Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Misheni kubwa za taasisi ya upelelezi MOSSAD!

Tuendelee....

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya pili.

Mauaji ya wanasayansi wa nyuklia wa Iran ilikuwa sehemu moja tu katika vita kubwa. Gazeti la 'Daily Telegraph' la London liliandika kuwa, Mossad chini ya Dagan ilipandikiza mshushushu waliowapa Iran taarifa za uongo zinazofanania na kweli ila kuchukua taarifa za kweli za Iran, ilitengeneza timu za wauaji, timu za kuharibu miundombinu inayohusiana na programu za nyuklia, ilisajili kampuni za uongo zilizoiuzia Iran vifaa feki na hivyo kudhoofisha sana nguvu za Iran kwa miaka na miaka ya operesheni za siri dhidi ya programu ya silaha za nyuklia za Iran.

Reva Bhalla, mkurugenzi wa uchambuzi taasisi ya Stratfor aliwahi kunukuliwa akisema: "Kwa ushirikiano na Marekani, operesheni za siri za Israel zilijikita kwenye kumaliza rasilimali watu waliojihusisha na programu ya nyuklia na kuhujumu utaratibu mzima wa Iran kupata malighafi". Mwanamama huyu alisema, Israel iliwahi kutumia mbinu hizohizo kwa Iraq miaka ya mwanzo ya themanini (80's), wakati Mossad ilipowaua wanasayansi watatu wa nyuklia wa Iraq hivyo kukwamisha kumalizika kwa kinu cha 'atom' cha Osiraq, karibu na Baghdad.

Katika vita hii dhidi ya programu ya nyuklia ya Iran, Mossad chini ya Dagan kwa ukamilifu kabisa ilikua inachelewesha utengenezaji wa bomu la nyuklia la Iran kwa muda mrefu itakavyowezekana, na hivyo kufurusha tishio la kuifuta Israel katika uso wa dunia kama ambavyo Ahmadinejad alivyokua akitishia.

Lakini hata hivyo haya mafanikio madogo hayawezi kulipia makosa makubwa zaidi yaliyofanywa na Mossad katika historia - kushindwa kugundua na kuanika mradi wa siri wa nyuklia wa Iran toka mwanzo wake.
Kwa miaka kadhaa sasa Iran imekua ikiimarisha uwezo wake kinyuklia - Na Israel haikuwa na habari.

Iran imewekeza kiasi kikubwa cha fedha, kufundisha wanasayansi, kujenga ngome za siri, kufanya majaribio ya kisasa yaliyofanikiwa- na Israel haikujua kitu. Kutokea wakati Iran chini ya Khomeini ilipoamua kuwa taifa lenye nguvu ya nyuklia, ilitumia udanganyifu, hila na mikakati iliofanya vyombo vya ujasusi vya magharibi na Israel kwa pamoja waonekane wapumbavu.

Shah Reza Pahlavi wa Iran, alianza kujenga kinu cha nyuklia, kwa matumizi ya amani na ya kivita. Mradi wa Shah ulianza miaka ya 1970 na Israel hawakushtuka; wakati huo, Israel alikuwa rafiki wa karibu wa Iran. Mwaka 1977, jenerali Ezer Weizman, waziri wa ulinzi wa Israel, alimkaribisha jenerali Hasan Toufanian, aliyekuwa akisimamia zoezi la kugeuza jeshi la Iran kuwa la kisasa, katika wizara ya ulinzi Tel Aviv- kama marafiki, Israeli ilikua ikiwapatia Iran vifaa vya kijeshi vya kisasa.

Kutokana na agenda zilizorekodiwa za mazungumzo yao ya siri, Weizman alitoa ofa ya kuwapatia Iran mfumo wa kisasa zaidi wa kurusha makombora ardhini kwenda ardhini (Surface- to - surface missiles), wakati huohuo katibu mkuu wa wizara ya ulinzi, Dr. Pinhas Zusman, akimhamasisha Toufanian kwa kusema, mfumo wa makombora wa Israel unaweza kufanyiwa marekebisho kidogo ukabeba bomu la nyuklia.

Ila kabla hawa maafisa hawajafanyia kazi mipangilio yao, mapinduzi ya Iran yakabadili mahusiano ya Israel na Iran. Serikali ya Kiislam ya mapinduzi iliwaua wafuasi wa Shah na kubadili mahusiano na Israel. Shah aliyekuwa mgonjwa kipindi hicho alitoroka nchi yake na nchi ikawa chini ya Ayatollah Khomeini na Mullah waliokua watiifu kwake.

Itaendelea....
 
Kuna kitu sijaelewa, wadau mko kimya sanaaa...
Au story inaboa tuiache...
Au naandika sana mpaka mnashindwa kucomment...
Nichukue lipi?
 
Unavyo igawa gawa kupata muunganikano inawachukua uzito watu wengi. Sema still iko vizuri pia. Napenda story kama hizi nitazame kwenye muvi. Kama ile series iliyotoka Netflix ya mpelelezi wa mossad Ali
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya tatu.

Khomeini alisimamisha mara moja mradi wa nyuklia, aliona uko kinyume na Uislam. Ujenzi wa kinu cha nyuklia ulisimamishwa na vifaa kuharibiwa. Ila katika miaka ya themanini (80's) vita iliyomwaga damu nyingi iliibuka kati ya Iraq na Iran. Saddam Hussein alitumia sumu ya gesi dhidi ya wa-Iran. Matumizi ya silaha zisizokulalika kivita na adui mbaya zaidi iliwafa ma-ayatollah wafikirie tena sera zao. Hata kabla ya kifo cha Khomeini, mrithi wake, Ali Khamenei, alielekeza jeshi lake kutengeneza silaha mpya - za kibiolojia, za kikemia, na za nyuklia - kushindana na silaha za maangamizi ambazo Iraq ilizitumia dhidi ya Iran.

Muda kidogo, viongozi waliokua mrengo wa serikali wakasimama kwenye mimbari kupingana na katazo la silaha zilizosemekana ziko kinyume na uislam. Habari nusunusu juu ya juhudi za Iran zikaanza kusambaa katikati ya miaka ya themanini (mid 80's). Baada ya kuanguka kwa umoja wa kisovieti 1989, Ulaya ilizagaa uvumi wa majaribio ya Iran kununua bomu la nyuklia kutoka kwa maofisa wasio na ajira au wanasayansi wenye njaa kali kutoka lililokuwa jeshi la kisovieti.

Vyombo vya habari vya magharibi vilielezea kwa undani kutoweka kwa wanasayansi wa Urusi na majenerali wa jeshi kutoka kwenye nyumba zao, waliokua wameajiriwa na Iran wakati huo. Kuna wanahabari waliongeza chumvi kwenye habari wakielezea jinsi malori yaliyofungwa vizuri yakielekea mashariki kutoka Ulaya, yakipita viunzi vya mipaka kuelekea mashariki ya kati. Vyanzo kutoka Tehran, Moscow, na Beijing viliweka wazi kuwa Iran iliweka saini makubaliano na Urusi kujenga kinu cha 'atom' Bushehr, ufukwe wa ghuba ya Persia, na makubaliano mengine na China, kujenga vinu viwili vidogo.

Kwa hofu ya hatari, Marekani na Israel wakatawanya timu za mashushushu waliotukuka kote ulaya kuwinda mabomu ya kisovieti aliyouziwa Iran na wanasayansi walioajiriwa. Hawakupata chochote. Marekani ikaweka presha kubwa kwa Urusi na China kuvunja makubaliano yao na Iran. China akakubali na akavunja makubaliano na Iran. Urusi ikaamua kuendelea ila ikawa inachelewesha utekelezaji. Kinu kikachukua zaidi ya miaka ishirini (20) kujengwa na kikawekewa sheria kali za matumizi na Urusi pamoja na waangalizi wa kimataifa.

Ila Israel na Marekani walioaswa kutanua utafiti wao wakati walipokosa viashiria vya walichokua wakitafuta. Kwa pamoja viongozi wa Mossad na CIA walishindwa kutambua kwamba vinu vya Urusi na China vilikuwa danganya toto tu! Ulikuwa mtego wa senene kwa vyombo mahiri zaidi vya ujasusi duniani. Nyuma ya mgongo, Iran ilianzisha kwa nguvu kubwa mradi mkubwa sana wa kuifanya kuwa taifa lenye nguvu ya nyuklia duniani.

Mwanzoni mwa mwaka 1987, kikao cha siri kiliitiswa Dubai. Watu nane walikutana kwenye ofisi ndogo yenye vumbi: wa-Iran watatu (3), wa-Pakistani wawili (2), wawakilishi wa Ulaya watatu (3)- wawili kati yao wajerumani waliokua wakifanya kazi na Iran.
Wawakilishi wa Iran na Pakistan wakasaini makubaliano ya siri.

Itaendelea....
 
Tuendelee...

MFALME WA VIVULI

Sehemu ya pili

Dagan alikuwa na miaka ishirini na sita tu (26) ila tayari alikuwa mpiganaji aliyetukuka. Aliiplani operesheni yote peke yake: kujifanya gaidi wa Lebanoni, kusafiri na boti ya kizamani kutokea Ashdod, bandari iliyopo Israel, usiku mrefu wa kujificha,kukutana na viongozi wa kigaidi, na njia ya kutorokea baada ya mauaji. Alipangilia pia tukio la kuigiza la kukimbizwa na boti ya kijeshi ya Israel.

Dagan alikua mpiganaji wa mstuni (guerilla) aliyeiva, mbunifu asiyesita, na sio mtu aliyefungwa na kanuni za mapigano. Yitzhak Rabin aliwahi kusema:" Meir ana uwezo wa kipekee wa kubuni operesheni za kupambana na magaidi zinazofanana na sinema za kusisimua".

Danny Yatom (mkurugenzi wa Mossad kwa siku za mbele) anamkumbuka Dagan kama kijana chipukizi mwenye mwili uliojengeka na mwenye nywele za kahawia, ambaye aliomba kujiunga na kikosi kilichotukuka sana cha makomandoo cha Sayeret Matkal,na akamshangaza kila mmoja kwa uwezo wake mkubwa wa kurusha kisu. Kwa kutumia kisu chake kikubwa cha makomandoo aliweza kulenga shabaha yoyote kwa uwezo mkubwa wa kufisha.
Japo alikuwa mlengaji mzuri wa shabaha ila alishindwa mitihani ya Sayeret Matkal hivyo alilazimika kuridhia medali ya shaba ya uaskari wa mwavuli.

Mapema miaka ya sabini alipelekwa ukanda wa Gaza, ambao ulikua umetekwa na Israel mwaka 1967 katika vita ya siku sita (Six-Day war) na baada ya hapa ukawa ni kiota cha operesheni hatari za kigaidi.
Magaidi wa kipalestina walikua wakiwaua waisraeli kila siku katika ukanda wa gaza na ndani ya Israeli kwa mabomu, milipuko, bunduki; Jeshi la Israel (IDF) lilishindwa kabisa kuweka utulivu katika kambi za wakimbizi zilizojaa matukio ya hatari.
Tarehe 2/01/1971, wakati watoto wazuri wa Arroyo, Avigal aliyekua na miaka mitano na Mark aliyekua na miaka nane walipopasuliwa vipande vipande na bomu lililotupwa kwa mkono ndani ya gari yao, jenerali Ariel (Arik) Sharon aliamua kuwa imefika wakati umwagaji wa damu huo wa kikatili ufike mwisho.

Aliamua kuwaingiza kwenye shughuli marafiki zake wachache waliopigana pamoja ujanani pamoja na vijana wachache wenye vipaji vya kipekee. Dagan alikua mmoja wao, kijana mwenye uso wa mviringo, mfupi na ofisa makini aliyetembea kwa kuchechemea- alikanyaga bomu la kutegwa ardhini katika ile vita ya siku sita. Wakati akipata huduma katika hospitali ya Soroka Beer-Sheva, alizama kwenye penzi na nesi aitwaye Bina. Na alipopona wakaoana. Hiki kikosi cha Sharon hakikutambuliwa kiofisi, kilikua hakipo. Misheni yao ilikua kuteketeza vikundi vya kigaidi kwa kutumia mbinu hatari na hata zisizokubalika kimapambano.

Dagan aliweka mazoea ya kutembea ukanda wa gaza akiwa na bakora, mbwa aina ya doberman, bastola kadhaa na aina mbalimbali za bunduki. Kuna wanaosema waliwahi kumuona akiwa amejinadili kama muarabu, akitembea na punda kwa starehe katika viunga hatari ukanda wa Gaza. Tatizo lake la mguu halikuondoa nia yake katika kutekeleza operesheni za hatari. Mtazamo wake ulikua rahisi sana. Hawa ni maadui, waarabu wabaya wanaotaka kutuua, hivyo tunatakiwa kuwaua wao kwanza.

Ndani ya hichi kikosi, Dagan akatengeneza 'Rimon', kikosi cha siri cha kwanza cha makomandoo wa Israel, ambacho kilifanya operesheni katikati ya ngome za maadui kwa kujibadilishabadilisha.
Ili kutembea kwa uhuru katikati ya umati wa waarabu na kufikia shabaha walizozitaka ilibidi wafanye hivyo kwa kujibadilibadili. Walifahamika haraka kama timu ya wauaji ya Arik na uvumi ulisambaa kwamba mara kadhaa waliwakamata magaidi na kuwaua hata kama walikua hawawezi kujitetea. Wakati mwingine inasemekana, waliwapeleka magaidi kwenye viunga vya giza na kuwaambia:"una dakika mbili za kutoroka", walipojaribu, waliwapiga risasi. Wakati mwingine walimuachia gaidi kisu au bunduki, akijaribu kukamata, anauawa papo hapo.

Waandishi wa habari waliandika hivyo kila asubuhi, Dagan alitoke kwenda mashambani, akitumia mkono mmoja kukojoa na mwingine kulengea kopo la koka. Dagan alikuwa akikataa habari hizo. "Hizo ni story za kufikirika tunazoziamini," alisema, "ila baadhi ya yanayoandikwa ni uongo kabisa".
Hiki kikosi kidogo cha makomandoo kilikua kinapigana vita ngumu, vita isiyo na huruma, wakihatarisha maisha yao kila uchwao. Karibu kila siku usiku kikosi cha Dagan kilivaa kama wanawake au wavuvi na kwenda kuwatafuta magaidi wasiojulikana.

Katikati ya mwezi wa kwanza 1971, wakijifanya kama magaidi wa kiarabu, walifanikiwa kuwadanganya wanachama wa Fatah kuingia katika shambulio, na mapambano ya bunduki yalipoanza, wanachama wa Fatah wote wakauawa.
Tarehe 29 januari 1971, wakati huu wakiwa katika sare, Dagan na watu wake walisafiri katika jeep mbili mpaka maeneo ya kambi ya Jabalia ( kambi ya wakimbizi wa Palestina). Njiani waliposhana na texi na Dagan alifanikiwa kumtambua moja kati ya abiria kama gaidi mbaya zaidi Abu Nimer. Akaziamuru geep kusimama na askari wake wakaizunguka ile texi. Dagan akaisogelea texi na wakati huo Abu Nimer alitoka ndani ya tex akiwa ameshikilia bomu la mkononi na kutoa pini yake. "Bomu!" Dagan alipaza sauti, ila badala ya kujificha, alimrukia na kumkamata, akamnyang'anya bomu mkononi.
Kwa kitendo hichi alizawadiwa medali ya ujasiri. Inasemekana kwamba baada ya kulitupa bomu mbali, Dagan alimuua Abu Nimer kwa mikono yake mitupu.

Miaka mingi badae katika mahojiano ya nadra na mwanahabari Ron Leshem, Dagan alisema:"Rimon haikuwa timu ya wauaji.. haikua wildwest, ambapo kila mtu alijisikia raha kupiga risasi. Kamwe hatukuumiza wanawake na watoto.. tulishambulia wauaji katili......


Kesho mchana tuendelee.....
Medali ya ujasiri mara nyingi wanaopata huwa ni marehemu. Kwa Tanzania miongoni mwa waliowahi kupata ni askari aliyejitolea kufa mtwara wakati wa mafunzo ya kijeshi baada ya kulalia bomu ili kuokoa maisha ya watu wengine, wengine ni askari walioanguka na ndege uwanja wa taifa ambao baada ya kugundua ndege ina matatizo waliamua kuepusha maisha ya watu wengi na kuipeleka sehemu nyingine ili kuokoa mamia ya watu waliokuwepo uwanjani. Pamoja na tuzo hii serikali inatakiwa kutunza familia ya marehemu mpaka kufa na kusomesha watoto wao mpaka elimu ya chuo kikuu
 
Tuendelee....

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya nne.

Kiasi kikubwa cha fedha wakapatiwa wa-pakistani, au- kuwa sahihi zaidi- Dr. Abdul Qadeer Khan, kiongozi wa programu za silaha za nyuklia Pakistani.

Miaka michache kabla, Pakistani ilianzisha mradi wake yenyewe wa nyuklia, ili kulingana uwezo kijeshi na adui wake wa jadi, India. Dr. Khan alihitaji kwa udi na uvumba malighafi za mlipuko (fissile substance) zilitakikana kutengenezea bomu la nyuklia. Ila aliamua kutotumia 'plutonium', ambayo huvunwa kwenye vinu vya nyuklia, ila aliamua kutumia 'uranium' iliyoongezewa ubora.

Mwamba wa 'uranium' uliochimbwa unakuwa na asilimia moja (1%) ya 'uranium-235', ambayo ni muhimu sana kwa utengenezaji wa silaha za nyuklia, na asilimia 99 (99%) ya 'uranium- 238' ambayo haina matumizi.

Dr. Khan alitengeneza mbinu ya kubadili 'uranium' halisi kuwa gesi, na kuipeleka hii kwenye msururu wa vizungushi vya kasi (centrifuges), kwapamoja viitwavyo 'cascade'. Wakati hivi vizungushi vya kasi (centrifuges) vikichakata hii gesi kwa kasi ya ajabu ya wastani wa mizunguko laki moja kwa dakika (100,000 spins per minute), uranium- 235 ambayo ni nyepesi hujitenga na uranium-238 ambayo ni nzito.
Kwa kurudia hili zoezi kwa maelfu ya mizunguko, hivi vizungushi vya kasi (centrifuges) huzalisha 'uranium-235' ambayo ni uranium iliyoboreshwa (enriched uranium).Hii gesi ikirudishwa kwenye hali ya ugumu/uimara (solid) inakuwa malighafi inayohitajika kutengeneza bomu la nyuklia.

Khan alikuwa ameiba ujuzi huu wa vizungushi vya kasi (centrifuges) kutoka Eurenco, kampuni ya ulaya aliyoifanyia kazi mapema 1970, na baada ya hapo akaanza uzalishaji wake mwenyewe huko Pakistani.

Muda kidogo, Khan akageuka kua "wakala wa kifo", akiuza mbinu zake, fomula, na vizungushi vya kasi. Iran akawa mteja wake mkubwa. Libya na Korea Kaskazini wakawa wateja pia.

Iran ilinunua hivi vizungushi vya kasi kwa mawakala wengine pia na wakajifunza kutengeneza wenyewe ndani ya Iran. Shehena kubwa ya uranium, vizungushi vya kasi, vifaa vya kielektroniki, na vipuri viliingia Iran kwa meli kila mara.
Vituo vikubwa vilijengwa ili kuboresha uranium, kutunza vizungushi vya kasi, na kugeuza gesi kuwa kitu kigumu; wanasayansi wa Iran walisafiri kwenda Pakistani na wataalamu wa Pakistani walisafiri kwenda Iran- na hakuna aliyejua.

Wa-Iran walikua wajanja kutoweka 'mayai yote kwenye kikapu kimoja'. Waliutawanya mradi wa nyuklia sehemu mbalimbali ndani ya Iran; kwenye ngome za kijeshi, maabara zinazohadaa, na vituo vilivyofichwa sana pembezoni. Vingine vilitengenezwa chini ya ardhi, na kuzungukwa na mitambo ya kurusha makombora kutoka Ardhini kwenda angani (surface - to - air missiles).

Kituo kimoja kilijengwa Isfahan, na kingine kikajengwa Arak; kituo muhimu zaidi- kituo cha vizungushi vya kasi- kilijengwa huko Natanz, na kituo cha nne kilijengwa katika mji mtakatifu wa Qom. Kama ingehisiwa tu kuwa eneo la moja ya hivi vituo limefahamika, Iran ingehamishia kituo hicho sehemu nyingine, hata kwa kukwangua matabaka ya ardhi ambayo yangeweza kuwa yameathiriwa na mionzi.

Itaendelea....
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya Tano.

Kwa akili kubwa waliwapoteza maboya na kuwadanganya wakaguzi kutoka taasisi ya kimataifa ya nishati ya 'atom'. Mwenyekiti wake kutoka Misri, Dr. Mohamed El-Baradei, alionyesha kama anaamini kila tamko la uongo kutoka Iran, na akachapisha repoti zinazoibeba Iran, zilizoiwezesha Iran kuendelea na mradi wake.

Juni 1, 1988, mamlaka za Marekani ziliona kwa ukweli upana wa shughuli za Iran kwa mara ya kwanza. Muasi kutoka Pakistani alijisalimisha na kuhojiwa na wapelelezi wa FBI huko New York, akiomba hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa. Alijitambulisha kama Dr. Iftikhar Khan Chaudhry na akaweka wazi upana wa ushirikiano wa siri kati ya Iran na Pakistan.
Akamtaja (kumchomea) Dr. Khan, akaelezea vikao alivyoshiriki, na kutaja wataalam wa Pakistani waliojihusisha na mradi wa Iran.

Ushuhuda wa Chaudhry ulichunguzwa na FBI na kuonekana kuwa kweli. FBI wakashauri kuwa Chaudhry aruhusiwe kukaa Marekani kama mkimbizi wa kisiasa - chaajabu, ushuhuda wake huu wakishangaza haukufuatiliwa wala kupewa mkazo. Labda kwaajili ya uzembe tu, viongozi wa juu wa Marekani wakapotezea ushuhuda wa Chaudhry, hawakuchukua hatua na zaidi hawakuionya Israel.

Ilichukua miaka mingine minne kwa ukweli juu ya Iran kuonekana kweupe.
Mara, Agusti 2002, Muasi wa Iran, Mujahedeenel Khalq (MEK), akaweka wazi uwepo wa vituo viwili vya nyuklia huko Arak na Natanz kwenye vyombo vikubwa vya habari hapa duniani.
Miaka iliyofuatia, MEK akaendelea kutoa ushuhuda zaidi juu ya maradi wa nyuklia wa Iran, na hii ilileta wasiwasi kua huenda taarifa zake zilitoka kwenye vyanzo vya nje. CIA bado ilikuwa na mashaka na kudhania kuwa Israel na Uingereza walijaribu kuwaingiza kwenye operesheni zenye madhara mabaya. Kwa mantiki zaidi, CIA iliamini kuwa Mossad na MI6 (shirika la kijasusi la uingereza) walikua wakimlisha MEK taarifa walizokusanya, kwa kutumia wapinzani wa Iran kama chanzo cha kuaminika.

Vyanzo vya taarifa vya Israel vilionyesha kuwa, ni kweli kwamba afisa wa Mossad ndiye aliyegundua kituo cha vizungushi vya kasi cha Natanz, katikati kabisa ya jangwa.
Mwaka huohuo, 2002, chanzo cha taarifa cha siri ndani ya Iran kiliwapatia CIA kompyuta mpakato iliyojaa taarifa. Muasi huyo hakusema aliipataje hiyo kompyuta; Wamarekani hawa waliojaa mashaka wakaamini kuwa taarifa hizo ziliingizwa kwenye kompyuta kipindi cha karibuni tu; waliwatuhumu Mossad kwa kuingiza baadhi ya taarifa kutoka kwenye vyanzo vyao - na kuwapatia viongozi wa MEK ili wazitoe kwa taasisi za ujasusi za magharibi.

Ila mpaka sasa ushahidi mwingi ulikuwa ukimiminika kwenye meza za wamarekani na mataifa ya Ulaya, ambao uliwalazimu kufungua macho yao.
Tetesi juu ya Biashara ya kitajiri na hatari ya Dr. Khan ilisambaa duniani kote. Mwisho, Dr. Khan akitokwa na machozi alitokeza kwenye televisheni za Pakistani akikubali kwamba kweli aliuza ujuzi, taaluma, na vizungushi vya kasi kwa Libya, Korea kaskazini na Iran na kujipatia ukwasi wa kupindukia. Serikali ya Pakistani ikajiwahisha kumpa msamaha huyu "Daktari wa vifo", baba wa bomu lao la nyuklia.

Itaendelea....
 
Mimi ndio maana natafuta mwanamke waki yahudi au mwenye asili hiyo nimuoe.
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya sita.

Israel sasa ikawa chanzo kikuu cha taarifa za Iran. Meir Dagan na Mossad yake walipatia vyombo vya ujasusi vya marekani taarifa zinazoendana na wakati juu ya kituo cha siri kilochojengwa na Iran Qom; Inasemekana pia Israel ilihusika na uasi wa baadhi ya maafisa wa juu wa jeshi la ulinzi wa mapinduzi na mradi wa 'atom'; Mossad iliyapatia baadhi ya mataifa taarifa zinazoendana na wakati, zilizoyasaidia haya mataifa kushikilia meli zilizobeba vifaa vya nyuklia kutoka kwenye bandari zao.

Ila, upatikanaji huu wa taarifa haukuitosha Israel. Wakati hawa wanafiki- Iran ilioptishia kulifuta taifa la Israel juu ya uso wa dunia, dunia nzima ilikaa kimya bila kuchukua hatua zozote kali.
Israeli haikuwa na namna nyingine isipokuwa kuanzisha vita kubwa ya chini kwa chini dhidi ya programu ya nyuklia ya Iran. Baada ya miaka kumi na sita (16) ya uzembe wa mtangulizi wake, Dagan aliamua kuchukua hatua.

Januari 2006, ndege ilianguka katikati ya Iran. Abiria wote walifariki. Kati yao walikuwepo maafisaa wa ngazi za juu katika jeshi la ulinzi, akiwemo Ahmed Kazami, moja wa makamanda wao. Iran ilitoa tamko kuwa ajali ile ilitokana na hali mbaya ya hewa ila taasisi ya Stratfor ilidokeza kuwa majasusi wamagharibi walikua wameihujumu ile ndege.

Mwezi mmoja tu kabla, ndege ya mizigo ya kijeshi ilipata hitilafu na kuparamia majengo ya makazi ya watu kule Tehran. Abiria wote tisini na nne walikufa. Wengi pia walikuwa maafisaa wa jeshi la ulinzi la mapinduzi na wanahabari wenye ushawishi walioegemea mrengo wa serikali.

Novemba 2006, ndege nyingine ya kijeshi ilianguka mara tu baada ya kuruka kutoka Tehran na kuua wanajeshi thelathini na sita wa jeshi la ulinzi la mapinduzi. Kwenye redio ya taifa, waziri wa ulinzi wa Iran alisikika akisema,"kutokana na taarifa tulizopata kutoka kwenye vyombo vyetu vya usalama, majasusi wa Marekani, Uingereza na Israel wanahusika na ajali hizi za ndege".

Wakati huo, kimyakimya, bila kutajwa sehemu yeyote ya wazi, Dagan ndio alikuwa mpanga mikakati mkuu katika sera ya Israel dhidi ya Iran. Aliamini inaweza kufikia mahali Israel isiwe na namna nyingine isipokuwa kupigana vita kubwa ya wazi dhidi ya Iran. Ila kitendo kama hicho, alifikiri, kinapaswa kuwa chaguo la mwisho kabisa.

Hujuma zilianza Februari 2005. Vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa viliripoti mlipuko katika kituo cha nyuklia cha Dialem ambacho kilipigwa na kombora kutoka kwenye ndege isiyojulikana. Na mwezi huohuo mlipuko ulitokea karibu na kituo cha Bushehr, kwenye bomba lililokuwa likipeleka gesi katika kinu kilichotengenezwa na Urusi.


Itaendelea.....
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya sita.

Israel sasa ikawa chanzo kikuu cha taarifa za Iran. Meir Dagan na Mossad yake walipatia vyombo vya ujasusi vya marekani taarifa zinazoendana na wakati juu ya kituo cha siri kilochojengwa na Iran Qom; Inasemekana pia Israel ilihusika na uasi wa baadhi ya maafisa wa juu wa jeshi la ulinzi wa mapinduzi na mradi wa 'atom'; Mossad iliyapatia baadhi ya mataifa taarifa zinazoendana na wakati, zilizoyasaidia haya mataifa kushikilia meli zilizobeba vifaa vya nyuklia kutoka kwenye bandari zao.

Ila, upatikanaji huu wa taarifa haukuitosha Israel. Wakati hawa wanafiki- Iran ilioptishia kulifuta taifa la Israel juu ya uso wa dunia, dunia nzima ilikaa kimya bila kuchukua hatua zozote kali.
Israeli haikuwa na namna nyingine isipokuwa kuanzisha vita kubwa ya chini kwa chini dhidi ya programu ya nyuklia ya Iran. Baada ya miaka kumi na sita (16) ya uzembe wa mtangulizi wake, Dagan aliamua kuchukua hatua.

Januari 2006, ndege ilianguka katikati ya Iran. Abiria wote walifariki. Kati yao walikuwepo maafisaa wa ngazi za juu katika jeshi la ulinzi, akiwemo Ahmed Kazami, moja wa makamanda wao. Iran ilitoa tamko kuwa ajali ile ilitokana na hali mbaya ya hewa ila taasisi ya Stratfor ilidokeza kuwa majasusi wamagharibi walikua wameihujumu ile ndege.

Mwezi mmoja tu kabla, ndege ya mizigo ya kijeshi ilipata hitilafu na kuparamia majengo ya makazi ya watu kule Tehran. Abiria wote tisini na nne walikufa. Wengi pia walikuwa maafisaa wa jeshi la ulinzi la mapinduzi na wanahabari wenye ushawishi walioegemea mrengo wa serikali.

Novemba 2006, ndege nyingine ya kijeshi ilianguka mara tu baada ya kuruka kutoka Tehran na kuua wanajeshi thelathini na sita wa jeshi la ulinzi la mapinduzi. Kwenye redio ya taifa, waziri wa ulinzi wa Iran alisikika akisema,"kutokana na taarifa tulizopata kutoka kwenye vyombo vyetu vya usalama, majasusi wa Marekani, Uingereza na Israel wanahusika na ajali hizi za ndege".

Wakati huo, kimyakimya, bila kutajwa sehemu yeyote ya wazi, Dagan ndio alikuwa mpanga mikakati mkuu katika sera ya Israel dhidi ya Iran. Aliamini inaweza kufikia mahali Israel isiwe na namna nyingine isipokuwa kupigana vita kubwa ya wazi dhidi ya Iran. Ila kitendo kama hicho, alifikiri, kinapaswa kuwa chaguo la mwisho kabisa.

Hujuma zilianza Februari 2005. Vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa viliripoti mlipuko katika kituo cha nyuklia cha Dialem ambacho kilipigwa na kombora kutoka kwenye ndege isiyojulikana. Na mwezi huohuo mlipuko ulitokea karibu na kituo cha Bushehr, kwenye bomba lililokuwa likipeleka gesi katika kinu kilichotengenezwa na Urusi.


Itaendelea.....
Paul Alex ahsante kwa kuulisha chakula ubongo wangu
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya sita.

Israel sasa ikawa chanzo kikuu cha taarifa za Iran. Meir Dagan na Mossad yake walipatia vyombo vya ujasusi vya marekani taarifa zinazoendana na wakati juu ya kituo cha siri kilochojengwa na Iran Qom; Inasemekana pia Israel ilihusika na uasi wa baadhi ya maafisa wa juu wa jeshi la ulinzi wa mapinduzi na mradi wa 'atom'; Mossad iliyapatia baadhi ya mataifa taarifa zinazoendana na wakati, zilizoyasaidia haya mataifa kushikilia meli zilizobeba vifaa vya nyuklia kutoka kwenye bandari zao.

Ila, upatikanaji huu wa taarifa haukuitosha Israel. Wakati hawa wanafiki- Iran ilioptishia kulifuta taifa la Israel juu ya uso wa dunia, dunia nzima ilikaa kimya bila kuchukua hatua zozote kali.
Israeli haikuwa na namna nyingine isipokuwa kuanzisha vita kubwa ya chini kwa chini dhidi ya programu ya nyuklia ya Iran. Baada ya miaka kumi na sita (16) ya uzembe wa mtangulizi wake, Dagan aliamua kuchukua hatua.

Januari 2006, ndege ilianguka katikati ya Iran. Abiria wote walifariki. Kati yao walikuwepo maafisaa wa ngazi za juu katika jeshi la ulinzi, akiwemo Ahmed Kazami, moja wa makamanda wao. Iran ilitoa tamko kuwa ajali ile ilitokana na hali mbaya ya hewa ila taasisi ya Stratfor ilidokeza kuwa majasusi wamagharibi walikua wameihujumu ile ndege.

Mwezi mmoja tu kabla, ndege ya mizigo ya kijeshi ilipata hitilafu na kuparamia majengo ya makazi ya watu kule Tehran. Abiria wote tisini na nne walikufa. Wengi pia walikuwa maafisaa wa jeshi la ulinzi la mapinduzi na wanahabari wenye ushawishi walioegemea mrengo wa serikali.

Novemba 2006, ndege nyingine ya kijeshi ilianguka mara tu baada ya kuruka kutoka Tehran na kuua wanajeshi thelathini na sita wa jeshi la ulinzi la mapinduzi. Kwenye redio ya taifa, waziri wa ulinzi wa Iran alisikika akisema,"kutokana na taarifa tulizopata kutoka kwenye vyombo vyetu vya usalama, majasusi wa Marekani, Uingereza na Israel wanahusika na ajali hizi za ndege".

Wakati huo, kimyakimya, bila kutajwa sehemu yeyote ya wazi, Dagan ndio alikuwa mpanga mikakati mkuu katika sera ya Israel dhidi ya Iran. Aliamini inaweza kufikia mahali Israel isiwe na namna nyingine isipokuwa kupigana vita kubwa ya wazi dhidi ya Iran. Ila kitendo kama hicho, alifikiri, kinapaswa kuwa chaguo la mwisho kabisa.

Hujuma zilianza Februari 2005. Vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa viliripoti mlipuko katika kituo cha nyuklia cha Dialem ambacho kilipigwa na kombora kutoka kwenye ndege isiyojulikana. Na mwezi huohuo mlipuko ulitokea karibu na kituo cha Bushehr, kwenye bomba lililokuwa likipeleka gesi katika kinu kilichotengenezwa na Urusi.


Itaendelea.....
Kiongoz naomba unitag ukiendelea
 
Tuendelee...

MAZISHI NDANI YA TEHRAN

Sehemu ya Saba.

Kituo kingine kilochofuatiwa kushambuliwa kilikuwa kituo cha majaribio cha Parchin karibu na Tehran. Pale, wataalam wa Iran walikua wakitengeneza "lensi ya mlipuko", utaalam ambao ungebadili bomu la msingi kuwa katika kiwango cha ujazo wa kutosha kukubali mnyororo wa matendo yatakayopelekea mlipuko wa kiatomiki. Vyanzo vya taarifa vya siri ndani ya Iran vilieleza kwamba mlipuko wa Parchin uliharibu sana maabara za siri.

Aprili 2006, mtakatifu wa watakatifu - kituo cha kati cha Natanz - lilikuwapo tukio la sherehe. Kundi kubwa la wanasayansi, wataalamu mbalimbali, na kiuongozi wa mradi wa nyuklia walikusanyika chini ya ardhi, ambapo maelfu vizungushi vya kasi 'centrifuges' vikiendelea kuchakata mzigo.

Katika hali ya shangwe la sherehe, walikuja kushuhudia jaribio la kwanza la msururu wa vizungushi vya kasi - cascade. Kila mtu alisubiria kwa hamu kubwa kuona vizungushi vya kasi vikifanya kazi. Injinia mkuu akabonyeza kitufe cha kuwashia na ghafla, mlipuko mkubwa ukatikisa vyumba vya chini ya ardhi. Bomba za gesi zililipuka kwa mlipuko wa kufanya mtu awe kiziwi na msururu wote wa vizungushi vya kasi ukaharibiwa vibaya.

Kwa hasira, kiongozi wa mradi wa nyuklia akataka uchunguzi mkali ufanyike.
"Watu wasiojulikana" kumbe walitegesha vipuri vibovu kwenye mtambo.
CBS waliripoti kuwa vizungushi vya kasi viliteketezwa na vilipuzi vidogo vidogo vilivyogundishwa kwenye hivyo vizungushi vya kasi, muda mchache kabla ya jaribio. Ilisema pia kuwa majasusi wa Israel walisaidiana na majasusi wa Marekani kufanya mlipuko wa Natanz uwezekane.

Januari 2007,tena, vizungushi vya kasi viliharibiwa kwa hujuma ya utaalamu wa hali ya juu. Taasisi za kijasusi za magharibi zilianzisha kampuni mashariki ya Ulaya zilizozalisha vifaa vya kuhami (insulation materials) vilivyotumika katika bomba katikati ya vizungushi vya kasi.

Iran haikuweza kununua vifaa hivi vya kuhami kwenye soko huru kwasababu ya vikwazo walivyowekewa na Umoja wa Mataifa (UN); hivyo waligeukia kampuni za 'dili' za Ulaya Mashariki na Urusi na watu waliofukuzwa Iran, waliokua wakifanya kazo kwa siri na taasisi za kijasusi za Magharibi. Mara baada ya vifaa hivi vya kuhami kufungwa, Iran ilifahamu kuwa vilikuwa vibovu na havikufaa kwa matumizi.

Kufikia 2007, rais George W. Bush alikuwa amesaini 'oda ya rais' ya siri, akiruhusu CIA kutekeleza operesheni za kificho kuchelewesha mradi wa nyuklia wa Iran.
Mapema baade, uamuzi ulichukuliwa na baadhi ya taasisi za kijasusi na Magharibi kuhujumu upatikanaji wa vipuri, vifaa na malighafi ambazo zingetumika kwenye mradi.

Ndani ya mwezi wa nane, Dagan alikutana na msaidizi wa katibu mkuu wa Marekani kujadili mikakati dhidi ya Iran.
Ajali, hujuma, milipuko imeendelea kutokea katika vituo vyote vya nyuklia kote Iran kwa miaka saba iliyopita.

Tatizo moja la ajabu lilitokea katika mfumo wa upoozaji katika kinu cha Bushehr na kukawiza kukamilika kwake kwa miaka miwili; Mei 2008, mlipuko ulitokea katika kiwanda cha vipodozi huko Arak na kusababisha uharibifu mkubwa wa kituo cha nyuklia kilochokua jirani; mlipuko mwingine uliharibu vibaya kambi ya ulinzi huko Osfahan ambako uranium ilikua ikobadilishwa kuwa gesi.

Itaendelea....
 
Back
Top Bottom