Miradi ya Maprofesa wa Bongo

Miradi ya Maprofesa wa Bongo

Kabla ya kukimbilia kutuletea miradi ya hao Maprofesa wa Bongo, ulitakiwa kwanza kutuwekea miradi yako unayoimiliki wewe kama wewe kwa 💯% huko uliko mpaka sasa, ili kuwamotivate wengine.

Maana ufahamu unapo mnyooshea mwenzako kidole kama hivi; 👉 basi ukumbuke kuna vidole vingine vitatu vinakuelekea wewe mwenyewe.

Kabla ya kukimbilia kutuletea miradi ya hao Maprofesa wa Bongo, ulitakiwa kwanza kutuwekea miradi yako unayoimiliki wewe kama wewe kwa 💯% huko uliko mpaka sasa, ili kuwamotivate wengine.

Maana ufahamu unapo mnyooshea mwenzako kidole kama hivi; 👉 basi ukumbuke kuna vidole vingine vitatu vinakuelekea wewe mwenyewe.
Salam kwako Prof😀
 
1.Ng'ombe wawili wa maziwa(SUA)
2.BAR(UDSM,OUT,UDOM,SAUT,DUCE,MUCE )
3.lodge (Mzumbe,UDOM)
4.Mboga mboga nusu heka (SUA)
5.Bwawa la samaki(SUA)
6.Stationary-vitini vinapatikana hapo na vitabu vyake(vyuo vyote)
7.Daladala (UDSM,OUT,SUA)
8.Saluni(DUCE,UDOM,MAKUMIRA,MIPANGO DOM,MZUMBE)
9.SHULE (Huyu amejitutumua sana ila usimamizi sio mzuri)

Ongeza na wewe unazo zikumbuka
tofauti kabisa na maprof wa mbele. though hao wa dodoma na mzumbe wa lodge na hotels, ndio wameona vizuri.
 
Nongeni bar kigurunyembe /sua
Groness hotel nanenane /sua
White inn hotel kikundi /sua
Bizzed hotel /Sua
Alc hotel karibu Jordan/ sua
Motel nanenane / sua.
Nkuu,ww Ni Ntu ya Morogoro kabisaa 😀😞
 
Kuna kamoja ka udsm kanaitwa Prof Bibi hukaambii kitu kuhusu kuku wa mayai kila siku kanatoroka vipindi kupeleka mayai town.kalinipea lift one day kanakimbiza gari Kama mshale
 
Naomba nieleze Tafiti za maprofesa wa Tanzania zilizo saidia mabadiliko makubwa katika nyanja za kimaisha ya watanzania kiujumla.

Angalau kwenye nyanja za kiuchumi, kielimu na Afya.
Mkuu wanasiasa wapo tayari kuchukua tafiti za wasomi na kuzifanyia kazi?
Phd thesis mojawapo ni ya mwanafizikia wa Udsm ambaye alienda kufanya utafiti wa mwenendo wa upepo pale makambako.
Tafiti hio ina muwezesha muwekezaji awexe kuwekeza sekta ya nishati jadidifu kwa kutumia andiko lile.
Hii ina maana iwapo muwekezaji au serikali ikiamua uwekezaji pale tayari wana data za kuanzia.
Hii ina maana wanasiasa wangekuwa wanajali tafiti tayari kungekuwa ba mradi mkubwa wa umeme pale Njombe makambako.
Hii ina maana kungekuwa na kituo kikubwa cha uzalishaji umeme upepo ambspo kungekuwa na mji mdogo wa watumishi, biashara zingefanyika , utalii ungefanyika, watafiti wangetembelea pale, viwanda vingeanzishwa. Kumgekuwa na multiplying
effect kubwa ambayo chanzo ni profesa mmoja tu ambaye tafiti yake imo kabatini inaliwa na panya..
 
Vilaza uwa mnajifariji kinoma.
Soma basi na wewe uwe Profesa.
Maprofesa hao walio soma wana misaada gani kwa taifa?

Kuna Tafiti ngapi za hao maprofesa waliosoma zilizoleta na kuchangia maendeleo ya nchi?

Maprofesa wa Tanzania ni njaa kali, wasaka teuzi, Machawa na wachumia matumbo.
 
Hii nchi kila mtu analaumiwa. Hivi nani mwenye nafuu ?
Hata MO, Bakhresa nao hulaumiwa.
Suluhisho ni nini ?
Kwa nini unataka mtu mwingine abebe majukumu yako? Kwani jukumu la kuanzisha biashara kubwa ni la professor peke ake?
Kwa nini mtoa mada na wewe sio tajiri ? Mbona USA matajiri hawajamaliza chuo kikuu.
Kwa nini mtoa mada usiwe professor ili uje utoe mfano wa kuwa professor tajiri?
Nahitimisha kwa kusema kila pungufu la hii nchi linamuhusu kila mtu, tumejitoa ufahamu na kubebesga lawama kundi fulani la watu watutatulie shida zetu.
Ukilinganisha kipato cha Professor wa USA na tajiri wa kule wap9 the same boat na wetu.
Prof wa USA analipwa Mpaka dola laki 1+ wakati tajiri wa kule USA ana miliki dolla bilioni 50 mpaka 200.
Ina maana hao professor wa marekani hawana akili?
CEO wa OPEN AI ni kijana mdogo alie acha shule, ila kwa muda mfupi ameisha washinda utajiri maprofesa wengi wa USA.
Fanyeni comparative analysis ya hawa watu dunia nzima, they were not prepared for making money but for finding solutions.
Bila wao watu wengi duniani tungesha kufa( nimeongea kiujumka).
 
Kwa maana yeye hatakiwi, kuishi vizuri wala kujihangaosha sababu siyo profesa.
Mama Tibaijuka hata akifuga ng'ombe wawili ni kwa ajili ya maziwa tu, siyo biashara. Profesa mwenye maisha magumu nani, Issa Shifji, ama Sarungi, ama Lipumba

Inawezakana nia kuwaamusha, ila amsha kada zinazoishi kwa shida baada ya kustaafu, maprofesa wanaishi vizuri sana, kama kuna wawili watatu wana maisha mabaya, siyo katika wengi.
Sawa hatujakataa lkn wana miradi ya aja ajabu isiyolingana na adhi yao.
 
Profeseri sasa umkute kwenye pindi la Business law, Accounting I&II, Financial MGT I & Ii, Econometrics au Calculus anavyovimba na kuwatisha kwamba atawakamata UE nusu ya darasa mkileta mchezo. Kivumbi ni kwenye kutafuta Course work test anawadaka nusu ya darasa ili mlundikane ofisini kwake na dada zetu kuvuliwa pichu. 😁
 
Hii nchi kila mtu analaumiwa. Hivi nani mwenye nafuu ?
Hata MO, Bakhresa nao hulaumiwa.
Suluhisho ni nini ?
Kwa nini unataka mtu mwingine abebe majukumu yako? Kwani jukumu la kuanzisha biashara kubwa ni la professor peke ake?
Kwa nini mtoa mada na wewe sio tajiri ? Mbona USA matajiri hawajamaliza chuo kikuu.
Kwa nini mtoa mada usiwe professor ili uje utoe mfano wa kuwa professor tajiri?
Nahitimisha kwa kusema kila pungufu la hii nchi linamuhusu kila mtu, tumejitoa ufahamu na kubebesga lawama kundi fulani la watu watutatulie shida zetu.
Ukilinganisha kipato cha Professor wa USA na tajiri wa kule wap9 the same boat na wetu.
Prof wa USA analipwa Mpaka dola laki 1+ wakati tajiri wa kule USA ana miliki dolla bilioni 50 mpaka 200.
Ina maana hao professor wa marekani hawana akili?
CEO wa OPEN AI ni kijana mdogo alie acha shule, ila kwa muda mfupi ameisha washinda utajiri maprofesa wengi wa USA.
Fanyeni comparative analysis ya hawa watu dunia nzima, they were not prepared for making money but for finding solutions.
Bila wao watu wengi duniani tungesha kufa( nimeongea kiujumka).
Maprofesa wa Tanzania wamefanya Tafiti gani zilizo leta mabadiliko makubwa nchini?
 
Ule utafiti wa Proffessor Bana ulikuwa kupitia taasisi ikiitwaje vile?

Mwenye kukumbuka atukumbushe tafadhali

Halafu ilikuwa nyakati za karibia na uchaguzi Mkuu ,

Wanatumika kuleta taarifa ambazo kwa haraka zinaonesha kuwa sio.
 
Redent sijui I am stand to be corrected if mistaken,

Hawa Jamaa bado wapo au ndio wanasubiri karibia na uchaguzi walete za kuleta?!

Mungu anawaona!
 
SUA wameweka sup za kulipia sup ni 20 ukipata zaid ya 1 unaongezea elf 10.

Wakati SUA sup wanapatakaga nusu ya chuo.
Muda unakimbia, kuna kipindi nilikuwa na sup 4, kwahiyo ningetoboka 60, kipindi napiga hapo Sua 2011-14 niliacha ni free, na freedom square ilikuwa inajaa, siyo mchezo, acha waingize mapato...
 
Nimetafakali na kuona huenda wachangiaji wengi wana hoja ya msingi pamoja na Mleta mada.

Kwamba wanatarajia Msomi mbobezi kiwango cha Professor afanye mambo ambayo ni extra ordinary and outstanding ukilinganisha na mtu ambae si msomi au ambae ni msomi wa kawaida wa kiwango cha shahada moja tu .

Sasa wanashangaa kuona maprofesa kufanya uchuuzi/biashara na mambo yale yale madogo madogo au ya kawaida ambayo hufanywa na Mamuma,

Je tofauti ya Professor na aso professor ni kitu gani?

Je ushawishi wa watu kwenye jamii watake kusoma kiwango cha u-Professor kinaweza kuwa ni nini?

Ikiwa mwisho wa siku hakuna ziada ktk kufanikiwa?
 
Back
Top Bottom