Mimi ni Mkristo ila Pongezi kwa Misikiti mingi ya Dar es Salaam kutoa Bure na kwa Bei nafuu Huduma ya Maji

Hapana FaizaFoxy miyeyusho..kuna mambo anayaendeleza hata PM. Mfano mm siwezi kumuwekea mtu kinyongo akija pm ana jambo lake kisa kutofautiana humu kwenye mijadala.
Mkuu huo Ni udhaifu wa wengi tu..hasa km Hoja ilihusu mambo ya siasa ...wengi hatuna personal torelance
 
Ila wewe jamaa ni mbishi sana ,ndugu zako wakristo wameprove hilo kuwa nyinyi mpo after money ila wewe unaangaika kupinga.Waislam wanafundishwa kwenye dini yao sio kama nyinyi
Huyo kichaa ndio umeweka hitimisho kuwa eti ndio kawasilisha mawazo ya wakristo? Tumia akili
 
Aaah Sinza kuna ujinga sana, maji ni Kero mno, jua kali.
Nami nikupongeze rafiki yangu GENTAMYCINE kwa kuliona hilo.
Hiyo hali sio Dar tu ni karibu nchi nzima, pale walipo waislam basi huduma hiyo ama ni bure au nafuu.
Ukifika Zanzibar ndio bure kabisaaa huduma ya maji.
Maji yametobolewa chini na michango ya watu ndio uyauze kweli?
 
Jambo pekee ninakowavutiwa na Waislamu ni kuwa Marais Waislamu wanakuwa na busara na nchi inastawi vyema kuliko wa upande wetu wa katoliki
Sawa basi. Huyu aliyepo naye ni muislam, amalize tatizo la maji.
Na kushangaa. Mbona marais waislam tumekuwa nao watatu vilevile na tatizo la maji liko pale pale?
 
Ni kweli..sio maji tu hata ukikwama nauli ukienda msikitini unachangiwa pesa mambo yanaenda..! Kule kwingine getini kuna mlinzi..! Na wao ndio wanachangia wachungaji wanunue magari..ila wao wakitaka magari wanaombewa..! Ila ngoja waje mkuu
Ni kweli mkuu,Kuna sadaka za kujiteketeza.hizo unatoa mpaka nauli ya kurudi kwako. Wenzio wana panda gari lenye AC na mabodigadi juu
 
Sawa basi. Huyu aliyepo naye ni muislam, amalize tatizo la maji.
Na kushangaa. Mbona marais waislam tumekuwa nao watatu vilevile.
Hapa Unakosea, hakuna tawala na awamu za hovyo kama za Hawa.Ni awamu zinazotawaliwa na Rushwa na ufisadi mkuu na uvivu wa watendaji. Ni watu wa matamko zaidi kuliko utendaji
 
utajiri au umasikini siyo kipimo cha utu. mwenzako anachokipata anasaidia jamii, wewe unachokipata unabaki nacho mwenyewe. kati ya ww na yeye nani atakuwa tajiri? we unatoa fungu la kumi kumpa mchungaji. mwenzako anatoa fungu la kumi kuwapa masikini, ndiyo maana kila ijumaa au sikukuu za idi, panapatikana sadaka (misaada) misikitini kwa masikini na mafukara. wema kama huu umeuona kwenye kanisa gani? naomba niishie hapa, lakini unisamehe kama nimekukwaza
 
Mwenyezi Mungu awabariki Waislamu wote, Misikiti yote na Vyuo vyenu kwa kutoa Bure kabisa na kwa Gharama Ndogo Huduma ya Maji kwa Wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Kwa Taasisi za Kikristo naomba GENTAMYCINE ninyamaze tu huku nikiwa na Maumivu yangu kwani kuna mahala Kanisa lina Matenki ya Maji Matano na Visima Viwili ila hakuna hata Mtu anayeambiwa akachote Maji sana sana GENTAMYCINE nimeona tu Nguo za Wanaotupigisha Magoti Kimakusudi kila Jumapili zikifuliwa huku Walinzi wakimwagiana Maji kwa Mmoja wao Kusheherekea Birthday yake huku akiwa ni Masikini wa Kutukuka kama GENTAMYCINE Mimi.

Waislamu Tanzania Asanteni, Mbarikiwe zaidi na sina Deni nanyi. Ndiyo maana nimeapa kuwa nikija Kuoa nitaoa Mwanamke wa Kiislamu na ikiwezekana hata GENTAMYCINE kutakiwa kuwa Muislamu nitafanya hivyo tena haraka mno kwa Kuitwa ama Mohamed GENTAMYCINE au Suleiman GENTAMYCINE kutokana na Roho Nzuri na ya Utu niliyoiona kwa Waislamu wengi tofauti na kwa Wakristo wenzangu.
Insha'Allah Mola akufanyia Tawakal uingie kwenye uislamu. Ila uislamu ni dini ya haki na ukweli. Ukiingia kwenye uislamu uache kujidanganya kwamba unaishi dar wakati unaishi Bunda mjini
 
Back
Top Bottom