mwenzenu nafikiri Karamagi alipitiwa tu, sasa kwa vile hatuna utamaduni wa kuomba msamaha na kukubali kukosea ndio imebidi agangamale hivyo hivyo, kwani nani kati yetu hakosei? tuachane na mambo haya na tusonge mbele.
asanteni
Kwanza kabisa heshima yako Bi.Senti 50.
Nakumbuka kunawakati ulimtaka Mkjj aache harakati zake kwani kwa madai yako ni kuwa ange 'lauliwa', leo tena unakuja na hili, kwa kweli kabisa mimi nashindwa kukuelewa... Sasa nikuulize;
--Ditto alipiga risasi mtu... naye tumsamehe na kusonga mbele?!
--Mikataba mibovu viongozi walisaini kuhusiana na IPTL na Richmond... nayo tu samehe na tusonge mbele?!
--Majengo mapya ya BoT yako inflated ujenzi wake na utunzaji...tusamehe na tusonge mbele?!
--Mabarabara yana mahandaki...tusamehe na tusonge mbele?!
--Maji masafi hayapatikani....tusamehe na tusonge mbele?!
--n.k.
--n.k.
--Majambazi yanavamia mabenki/maduka...tuyasamehe na tusonge mbele?!
--Mikopo ya wanafunzi inaibiwa...tuwasamehe wezi na tusonge mbele?!
--Dala dala zinakatisha route... tuzisamehe na tusonge mbele?!
--Lecturer kapokea hongo... tumsamehe na tusonge mbele?!
--Wanamziki/mijibaba wanalaghai watoto wadogo wa shule...tuwasamehe na tusonge mbele?!
--n.k.
--n.k.
--Paka/mbwa wako kajisaidia chumbani mwako...msamehe na usonge mbele?!
--Jirani anatembea na mume/mke wako...msamehe na usonge mbele?!
--WAZIRI ANASADIKIKA KUFANYA MAKOSA YA KUINGIA MIKATABA...TUMFUNGIE ALIYESEMA HIVYO,TUMSAMEHE WAZIRI HUYO NA TUSONGE MBELE?!
--N.K.
--N.K.
Ndugu, hivi mwanzo wa kuwa ajibisha wafanyao makosa,kuwa lazimu kutambua makosa yao, kuwa kosoa, na kuwa lazimisha watubu hadharani makosa hayo na kuweka kikomo kwa makosa haya yanayo jirudia rudia mwaka nenda rudi, ni lini mawazoni kwako?! Huoni kuwa tumechoka na kusamehe na kusonga mbele gizani?! Matokeo yake ni kuambiwa kuwa chukueni hizo 30% za madini yenu tuliyachimbua ardhini kwenu nasi hii 70% ni yetu, tutawaachia hayo mashimo kuyafukia baada ya miaka 25 pale ndege yenu itakuwa inajaza mafuta Kiwalani tayari KUPAA!!
Kwanini viongozi wetu hawa adhibiwi?..Lini chanzo cha hili, wanao ua hawafungwi, wanao iba hawafungwi, hamna anayetubu makosa, kila kukicha tunaambiwa ni makosa yakiutendaji ya viongozi...ni wapi hawa kama hatu wakani hadharani na kuwaadhibu wanao ligharimu Taifa letu mabilioni baada ya kuingia bichwa bichwa kwenye wasiyo yajua na bila kuwa na subira?! Tusubiri mpaka lini kuona kiongozi wa Tanzania amefungwa?!
Je, viongozi wetu wamesahau kuwa kila kitu kina mwisho?! je wamesahau kuwa njia za mawasiliano na kimtandao kupitia radio,simu,television,internet zinabadilika na hawana uwezo wa kuzuia hili?!
Kwa kweli Bi.Senti 50 nakusihi uwaambie viongozi kuwa MWANZO WA MWISHO UMEANZA; KUTIMIZA AHADI NI WAJIBU NA ZA MWIZI NI AROBAINI. Usipofanya hivyo nao wakawa hawajui hili, toba, tutaisha kwa kutegemea kusamehe na kusonga mbele tusikokujua...tuking'ang'ania unachodai,nami hapa nitaondoa heshima yako kwa kubadilisha jina lako na kuwa- Bi.Senti TANO!! 🙂 Ahsante.
SteveD.