Misamiati maarufu vyuo vikuu

mapanki....Fisrt year wa mwaka 2006/2007 udsm huo ndo wakati ule movie ya mfaransa kuhusu mapanki ilikua inaisumbua serikali

yep mapank! Mapank na bodi ya mikopo! Mapank wenye dv2 boy wamenyimwa boom,mapank waliishi maisha ya shida sana kipindi hicho. Akikatiza fst year tu utasikia Pank hilo
 
teh teh teh,wadada wengi huwa wanapga code 011 ili wasishtukiwe kuwa hawana kitu.

tena sana,madada ni bingwa wa kupiga hii code hasa kile kipindi cha ue kinapokaribia kuanza na boom limekata,ukinda ud pale manzese code 011 kibao.
 
1.'Boom'(fedha za kujikimu zitolewazo na Bodi ya Mikopo ya Elimu Ya Juu kwa wanachuo/wanafunzi)
2. 'Kuuza chai'(Kupiga stori hasa za kuchekesha/au sizizo za kweli)
3.'Nyanga'(Supplementary exams)
4.Kutiwa nyavuni/kukamatwa(kufeli somo hivyo kutakiwa kulirudia)
5.Nondo(vitu visivyoruhusiwa mtihanini lakini vinavyoingizwa kimagendo)
6.Exile(kumpisha mwanachumba mwenzako 'atumie' chumba pekeyake kwa muda fulani
7.'Kupiga Dash'(kushinda bila kula kwasababu ya kuishiwa fedha za kujikimu)
8.Kipanga(mwanafunzi anayejiweza darasani kwa kuelewa haraka au kutosahau haraka)
9.Kilaza(mwanafunzi ambaye uelewa wake ni wa mashaka/haelewi mapema na hachelewi kusahau)
10.'Ungwini'(Masomo ambayo hayaambatani na mahesabu)
Street game = demu wa uswazi, hii ni pale Cbe dom
 
Blong's= kijiwe zilikokuwa zinapatikana ndete/gamuma(bangi)na mpodo(sigara kali isted of rizla )
 
jembe- mtu yupo vizuri kimasomo
matuta(penalty)- probation (paper ya mwisho bada ya sup)
kusajili- kujipanga kenye paper kwwjili ya chabo. (4-4-2 format ya mchezo
 
yep mapank! Mapank na bodi ya mikopo! Mapank wenye dv2 boy wamenyimwa boom,mapank waliishi maisha ya shida sana kipindi hicho. Akikatiza fst year tu utasikia Pank hilo

ahaaa kweli bwana mapanki.na badae likaja bambucha yote yakimaanisha first year.
 
karai - score ya "C" kwenye somo (mtihani) ambayo... wakati ule ilikuwa ndiyo lowest grade, sijui siku hizi

kutoboa karai - kufeli somo (mtihani)..i.e kupata chini ya "C"

kitafunio - picha za "X"

HS - siku hizi mngewaita masharobaro!
 
Kuchana neti-Anaesoma sana mida ya usiku,wauza sura - flat screen,kuingia na material kwenye chumb cha exam -kujilipuwa au kujitoa muhanga
 
Tutorial-picha za ngono
Big brother-block f mabibo hstl.
Manzese-cafeteria 2
Mangwini-w'chuo wanaosoma kozi zisizo na maths.
Course work-makalio
Mdegree-sehemu ya kukaa kila m2 lazima ukae pale.

Aah kaka magwini ni kama wewe msiosoma engineering. usijivue gamba ngwine.
 
call box. - ni dirisha end of a hall block. wanatumia usiku 4 privacy kuongea na simu.
 
1.'boom'(fedha za kujikimu zitolewazo na bodi ya mikopo ya elimu ya juu kwa wanachuo/wanafunzi)
2. 'kuuza chai'(kupiga stori hasa za kuchekesha/au sizizo za kweli)
3.'nyanga'(supplementary exams)
4.kutiwa nyavuni/kukamatwa(kufeli somo hivyo kutakiwa kulirudia)
5.nondo(vitu visivyoruhusiwa mtihanini lakini vinavyoingizwa kimagendo)
6.exile(kumpisha mwanachumba mwenzako 'atumie' chumba pekeyake kwa muda fulani
7.'kupiga dash'(kushinda bila kula kwasababu ya kuishiwa fedha za kujikimu)
8.kipanga(mwanafunzi anayejiweza darasani kwa kuelewa haraka au kutosahau haraka)
9.kilaza(mwanafunzi ambaye uelewa wake ni wa mashaka/haelewi mapema na hachelewi kusahau)
10.'ungwini'(masomo ambayo hayaambatani na mahesabu)
11.'kudesa'(kuiga kwa mwanafunzi mwingine au kuandika kitu kama kilivyokutwa mahali fulani au kwa mtu fulani)
12.'desa'/'madesa'(kitabu/vitabu visivyo rasmi

wana jf tuendelee...

hii code
 
Back
Top Bottom