Mishahara ya madaktari wetu; wanastahili nini?

Mimi nasema hivi, uwezo wa kuwalipa madaktari, walimu, manesi, polisi, wanajeshi, magereza, mabwana kilimo nk kwa kiwango cha kuridhisha kiko ndani ya uwezo wa serikali.
Naomba wachumi wadiscuss zaidi namna ya kuimplement hili ongezeko la mishahara ambalo naamini ni muhimu sana.


Moelex.. wakati Kikwete anazungumza mwaka jana kuhusu hali mbaya ya uchumi Chama chake walikuwa wanafikiria kuongeza mishahara na marupurupu ya wabunge; katika hali mbaya ya uchumi hawakufikiria kupunguza matumizi kwa kukata mishahara. Hapa US kuna majimbo ambayo kutokana na hali ngumu ikabidi ipunguze matumizi.

Mapendekezo unayoyatoa yakitekelezwa guess what will happen.. waliojuu nao watataka waongezewe kureflect jambo hilo matokeo yake yanakuwa yale yale.. waliojuu hawataki kufikiwa na walio chini..
 
explain to me kwanini mtu wa NGO naye anakuwa miongoni mwa wanaolipwa kwa juu; kwa sababu kuna watu kadhaa wameniomba sana tuanze NGO... hasa ya kusaidia watoto Yatima na niwasaidie kuandika project... si kwa sababu wanataka kusaidia Yatima lakini njia rahisi ya kupata misaada toka nje itakayowasaidia wao na familia zao. Kwa maneno mengine yatima wanakuwa ni kama chambo cha utajiri.

.......Inategemea hiyo NGO imekuwa sponsorship na watu wa aina gani, maana kwenye NGO mtu unalipwa mfumo wa pesa wa yule sponsor wako..........NGO nyingi zinalipa kwa mfumo wa $.
........Hao wanaotumia yatima kama chambo cha utajiri wanakosea, ndio hao utakuta baada ya muda NGO zinakufa.
 
Kwa sababu kila kitu sisi tunalaumu serikali tu. Kwani serikali inapanga hata mishahara ya sekta binafsi?

Kwa nini madaktari wengi wasianzishe practice zao wenyewe....kwa nini makanisa yasianzishe hospitali zao yenyewe. Mimi majuu sijawahi kwenda hospitali ya serikali. Kwanza sijui hata kama kuna hospitali za serikali....
Omega,
Kitu unasahau ni kwamba unahitaji capital kuanzisha practice yako mwenyewe. Hiyo inaweza kufanywa na daktari ambaye amefanya kazi miaka mingi kajiwekea pembeni hela kidogo na ana uwezo wa kufungua ka ofisi na kununua mitambo ya blood presha. Sasa daktari anayemaliza shule aende wapi? Serikali bado inao wajibu.
 
Omega,
Kitu unasahau ni kwamba unahitaji capital kuanzisha practice yako mwenyewe. Hiyo inaweza kufanywa na daktari ambaye amefanya kazi miaka mingi kajiwekea pembeni hela kidogo na ana uwezo wa kufungua ka ofisi na kununua mitambo ya blood presha. Sasa daktari anayemaliza shule aende wapi? Serikali bado inao wajibu.

Daktari anayemaliza shule aombe mkopo benki. Mkopo huo ndio mtaji.
 
halafu anaweka nini rehani ili apate mkopo?

Cheti chake halisi cha kuhitimu taaluma ya udaktari...

Au leseni yake ya uganga (hivi bongo madaktari wanahitaji leseni?) iwe tied kwa namna moja au nyingine kwenye huo mkopo...

We've got to be creative, you know...
 
Cheti chake halisi cha kuhitimu taaluma ya udaktari...

Au leseni yake ya uganga (hivi bongo madaktari wanahitaji leseni?) iwe tied kwa namna moja au nyingine kwenye huo mkopo...

We've got to be creative, you know...
Yes, we have to be creative but we also have to hold our government responsible to meet its obligations. That is all I am asking for. Daktari aliyesomeshwa kwa mkopo hata kabla hajaulipa mkopo huo aende benki kukopa tena ili aanzishe private practice? Does it really make sense?
 
Yes, we have to be creative but we also have to hold our government responsible to meet its obligations. That is all I am asking for. Daktari aliyesomeshwa kwa mkopo hata kabla hajaulipa mkopo huo aende benki kukopa tena ili aanzishe private practice? Does it really make sense?

Mbona wa majuu wanaweza bana ingawa siyo wote. I mean, madaktari watatu wanaweza waka partner na kuanzisha ki practise chao na baadaye kikashamiri.

Terms na conditions za mikopo kama hiyo zinaweza kuwa tofauti na mikopo mingine. Kwa nini isiwezekane? I say, yes it can.
 
Omega.. kwenye kampuni yenu hapo kijijini mnapata mikopo ya kujengea toka kwenye kampuni yenu?
 
Nimevutiwa na jinsi wengi wanavyojaribu kutetea maslahi ya madaktari. Hivi ndugu zetu 'mnaoishi' au hata wale 'wanaobeba maboksi' huko ughaibuni, mtuambie gharama ya matibabu ikoje huko? Na je, na huku nyumbani gharama ikiwekwa katika ulinganifu kama huko ughaibuni ni watz wangapi watamudu gharama ya afya? Nadhani wanacholipwa ukilinganisha na kada zingine ni angalau japo si sana!

gharama za matibabu (UK) ni bure kama TZ kwa kila resident(raia na hata international students sio VISITORS) kuna NHS-NATIONAL HEALTH SERVICE,private sijawahi kwenda ila nasikia ni expensive sana.US nasikia mpaka uwe na health insurance(sijui system inafanyaje labda wa huko watueleze vizuri)
 
Mbona wa majuu wanaweza bana ingawa siyo wote. I mean, madaktari watatu wanaweza waka partner na kuanzisha ki practise chao na baadaye kikashamiri.

Terms na conditions za mikopo kama hiyo zinaweza kuwa tofauti na mikopo mingine. Kwa nini isiwezekane? I say, yes it can.
Wamajuu wanaweza kwa sababu tayari kuna institutions zilizokwishajengwa
kuwezesha mazingira kama hayo. Kwa Tanzania hiyo ni pipe dream. Hata hao watatu wakipartner bado wanahitaji fedha za mtaji. Mitambo ya x-ray, sujui ma-scanners, na madudu kibao ya upimaji. You are talking of millions of dollars just setting up. At the same time tuna hospitali nyingi tu ambazo hazina madaktari wa kutosha. That is where the government comes in. Usiiangalie Tanzania kwa macho ya majuu. Iangalie Tanzania kuanzia ngazi ya vijijini ambako hata kuchota maji tu ni ordeal.
 
MM Nashukuru sana kwa kuleta hii hoja kwenye uwanja wa majadiliano. Mimi ni daktari na kutokana na huo mshaara ushuzi ulioonyeshwa hapo juu nimejiamulia kubwaga manyanga nafanya vitu vingine kabisa. kwa nini nipate dhambi za bure? Kama unashindwa kutimiza wajibu wako hiyo ni dhambi na mimi sikuwa tayari kufanya hivyo.

Kuna neno uzalendo limeimbwa hapo juu but sijui huyo mdau anaanisha uzalendo gani? Kama keki ya taifa ni yetu tugawane wote. Wewe huwezi kusema mbunge wa darasa la nne posho kwa siku laki moja kwa vile maisha magumu halafu daktari unampa laki sita na nusu kwa siku 30! Jamani tumuogope Mungu. Hana vikao, hana posho, hana mafuta hata gloves za kupiga PR na PV hamna pia, mazingira ya kazi magumu, vitendea kazi hamna yeye ni nani haswa hadi akae hapo...

Hawa viongozi wetu wataendelea kufa vifo vya mende. Wanaweza kwenda India kwa Check up na elective procedures lakini akipata heart attack au emergency nyingine hawezi fika hata airport kutoka Kimara achilia mbali India! Kama hakutakuwa na mwamko wa kuimarisha huduma za afya hali itaendelea kuwa mbaya. Wadanganyika nawasikitikia sana.

Kinachotokea sasa kutokana na utandawazi na fursa mbali mbali vijana madaktari wazuri wanaacha kutibu na kufanya mambo mengine yenye kipato. Mnachotakiwa kujua ni kuwa madaktari wengi ni watu wernye akili kuliko watu wa kawaida na akijitune kidogo tu anafanya kazi nyingine vizuri sana kwa hiyo wanaondoka kimya kimya.

Hesabu zinaonyesha kuna kama madaktari 2400 Tanzania lakini wanaotibu najua hawafiki 800. Wapo hapo hapo mjini wanapambana na MKUKUBI wao(Mkakati wa Kupambana na Umaskini Binafsi).

Sintosahau mwaka 2005 wakati tukiwa na mgomo kutaka mshahara uongezwe kutoka laki na nusu(150,000) kwenda milioni moja (1,000,000) Usicheke ukweli ndo huo nilikutana na afisa mwajiri wa Wizara ya afya jina lake nalihifadhi, Tukawa tunamwambia kama Wizara haiongezi hela tunaacha kutibu na kumwambia kuwa tupo adimu, akasema kuwa Nani kakwambia hata mkiondoka Watanzania watatibiwa kwa dharau ya hali ya juu. Niliinua macho juu nikamwambia Mungu niepushe na hawa vihiyo, nikaangalia mbele na sijarudi tena kudai milioni moja baada ya kusoma kwa jumla ya miaka 20! Give me a break.

Tatizo kubwa Tanzania kila mtu anayevaa koti jeupe anaitwa daktari. Hata akiwa mchinja nyama. Mtu akienda hospitali kuanzia karani, mfagiaji, nurse assistance, binzari wote wanaitwa madaktari. Serikali imetumia huu mwaya kuwakanya madaktari sana lakini kwa anayejua kitu ambacho Daktari anachoweza kufanya in relation to Medical Assistant, AMO na kada nyingine anajua namaanisha nini.

Nisijekuwachosha kusoma ila kwa mwendo huu wa serikali yetu kwa kuwa na double standards kwa wafanyakazi wake sioni mwanga. Nilishang'atuka kazi kwenu mliopo kwenye fani. Njaa na maendeleo havipikiki kwenye chungu kimoja.

Naomba kuwakilisha
 
MM Nashukuru sana kwa kuleta hii hoja kwenye uwanja wa majadiliano. Mimi ni daktari na kutokana na huo mshaara ushuzi ulioonyeshwa hapo juu nimejiamulia kubwaga manyanga nafanya vitu vingine kabisa. kwa nini nipate dhambi za bure? Kama unashindwa kutimiza wajibu wako hiyo ni dhambi na mimi sikuwa tayari kufanya hivyo.

Kuna neno uzalendo limeimbwa hapo juu but sijui huyo mdau anaanisha uzalendo gani? Kama keki ya taifa ni yetu tugawane wote. Wewe huwezi kusema mbunge wa darasa la nne posho kwa siku laki moja kwa vile maisha magumu halafu daktari unampa laki sita na nusu kwa siku 30! Jamani tumuogope Mungu. Hana vikao, hana posho, hana mafuta hata gloves za kupiga PR na PV hamna pia, mazingira ya kazi magumu, vitendea kazi hamna yeye ni nani haswa hadi akae hapo...

Hawa viongozi wetu wataendelea kufa vifo vya mende. Wanaweza kwenda India kwa Check up na elective procedures lakini akipata heart attack au emergency nyingine hawezi fika hata airport kutoka Kimara achilia mbali India! Kama hakutakuwa na mwamko wa kuimarisha huduma za afya hali itaendelea kuwa mbaya. Wadanganyika nawasikitikia sana.

Kinachotokea sasa kutokana na utandawazi na fursa mbali mbali vijana madaktari wazuri wanaacha kutibu na kufanya mambo mengine yenye kipato. Mnachotakiwa kujua ni kuwa madaktari wengi ni watu wernye akili kuliko watu wa kawaida na akijitune kidogo tu anafanya kazi nyingine vizuri sana kwa hiyo wanaondoka kimya kimya.

Hesabu zinaonyesha kuna kama madaktari 2400 Tanzania lakini wanaotibu najua hawafiki 800. Wapo hapo hapo mjini wanapambana na MKUKUBI wao(Mkakati wa Kupambana na Umaskini Binafsi).

Sintosahau mwaka 2005 wakati tukiwa na mgomo kutaka mshahara uongezwe kutoka laki na nusu(150,000) kwenda milioni moja (1,000,000) Usicheke ukweli ndo huo nilikutana na afisa mwajiri wa Wizara ya afya jina lake nalihifadhi, Tukawa tunamwambia kama Wizara haiongezi hela tunaacha kutibu na kumwambia kuwa tupo adimu, akasema kuwa Nani kakwambia hata mkiondoka Watanzania watatibiwa kwa dharau ya hali ya juu. Niliinua macho juu nikamwambia Mungu niepushe na hawa vihiyo, nikaangalia mbele na sijarudi tena kudai milioni moja baada ya kusoma kwa jumla ya miaka 20! Give me a break.

Tatizo kubwa Tanzania kila mtu anayevaa koti jeupe anaitwa daktari. Hata akiwa mchinja nyama. Mtu akienda hospitali kuanzia karani, mfagiaji, nurse assistance, binzari wote wanaitwa madaktari. Serikali imetumia huu mwaya kuwakanya madaktari sana lakini kwa anayejua kitu ambacho Daktari anachoweza kufanya in relation to Medical Assistant, AMO na kada nyingine anajua namaanisha nini.

Nisijekuwachosha kusoma ila kwa mwendo huu wa serikali yetu kwa kuwa na double standards kwa wafanyakazi wake sioni mwanga. Nilishang'atuka kazi kwenu mliopo kwenye fani. Njaa na maendeleo havipikiki kwenye chungu kimoja.

Naomba kuwakilisha
Dokta,
' That is what I am talking about. Ningekuwa na uwezo huo ningekuwekea senkyuu mbili.
 
Back
Top Bottom