Kuna wanafunzi kama 10 hivi wa kdt cha nne(wawili hadi jela walishafungwa), hawa kwanza wangekuwa waache shule kabisa tokea kdt cha tatu, walimu tumehangaika kweli, wakarudi shule ila kila siku ni majanga,ni wavuta bangi na watumiaji wa miraa na virobakwenye mitihani wakiingia wanaandika majina tu then haoo wanasepa, wakitoka wanaanza kujisifia.
Tukaita wazazi, akaja mzazi wa mmoja tu nae alimpiga mwanae hadi mtoto kakimbia, akatuambia 'ndugu walimu kuanzia leo huyu sio mwanangu na hata mkiniita tena siji hata kwa mtutu'
Nikaamua kuubeba mzigo wa hawa watoto, kuongea nao nikakuta historia zao zinakaribiana wooote, wamelelewa ktk mazingira yasiyo na upendo kabisa, wengine wanajilea wenyewe, nikaanza nao councelling n other programs, nilijua wakibadilika atleast wawili itasaidia kuwabadili wote.
Mwisho wa siku wakabadilika ila ndio ile too late, now wanajutia hatari wanatamani angalau wapate cheti ila ndio labda Mungu atende miujiza.
Tunafanya kazi ngumu mno alafu mnakuja kuleta fyoko fyoko wakati nyie ndio chanzo cha hayo matatizo yote!! Msitegemee walimu tutende miujiza, badilikeni nyie mlee watoto wenu. Wengi watoto wanalelewa na mahouse girls wengine mtoto anaanza boarding akiwa chekechea, huyu upendo wa mzazi anaujua saa ngapi!!!