Ndg mshana jr;
Tahadhari yako nimeifurahia sana, ila unapowaambia watu kuwa wajihadhari na hao wanaojiita manabii sijakuelewa. Ina maana kuwa tusiwakubali tena hao manabii?? Tusipo wakubali manabii tuwaendee wanani?? Sitetei nabii yeyote kwani ninavyo amini mimi ni kwamba, kama kweli huyo ni mtumishi wa Mungu aliye hai, Mungu mwenyewe atamtetea tu. Mungu hatazuiwa na mshana jr au yeyote.
Sisemi kuwa manabii wote ni waongo, ila Neno la Mungu linasema; Kwa matunda yao, mtawatambua. Kwa maneno mengine ni kuwa, tunaweza kuwatofautisha tu kwa matunda yao. Mungu wetu hadhihakiwi, hivyo hawezi kumdhihaki mtu yeyote. Yaani mama amemwomba mtoto, tena kwa uchungu mwingi, miaka 38, halafu Mungu wetu ambaye tunajua jina lake ni UPENDO. amdhihaki, abebe mimba miezi 9 halafu aje kujifungua hizo sura ulizoweka kwenye picha zako. HAPANA. Nasema, haitotokea kamwe.
Kama umemwendea nabii wa kweli, atamwomba Mungu kwa uchungu naye Mungu atakupa mtoto. Ombeni watoto kwa manabii wa kweli. Ishara; Nabii wa kweli hataomba fedha wala zawadi yeyote kwako. Ameambiwa kuwa, ulipewa bure, toa bure. Nimpe pesa kwani yeye ndiye ananipa huyo mtoto??
Mganga, wa kienyeji, hana uwezo wowote wa kukupa mtoto. Akikupa, labda mama ulilala naye na mbegu yake ikarutubisha yai lako. Akikupa mtoto kwa dawa, umempata huyo mshana jr aliyekuambia. Muogope huyo mganga kwani anauwezo na huyo mtoto kwani ni wake sio wako. Akimtaka saa yeyote kama hukutimiza sharti lake anamtwaa. Ni wake maisha yote.
Tahadhari yako nimeifurahia sana, ila unapowaambia watu kuwa wajihadhari na hao wanaojiita manabii sijakuelewa. Ina maana kuwa tusiwakubali tena hao manabii?? Tusipo wakubali manabii tuwaendee wanani?? Sitetei nabii yeyote kwani ninavyo amini mimi ni kwamba, kama kweli huyo ni mtumishi wa Mungu aliye hai, Mungu mwenyewe atamtetea tu. Mungu hatazuiwa na mshana jr au yeyote.
Sisemi kuwa manabii wote ni waongo, ila Neno la Mungu linasema; Kwa matunda yao, mtawatambua. Kwa maneno mengine ni kuwa, tunaweza kuwatofautisha tu kwa matunda yao. Mungu wetu hadhihakiwi, hivyo hawezi kumdhihaki mtu yeyote. Yaani mama amemwomba mtoto, tena kwa uchungu mwingi, miaka 38, halafu Mungu wetu ambaye tunajua jina lake ni UPENDO. amdhihaki, abebe mimba miezi 9 halafu aje kujifungua hizo sura ulizoweka kwenye picha zako. HAPANA. Nasema, haitotokea kamwe.
Kama umemwendea nabii wa kweli, atamwomba Mungu kwa uchungu naye Mungu atakupa mtoto. Ombeni watoto kwa manabii wa kweli. Ishara; Nabii wa kweli hataomba fedha wala zawadi yeyote kwako. Ameambiwa kuwa, ulipewa bure, toa bure. Nimpe pesa kwani yeye ndiye ananipa huyo mtoto??
Mganga, wa kienyeji, hana uwezo wowote wa kukupa mtoto. Akikupa, labda mama ulilala naye na mbegu yake ikarutubisha yai lako. Akikupa mtoto kwa dawa, umempata huyo mshana jr aliyekuambia. Muogope huyo mganga kwani anauwezo na huyo mtoto kwani ni wake sio wako. Akimtaka saa yeyote kama hukutimiza sharti lake anamtwaa. Ni wake maisha yote.