Mimba za kuzimu

Mimba za kuzimu

.

Jr
 
Mada namna hii ni nzuri maana naishi ndani ya yanazungumzwa na nayajua......binafsi kuna dada mmoja wa miaka kama 37 hivi ambae hakuwahi kushika mimba tangu kuvunja ungo kwake.
Alinifuata kuhitaji msaada wangu maana ameshapoteza matumaini na tiba za kizungu hazionyeshi manufaa kwake, nikafanya nnachokijua akashika mimba na kujifungua (japo alijifungua kwa tabu mpaka nikatuma nguvu za ziada)
Jana amenitembelea akiwa na furaha kuu na yeye kuwa na mtoto na alikuwa mtoto ameshafikisha siku arobaini.
Narudi kwenye mada.....nayajua maagano yake na roho zinazomuandama yule mtoto na mama......najua anahitaji ukaribu na mimi ili mambo yaendelee kuwa sawa......najua pindi mambo akiyaacha njiani kwa kunidharau kisa katimiza lengo lake nini kitampata......nk nk
Mwenyezi Mungu atusaidie kwakweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jihadhari za mimba na mimba za kutafuta kwa manabii na waganga wa kienyeji.

Jaribu kufuatilia hizo mimba mpaka mwisho wake au kama watoto walizaliwa salama na kama wako hai mpaka leo hii na kama tabia zao ni za kawaida
Nimeshuhudia mara nyingi matangazo kwenye tv magazeti na radii hao wanaojiita manabii mitume na waganga wakijinasibu kuwa wamewasaidia akina mama wengi kupata ujauzito na hatimaye kujifungua watoto.

Lakini kamwe hatujawahi kuletewa mrejesho wa wale watoto maendeleo yao....kiukweli ni kwamba wengi walikufa au kupotea katika mazingira ya ajabu mno..hawa si watoto halisi.

Kujiepusha na maumivu haya nendeni hospital kapimeni wote ijulikane tatizo liko wapi au tatizo ni la nani halafu tiba yake ninini! Kama hakuna shida kila kitu kiko sawa lakini mimba hazishiki mwombeni Mungu atawajaalia mtoto wa haki...!

Msijaribu kwingineko haitawalipa.
Asante Jr.ila ungefunguka maana inaelekea kuna kamfano unako live

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingawa umeandika mengi na maswali kumuuliza Mshana Jr mimi nataka nikwambie jambo 1 kuhusu hawa wahuni wanaopenda kujiita Manabii hawa ni matapeli wakawaida kabisa....sasa kumetokea huo ujinga has a wanawake wanaibiwa sana wengi wao badala yakwenda kwa Waganga wanajificha kwenye KOTI la kutabiriwa hii ni style ya uaGUZI....Ninachofahamu khs Huduma ya unabii nikwamba NABII kabla hajajakukuambia kwamba MUNGU amenionyesha kitu flan kwako kitatokea nini kawaida anaanza MUNGU mwenyewe kukuonyesha the NABII akija kukwambia nikama cornfimation tu lkn watu wengi hawajui hii mambo
Umemaliza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
 
Jihadhari za mimba na mimba za kutafuta kwa manabii na waganga wa kienyeji.

Jaribu kufuatilia hizo mimba mpaka mwisho wake au kama watoto walizaliwa salama na kama wako hai mpaka leo hii na kama tabia zao ni za kawaida
Nimeshuhudia mara nyingi matangazo kwenye tv magazeti na radii hao wanaojiita manabii mitume na waganga wakijinasibu kuwa wamewasaidia akina mama wengi kupata ujauzito na hatimaye kujifungua watoto.

Lakini kamwe hatujawahi kuletewa mrejesho wa wale watoto maendeleo yao....kiukweli ni kwamba wengi walikufa au kupotea katika mazingira ya ajabu mno..hawa si watoto halisi.

Kujiepusha na maumivu haya nendeni hospital kapimeni wote ijulikane tatizo liko wapi au tatizo ni la nani halafu tiba yake ninini! Kama hakuna shida kila kitu kiko sawa lakini mimba hazishiki mwombeni Mungu atawajaalia mtoto wa haki...!

Msijaribu kwingineko haitawalipa.
Kuna waganga ambao product ya kazi zao ni mtu kuzaa albino. Umewahi kusikia hili?
 
Dah! Ila mshana jr sipati picha ulivyojichanachana chale, hivi nyumban kwako unasali? Au kwamfano kikatokea kitu chochote ktk mazingira ya kutatanisha hapo si unashinda unatwanga mitishamba?

Unajua nmekumbuka kipind nasoma kuna chumba nilikuwa nakaa sasa alikuja jamaa yangu mmoja kuomba hifadhi kwakuwa nyumban kwao walikuwa na migogoro yule jamaa alikuwa mshirikina hatari, yaan akiona hata mbwa kakatisha tu tayar anaanza kujipaka midawa yake, siku moja nipo kitandan napiga msuli bed nikashangaa nmemwagiwa maji hata mtu aliyenimwagia simuon na hakukuwa na mtu yeyote ndan halafu nikasikia sauti ikijisonya kutoka darini. Ikabidi nimwambie baba alimfukuza yule jamaa.
Mshana ana sifa zote za kuwa mzee wa kanisa.
 
Mmh.. Sijakupata vema hapa
Mganga mmoja huko Buguruni. Akina mama wengi waliomwendea walipata watoto lakini albino in almost the cases. Personally, namjua kijana mmoja mtu wa IT yupo mjini kwa wahindi baada ya kuhangaika mno aliishia huko na kupata albino
 
Mganga mmoja huko Buguruni. Akina mama wengi waliomwendea walipata watoto lakini albino in almost the cases. Personally, namjua kijana mmoja mtu wa IT yupo mjini kwa wahindi baada ya kuhangaika mno aliishia huko na kupata albino
Mmh.... Nitataka kufika kwake tafadhali... Naomba direction
 
Back
Top Bottom