - sehemu ya kumi na moja itakuwa ndio ya mwisho katika sura ya pili..

Baada ya hapo tutaanza sura ya tatu...
UNYONGAJI NDANI YA BAGHDAD!

Baada ya Mechi ya Simba tumalizie sura ya pili.. kisha kesho ikikaa poa, mdogomdogo tutembee na sura ya tatu!
Mechi ishaisha mkuu hebu lete mambo ubongo upate dayati
 
Kesho tuendelee mkuu hadithi tamu sana hii na inafikirisha sana na kuchangamsha ubongo kabisa.
 
Back
Top Bottom