hahahahahaha
snowhite kwani mie nina tatizo na kushare cost? Sina tatizo hata, ila Mume asisahau nafasi yake kama kiongozi....
In reality hata mume akianguka kama mkewe na namshika mkono, aibu yake aibu yangu, anguko lake anguko langu .....
Ninachopinga ni kupitiliza, kuna wanaume wengine hajui hata msosi unatoka wapi sasa uanaume uko wapi?
Wengine hata uniform za watoto hawajui ukihoji atakwambia cost sharing, hizo sharing ni kwa mke tu mbona nyumba ndogo wanatapanya?
Nikupe mfano hai kuna mtu walikuwa na joint akaunti na mumewe, mke hakuwahi kuzoa hela kwenye ile akaunti..mwanzoni woze walikuwy wanacontribute wanaweka hela (akaunti ilikuwa mahususi kwa emergency, shurti hakuna kutoa kati yao) ikaanza taratibu mume akaacha kupeleka pesa..... Mke kuuliza mume haeleweki, kumbuka hapo hawajengi wala hawajanunua kitu, mke akaendelea kuweka (bahati ana kipato kizuri) siku ya a siku mke kuuliza balance almanusra amneep israeli hela ilivyokombwa (akaunti ilikuwa any one to sign, hivyo mume au mke aliweza kuchukua bila uhitaji wa mwenzie) kupeleleza mume ana nyumba ndogo kainunulia gari na kiwanja, kwa hela ya mkewe..... mke akaamua kukomba hela zote akaingiza kwenye akaunti yake kimya kimya.....
Sasa kwa hali kama hii mke atataka kuchangia?
Uswazi huku mara ngapi tunaona mume kahangaika na mkewe maisha yakiwa mazuri anamfukuza mke na wanae?
Wanaume wangapi mke anashindia ugali na mchiche yeye anahonga na kuzoa ofa?
Wnawake wameshtuka banaaaa
kabla ya cost sharing inabidi utagakari kwa tabia za mume wangu hatokuja kuniumiza? Akiona utakuja muumiza hela yake hushiki ng'ooooooooooooooooooooooooo