Kwanza ni hivi; kujenga maswali na kujiuliza au kuuliza ndiyo asili ya sifa au tabia ya akili ya mwanadamu, viumbe hai wengine minghairi ya wanadamu hawana akili yenye sifa hiyo na ndiyo maana sisi wanadamu huwa tunajitambua kila mtu kwa kadiri ya utambuzi wake aliojaliwa na Allah na ni kutokana na utambuzi wetu huo ndipo tukawekewa Sheria na Allah na hatimaye twende kuhukumiwa siku ya Qiyama, viumbe wengine kamwe hawahusiki na Qiyama.
Sasa, uongo au ujinga wa mtu hutokea baada mtu kujiuliza maswali na kupata jawabu la maswali hayo, kama jawabu ni la uongo au ujinga ndipo hapo utakapo sema mtu huyo ni muongo au mjinga, mfano mtu aulize je Allah anaweza kuumba Mungu mwingine atakayefanana naye??--- hilo sio swali la uongo kwasababu lipo na wala sio la kijinga kwasababu linahitaji mantiki kupata jibu, mantiki inakataa kutokana na sifa hizi za Allah kwamba Yeye ni mmoja na wala hana mshiriki na hafanani na chochote hivyo kamwe hawezi kumuumba Mungu mwingine ili wafanane na wawe sawa na juu yote hata tufanye aweze kumuumba bado mmoja atakuwa kaumbwa (kiumbe cha mmoja) na mwingine atakuwa Muumbaji hivyo hawatofanana kwa sifa. Sasa akitokea mtu akasema kuwa Allah anaweza kuumba Mungu mwingine kama yeye hapo sasa huyo mtu huwa ndiye Mjinga na Muongo na hapo wa kulaumiwa sio swali bali ni matokeo ya swali (jibu) na muhusika wa hilo jibu, kinyume chake ni mtu atakaye toa majibu ya kimantiki basi atapongezwa yeye pamoja na majibu yake.
Kama nitakuwa nimekuelewa, hivyo ndivyo nionavyo.