Mimba za kuzimu

Mimba za kuzimu

Jihadhari za mimba na mimba za kutafuta kwa manabii na waganga wa kienyeji.

Jaribu kufuatilia hizo mimba mpaka mwisho wake au kama watoto walizaliwa salama na kama wako hai mpaka leo hii na kama tabia zao ni za kawaida
Nimeshuhudia mara nyingi matangazo kwenye tv magazeti na radii hao wanaojiita manabii mitume na waganga wakijinasibu kuwa wamewasaidia akina mama wengi kupata ujauzito na hatimaye kujifungua watoto.

Lakini kamwe hatujawahi kuletewa mrejesho wa wale watoto maendeleo yao....kiukweli ni kwamba wengi walikufa au kupotea katika mazingira ya ajabu mno..hawa si watoto halisi.

Kujiepusha na maumivu haya nendeni hospital kapimeni wote ijulikane tatizo liko wapi au tatizo ni la nani halafu tiba yake ninini! Kama hakuna shida kila kitu kiko sawa lakini mimba hazishiki mwombeni Mungu atawajaalia mtoto wa haki...!

Msijaribu kwingineko haitawalipa.
Mshana nakuelewa sana bro ......... Napenda sana post zako
 
Enyi kizazi cha Nyoka... Yesu aliwaita baadhi ya watu hivyo... na yasemekana Cain alikuwa ni mzaliwa wa Nyoka na aliendeleza uzao wake hadi leo hii upo... kipindi cha Yesu aliwaita kabisa kwa mdomo wake... Mtoto wake alikuwa ni Abel naye alidanja
 
Akhsante mkuu
Unayosema ni mambo makubwa sana na jamii inaangamia pasipo kujua kwamba milki za giza zipo kazini, watazameni kwa macho mawili watoto wanaozaliwa na miujiza......nasisitiza watazameni na ukuaji wao!
Nikirudi kwa viongozi wa dini wanaopotosha kama ulivyoeleza...ni hakika.....kipindi kirefu kilichopita walinitembelea viongozi fulani wa dini fulani na kuniambia kuwa ili waaminike katika ibada inatakiwa kipawa hivyo niwasaidie.
Niliingia kwa wakuu na nifanya maagano kwa niaba ya viongozi wale wa dini na nikawapatia jinn mmoja wa kuogofya na mwenye nguvu na ubabe hata kwa majini wenzake, nikawapatia watu wale na kwenda kuongoza ibada kama kawaida......ila kila walipokuwa wakiombea watu jinn yule ndiye aliyekuwa akijibu maombi na sio Mungu.

KIVIPI?
Wenye mapepo walianguka wenyewe kwa kumuogopa jinn yule wa kifalme, vifungo vya kichawi alivifungua yeye, majini wabaya wa waumini walikimbia wenyewe kwa kumuogopa huyo bwana na nyumba ya ibada ikasifika kiasi kwamba wale viongozi wakanawiri.
Je, ni haki? Mungu anapenda kuona nafasi yake inafanyiwa dhihaka?
Niishie hapa.
Sasa apo nieleweshe vizur inakuwaje mtu anasema kwajina la yesu na kuombea kumbe anatumia jini
Uku navojua mapepo na ata ibilisi akitajiwa jina la yesu anashindwa kuzur.
 
Mada namna hii ni nzuri maana naishi ndani ya yanazungumzwa na nayajua......binafsi kuna dada mmoja wa miaka kama 37 hivi ambae hakuwahi kushika mimba tangu kuvunja ungo kwake.
Alinifuata kuhitaji msaada wangu maana ameshapoteza matumaini na tiba za kizungu hazionyeshi manufaa kwake, nikafanya nnachokijua akashika mimba na kujifungua (japo alijifungua kwa tabu mpaka nikatuma nguvu za ziada)
Jana amenitembelea akiwa na furaha kuu na yeye kuwa na mtoto na alikuwa mtoto ameshafikisha siku arobaini.
Narudi kwenye mada.....nayajua maagano yake na roho zinazomuandama yule mtoto na mama......najua anahitaji ukaribu na mimi ili mambo yaendelee kuwa sawa......najua pindi mambo akiyaacha njiani kwa kunidharau kisa katimiza lengo lake nini kitampata......nk nk
Duh wewe jichawi ni kivumbi
 
Akhsante mkuu
Unayosema ni mambo makubwa sana na jamii inaangamia pasipo kujua kwamba milki za giza zipo kazini, watazameni kwa macho mawili watoto wanaozaliwa na miujiza......nasisitiza watazameni na ukuaji wao!
Nikirudi kwa viongozi wa dini wanaopotosha kama ulivyoeleza...ni hakika.....kipindi kirefu kilichopita walinitembelea viongozi fulani wa dini fulani na kuniambia kuwa ili waaminike katika ibada inatakiwa kipawa hivyo niwasaidie.
Niliingia kwa wakuu na nifanya maagano kwa niaba ya viongozi wale wa dini na nikawapatia jinn mmoja wa kuogofya na mwenye nguvu na ubabe hata kwa majini wenzake, nikawapatia watu wale na kwenda kuongoza ibada kama kawaida......ila kila walipokuwa wakiombea watu jinn yule ndiye aliyekuwa akijibu maombi na sio Mungu.

KIVIPI?
Wenye mapepo walianguka wenyewe kwa kumuogopa jinn yule wa kifalme, vifungo vya kichawi alivifungua yeye, majini wabaya wa waumini walikimbia wenyewe kwa kumuogopa huyo bwana na nyumba ya ibada ikasifika kiasi kwamba wale viongozi wakanawiri.
Je, ni haki? Mungu anapenda kuona nafasi yake inafanyiwa dhihaka?
Niishie hapa.
Jichawi ni njni ushauri wako katika hili? Tufanyeje? It is becoming complicated really. Je tusali vipi na wapi?
 
Na ndio maana tuliaswa kwa uwazi kabisa kuhusu manabii wa siku za mwisho kuwa watakuwa na uwezo hata wa kuhamisha milima na kufufua watu lakini .TUSIWAAMINI HAO.
Mshana. Tufanyeje sasa? Kule roman catholic tunaambiwa hawaneni kwa neno hivyo hawawezi kupambana na nguvu za giza. Hawa kina gwajima dizaini ndo mnasema hivyo. Tusalije na wapi sasa? Au chumbani tu peke yangu ndio mpango mzima?
 
Jihadhari za mimba na mimba za kutafuta kwa manabii na waganga wa kienyeji.

Jaribu kufuatilia hizo mimba mpaka mwisho wake au kama watoto walizaliwa salama na kama wako hai mpaka leo hii na kama tabia zao ni za kawaida
Nimeshuhudia mara nyingi matangazo kwenye tv magazeti na radii hao wanaojiita manabii mitume na waganga wakijinasibu kuwa wamewasaidia akina mama wengi kupata ujauzito na hatimaye kujifungua watoto.

Lakini kamwe hatujawahi kuletewa mrejesho wa wale watoto maendeleo yao....kiukweli ni kwamba wengi walikufa au kupotea katika mazingira ya ajabu mno..hawa si watoto halisi.

Kujiepusha na maumivu haya nendeni hospital kapimeni wote ijulikane tatizo liko wapi au tatizo ni la nani halafu tiba yake ninini! Kama hakuna shida kila kitu kiko sawa lakini mimba hazishiki mwombeni Mungu atawajaalia mtoto wa haki...!

Msijaribu kwingineko haitawalipa.
Asante kwa some hili, nimejifunza mengi sana mkuu
 
Naamini wewe ni mganga wa kienyeji,mtume au nabii,ingawa kiuhalisia mko kwenye chungu kimoja.Mimi binafsi naomba kujua,hivi ulifanya fanyaje mpaka huyo dada akapata mimba ya kuzimu?Tafadhali tufahamishe.
Mada namna hii ni nzuri maana naishi ndani ya yanazungumzwa na nayajua......binafsi kuna dada mmoja wa miaka kama 37 hivi ambae hakuwahi kushika mimba tangu kuvunja ungo kwake.
Alinifuata kuhitaji msaada wangu maana ameshapoteza matumaini na tiba za kizungu hazionyeshi manufaa kwake, nikafanya nnachokijua akashika mimba na kujifungua (japo alijifungua kwa tabu mpaka nikatuma nguvu za ziada)
Jana amenitembelea akiwa na furaha kuu na yeye kuwa na mtoto na alikuwa mtoto ameshafikisha siku arobaini.
Narudi kwenye mada.....nayajua maagano yake na roho zinazomuandama yule mtoto na mama......najua anahitaji ukaribu na mimi ili mambo yaendelee kuwa sawa......najua pindi mambo akiyaacha njiani kwa kunidharau kisa katimiza lengo lake nini kitampata......nk nk
 
Mkuu jichawi kuna sehem umezungumzia juu ya jinn mkubwa mwenye kuogopewa na wenziwe......kwani wanatofautiana? Na je, kama wewe unapotaka kumfuga jini wa namna hiyo unampata wapi na unamuhifadhi wapi na chakula unampa kipi?
Ni katika kubadilishana Elimu mkuu usione tabu
 
Sheitwani hajui kuumba kabisa,hapa naona kina SINUNA.com.....
Swala la kuumba ni uwezo wa Kimungu na hapa hakuna sehemu yeyote palipoandikwa anaumba, kuwa makini hapa unazungumza na watu wenye fani zao kama ilivyo fani nyingine, ukiniambia kwenye injini ya ndege kuna kitu chaitwa jina fulani siwezi kukubishia maana sina elimu hiyo, hivyo naweza tu kukuuliza na sio kubisha kwamba hakipo wakati sijawahi shika hata spana.
Ufafanuzi; jinn ana miujiza hivyo anaweza fanya miujiza ili wewe umuamini na kumuacha Mungu wako.
Je, umesahau uweza wa jinn? Rejea kitabu pale ibilisi alipompaisha Yesu mpaka juu ya mlima na kumwambia amuabudu na kumuonyesha milki za dunia kuwa atampa, umeona nguvu ya shetani? Ikiwa yeye aliyetakaswa yamemkuta hayo sembuse sisi? Ikiwa yeye alibebwa na kupaishwa je, hawa wanaovaa suti na kusema shetani toka ndio bora? Tulia Mkuu uijue dunia
 
Ujumbe murua kwa wanao mkufuru Mungu kwani kwa kila jambo unapaswa kumwona Mungu akusaidie sasa unakuta kila kukicha dada zetu miguu na njia kwa waganga, huko akiambia nipe p.... au t... GO hawezi kataa mwisho wa siku wanaambulia magonjwa nk
 
Back
Top Bottom