Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
- Thread starter
- #41
Mimi nasema hivi, uwezo wa kuwalipa madaktari, walimu, manesi, polisi, wanajeshi, magereza, mabwana kilimo nk kwa kiwango cha kuridhisha kiko ndani ya uwezo wa serikali.
Naomba wachumi wadiscuss zaidi namna ya kuimplement hili ongezeko la mishahara ambalo naamini ni muhimu sana.
Moelex.. wakati Kikwete anazungumza mwaka jana kuhusu hali mbaya ya uchumi Chama chake walikuwa wanafikiria kuongeza mishahara na marupurupu ya wabunge; katika hali mbaya ya uchumi hawakufikiria kupunguza matumizi kwa kukata mishahara. Hapa US kuna majimbo ambayo kutokana na hali ngumu ikabidi ipunguze matumizi.
Mapendekezo unayoyatoa yakitekelezwa guess what will happen.. waliojuu nao watataka waongezewe kureflect jambo hilo matokeo yake yanakuwa yale yale.. waliojuu hawataki kufikiwa na walio chini..