Miongoni mwa maswali ya UONGO na KIJINGA

Miongoni mwa maswali ya UONGO na KIJINGA

hapo uliposema ujinga ni kinyume cha elimu una maanisha nini?
mtoa mada ndio unatakiwa uzibitishe hayo maswali ni ya kijinga na ya uongo,

Nakujibu kwa kukupa maana ya Elimu,kisha kile kinyume chake ndio Ujinga.

Elimu maana yake ni kukidiriki kitu kama kilivyo. Yaani nikisema haya ni Maji,basi yawe maji kweli na si vinginevyo. Kwa ufupi hiyo ndio maana ya Elimu.
 
Nimeandika Kiswahili chepesi ya kuwa mimi sina swali la kujibu hapo,sababu hayo maswal ya Uongo huwa tunaelekezewa sisi na Wakana Mungu,ndio sisi tunawaambia ya kuwa maswali hayo ni ya UONGO.
Kabla hujajibu haya maswali kwanza thibitisha kwamba ni ya uongo
 
Kabla hujajibu haya maswali kwanza thibitisha kwamba ni ya uongo
Kwanza sipaswi kujibu hayo maswali sababu ni uongo. Uongo ni kinyume cha Ukweli.

Ukweli maana yake ni kauli au kitendo kuafikiana na hali halisi.

Bila shaka umenielewa. Hayo maswali huwa tunaulizwa na wakanamungu na ni ya uongo sababu hayakai katika sifa anuai za Mola muweza.

Nakuonyesha uongo wa hayo maswali kwa mfano mmoja,sisi Mola wetu ni muweza wa yote,vipi mtu aulize swali tena kuhusu uwezo wake ? Wakati anaweza yote ?
 
Kwasababu utukufu wake ni "intact" na sifa yake ni umoja (Allah ahad) basi hawezi kuumba kitu sawa na yeye..
"hawezi kuumba kitu sawa na yeye " hii kauli inafuta kabisa zile kelele kuwa Allah anaweza kuumba kitu chochote atakacho
 
1.Je Mola anaweza kuumba kitu sawa na yeye ?

Hili swali ni la uongo,na haulizi swali isipokuwa mchachefu wa maarifa juu ya Mola muumba.

Anasema Allah aliye juu :
1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
2. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
3. Hakuzaa wala hakuzaliwa
4. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja. (al Ikhlaswi : 1 - 4 )

Sifa moja wapo ya Mola wetu hafanani na chochote,vipi aumbe kiumbe sawa na yeye ? Jibu ni haiwezekani,na hapa ndipo ulipo uongo wa swali hilo.
 
Nimeandika Kiswahili chepesi ya kuwa mimi sina swali la kujibu hapo,sababu hayo maswal ya Uongo huwa tunaelekezewa sisi na Wakana Mungu,ndio sisi tunawaambia ya kuwa maswali hayo ni ya UONGO.
Kwahiyo kila anaeuliza swali hilo ni mkana Mungu ? wapo watu wengi wanauliza kujifunza usipende kutoa hukumu ya jumla kijana duniani tunatofautiana aya jibu swali
 
Hili swali ni la uongo,na haulizi swali isipokuwa mchachefu wa maarifa juu ya Mola muumba.

Anasema Allah aliye juu :
1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
2. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
3. Hakuzaa wala hakuzaliwa
4. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja. (al Ikhlaswi : 1 - 4 )

Sifa moja wapo ya Mola wetu hafanani na chochote,vipi aumbe kiumbe sawa na yeye ? Jibu ni haiwezekani,na hapa ndipo ulipo uongo wa swali hilo.
Kama.afanani na chochote basi aumbe kiumbe kilichomzidi yeye Mola wako , hapo mfanano utakuwa haupo kabisa
 
"hawezi kuumba kitu sawa na yeye " hii kauli inafuta kabisa zile kelele kuwa Allah anaweza kuumba kitu chochote atakacho
Sio kweli,hiyo kauli ipo dhidi yenu,kwani Mola aliye juu anasema :

62. Hii ni ada ya Mwenyezi Mungu iliyo kuwa kwa wale walio pita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika ada ya Mwenyezi Mungu. ( al Ahzab : 62 )

Hukuti katika ada ya Mola wetu yenye kibadilika,ndio maana leo hii huwezi kukuta jua limechomoza magharibi na kuzama mashariki,au mtoto aka mzaa mama,hili halipo sababu Mola ameshahukumu jambokuwa hivyo na ndivyo ilivyo hata kwa atakaye taka Mola aumbe kiumbe sawa na yeye hilo haliwezekani na sio kwamba hawezi,na kila jambo linahekima zake.
 
Kama.afanani na chochote basi aumbe kiumbe kilichomzidi yeye Mola wako , hapo mfanano utakuwa haupo kabisa
Mola wetu sifa zake zote ni kmalifu kwahiyo hakuna kitakacho toka nje ya uwezo wake wala kumzidi yeye,kwani akiumba kinachomzidi ataonyesha udhaifu,na udhaifu sio sifa yake.
 
Mola wetu sifa zake zote ni kmalifu kwahiyo hakuna kitakacho toka nje ya uwezo wake wala kumzidi yeye,kwani akiumba kinachomzidi ataonyesha udhaifu,na udhaifu sio sifa yake.
Kwahiyo tunakubaliana kuwa Mola wako kuna vitu hawezi kuumba ?
 
Sio kweli,hiyo kauli ipo dhidi yenu,kwani Mola aliye juu anasema :

62. Hii ni ada ya Mwenyezi Mungu iliyo kuwa kwa wale walio pita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika ada ya Mwenyezi Mungu. ( al Ahzab : 62 )

Hukuti katika ada ya Mola wetu yenye kibadilika,ndio maana leo hii huwezi kukuta jua limechomoza magharibi na kuzama mashariki,au mtoto aka mzaa mama,hili halipo sababu Mola ameshahukumu jambokuwa hivyo na ndivyo ilivyo hata kwa atakaye taka Mola aumbe kiumbe sawa na yeye hilo haliwezekani na sio kwamba hawezi,na kila jambo linahekima zake.
Hilo jibu kamjibu mwenzako alietoa hiyo kauli kuwa "mola hawezi kuumba kitu sawa na yeye " au ww unapinga hili ?
 
"hawezi kuumba kitu sawa na yeye " hii kauli inafuta kabisa zile kelele kuwa Allah anaweza kuumba kitu chochote atakacho


Ndiyo, Sio kila kitu Mungu anaweza kufanya, Kazi zote za shetani Mungu hawezi kufanya mfano, Mungu HAWEZI kumsaidia mtu kuiba, hawezi kumsaidia mtu kuzini, hawezi kumsaidia mtu kufanya uhalifu nk, pia Mungu hawezi Kumfufua mtu aliyekufa arejee tena duniani.

Mungu anazo kanuni zake ambazo HAWEZI kamwe kuzibadilisha ili kulinda utukufu wake, hadhi na heshima yake kama Mungu, kwani kama atabadilisha baadhi ya kanuni zake basi hapo atakuwa Mungu kigeugeu (Apishe mbali) na hii sio sifa yake katika hali hiyo maisha ya hapa duniani yatakuwa hovyo na ya kubadilika kila wakati na hiyo itakuwa "lawlessness" na Mungu hayupo hivyo, ndiyo maana akasema; wa lan tajida li sunnatllah tabdila" yaani; Wala huwezi kukuta sunna/kanuni za Mungu zikibadilika.
 
Kwahiyo tunakubaliana kuwa Mola wako kuna vitu hawezi kuumba ?
Unaelewa nini unapo ambiwa kwamba Mola hashindwi na jambo na sifa zake ni kamilifu na nilipokwambia hukuti ada ya Mola wetu ni yenye kubadilika ?

Pili,kuna mambo kadha wa kadha ambayo Mola wetu amejiharamishia kuyafanya yeys mwenyewe,mfano amejiharamishia DHULMA,yaani Mola wetu hadhulumu.
 
Ndiyo, Sio kila kitu Mungu anaweza kufanya, Kazi zote za shetani Mungu hawezi kufanya mfano, Mungu HAWEZI kumsaidia mtu kuiba, hawezi kumsaidia mtu kuzini, hawezi kumsaidia mtu kufanya uhalifu nk, pia Mungu hawezi Kumfufua mtu aliyekufa arejee tena duniani.

Mungu anazo kanuni zake ambazo HAWEZI kamwe kuzibadilisha ili kulinda utukufu wake, hadhi na heshima yake kama Mungu, kwani kama atabadilisha baadhi ya kanuni zake basi hapo atakuwa Mungu kigeugeu (Apishe mbali) na hii sio sifa yake katika hali hiyo maisha ya hapa duniani yatakuwa hovyo na ya kubadilika kila wakati na hiyo itakuwa "lawlessness" na Mungu hayupo hivyo, ndiyo maana akasema; wa lan tajida li sunnatllah tabdila" yaani; Wala huwezi kukuta sunna/kanuni za Mungu zikibadilika.
acha kujichanganya tunazungumzia Mungu kuumba ayo mambo ya shetani yametoka wapi ? acha kutoa maelezo ambayo ayaitajiki
 
Unaelewa nini unapo ambiwa kwamba Mola hashindwi na jambo na sifa zake ni kamilifu na nilipokwambia hukuti ada ya Mola wetu ni yenye kubadilika ?

Pili,kuna mambo kadha wa kadha ambayo Mola wetu amejiharamishia kuyafanya yeys mwenyewe,mfano amejiharamishia DHULMA,yaani Mola wetu hadhulumu.
1. Hashindwi na jambo maana yake kwake hakuna linaloshindikana , sasa anaposhindwa kuumba kitu kilichomzidi au kama yeye maana yake anashindwa
2.unaposema ADA maana yake ni desturi ,mara kadhaa Mbona Mola wako amekwenda nje ya ADA , mfano alipojaalia Mimba tumboni mwa Mariamu bila kuingiliwa na mwanaume pale ameondoka kwenye ADA akatumia uungu wake, sasa unapoijadili ada kama jambo kubwa unashangaza sana
3. Mambo ya kujiaramishia ndio nini , Mola ametangaza mwenyewe hakuna jambo linalomshinda kwake , acha kuchanganya madawa
 
Back
Top Bottom