Miradi ya Maprofesa wa Bongo

Miradi ya Maprofesa wa Bongo

Huna unachojua mwehu wewe! Unafahamu Prof. Mdegela wewe? Wacha nisitaje miradi yake! Mbona wengi tu wanapiga hela kwenye fani zao! Unataka prof. Wa SUA asifuge ng'ombe? Eti unasema ng'ombe wawili, hujawahi kumwona Prof mwenye ranch ya ng'ombe wa nyama na maziwa pale SUA?
Ni vya kwake? Prof. Mzima unaendesha stationery? au mpesa, waachie darasa la saba bwana, ipo siku utakuta prof. Anauza chapati na utasema ni sawa.
 
Dogo ni mpuuzi anaongea asichokijua! Hakuna mtu anapiga life kama ma professor. Tena hata huo mshahara uliomtajia ni wa lecturer wa kawaida senior lecturers wako 10m na kuendelea!
Kama wana mishahara mizuri yanini kujifanyisha biashara mbuzi, kuendesha stationery na mpesa ndio biashara gani kwa prof. Wanatakiwa wafanye mambo makubwa yanayoendana na elimu zao na vipato vyao.
 
Nafikiri mtoa mada anaongelea maprofesa, sidhani kama yeye ni profesa.
Kwa maana yeye hatakiwi, kuishi vizuri wala kujihangaosha sababu siyo profesa.
Mama Tibaijuka hata akifuga ng'ombe wawili ni kwa ajili ya maziwa tu, siyo biashara. Profesa mwenye maisha magumu nani, Issa Shifji, ama Sarungi, ama Lipumba

Inawezakana nia kuwaamusha, ila amsha kada zinazoishi kwa shida baada ya kustaafu, maprofesa wanaishi vizuri sana, kama kuna wawili watatu wana maisha mabaya, siyo katika wengi.
 
Wewe ulitaka wabuni miradi gani?

Tupe refference ya maprofessor wakubwa duniani na miradi waliyoanzisha ili tulinganishe
Kwanza profesa siyo mfanya biashara, hata ikitokea inatokea tu, ila siyo eneo lao, tuwalaumu kwa kuto kufanya tafiti za maana na kugundua, mambo muhimu ya kuisaidia mchi.
Biashara siyo eneo lao, hata kwa maprofesa wa Dunia mzima.
 
Huwajui ma prof wewe, profesa wa SUA anafadhiliwa na USA milions of TSh kwa utunzaji wa Mazingira au Milima au Ufugaji,hawezi hangaika na bar au mifungo
Mkuu, kweli Tz hii kuna prof ambaye ana maisha kiasi kwamba hatamani kufanya biashara ya Bar/mifugo ? Serikali ya Marekani ina pesa kiasi hiko cha kuwafadhili ma professor wote wa SUA kiasi kwamba wameridhika ?

Mimi nafikili hamjaelewa lengo kuu la mleta mada ama kuna panick. Anyway, ningependa nijibiwe hayo maswali yangu mimi kama observer wa huu mjadala
 
Hawa jamaa ni watu wa ajabu pale UD wengine ukienda ofisi zao kuwaulizia usipotaja mwanzoni title ya Prof...

Ukasema Mr...

Wanakukaushia. Jamaa wana mambo ya ajabu sana. Wanapenda sana sifa na kunyenyekewa
Hiyo ni nature ya Binadamu wengi wa fani hoyo, they always seek comfort, kwa mfano, una miaka 40+ na nyumba moja ya kawaida tu na gari moja au mbili second hand au fourth hand hasa hizi IST, Harrier nk, huna mradi wowote wa kuingiza pesa nzuri yani una maisha ya kawaida wakati wewe ni mpenda misifa na kujikweza unaamini kwanza una akili sana na uliamini Elimu ingekufanya uwe bora kuliko binadamu wote.

Tatizo linaanzia hapo sasa ndio unaanza kuwa na vijitabia kama hivo vya kutaka lazima watu wakuite prof, lazima watu wakunyenyekee, unataka ku prove kila mara kwamba wewe ndio wewe (delusion) apparently this is a mental illness ( alimalizia hivo mlevi mmoja nilikuwa naye hapa kijiweni)
 
Sasa milion 6 Kwa mwaka si milion 72.


Kuna wafanyabiashara hiyo Hela ni ya mwezi tu.
Unajua watu mnachekesha sana....

Nataka unitajie huyo mfanyabiashara anayepata faida ya million 72 kwa mwezi...siongelei mauzo mimi...naongelea faida kama faida yaan ushatoa kodi zote....

Tena professor wana semina nyingi sana na unakuta hapo anafundisha kipindi kimoja kimoja vyuo vitano na kila kipindi au lecture ni 1m per month..

Hapo hujahesabu research na wanafamilia wake kunufaika na bima, makazi nk...



Unajua bongo tuna akili ndogo sana

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Utakuwa humjui Tibaijuka wew....utajiri wake ni ukoo wenu mara 10 na bado hamfikii...

Fuatilia shule za Babro johson na Kajumlo alexender kule bukoba
Upo nje ya point ya huyo jamaa, ameuliza hao ma professor aliowataja wamefanya nini cha maana ? Anadai ni weupe kichwani sababu hawajaleta input yeyote kwenye Taifa, hilo swala la mali sio hoja yake ya msingi ni kama kibwagizo tu. Kina kabudi wamefanya nini ?

Mimi nadhani huu mjadala utakuwa na maana sana kama mkijibizana hoja kwa hoja. Hata kama mkiamua kuzungumzia uchumi binafsi wa ma professor basi jikiteni kuwa general kama alivofanya mleta mada sio hivo kutoa mifano michache ya professors matajiri ambao wote wamepata pesa kwenye siasa tena wengi wao utajiri wa upigaji.

Taifa lilitegemea ma professor ndio watumie elimu yao kutukomboa, CCM imejaa Doctors kuliko chama chochote ndani na nje ya East Africa lakini kwa mtu yeyote mwenye akili timamu akisikiliza hoja za CCM anaona ni upuuzi, Dkt Tulia ni wakusainishwa bogus treat kweli !!!
 
Dogo ni mpuuzi anaongea asichokijua! Hakuna mtu anapiga life kama ma professor. Tena hata huo mshahara uliomtajia ni wa lecturer wa kawaida senior lecturers wako 10m na kuendelea!
nafikili you are just being sarcastic, Mkuu wa wilaya mwenyewe hali 10m ije kuwa lecturer (mwalimu aliyechangamka) milioni kumi (kwa heshima yake nimeamua kuiandika kwa maneno) ki bongo bongo ni pesa ndefu sana wanaoila ni watu wazito hasa na daily routine zao hazina pilikapilika mara kuwahi kipindi, mara kusahihisha mitihani yani wanaipata kilaini sana unless ni engineers
 
Mkuu, kweli Tz hii kuna prof ambaye ana maisha kiasi kwamba hatamani kufanya biashara ya Bar/mifugo ? Serikali ya Marekani ina pesa kiasi hiko cha kuwafadhili ma professor wote wa SUA kiasi kwamba wameridhika ?

Mimi nafikili hamjaelewa lengo kuu la mleta mada ama kuna panick. Anyway, ningependa nijibiwe hayo maswali yangu mimi kama observer wa huu mjadala

Kaka tembea uone,SUA hakuna prof masikini nakuambia wale jamaa wanamiradi wanaandika na proposal na yanafadhiliwa vizuri
 
Back
Top Bottom