Kwanini hadi leo makao makuu ya mikoa 18 bado kuunganishwa kwa barabara za lami? Je, ni umasikini, ukubwa wa nchi au ufisadi na kukosa akili?

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,042
49,727
Ifahamike kwamba Barabara ndio kichocheo kikubwa Cha Maendeleo ikifuatuwa na umeme.

Mwaka 2005 Serikali ilitangaza Bungeni Hadi kufikia 2020 ,Makao Makuu ya Mikoa yote Tanzania Yatakuwa Yameunganishwa na Barabara za Lami.

Hawakuishia hapo wakasema Barabara zote Kuu za Kuunganisha Nchi na Nchi jirani Zitakuwa na lami.

Lakini Hadi naandika Makala hii,kina Jumla ya Mikoa 21 ya Tanzania ambayo Bado haijaunganishwa Kwa Barabara za lami.

Kuna vipande vina lami na vumbi na Kuna vipande havina lami kabisa Toka mkoloni alivyozianzisha na Baadhi ya Barabara hazipitiki kabisa kipindi Cha mvua.

Nimekuwa najiuliza kama miaka zaidi ya 60 Bado tumeshindwa kuifungua Mikoa yetu Kwa lami,Sasa Wilaya tutazifungua lini? Je kama Taifa tunakwama wapi? Je hatuoni Kuna haja ya Kupitia Upya vipaombele vyetu?

Mikoa ifuatavyo Bado haijaungamishwa na Barabara za lami.Yaank ukitaka kuifikia lazima uzunguke kwingine ambapo ni time consuming,expensive and boring.
1.Mbeya-Singida
2.Mbeya-Tabora
3.Ruvuma-Morogoro
4.Ruvuma-Lindi
5.Morogoro-Lindi
6.Iringa-Singida
7.Tanga-Manyara
8.Arusha-Mara
9.Arusha-Simiyu
10.Njombe-Morogoro
11.Tabora-Kigoma
12.Songwe-Katavi
13.Tanga-Morogoro
14.Kigoma-Kagera/Geita
15.Singida-Simiyu
16.Iringa-Tabora
17.Kigoma-Katavi
18.Kilimanjaro-Manyara.
19.Mbeya-Katavi
20.Mtwara-Iringa
21.Iringa-Katavi.

Ushauri Wangu Kwa Serikali
Kama tunataka kutimiza lengo na Ufanisi wa Ujenzi wa Barabara na kufungua Uchumi wa watu Wetu basi tuzingatie yafuatayo;

1.Tujenga Barabara chache Kwa Vipaombele badala ya mtindo wa Sasa wa kutapanya Rasilimali kukidhi matakwa ya Kisiasa.
-Una Bajeti ya Bil.600 unaigawanya Kwa Barabara zote Nchi nzima ambako Barabara ya km 200 au 500 unaipa pesa bil 10-25 ambapo itakuchukua miaka zaidi ya 10 kuzimaliza.Lakini tungechagua Barabara za kipaombele chache na kuzipa Rasilimali Kila mwaka tungekuwa tunatoka na Barabara zilizokamiliaka na zinazozalisha.

2.Tubadili mtindo wa financing.
-Badala ya kusubiria makusanyo ya kudunduliza Kwa Wananchi wakiuza pamba na dengu,ni Bora Serikali itoe infrastructure bond ambazo Taasisi mbalimbali,makampuni na watu biabafsi watatoa pesa na pesa ya ujenzi kupatika.Unavyochelewa ujenzi ndivyo hata gharama zinaongezeka.

3.Tuwe na mifumo ya Kushirikisha Sekta binafsi kujenga Barabara
-Mfano badala ya kutegemea Serikali kuu Moja kwa Moja tunaweza tumia mifumo ya kushirikiana na sekta binafsi kwenye ujenzi kama Nchi zingine zinavyofanya.

4.Tuwezeshe Wakandarasi Wetu wa Ndani Badala ya kutegemea Wageni Kila kitu.
-Ukiwa na mkandarasi wako wa ndani Badala ya kimlipa Dola kama hao wa Nje tutawalipa Kwa Shilingi yetu hivyo kuokoa Fedha za kigeni na kuleta mzunguko wa pesa ndani ya Nchi.

5.Serikali Isiogope Kukopa Kwa Ajili ya Kuwekeza Kwenye Miundombinu.
-Huwa zinatoka ripoti hapa kwamba Tanzania ni Kati ya Nchi Zenye Madeni madogo.Unajiuliza nafasi ya kukopa unayo harafu unashangilia kutokopa wakati unaogelea kwenye umaskini,tumelalia uchumi Kwa sababu Nchi haifikii.Ni ujinga kushangilia umaskini.Tukope tuweke pesa kwenye Barabara, uzalishaji ukianza pesa zitarudishwa.
Screenshot_20240412-114625.jpg


My Take
Serikali ijitathmini na kujisahihisha.

Pia Soma Serikali kopeni pesa WB/IMF/AfDB mjenge barabara kutoka Mpanda-Iringa-Mtwara ili kuunganisha DRC na Bandari ya Mtwara
Screenshot_20240206-105613.jpg
 
Ifahamike kwamba Barabara ndio kichocheo kikubwa Cha Maendeleo ikifuatuwa na umeme.

Mwaka 2005 Serikali ilitangaza Bungeni Hadi kufikia 2020 ,Makao Makuu ya Mikoa yote Tanzania Yatakuwa Yameunganishwa na Barabara za Lami.

Hawakuishia hapo wakasema Barabara zote Kuu za Kuunganisha Nchi na Nchi jirani Zitakuwa na lami.

Lakini Hadi naandika Makala hii,kina Jumla ya Mikoa 18 ya Tanzania ambayo Bado haijaunganishwa Kwa Barabara za lami.

Kuna vipande vina lami na vumbi na Kuna vipande havina lami kabisa Toka mkoloni alivyozianzisha na Baadhi ya Barabara hazipitiki kabisa kipindi Cha mvua.

Nimekuwa najiuliza kama miaka zaidi ya 60 Bado tumeshindwa kuifungua Mikoa yetu Kwa lami,Sasa Wilaya tutazifungua lini? Je kama Taifa tunakwama wapi? Je hatuoni Kuna haja ya Kupitia Upya vipaombele vyetu?

Mikoa ifuatavyo Bado haijaungamishwa na Barabara za lami.Yaank ukitaka kuifikia lazima uzunguke kwingine ambapo ni time consuming,expensive and boring.
1.Mbeya-Singida
2.Mbeya-Tabora
3.Ruvuma-Morogoro
4.Ruvuma-Lindi
5.Morogoro-Lindi
6.Iringa-Singida
7.Tanga-Manyara
8.Arusha-Mara
9.Arusha-Simiyu/Shinyanga
10.Njombe-Morogoro
11.Tabora-Kigoma
12.Tabora-Kagera
13.Tanga-Morogoro
14.Rukwa-Katavi
15.Rukwa-Tabora
16.Iringa-Tabora
17.Kigoma-Katavi
18.Kilimanjaro-Manyara.

Ushauri Wangu Kwa Serikali
Kama tunataka kutimiza lengo na Ufanisi wa Ujenzi wa Barabara na kufungua Uchumi wa watu Wetu basi tuzingatie yafuatayo;

1.Tujenga Barabara chache Kwa Vipaombele badala ya mtindo wa Sasa wa kutapanya Rasilimali kukidhi matakwa ya Kisiasa.
-Una Bajeti ya Bil.600 unaigawanya Kwa Barabara zote Nchi nzima ambako Barabara ya km 200 au 500 unaipa pesa bil 10-25 ambapo itakuchukua miaka zaidi ya 10 kuzimaliza.Lakini tungechagua Barabara za kipaombele chache na kuzipa Rasilimali Kila mwaka tungekuwa tunatoka na Barabara zilizokamiliaka na zinazozalisha.

2.Tubadili mtindo wa financing.
-Badala ya kusubiria makusanyo ya kudunduliza Kwa Wananchi wakiuza pamba na dengu,ni Bora Serikali itoe infrastructure bond ambazo Taasisi mbalimbali,makampuni na watu biabafsi watatoa pesa na pesa ya ujenzi kupatika.Unavyochelewa ujenzi ndivyo hata gharama zinaongezeka.

3.Tuwe na mifumo ya Kushirikisha Sekta binafsi kujenga Barabara
-Mfano badala ya kutegemea Serikali kuu Moja kwa Moja tunaweza tumia mifumo ya kushirikiana na sekta binafsi kwenye ujenzi kama Nchi zingine zinavyofanya.

4.Tuwezeshe Wakandarasi Wetu wa Ndani Badala ya kutegemea Wageni Kila kitu.
-Ukiwa na mkandarasi wako wa ndani Badala ya kimlipa Dola kama hao wa Nje tutawalipa Kwa Shilingi yetu hivyo kuokoa Fedha za kigeni na kuleta mzunguko wa pesa ndani ya Nchi.

5.Serikali Isiogope Kukopa Kwa Ajili ya Kuwekeza Kwenye Miundombinu.
-Huwa zinatoka ripoti hapa kwamba Tanzania ni Kati ya Nchi Zenye Madeni madogo.Unajiuliza nafasi ya kukopa unayo harafu unashangilia kutokopa wakati unaogelea kwenye umaskini,tumelalia uchumi Kwa sababu Nchi haifikii.Ni ujinga kushangilia umaskini.Tukope tuweke pesa kwenye Barabara, uzalishaji ukianza pesa zitarudishwa.

My Take
Serikali ijitathmini na kujisahihisha.
barabara zinazunguka sana
mfano mtu anayetoka bariadi kwenda singida ,why azunguke tinde hadi nzega. why asipite meatu akatokea kiomboi na misigiri- hiyo barabara iwekwe lami
Kuna basi linatoka musoma kwenda arusha linazunguka shinyanga, singida manyara ndo liende arusha
kuna barabara ya vumbi karatu hadi bariadi na meatu . why isiwekwe lami
 
Umeshajiuliza barabara ya Mbeya - Singida direct itapita wapi? Na ikijengwa inakuwa umbali gani toka hii iliyopo sasa? USIKURUPUKE KUANDIKA. FIKIRI KWANZA.
Kwamba kutoka Mbeya direct to singida ni parefu kuliko kupitia huko Iringa na Dodoma ?
 

Attachments

  • Screenshot_20240206-122055.png
    Screenshot_20240206-122055.png
    117.9 KB · Views: 7
Kwamba kutoka Mbeya direct to singida ni parefu kuliko kupitia huko Iringa na Dodoma ?
Kwa akili zako fupi sana unadhani barabara zinajengwa kwa kuangalia tu hiyo ramani kama ulivyofanya? Umezingatia uwepo wa milima, game reserve, mito, mabwawa na maziwa? Ingekuwa hivyo basi barabara kwenda Kenya zingekatisha tu Mlima Kilimanjaro kwasababu nyuma yake ni Kenya.
 
barabara zinazunguka sana
mfano mtu anayetoka bariadi kwenda singida ,why azunguke tinde hadi nzega. why asipite meatu akatokea kiomboi na misigiri- hiyo barabara iwekwe lami
Kuna basi linatoka musoma kwenda arusha linazunguka shinyanga, singida manyara ndo liende arusha
kuna barabara ya vumbi karatu hadi bariadi na meatu . why isiwekwe lami
Ndio maana ya hoja yangu.Kwamba Mikoa Bado haijaunganishwa ndio maana tunazunguka na hii iantoka a na kujenga Barabara bila kipaombele.
 
Geography ya nchi

Ukubwa wa nchi, 945,087 km² sio mchezo


Miradi ya mikubwa na ya pesa nyingi kuishia Dar. Unashamgaa mara bilioni 600 kwa ajili ya mafuriko Dar, mara bilioni 500 kujenga Barabara na madaraja Dar, mara bilioni mia tisa kujenga mto msimbazi na jangwani, mara bilioni mia tisa nyingine kuboresha usafirishaji Dar. Dar inanyonya sana nchi. Ni basi tu watu hawajashtuka. Labda ndio maana jpm aliona serikali ihamia dodoma.
 
Back
Top Bottom