Pongezi ziwaendee wote walioshiriki kupanga mkakati huu.
Mkatakati umezaa matunda.
Imewachanganya sana, hawajui anawaza nini, je anatoka au inakuwaje! Anarudi alikotokea miaka ile au inakuwaje!! Je anaacha siasa au ni vipi!!! Yote haya ni maswali wanajiuliza hawapati majibu.
Wengine wameenda mbali zaidi, eti kwa kuwa hawa wamesajiri Messi, basi wao wanataka wasajiri Ronaldo.
Yaani ni hatari upande ule.
Hawatumii akili tena, mwanzoni walidai ni yeye, Lissu na Mnyika. Akaanza Lissu, akaja, sasa Mnyika kaja. Hawajashituka tu kuwa huu ni mkakati wa kuwapoteza. Sasa kabaki huyu, wanajipa moyo tu, wanaendelea kusubiri tu, wanafuata nyuma ile ya Fisi kusubiri mkono udondoke, kumbe muda unaenda.
Walivyo wajinga wamemsahau MTU wao, sasa hata haijulikani yupo wapi na anafanya nini.
Media zote kwa sasa ni Mgeni na Katibu ndo habari ya mjini.
UKAWA/CDM mnatisha aisee.
Wamepoteana.
Katibu ngoja ngoja siku zisogee kwanza, ukija kwa sasa itakuwa bado mapema mno.
Subiria wazidi kupoteana zaidi.
Big up mpango huu.[/QUO
Unapocheza gama ya politics inabidi uwe so strategic uwanjani.
Hadi hivi sasa kwenye game hii ya CCM vs CDM, mpaka sasa CDM inawachezea half ground CCM na imewazidi kwa kila kitu, kuanzia ball possession, goal attempts na zaidi sana wanawachezea half ground kwenye eneo la CCM.
Ni dhahiri kwa namna game inavyoendelea, refa atakapopuliza filimbi ya kumaliza mchezo, CCM atakuwa amelala.