NOT ENOUGH
JF-Expert Member
- Dec 8, 2010
- 596
- 307
Shikamoo Mh Mbunge, napenda kukumbusha kwamba sasa hivi imeshatimia miezi sita tangu uingie bungeni rasmi nafasi ambayo uliipigania sana na Mungu akakusaidia ukaipata. Nadhani umeshahudhuria vikao kama vinne hivi vya bunge ikiwemo hiki cha bajeti. Nimeona leo tuae chini mimi na wewe tupitie ile check list yetu yaani mimi mwananchi na wewe Mh Mbunge. Check list inajumuisha yote yale uliyoongea mwaka jana katika kipindi cha miaka mitatu ukiwa unapambana na Mama yetu Batilda. Mimi check list yote ninayo ila mwenzangu sijui kama ullitunza ili ikusaidie kwenye safari yako ya 2015. Kama hutojali naomba uniwekee check list yako hapa ili niangalie ni lipi umekwishalifanya ndani ya kipindi hiki cha miezi sita.