Ujinga ni kinyume cha elimu. Huu ujinga umegawanyika sehemu mbili :
1. Ujinga ambao dhidi yake ni elimu.
2. Ujinga ambao dhidi yake ni hila
Aina zote hizi mbili nimezizingatia katika mada yangu hii.
Ama kuhusu uongo ni kinyume cha ukweli. Huu nao umegawanyika sehemu kuu mbili:
1. Uongo wa Kauli
2. Uongo wa matendo
Hapa katika uongo natilia mkazo kauli ya mja mwema mmoja tena mwanazuoni aliposema "Laiti kama UONGO ungekuwa ni jambo jema na lenye kuruhusiwa basi mimi nisingesema uongo kwa ajili ya kujitakasa"
Uongo ni tabia mbaya,tabia ambayo hatakiwi yeyote yule apambike kwayo.
Baada ya utangulizi huo. Yafuatayo ni maswali ya uongo na kijinga.
1. Je Mola anaweza kuumba kitu sawa na Yeye ?
2. Je Mola anaweza kumtoa kiumbe wake nje ya milki yake ?
3. Je Mola anaweza anaweza kuumba jiwe ambalo hawezi kulibeba ?
4. Kwa kuwa Mola ameumba viumbe baada ya kutokuwepo viumbe hivyo hapo kabla,Je Mola anaweza kuona au kujua kitu tu ambacho hakipo ?
Haya ni maswali ya uongo na ya kijinga,kama yupo anae pinga athibitishe kwamba maswali haya si ya uongo wala sio ya kijinga.
1. Ujinga ambao dhidi yake ni elimu.
2. Ujinga ambao dhidi yake ni hila
Aina zote hizi mbili nimezizingatia katika mada yangu hii.
Ama kuhusu uongo ni kinyume cha ukweli. Huu nao umegawanyika sehemu kuu mbili:
1. Uongo wa Kauli
2. Uongo wa matendo
Hapa katika uongo natilia mkazo kauli ya mja mwema mmoja tena mwanazuoni aliposema "Laiti kama UONGO ungekuwa ni jambo jema na lenye kuruhusiwa basi mimi nisingesema uongo kwa ajili ya kujitakasa"
Uongo ni tabia mbaya,tabia ambayo hatakiwi yeyote yule apambike kwayo.
Baada ya utangulizi huo. Yafuatayo ni maswali ya uongo na kijinga.
1. Je Mola anaweza kuumba kitu sawa na Yeye ?
2. Je Mola anaweza kumtoa kiumbe wake nje ya milki yake ?
3. Je Mola anaweza anaweza kuumba jiwe ambalo hawezi kulibeba ?
4. Kwa kuwa Mola ameumba viumbe baada ya kutokuwepo viumbe hivyo hapo kabla,Je Mola anaweza kuona au kujua kitu tu ambacho hakipo ?
Haya ni maswali ya uongo na ya kijinga,kama yupo anae pinga athibitishe kwamba maswali haya si ya uongo wala sio ya kijinga.