Starehe ya ubongo wangu na kilevi Cha kwanza ni kusoma.cha pili ni kulakula
Cha tatu movie na mziki.vingine vitafuatia.
Mie Niko addicted na kusoma tangu Niko mdogo hata kabla sijaanza shule.hata kabla sijaanza chekechea tayari najua kusoma na kumultiply,kujumlisha.kuna muda nlikuwa nasoma kitabu chote Kisha nangojea ufafanuzi tu darasani.imagine mwalimu anasema haya Fulani nyanyuka utusonee hadithi sijui ya pwagu na pwaguzi,mie nakaa pembeni Kila aya tayari nshaisoma ipo kichwani.
Turudi Sasa kwenye kusoma mie sijui ndio nimeumbwa,ubongo wangu hauchoki,ukichoka basi nasinzia.
Tangu Niko mdogo biblia naijua kuanzia mwanzo mpaka ufunuo namaliza. Magazeti ya kiu,the guardian,mwananchi,nipashe,sani.nasoma kuanzia ukurasa wa mbele mpaka mwisho.
Majarida ya FEMA yote nimesoma.na ndipo nlipopatia elimu ya ujana.yani ninyime chochote ila sio kitabu nlichokipenda,ninyime vyote ila sio gazeti.nlikuwa nkiboreka natafuta gazeti au kitabu,nkikukuta unasoma nakwambia kabisa ukimaliza naomba.nilikuwa nikitembea njiani naokota vipande vya magazeti nasoma huku natembea.ukinikuta nasoma Niko mbali hata ulimwengu wa nje sijui Nini kinaendelea.marafiki wa utotoni baba Yao alikua anafanya kazi ipp media,wanapewa magazeti Kila siku anarudi nayo.imagine natoka Naenda kwao kuchukua magazeti nasoma Kisha narudisha.majirani kule kwingine wanajua kabisa Abby anakuja kufata gazeti,ama akishasoma ananipa.
Ilifika kipindi nkipata pocket money nanunua magazeti njiani Kwa wale walikuwa wanauza kwenye meza.ni nadra kukuta kabinti kadogo miaka Ile kunanunua gazeti zaidi wazee na wafanyakazi.
Nlipopata kuingia kwenye zama zingine za tech nikaacha taratibu magazeti na vitabu hardcopy na kuhamia huku.
Huo ulevi ndio ulinifanya niijue jamiiforums tangu 2015 na tagu niingiie humu nikaona ni eneo mojawapo sahihi Kwa ulevi wangu..kusoma!
Mie bila kusoma Kwa siku ni kama Teja wa visungura au madawa akikosa ndio ubongo wangu unakuwa hivyo.
Simu ikiharibika huwa napata tabu sana.kama nlitaka siku isonge nikae karibu na rundo la vitabu.
Ilifika wakati watu nliokuwa naishi nao wananishangaa.niko tofauti na wengi.
kati ya zawadi niletee gazeti au kitabu au jarida nafurahi mno
Je hii ni kawaida?