NE, Nakupongeza kwa kuanza na hili la MP wetu hapa A-town, katika ku-evaluate miezi yake 6 toka awe Mbunge.Naamini kuna watu wa karibu na huyu jamaa watamkumbushe kuhusu ahadi zake, na tahadhari kubwa kwa Lema ni kwamba atumie sana busara katika harakati zake za kuleta maendeleo na kuondoa utawa dhalimu wa Manispaa ya Arusha, hii ikiwa na maana kwamba Lema ana nguvu ya umma nyuma yake lakini asitumie nafasi hii vibaya. Atashangaa kufumba na kufumbua miaka tano tayari na hana la kujitetea nalo. <br><br>Lema unanafasi nzuri ya kutekeleza mambo yote uliyoahidi, ila angalizo kubwa kwako ni kwamba usije ukabweteka na uungwaji mkono wa wananchi wa Arusha. Songa mbele tafuta njia nzuri ya kuwaunganisha wananchi wa Arusha, tatua tatizo la Manispaa ya Arusha kwa BUSARA zaidi kuliko maandamano na ushawishi ufanana na kuleta vurugu.