Mishahara ya madaktari wetu; wanastahili nini?

Mishahara ya madaktari wetu; wanastahili nini?

Hizi takwimu umezipika ama mmbebabox ?

Hakuna ukweli eti bila aibu

Fanya tafiti kabla ya kuweka yasiyo na ukweli

hiyo ni sawa kabisa kwa UK mzee hebu soma habari hii

"..........If you compare a police constable on overtime, I think you will find that an individual serviceman gets quite a lot less."

A soldier's starting salary is £12,572 a year, rising to £15,677 as a Level 1 private. A traffic warden's basic pay is £17,000........''


source http://www.thesun.co.uk/sol/homepage/news/campaigns/our_boys/1247731/General-says-British-soldiers-are-underpaid.html
 
Je mwajua mshahara wa daktari akimaliza internship? Ni shs 650,000/- kwa mwezi sasa fanya hesabu zile bil 1.5 zilizotumika kujenga nyumba ya gavana zingeweza kuwaongezea mara mbili madaktari wetu 2,308 mshahara wao na kuwa 1,300,000/- na hata kwa kiwango hicho bado hakijafika nusu ya mshahara anaolipwa daktari Rwanda US$ 2400.......Hadithi ni hiyo hiyo kwa wahandisi, walimu n.k
Na wala serikali haina haja ya kupandisha kodi kuongeza mapato NI FAIR distribution...punguza posho na mishahara ya mawaziri, wabunge, makatibu wakuu, wakurugenzi.......tutaweza lipana mishahara sawia!

Naunga mkono hoja.
 
Hizi takwimu umezipika ama mmbebabox ?

Hakuna ukweli eti bila aibu

Fanya tafiti kabla ya kuweka yasiyo na ukweli


masanilo,nimefanya tafiti,nimeweka average ya hao wafanyakazi(polisi,walimu,nurses)after tax....before tax polisi ni around £23000+., nurses £19,000+ based on estimation after tax hawapati hio figure unayaiona,kuna source nyingi kama wewe ulivyotumia the sun,
source nyingi wanatumia estimation zao,cha muhimu umeona si tanzania tu hata nje kuna tofauti kati ya mwalimu,polisi,daktari na governor wana tofauti kubwa katika mishahara yao
 
I just love ma profession..that's Y bado nakomaa na hii medicine...nina enjoy ninapopata new findings in my study....the most pleasing ni pale unaitwa kwenye emergency room kumhudumia mtu ambae ni unconscious then kwa uwezo wa Mungu unasababisha anatembea mwenyewe kurudi home..tena bila kuhitaji ahsante yake.
But bcoz that's is my life...it shud support my living ili harmony ipatikane.Napenda sana nirudi nyumbani nikasaidie ndugu zangu Watz,napenda hali ya hewa,napenda social network ya Kitz....I just love my big family n love Tanzania,sasa hii mambo ya mishahara inatavunja mori jamani,ndio maana tunaamua tuoe na kupotolea hukuhuku ingawa to be honest sikupendi pamoja na maendeleo yake na kila kitu.ila ndio hivyo tena,wanakujali,wanakuheshimu,wanakulipa vizuri..kwa hiyo hamna jinsi.
Ila nilichojifunza ni kwamba,taasisi kubwa kama muhimbili/kcmc/bugando ingeweza kubuni namna ya kupata capital(hata kama kwa kuongeza tshs 100/huduma,kukopa benki) ya kuweza kuanzisha miradi mbadala ili kuweza ku accommadate wataalam wake,na ingeweza kuwa ni stimulant kwa serikali.....tatizo letu sisi tunakula ile miradi/capital badala ya ku invest them ili kula matunda yake.
 
Mpaka leo sijaona sababu kwa nini mbunge alipwe mshahara zaidi ya daktari. Daktari should be making more than wabunge, jamani.
 
mshahara wa daktari intern ni 450,000,na kwa anayeanza kazi kama registrar mshahara una anza na TGS G,ambayo ni kama 550,000,bila makato.kodi ambayo daktari wa tGs G analipwa mshahra wa 720,000, na baada ya makato ya kodi inakuja kwenye 580,000 net.yaani kodi tunayolipa ni kubwa zaidi ya mfanya biashara kila mwaka.na ile tume ambayo ilundwa na mh mkapa ilpendekeza serikali ina uwezo wa kumlipa daktari 1.2 milion bila wasi wasi wowote.sijui hizi commision ambazo ziliundwa zilikuwa za ku peana hela tu,kwa sababu hakuna pendekezo lililofanyiwa kazi.kwa kweli daktari ana hali ngumu,kila kukicha the life is in danger due to serious infections encountered everyday esp in government hospitals.god bless tz doctors.otherwise they will all one day leave this country for greener pastures.


Mara mbili? Tuulize sisi tuko wapi. Kuna wakati nikiwa bado nyumbani ubalozi wa Rwanda ulikuja katika hospitali niliyofanyia kazi (ni hospitali ya rufaa nje iliyoko mkoani) kwa ajili ya ku recruit madaktari. Naweza kusema wameweza kushawishi watu na madaktari wanaenda Rwanda sasa kwa wingi, imekuwa kama Botswana/Namibia (madaktari wao wengi ni watanzania)
 
Tatizo ni kwamba Tanzania hatuna scales, natural or artificial, zilizo equitable au reasonable. Hatuna scales, hatuna uchumi rasmi unaoeleweka, hatuna bajeti, hatuna watchdogs, hatuna pressure groups, hatuna civil society, hatuna wa kusema mbunge na gavana si muhimu zaidi ya daktari (zaidi ya sauti chache za hapa na magazeti machache sana).

Hatuna, hatuna hata sensa ya kujua tuna wafanyakazi wangapi wa serikali na wangapi ni madaktari, walimu etc.

Hatuna.

Nikaogopa kwamba tusije kukosa hata mtu wa kusema hatuna, nikasema hatuna.
 
Kwani mishahara ya madaktari kwenye hospitali na kliniki binafsi ni kiasi gani? Maana hapa tunazungumzia wanao fanya kazi kwenye hospitali za serikali....
 
Tatizo ni kwamba Tanzania hatuna scales, natural or artificial, zilizo equitable au reasonable. Hatuna scales, hatuna uchumi rasmi unaoeleweka, hatuna bajeti, hatuna watchdogs, hatuna pressure groups, hatuna civil society, hatuna wa kusema mbunge na gavana si muhimu zaidi ya daktari (zaidi ya sauti chache za hapa na magazeti machache sana).

Hatuna, hatuna hata sensa ya kujua tuna wafanyakazi wangapi wa serikali na wangapi ni madaktari, walimu etc.

Hatuna.

Nikaogopa kwamba tusije kukosa hata mtu wa kusema hatuna, nikasema hatuna.

Kiranga kuna hotuba moja ambayo Nyerere aliitoa in 1970s ambapo alilazimisha kupunguzwa mishahara ya watumishi wote wa serikali. Hotuba ile imepigwa marufuku (in effect) na kizazi cha Watanzania wengi hawajawahi kusikia kuwa imewahi kutolewa!
 
Yaleyale tu mkuu km kuna tofauti basi elfu 50.....

Kwa sababu kila kitu sisi tunalaumu serikali tu. Kwani serikali inapanga hata mishahara ya sekta binafsi?

Kwa nini madaktari wengi wasianzishe practice zao wenyewe....kwa nini makanisa yasianzishe hospitali zao yenyewe. Mimi majuu sijawahi kwenda hospitali ya serikali. Kwanza sijui hata kama kuna hospitali za serikali....
 
Kiranga kuna hotuba moja ambayo Nyerere aliitoa in 1970s ambapo alilazimisha kupunguzwa mishahara ya watumishi wote wa serikali. Hotuba ile imepigwa marufuku (in effect) na kizazi cha Watanzania wengi hawajawahi kusikia kuwa imewahi kutolewa!

atakayeipost hiyo hotuba humu atakuwa amefanya jambo la maana sana..
 
Kwa sababu kila kitu sisi tunalaumu serikali tu. Kwani serikali inapanga hata mishahara ya sekta binafsi?

Yes sir! Inapanga kima cha chini hadi cha mfanyakazi wako wa nyumbani! Just like in the US.. the federal govt inapanga kima cha chini ya kitaifa, na majimbo yana uhuru wa kupanga kima chao cha chini as long as hakiwi chini ya kile cha kitaifa.

Kwa nini madaktari wengi wasianzishe practice zao wenyewe....kwa nini makanisa yasianzishe hospitali zao yenyewe. Mimi majuu sijawahi kwenda hospitali ya serikali. Kwanza sijui hata kama kuna hospitali za serikali....


madaktari wanafanya hivyo na matokeo yake ni kuwa wana charge kiasi kikubwa sana kiasi kwamba wanaoweza kwenda na kupata huduma nzuri ya kiasi hicho ni aidha wale wanaopelekwa na maofisi yao, maafisa wa serikali, au watu ambao tayari wameshakusanya njuluku ya kutosha. Mtu wa kawaida bado anategemea hospitali ya serikali.
 
........Mishahara ni maumivu hapa bongo kwa wafanyakazi wa public sector, wanaofaidi ni wakubwa wa nchi na watu wanaofanya kazi kwenye NGO na private sector.
Inasikitisha nchini kwetu eti kima cha chini cha mshahara ni laki moja, hii kweli itamfikisha wapi mtu mwenye family!!
 
Nimevutiwa na jinsi wengi wanavyojaribu kutetea maslahi ya madaktari. Hivi ndugu zetu 'mnaoishi' au hata wale 'wanaobeba maboksi' huko ughaibuni, mtuambie gharama ya matibabu ikoje huko? Na je, na huku nyumbani gharama ikiwekwa katika ulinganifu kama huko ughaibuni ni watz wangapi watamudu gharama ya afya? Nadhani wanacholipwa ukilinganisha na kada zingine ni angalau japo si sana!
 
Yes sir! Inapanga kima cha chini hadi cha mfanyakazi wako wa nyumbani! Just like in the US.. the federal govt inapanga kima cha chini ya kitaifa, na majimbo yana uhuru wa kupanga kima chao cha chini as long as hakiwi chini ya kile cha kitaifa.

Mbona wakati nafanya kazi kama waiter pale Applebees malipo kwa saa yalikuwa chini ya kima cha chini? Hela ya maana nilikuwa napata kwenye bakshishi (tip - sina hakika na tafsiri). Au watu wa migahawa sheria ya kima cha chini haiwahusu?
 
Mimi nasema hivi, uwezo wa kuwalipa madaktari, walimu, manesi, polisi, wanajeshi, magereza, mabwana kilimo nk kwa kiwango cha kuridhisha kiko ndani ya uwezo wa serikali.

Nasuggest kwa kuanzia, Tudouble mishahara ya hao wanataaluma hapo juu kuanzia July 1, 2010 na KUONDOA KODI ZOTE KWENYE MISHAHARA YA WAFANYAKAZI WOTE up to Tshs 750,000 kwa mwezi, kiasi kinachozidi >> 750,000 ndio kodi ikatwe at a standard rate of say 40%.

Swali litakuja, serikali itatoa wapi pesa. Jibu ni kuondoa misamaha ya kodi wanayopata wafanyabiashara to the tune of hundreds of billions of Tshs per year.

Mishahara hii itasaidia sana kukuza uchumi sababu almost kiasi chote kitatumika nchini kama matumizi ya hao wafanyakazi, tofauti na sasa hivi ambazo hizo billions wafanyabiashara wanazipark huko kwenye foreign accounts.

Naomba wachumi wadiscuss zaidi namna ya kuimplement hili ongezeko la mishahara ambalo naamini ni muhimu sana.
 
........Mishahara ni maumivu hapa bongo kwa wafanyakazi wa public sector, wanaofaidi ni wakubwa wa nchi na watu wanaofanya kazi kwenye NGO na private sector.
Inasikitisha nchini kwetu eti kima cha chini cha mshahara ni laki moja, hii kweli itamfikisha wapi mtu mwenye family!!

explain to me kwanini mtu wa NGO naye anakuwa miongoni mwa wanaolipwa kwa juu; kwa sababu kuna watu kadhaa wameniomba sana tuanze NGO... hasa ya kusaidia watoto Yatima na niwasaidie kuandika project... si kwa sababu wanataka kusaidia Yatima lakini njia rahisi ya kupata misaada toka nje itakayowasaidia wao na familia zao. Kwa maneno mengine yatima wanakuwa ni kama chambo cha utajiri.
 
Back
Top Bottom