Mikoa ambayo Wanawake wanafahamu kupika Chakula na mikoa mbayo wanawake hawafahamu kupika Chakula kizuri ni hii hapa...

hahahaha mchanyato wa ndizi na nyama mkuu

Ndio nafahamu lakini umeona eneo moja la mtori ambao wanavuruga ndizi ule uji wanaweka kwenye chupa ya chai ili usipoe halafu nyama wanakata finyango ndogo ndogo wanakuwekea kwenye bakuri, una maana wali wachaga hawafahamu kupika
 
Ndio nafahamu lakini umeona eneo moja la mtori ambao wanavuruga ndizi ule uji wanaweka kwenye chupa ya chai ili usipoe halafu nyama wanakata finyango ndogo ndogo wanakuwekea kwenye bakuri, una maana wali wachaga hawafahamu kupika


Hahahaa mm napenda pishi 1 tu la mtori..wali mpe msukuma..ila usimpe aunge mchuzi..
 
Wakuu.
Nimetembelea mikoa mbalimbali katika harakati za kusaka maisha lakini kama mnavofahamu mikoa mingi kuna tamaduni tofauti za mapishi
Kuna mikoa chakula unaweza kula ukaona ladha ya chakula japo ni kwa mama ntilie lakini chakula kitamu na mikoa mingine imejaa laana bin balaa yaani ukila chakula utahisi hadi kuugua homa ya manjano.
A: Mikoa Wanayojitahidi Kupika vizuri
1. Tanga
2. Pwani
3.Lindi
4. Mtwara
5.Dodoma
6. Morogoro
7. Mwanza
8. Kigoma maeneo ya Ujiji
9. Dar Es Salaam.
10. Tabora.
Ifuatayo ni Mikoa yenye laana bin balaa sijui hua wanaloweka au maana chakula asilimia kubwa hakina ladha kabisa.
B:Mikoa hiyo ni Kama Ifuatavo
1. Mara
2.Arusha
3.Manyara
4.Singida
5.Ruvuma
6. Rukwa
7. Katavi
8. Iringa
9. Mbeya
10.Njombe
11.Geita
12. Simiyu
13.Kagera/Bukoba
14. Kilimanjaro.
Huo ni utafiti mdogo kabisa sijui wanatatizo gani
Aisee mbona sisi ambao tumezaliwa, kukulia na kuoa kwenye hiyo mikoa ya list B tukipikiwa chakula huwa kitamu sana lakini mwisho wa yote kupika inategemea na mtu bila kujali katokea mkoa gani labda uwe na chuki na watu wa hiyo mikoa ndo unaweza usione kwamba wanapika vizuri
 
Unatakiwa ufahamu kuwa kila chakula kina asili yake so ni nadra sana mtu ambae aina fulani ya chakula sio asili yake aweze kukipika ipasavyo. Mfano matumizi ya nazi kuna mikoa mingine ukimwambia atumie nazi atakamua tui anamwaga machicha anapikia.
Ndizi hakuna mkoa utakupikia ndizi tamu zaidi ya Kagera,Kilimanjaro na Mbeya.
Biryani hakuna mtu atapika liwe tamu kama afanyavyo mtu wa pwani na jamii zake.
Matobolwa wasukuma.
Makande wapare.
Ugali watu wa kusini.
 
Huu utafiti uko very wrong kwa uzoefu wangu juu ya hii mikoa.

Pwani, Lindi na Mtwara haikupaswa kuwa pale ilipo.

Ruvuma, Singida, Manyara na Arusha halikadhalika imekosewa kuwekwa ilipo.

Unless mtoa mada umeongea tu kwa hisia.
 
Kwa Tanga sina ubishi,kama ndio umepakuliwa halafu umejifungia chumbani na hakuna mtu anakuona unaweza kujikuta unalamba na sahani...
Mkuu Singida na Manyara pande za Kondoa wale washenzi wanajua kupika bana! Tanga hawaoni ndani..
 
Unachotafta toka kwa wachaga utakipata japo umenena ukweli mtupu

Subiri wanakuja
Wachaga ni wapishi wazuri mno ndio maana mahotel makubwa wapishi wakuu ni wachaga,hata matamasha ta nyama choma wamiliki ni.wachaga
Kilimanjaro mapishi ndio kwenyewe ndizi ,nyama,mtori
 
Back
Top Bottom