Tamaa, Usaliti na Matokeo Yake Wanaume na Wanawake Wengi Wanaharibu Familia Zao Wenyewe

Tamaa, Usaliti na Matokeo Yake Wanaume na Wanawake Wengi Wanaharibu Familia Zao Wenyewe

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
13,386
Reaction score
30,687
Kuna wanaume Mungu kawajalia familia nzuri sana mke mwema, anayejitunza, anayeheshimu ndoa yake, anayekutii na kusimama kwenye nafasi yake kama mke.

Pengine amekuzalia watoto na amekuwa nawe kipindi kigumu na chepesi.

Lakini kutokana na tamaa, unaanza kuchezea amani ya familia yako mwenyewe.
Unaingia kwenye umalaya wa wazi wazi bila hata kujificha, ukiwa na ego kubwa kwamba hakuna atakayekufanya chochote

Sasa hapo mwanamke kakufanyia nini mpaka umtendee hivyo?

Tatizo kubwa si tu kucheat
Tatizo ni dharau, maudhi na mabadiliko ya tabia baada ya kupata (nyama mpya)huko nje

Na unataka mke aendee kukuheshimu kama zamani wakati wewe mwenyewe umebadilika
Heshima haiji yenyewe, heshima inatengenezwa

Kama zamani ulikuwa unaheshimiwa, basi jiulize: nini kimebadilika?

Kwa nini leo unaonekana wa kawaida tu machoni mwa mke wako?
Huenda ni tabia zako mpya dharau, ukali, kiburi na kutothamini familia


Lakini pia nisieleweke vibaya sizungumzii wanawake wenye tabia mbaya, wenye matusi, visirani na gubu kupitiliza Hapana

. Nazungumzia mwanamke mwema ambaye anajitahidi kuijenga familia lakini bado anatendewa vibaya.
Wanasema mshahara wa dhambi ni mauti.

Na kuna kisa nilikishuhudia karibu kabisa kwenye familia
Kuna dada mmoja alikuwa na maisha ya kudanga sana Akapata mimba ya kwanza, mwanaume akamkimbia na kumuachia mtoto
Hakutulia, akapata mimba ya pili, akaolewa haraka haraka kuficha aibu ya ujauzito, lakini ndoa nayo haikudumu akaachika akiwa na mtoto mwingine
.
Bado hakutulia.
Akabeba mimba ya tatu. Siku moja akaja kwangu baada ya swala ya Magharibi. Akanambia:
Mdogo wangu, nimejifunga
Lakini hakuwa na furaha hata kidogo. Nilipomuuliza kulikoni, akasema hajui mimba ni ya nani kwa sababu alikuwa ametembea na wanaume wawili kwa nyakati zinazokaribiana

Tulivyohesabu tarehe, ikaonekana wazi mimba ni ya kijana mmoja wa kawaida anayejitafuta. Lakini yeye alitaka mimba ihesabike kwa mwanaume mwingine mume wa mtu mwenye pesa

Bahati mbaya kwake, yule mwanaume mwenye pesa alikataa na hata akatoa pesa mimba itolewe

Mimba haikutolewa
Mwisho wa siku yule kijana wa kawaida akaambiwa ndiyo mwenye ujauzito na akakubali

Lakini baadaye wakaja kuachana.
Cha kushangaza zaidi, mimba ile ile ikapewa mwanaume mwingine 🙌

ambaye hata hakuhusika kabisa kwenye huo mchezo
Na kwa sababu ya upendo au ujinga, akaikubali mpaka akaanza kuhangaika na majukumu ya mtoto ambaye si wake

Leo hii huyo mwanaume amemuoa kabisa last kama mke wa pili

Nilipomuangalia siku ya harusi nilihuzunika sana
Nikajiuliza
Kama huyu mwanaume angeweza kutuliza tamaa zake na kuwa makini, angejikuta kwenye hali hii kweli?

Kwa sababu wakati mwingine tamaa na uzembe vinaweza kukufanya ubebe majukumu ambayo si yako, huku ukiwaumiza watoto au familia yako halisi

Swali langu kwa wanaume ni hili:
Una uhakika huyo mtoto unayemhudumia ni wako?
Pima hata DNA 🤪

Na kabla hamjaharibu familia zenu kwa tamaa za nje, kumbukeni kuwa amani ya nyumba hujengwa kwa uaminifu, heshima na kujitambua si kwa starehe za muda mfupi

ShesRise_1 👋
 
Screenshot_20251007-195716~2.jpg
 
Kwa ninavyojua mwanamke ana uwezo mkubwa wakuamua apate mimba au asipate kama ana akili timamu , ila huyo mpaka mmekaa chini na kuhesabu ina onekana ni goigoi sana ndio maana analalwa na wanaume kibao mpaka asijue mimba ni ya nani.


Naunga hoja zako mkono .
 
Kuna wanaume Mungu kawajalia familia nzuri sana mke mwema, anayejitunza, anayeheshimu ndoa yake, anayekutii na kusimama kwenye nafasi yake kama mke.

Pengine amekuzalia watoto na amekuwa nawe kipindi kigumu na chepesi.

Lakini kutokana na tamaa, unaanza kuchezea amani ya familia yako mwenyewe.
Unaingia kwenye umalaya wa wazi wazi bila hata kujificha, ukiwa na ego kubwa kwamba hakuna atakayekufanya chochote

Sasa hapo mwanamke kakufanyia nini mpaka umtendee hivyo?

Tatizo kubwa si tu kucheat
Tatizo ni dharau, maudhi na mabadiliko ya tabia baada ya kupata (nyama mpya)huko nje

Na unataka mke aendee kukuheshimu kama zamani wakati wewe mwenyewe umebadilika
Heshima haiji yenyewe, heshima inatengenezwa

Kama zamani ulikuwa unaheshimiwa, basi jiulize: nini kimebadilika?

Kwa nini leo unaonekana wa kawaida tu machoni mwa mke wako?
Huenda ni tabia zako mpya dharau, ukali, kiburi na kutothamini familia


Lakini pia nisieleweke vibaya sizungumzii wanawake wenye tabia mbaya, wenye matusi, visirani na gubu kupitiliza Hapana

. Nazungumzia mwanamke mwema ambaye anajitahidi kuijenga familia lakini bado anatendewa vibaya.
Wanasema mshahara wa dhambi ni mauti.

Na kuna kisa nilikishuhudia karibu kabisa kwenye familia
Kuna dada mmoja alikuwa na maisha ya kudanga sana Akapata mimba ya kwanza, mwanaume akamkimbia na kumuachia mtoto
Hakutulia, akapata mimba ya pili, akaolewa haraka haraka kuficha aibu ya ujauzito, lakini ndoa nayo haikudumu akaachika akiwa na mtoto mwingine
.
Bado hakutulia.
Akabeba mimba ya tatu. Siku moja akaja kwangu baada ya swala ya Magharibi. Akanambia:
Mdogo wangu, nimejifunga
Lakini hakuwa na furaha hata kidogo. Nilipomuuliza kulikoni, akasema hajui mimba ni ya nani kwa sababu alikuwa ametembea na wanaume wawili kwa nyakati zinazokaribiana

Tulivyohesabu tarehe, ikaonekana wazi mimba ni ya kijana mmoja wa kawaida anayejitafuta. Lakini yeye alitaka mimba ihesabike kwa mwanaume mwingine mume wa mtu mwenye pesa

Bahati mbaya kwake, yule mwanaume mwenye pesa alikataa na hata akatoa pesa mimba itolewe

Mimba haikutolewa
Mwisho wa siku yule kijana wa kawaida akaambiwa ndiyo mwenye ujauzito na akakubali

Lakini baadaye wakaja kuachana.
Cha kushangaza zaidi, mimba ile ile ikapewa mwanaume mwingine 🙌

ambaye hata hakuhusika kabisa kwenye huo mchezo
Na kwa sababu ya upendo au ujinga, akaikubali mpaka akaanza kuhangaika na majukumu ya mtoto ambaye si wake

Leo hii huyo mwanaume amemuoa kabisa last kama mke wa pili

Nilipomuangalia siku ya harusi nilihuzunika sana
Nikajiuliza
Kama huyu mwanaume angeweza kutuliza tamaa zake na kuwa makini, angejikuta kwenye hali hii kweli?

Kwa sababu wakati mwingine tamaa na uzembe vinaweza kukufanya ubebe majukumu ambayo si yako, huku ukiwaumiza watoto au familia yako halisi

Swali langu kwa wanaume ni hili:
Una uhakika huyo mtoto unayemhudumia ni wako?
Pima hata DNA 🤪

Na kabla hamjaharibu familia zenu kwa tamaa za nje, kumbukeni kuwa amani ya nyumba hujengwa kwa uaminifu, heshima na kujitambua si kwa starehe za muda mfupi

ShesRise_1 👋
Mara nyingi washamba wa uchi ndio huangushiwa jumba bovu.
Mhaini Hi😎
 
Ndoa nyingi matatizo yake makuu;

1. Kutokufanana.
Unaoa au kuolewa na mtu ambaye hamfanani kifikra, kimaono, kimaadili, kimaumbike n.k

2. Wanawake kuolewa kama Ajira, nitoke vipi
Ni wanawake wachache wameolewa na wanaume wa ndoto zao. Hilo linapelekea matatizo ya ndoa

3. Matarajio ya wanawake na tamaa ya mafanikio.
Wanawake wengi huolewa wakiwa na matarajio kwamba maisha yatabadilika kwa haraka. Wengi sio wavumilivu.
Mwanaume anamtia moyo mke wake kuwa mambo yatabadilika na kuwa mazuri.
Mwanamke kutwa kulalamika kwamba mumewe mzembe, anamuona Hana jitihada.

Mwanaume anachoka, na anaamua kupata tulizo la moyo nje au kuwa chapombe.

4. Wanawake kujizira na kuwa wachafu.
Kulakula hovyo na kunenepeana hovyo.
Kutovaa nguo za mvuto.
Unakuta mwanamke wa miaka 30 kama Mzee vile.
Wanaume hatupendi wanawake waliojichokea, wasiojijali

Wengi wanasingizia uzazi.
Lakini mimi nawajua wadada wanawatoto mpaka wanne lakini wanavutia balaa.
Mazoezi hutaki kufanya, unakulakula hovyo unadhani sifa.

Haya usafi zero. Hapana

5. Hakuna kusema umemzalia mwanaume.
Mtoto huyo NI wenu wote. Hakuna uliyemzalia. Ni wako pia.

Wanawake wengi hufikiri kuzaa na mwanaume kunamuongezea pointi fulani. Nope! Kila mwanamke unayemuona barabarani anauwezo wa kuzaa na mwanaume wako. Tena wako wanawake wenye uwezo wa kuzaa mpaka mapacha.

Kuzaa ni jukumu lenu wote.
Kauli ya kusema nimemzalia ni kauli ya vita vya kisaikolojia ambavyo wanawake wengi huitumia kumfanya mwanaume asiyejielewa ajione ana msalaba, deni kwa mwanamke.

6. Kuhusu Tamaa,
Wanawake pia wanatamaa. Tena Siku hizi wanawake wanatamaa zaidi kuliko wanaume.

Ukitaka upime hilo,
Ipitishwe kampeni ya Kila Kaya DNA ni lazima. Kisha tusubiri matokeo. Utagundua kuwa kusema wanaume pekee wanatamaa ni mbinu tuu za kimedani wanawake wanazitumia.

Ukweli ni kuwa Wote(mwanamke na mwanaume) wanatamaa.

Na nikikusaidia tuu.
Kwa sasa ni ngumu kumkuta Mwanaume mwenye wanawake kuanzia wawili.
Ila ni rahisi kukuta wanawake wenye wanaume zaidi ya watatu tena wengine mpaka watano.

Ndoa ni kwaajili ya watu waaminifu wenye kupendana
 
Kwa ninavyojua mwanamke ana uwezo mkubwa wakuamua apate mimba au asipate kama ana akili timamu , ila huyo mpaka mmekaa chini na kuhesabu ina onekana ni goigoi sana ndio maana analalwa na wanaume kibao mpaka asijue mimba ni ya nani.


Naunga hoja zako mkono .
Inaonekana ni goi goi👊
Asante kwa kuunga hoja
 
Back
Top Bottom