Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,346
- 9,846
1.MFALME WA VIVULI
Sehemu ya kwanza
Wakuu naomba niwatafsirie kitabu kilichoandikwa na Michael Bar-Zohar na Nissim Mishal 'The greatest mission of the Israel secret service Mossad'.
Natafsiri kitabu hiki kama shukrani kidogo kwa makala nyingi nilizosoma hapa kwenye jamii intelligence... watu wametumia muda wao na vipaji vyao kunipa taarifa na kupanua uwezo wangu wakuona mambo hivyo sioni vibaya kama nami nikijita kuandika kidogo...
Story zinazoelezwa katika kitabu hiki ni za kweli kabisa na hata rais wa Israel - Shimon Peres alisema, 'ni mambo ambayo ulimwengu ulipaswa kuwa umeyajua kwa muda mrefu'.
Moja kwa moja nitaanza na sura ya kwanza- King of the shadows au mfalme wa vivuli kwa kiswahili...
Ilikua ni mwishoni mwa majira ya joto, mwaka 1971, mawimbi makali yakipiga katika ufukwe wa Mediterranean na mawimbi makali zaidi yakionekana kuushinda ufukwe wa Gaza. Kwa busara kabisa wavuvi wadogowadogo wa Kiarabu walikaa mbali na fukwe; hii haikuwa siku nzuri ya kushindana na bahari iliyoonyesha kuchanganyikiwa.
Walitazama kwa mshangao wakati boti moja ilipojitokeza katika mawimbi yaliyokua yakinguruma ilipotua kwanguvu katika mchanga ulioloana maji ufukweni. Wapalestina wachache, nguo zao na shungi zao zikiwa zimeloana maji, waliruka kutoka kwenye boti na kukimbilia ufukweni. Sura zao zilizokua hazijanyolewa ndevu zilionyesha uchovu wa safari ndefu baharini, ila hawakua na muda wa kupumzika, walikua wakikimbia kuokoa maisha yao.
Kutoka kwenye bahari iliyokasirika, boti ya kivita ya Israeli ilitokea, ikiwakimbiza kwa speed kali ikiwa na wanajeshi waliovalia kivita. Iliposogelea ufukwe, wale wanajeshi waliruka kwenye maji madogo na kuanza kumimina risasi kwa uelekeo wa wale wapalestina waliokua wanakimbia. Vijana kadhaa wa Gaza waliokua wakicheza kwenye ufukwe waliwakimbilia wale wapalestina na kuwaelekeza sehemu salama kwenye shamba la matunda; wanajeshi wa kiisrael wakapoteza uelekeo wa wale wapalestina ila wakaendelea kuwatafuta ufukweni.
Baadae kabisa usiku huo kijana wa kipalestina aliyebeba bunduki ya Kalashnikov aliingia kwenye shamba la matunda kuchunguza.
Akawakuta wale wapalestina wamejikusanya pamoja kwenye moja ya kona za shamba."Nyie ni akina nani, ndugu?". Aliuliza.
"Sisi ni wanachama wa chama cha ukombozi wa wapalestina- PFLP" likawa jibu."Kutoka katika kambi ya wakimbizi ya Tyre, Lebanon." "Marhaba, karibuni," yule kijana akasema. "Mnamjua Abu-Seif, kamanda wetu? Alitutuma tukutane na kamanda wenu Beth Lahia (kambi kuu ya magaidi kusini mwa ukanda wa gaza).Tuna hela na silaha, na tunataka kuunganisha oparesheni zetu.”"Nitawasaidia kwa hilo", yule kijana akasema.
Asubuhi iliyofuata, magaidi kadhaa wenye silaha wakawasindikiza wageni kwenye nyumba iliyojitenga pembezoni ndani ya kambi ya wakimbizi ya Jabalia. Wakaongozwa katika chumba kikubwa na wakakaribishwa kukaa mezani. Muda kidogo baadae, kamanda wa popular front waliyetegemea kukutana nae akaingia. Wakabadilishana salamu za upendo na ndugu zao wa Lebanoni, na wakakaa kwa kwa kuangaliana.
"Tunaweza kuanza?" Aliuliza kijana mwenye mwili uliojengeka aliyevalia ushungi mwekundu, ambaye alionekana kuwa kiongozi wa lile kundi la walebanoni.
"Kila mtu yupo?"
"Watu wote wapo!". Yule mlebanoni akanyanyua mkono wake kuangalia saa. Hii ilikua ishara waliyokubaliana kabla. Ghafla, 'wale wageni wa Kilebanoni' wakatoa bastola zao na kuanza kumimina risasi. Ndani ya dakika moja, magaidi wa Beth Lahia walikua wamekufa.
'Walebanoni' wakakimbia kutoka kwenye nyumba, wakapita katika viunga vya kambi ya Jabalia na mitaa iliyojaa watu ya Gaza na muda mfupi wakawa ndani ya ardhi ya Israel. Jioni ile, kijana aliyekua na ushungi mwekundu, kapteni Meir Dagan, kamanda wa IDF (Israel Defense Forces) na kikundi cha siri cha makomando (Rimon Commando unit), Akaripoti kwa jenerali Ariel (Arik) Sharon kuwa operesheni 'kinyonga' imefanikiwa. Viongozi wote wa Popular Front Beth Lahia, kikundi hatari cha kigaidi, wameuawa.
Itaendelea....
Sehemu ya kwanza
Wakuu naomba niwatafsirie kitabu kilichoandikwa na Michael Bar-Zohar na Nissim Mishal 'The greatest mission of the Israel secret service Mossad'.
Natafsiri kitabu hiki kama shukrani kidogo kwa makala nyingi nilizosoma hapa kwenye jamii intelligence... watu wametumia muda wao na vipaji vyao kunipa taarifa na kupanua uwezo wangu wakuona mambo hivyo sioni vibaya kama nami nikijita kuandika kidogo...
Story zinazoelezwa katika kitabu hiki ni za kweli kabisa na hata rais wa Israel - Shimon Peres alisema, 'ni mambo ambayo ulimwengu ulipaswa kuwa umeyajua kwa muda mrefu'.
Moja kwa moja nitaanza na sura ya kwanza- King of the shadows au mfalme wa vivuli kwa kiswahili...
Ilikua ni mwishoni mwa majira ya joto, mwaka 1971, mawimbi makali yakipiga katika ufukwe wa Mediterranean na mawimbi makali zaidi yakionekana kuushinda ufukwe wa Gaza. Kwa busara kabisa wavuvi wadogowadogo wa Kiarabu walikaa mbali na fukwe; hii haikuwa siku nzuri ya kushindana na bahari iliyoonyesha kuchanganyikiwa.
Walitazama kwa mshangao wakati boti moja ilipojitokeza katika mawimbi yaliyokua yakinguruma ilipotua kwanguvu katika mchanga ulioloana maji ufukweni. Wapalestina wachache, nguo zao na shungi zao zikiwa zimeloana maji, waliruka kutoka kwenye boti na kukimbilia ufukweni. Sura zao zilizokua hazijanyolewa ndevu zilionyesha uchovu wa safari ndefu baharini, ila hawakua na muda wa kupumzika, walikua wakikimbia kuokoa maisha yao.
Kutoka kwenye bahari iliyokasirika, boti ya kivita ya Israeli ilitokea, ikiwakimbiza kwa speed kali ikiwa na wanajeshi waliovalia kivita. Iliposogelea ufukwe, wale wanajeshi waliruka kwenye maji madogo na kuanza kumimina risasi kwa uelekeo wa wale wapalestina waliokua wanakimbia. Vijana kadhaa wa Gaza waliokua wakicheza kwenye ufukwe waliwakimbilia wale wapalestina na kuwaelekeza sehemu salama kwenye shamba la matunda; wanajeshi wa kiisrael wakapoteza uelekeo wa wale wapalestina ila wakaendelea kuwatafuta ufukweni.
Baadae kabisa usiku huo kijana wa kipalestina aliyebeba bunduki ya Kalashnikov aliingia kwenye shamba la matunda kuchunguza.
Akawakuta wale wapalestina wamejikusanya pamoja kwenye moja ya kona za shamba."Nyie ni akina nani, ndugu?". Aliuliza.
"Sisi ni wanachama wa chama cha ukombozi wa wapalestina- PFLP" likawa jibu."Kutoka katika kambi ya wakimbizi ya Tyre, Lebanon." "Marhaba, karibuni," yule kijana akasema. "Mnamjua Abu-Seif, kamanda wetu? Alitutuma tukutane na kamanda wenu Beth Lahia (kambi kuu ya magaidi kusini mwa ukanda wa gaza).Tuna hela na silaha, na tunataka kuunganisha oparesheni zetu.”"Nitawasaidia kwa hilo", yule kijana akasema.
Asubuhi iliyofuata, magaidi kadhaa wenye silaha wakawasindikiza wageni kwenye nyumba iliyojitenga pembezoni ndani ya kambi ya wakimbizi ya Jabalia. Wakaongozwa katika chumba kikubwa na wakakaribishwa kukaa mezani. Muda kidogo baadae, kamanda wa popular front waliyetegemea kukutana nae akaingia. Wakabadilishana salamu za upendo na ndugu zao wa Lebanoni, na wakakaa kwa kwa kuangaliana.
"Tunaweza kuanza?" Aliuliza kijana mwenye mwili uliojengeka aliyevalia ushungi mwekundu, ambaye alionekana kuwa kiongozi wa lile kundi la walebanoni.
"Kila mtu yupo?"
"Watu wote wapo!". Yule mlebanoni akanyanyua mkono wake kuangalia saa. Hii ilikua ishara waliyokubaliana kabla. Ghafla, 'wale wageni wa Kilebanoni' wakatoa bastola zao na kuanza kumimina risasi. Ndani ya dakika moja, magaidi wa Beth Lahia walikua wamekufa.
'Walebanoni' wakakimbia kutoka kwenye nyumba, wakapita katika viunga vya kambi ya Jabalia na mitaa iliyojaa watu ya Gaza na muda mfupi wakawa ndani ya ardhi ya Israel. Jioni ile, kijana aliyekua na ushungi mwekundu, kapteni Meir Dagan, kamanda wa IDF (Israel Defense Forces) na kikundi cha siri cha makomando (Rimon Commando unit), Akaripoti kwa jenerali Ariel (Arik) Sharon kuwa operesheni 'kinyonga' imefanikiwa. Viongozi wote wa Popular Front Beth Lahia, kikundi hatari cha kigaidi, wameuawa.
Itaendelea....