Mimi ni Mwalimu, nisome nilivyo

Mimi ni Mwalimu, nisome nilivyo

Wasalaamu wakuu!!

kwanza kabisa napenda kuwa omba mods wasiunganishe huu Uzi licha ya trend tuliyonayo, kwani Mimi ni mwalimu naomba nieleze nilivyo, yes waalimu tulivyo.

Napenda kutoa pole yangu ya dhati kabisa kwa mkuu wa shule kwa yaliyomfika, waalimu waliofikwa na janga na mtoto aliyepatwa.

maisha ya shule yana mengi, nadhani na pia ni hakika kuwa wengi humu tumepita shule ( ndio, hata la saba ni shule), Mimi kama mwalimu na kwa uzoefu wangu niliokaa kazini ningeweza kumwadhibu mtoto kama huyo wa mbeya kwa sababu zifuatazo;
(a) Ameonesha kunigomea mbele ya wanafunzi wenzake.
Kama kawaida hakuna mtu mzima yeyote ambaye anapenda kudhalilishwa mbele ya watoto.
Inatokea mwlm unataka kutoa adhabu kwa mwanafunzi eidha kwa kuwa ana kidemu chake darasani anaamua kuonesha dharau na migomo ya waziwazi. Hapo mi ambacho nafanya ni kupiga kama naua NYOKA ili wenzake wakiona wasijiingize kwenye kosa kama lake kamwe. HII INAITWA HESHIMA KWANZA, KAZI BAADAE.

(b) Mwanafunzi ameletwa Ofisini na Mwalm A ambaye anaonekana mnyonge au mpole hana makuu kwasababu hiyo mwanafunzi anamgomea adhabu eidha ya kupiga magoti au kuchapwa! wanafunzi wa aina hiyo Mimi huwa naomba SUB then naagiza mzigo wa kuni badala ya kupikia nabadili matumizi kwa manufaa ya ofisi.

(c) Nimetoka kwenye ATM nakuta mshahara Wangu umekatwa Tsh 60000 bila maelezo ya msingi, narudi shule nakutana na mtoto aliyeshindikana kwao kajichanganya mbele yangu hapo lazima ni convert tsh 60000 to 60000 sticks of coplar punishment.


Mnaojifanya kutetea humu wengi wenu hii kazi ya ualimu hamuijui au mnadhani kwa vile watoto wenu wanapenda shule, basi mnahisi ni wote dunia nzima.

Hakuna mwalimu kichaa hapa duniani ambaye mtoto hajagomea au kusumbua kupokea adhabu, atapigwa kiasi kile.

wito wngu.

waalimu wenzangu, pesa hatuna bado tunatafutwa kufungwa, unapopiga hakikisha kamera ya simu yako iko ofu.

Mpaka pale wanaotokwa mapovu hapa JF watakapowafunza maadili mema watoto wao na fimbo zitafutika zenyewe.

Kwa ukurya nilionao, ujinga darasani + ukorofi mwanao alionao, ACHUNGE SANA.
Mimi kichapo cha hivyo nimekulaga sana halafu nikirudi home mzee ananiuliza na akiona nilizingua ananishushia kichapo kingine yaaani nashukuru mpaka leo nna nidhamu ya hali ya juu na nnajitambua mwenyewe na kuwa mkweli wa nafsi yangu na si kupalilia ujinga
 
Mimi kichapo cha hivyo nimekulaga sana halafu nikirudi home mzee ananiuliza na akiona nilizingua ananishushia kichapo kingine yaaani nashukuru mpaka leo nna nidhamu ya hali ya juu na nnajitambua mwenyewe na kuwa mkweli wa nafsi yangu na si kupalilia ujinga
Asante
 
Kuna wanafunzi kama 10 hivi wa kdt cha nne(wawili hadi jela walishafungwa), hawa kwanza wangekuwa waache shule kabisa tokea kdt cha tatu, walimu tumehangaika kweli, wakarudi shule ila kila siku ni majanga,ni wavuta bangi na watumiaji wa miraa na virobakwenye mitihani wakiingia wanaandika majina tu then haoo wanasepa, wakitoka wanaanza kujisifia.

Tukaita wazazi, akaja mzazi wa mmoja tu nae alimpiga mwanae hadi mtoto kakimbia, akatuambia 'ndugu walimu kuanzia leo huyu sio mwanangu na hata mkiniita tena siji hata kwa mtutu'

Nikaamua kuubeba mzigo wa hawa watoto, kuongea nao nikakuta historia zao zinakaribiana wooote, wamelelewa ktk mazingira yasiyo na upendo kabisa, wengine wanajilea wenyewe, nikaanza nao councelling n other programs, nilijua wakibadilika atleast wawili itasaidia kuwabadili wote.

Mwisho wa siku wakabadilika ila ndio ile too late, now wanajutia hatari wanatamani angalau wapate cheti ila ndio labda Mungu atende miujiza.

Tunafanya kazi ngumu mno alafu mnakuja kuleta fyoko fyoko wakati nyie ndio chanzo cha hayo matatizo yote!! Msitegemee walimu tutende miujiza, badilikeni nyie mlee watoto wenu. Wengi watoto wanalelewa na mahouse girls wengine mtoto anaanza boarding akiwa chekechea, huyu upendo wa mzazi anaujua saa ngapi!!!
 
Amina.
Tena mzazi bila aibu anasema, mie huyu mtoto nimemchoka, nimemleta kwenu.
Kwani aliambiwa sie tuna makapu ya kuwabebea?
Wazazi wengine ni wasumbufu sana, sana.

Kwa vile tuna mioyo, tunavumilia, lakini yakizidi...akha!!!
Acha tu turukwe na akili aisee
Asiefunzwa na wazazi, walimu watamnyoosha 😀
 
Mzazi akitimiza majukumu yake kisawa sawa na mtoto akawa mtiifu nani atapoteza muda kumtandika??

Tatizo wazazi tumeshindwa malezi tunawapelekea waalimu mitoto iliyoshindikana. .... Halafu mnataka waalimu wawachekee.

Mlee mwanao ktk maadili mema uone kama atapigwa hicho kipigo cha kifedhuli..... Huyo mwanafunzi ni fedhuli alistahili kunyooshwa.


Mtoto asiyefunzwa na ***** hufunzwa na Ulimwengu.. Huyo dogo ulimwengu ulikuwa unamfunza.....
 
Na nyie wazazi mnaotujia usiku wa manane wakati tumepumzika na ma-baby zetu ili kusolve kesi zenu za kifamilia, mkome.

Kwani Mwenyekiti wa serikali ya mtaa au Mtendaji wake hukuwaona?
Mwanao nimfundishe, bado mambo yenu ya unyumba niyatatue.

Mnanilipa mishahara mingapi?
Cc: Evelyn Salt, atoto

Nimechefukwaaaa walahhh!!!
Hahaaaaa!!! Hodi kwa mwalimu haziishi hadi kesi za nyumbani utadhani mwalimu ndio mjumbe wa nyumba kumi, leo wanajifanya wajuajiii, narudia tena nyambafuuuuuuu!!!

Wametukalia kooni hatupumui, kesi zao na watoto wao waende polisi huko ndiko wanaojua sheria.
 
Wale waalimu nawasifu kwa kumnyoosha yule dogo ..Sema tu wamenikwaza hawakumpa kichapo kizuri...


Yule wangempiga wanachanganya na adhabu za kijeshi ..... Hadi mkojo umtoke. Hapo asingerudia tena
Wazazi wanatamani kupasuka 😀😀😀😀
Ila serious, tubayokutana nayo ni mengi asee
 
Tulipomaliza masomo waliofeli wote ndio wakaenda ualimu sasa sijui unaongea nini? By the way walimu walionifundisha mimi wengi wao walikuwa timamu, hawakuwa na akili kama zako. Na nikikutana nao mpaka kesho wanakula lager za kutosha kisha wanaondoka na nauli ya taxi.
Ukiwapa hela ya tax unaona umewasaidia wakat serikali inawanyanyasa? Upuuzi mtupu bora wamalizie hasira kwa matoto yenu
 
Wasalaamu wakuu!!

kwanza kabisa napenda kuwa omba mods wasiunganishe huu Uzi licha ya trend tuliyonayo, kwani Mimi ni mwalimu naomba nieleze nilivyo, yes waalimu tulivyo.

Napenda kutoa pole yangu ya dhati kabisa kwa mkuu wa shule kwa yaliyomfika, waalimu waliofikwa na janga na mtoto aliyepatwa.

maisha ya shule yana mengi, nadhani na pia ni hakika kuwa wengi humu tumepita shule ( ndio, hata la saba ni shule), Mimi kama mwalimu na kwa uzoefu wangu niliokaa kazini ningeweza kumwadhibu mtoto kama huyo wa mbeya kwa sababu zifuatazo;
(a) Ameonesha kunigomea mbele ya wanafunzi wenzake.
Kama kawaida hakuna mtu mzima yeyote ambaye anapenda kudhalilishwa mbele ya watoto.
Inatokea mwlm unataka kutoa adhabu kwa mwanafunzi eidha kwa kuwa ana kidemu chake darasani anaamua kuonesha dharau na migomo ya waziwazi. Hapo mi ambacho nafanya ni kupiga kama naua NYOKA ili wenzake wakiona wasijiingize kwenye kosa kama lake kamwe. HII INAITWA HESHIMA KWANZA, KAZI BAADAE.

(b) Mwanafunzi ameletwa Ofisini na Mwalm A ambaye anaonekana mnyonge au mpole hana makuu kwasababu hiyo mwanafunzi anamgomea adhabu eidha ya kupiga magoti au kuchapwa! wanafunzi wa aina hiyo Mimi huwa naomba SUB then naagiza mzigo wa kuni badala ya kupikia nabadili matumizi kwa manufaa ya ofisi.

(c) Nimetoka kwenye ATM nakuta mshahara Wangu umekatwa Tsh 60000 bila maelezo ya msingi, narudi shule nakutana na mtoto aliyeshindikana kwao kajichanganya mbele yangu hapo lazima ni convert tsh 60000 to 60000 sticks of coplar punishment.


Mnaojifanya kutetea humu wengi wenu hii kazi ya ualimu hamuijui au mnadhani kwa vile watoto wenu wanapenda shule, basi mnahisi ni wote dunia nzima.

Hakuna mwalimu kichaa hapa duniani ambaye mtoto hajagomea au kusumbua kupokea adhabu, atapigwa kiasi kile.

wito wngu.

waalimu wenzangu, pesa hatuna bado tunatafutwa kufungwa, unapopiga hakikisha kamera ya simu yako iko ofu.

Mpaka pale wanaotokwa mapovu hapa JF watakapowafunza maadili mema watoto wao na fimbo zitafutika zenyewe.

Kwa ukurya nilionao, ujinga darasani + ukorofi mwanao alionao, ACHUNGE SANA.
Kweli kabisa watoto wengine no problematic hasa akimuona mwalimu mpole. My take...if u c this report to the headteacher and suggest asiudhurie vipindi vyako kuepuka kufungwa au kupoteza kaxi kwa jaziba. Wote we know we have igos once bruised u can do the imaginables. ...poleni walimu.
 
Amina.
Tena mzazi bila aibu anasema, mie huyu mtoto nimemchoka, nimemleta kwenu.
Kwani aliambiwa sie tuna makapu ya kuwabebea?
Wazazi wengine ni wasumbufu sana, sana.

Kwa vile tuna mioyo, tunavumilia, lakini yakizidi...akha!!!
Acha tu turukwe na akili aisee
We mzazi umemshindwa mwanao ulomzaa si aibu hiyo, unategemea nini zaidi!! Si umpeleke polisi angalau apelekwe jela akafanye shughuli za ujenzi wa taifa.
Tukiamua kucharukiana watakaoumia ni watoto so msijitoe ufahamu kabisa.
Tushirikiane tu ili tuwasaidie watoto wa taifa lijalo.
 
Usijali, Ila mie napingana na hao wanaojifanya miungu watu, mabingwa wa kutoa findings bila kufanya research.
Secondary school hizi ndio balaa, heri primary.
Secondary mtoto anakudindia kabisa, na hivi akikuangalia unamfikia mabegani, unam-batua tu.
Kuna mdau kaongea vizuri sana kule juu.....nimempenda bure.
Yaani kuna muda huwa natamani ningekuwa mwalimu wa primary maana sekondari khaaaaaaah!!!
 
Back
Top Bottom