MTENDAHAKI
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 4,013
- 1,448
Siasa za kinafiki nazichukia sana. Sizipendi kuziona,kuzishiriki,kuzisikia wala kuzinusa. Hukasirishwa nazo sana. Eti leo Dr. Slaa amekuwa kipenzi cha CCM. Eti leo Dr. Slaa wa CHADEMA anaonewa huruma na wanaCCM na hata viongozi waandamizi. Tangu lini mambo haya? Si huyu aliyekataliwa chamani,kwa hila, mwaka 1995 kule Karatu na ukawa ndiyo mwanzo wa yeye kuhama CCM na kujiunga CHADEMA?
Ni Dr. Slaa huyuhuyu alikuwa akiitwa majina mbalimbali ya kukereketa na kufukuta masikion mwa watanzania. Dr. Slaa, ashakum si matusi, ameitwa Padre Mzinifu na hata Babu Slaa. Aliitwa hivi kumpotezea maboya na kumtweza mbele ya watanzania. Dr. Slaa wa CHADEMA aliandikwa,kutangazwa na kusemwa kama asiyefaa. Leo,walewale wapondaji wanamsifu Dr. Slaa na kumuonea huruma kuwa amepokwa nafasi ya kugombea Urais. Unafiki.
Makada wa CCM,wale wenye uelewa finyu wa mambo ya kisiasa, wanaona kuwa kwakufanya hivyo watawavuruga CHADEMA. Vipi kuhusu patashika-nguo kuchanika ndani ya CCM? Muda huu tuutumie kujipanga dhidi ya UKAWA na mchezaji wao mpya Lowassa. Ya Dr. Slaa yatatudumaza na kutukwamisha. Dr. Slaa bado yuko CHADEMA na mwenye ari kubwa. Wabobezi tunajua.
Mchezo anaoucheza Dr. Slaa na CHADEMA ni kama ule wa kwenye filamu maarufu ya kikorea ya Jumong. Jumong alipotea na kujipoteza mara kadhaa kuhadaa mahasimu wake. Alipojitokeza kwa surprise, mahasimu wake waliipata habari yao. Makada wenzangu, Dr. Slaa hatuhusu. Tuendelee kuzichanga vyema karata zetu kwa mpambano wa Oktoba 25 mwaka huu.
Siasa za kinafiki hazina rafiki na hatufiki!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Leo ndio nimekufahamu vema; chadema mkubwa wewe!!