Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,870
- Thread starter
- #381
SEHEMU YA 50
Keith hakutaka kubaki nchini Marekani, aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima Fareed afe kama alivyokuwa amepanga hivyo ilikuwa ni lazima aondoke na kuelekea Dubai.
Njiani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo, aliuumiza moyo wake vilivyo, alitumia kiasi kikubwa cha fedha kumlea lakini kama kunguru vile alishindwa kufugika kabisa.
Aliamua kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuua ili kuupa furaha moyo wake. Wakati mwingine aliiona ndege ikienda taratibu sana, alitamani hata kuiongezea kasi kwani ilikuwa ni lazima afike mapema, amuue Fareed na kurudi zake nchini MArekani.
Baada ya saa zaidi ya ishirini, ndege ikatua uwanja wa ndege ambapo moja kwa moja akaondoka na kuelekea hotelini. Akawasiliana na Mickey, kijana wake aliyempa kazi ya kufanya mauaji na kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima waonane hotelini na vijana wenzake kwa ajili ya kupanga ni kwa namba gani wangeweza kufanya mauaji hayo.
Ndani ya dakika ishirini, vijana wote walikuwa hotelini humo. Akazungumza nao na kuwaambia mipango iliyokuwepo, wakajadili ni kifo cha namna gani mwanaume tata huyo alitakiwa kufa, wakakubaliana kwamba ilikuwa ni lazima abakwe, aingizwe kwenye boti, iende katikati ya bahari huku akiwa amefungwa miguu kwa jiwe kubwa kisha kufa hukohuko.
“Sawa. Wewe endelea kuwasiliana naye,” alisema Keith.
Hapo akawa na amani moyoni mwake, Mickey hakuwa na hofu alijua kwamba Fareed hawezi kutoka mikononi mwake hivyo ilikuwa ni lazima kufanya kama alichoambiwa.
Ili kumtia mshawasha Fareed, siku hiyo alizima simu siku nzima kitu kilichomnyima raha Fareed na kumpigia kila wakati lakini simu haikuweza kupatikana.
Ilipofika saa moja usiku na Fareed kupiga simu, ikawa inaita, mapigo yake ya moyo yakawa juu, hakuamini kama kweli simu hiyo ilikuwa hewani. Alikumbuka Mickey, hakujua kama mwanaume huyo alikuwa mtu mbaya aliyetaka kumuua baada ya kumbaka yeye na wenzake.
Keith hakutaka kubaki nchini Marekani, aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima Fareed afe kama alivyokuwa amepanga hivyo ilikuwa ni lazima aondoke na kuelekea Dubai.
Njiani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo, aliuumiza moyo wake vilivyo, alitumia kiasi kikubwa cha fedha kumlea lakini kama kunguru vile alishindwa kufugika kabisa.
Aliamua kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuua ili kuupa furaha moyo wake. Wakati mwingine aliiona ndege ikienda taratibu sana, alitamani hata kuiongezea kasi kwani ilikuwa ni lazima afike mapema, amuue Fareed na kurudi zake nchini MArekani.
Baada ya saa zaidi ya ishirini, ndege ikatua uwanja wa ndege ambapo moja kwa moja akaondoka na kuelekea hotelini. Akawasiliana na Mickey, kijana wake aliyempa kazi ya kufanya mauaji na kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima waonane hotelini na vijana wenzake kwa ajili ya kupanga ni kwa namba gani wangeweza kufanya mauaji hayo.
Ndani ya dakika ishirini, vijana wote walikuwa hotelini humo. Akazungumza nao na kuwaambia mipango iliyokuwepo, wakajadili ni kifo cha namna gani mwanaume tata huyo alitakiwa kufa, wakakubaliana kwamba ilikuwa ni lazima abakwe, aingizwe kwenye boti, iende katikati ya bahari huku akiwa amefungwa miguu kwa jiwe kubwa kisha kufa hukohuko.
“Sawa. Wewe endelea kuwasiliana naye,” alisema Keith.
Hapo akawa na amani moyoni mwake, Mickey hakuwa na hofu alijua kwamba Fareed hawezi kutoka mikononi mwake hivyo ilikuwa ni lazima kufanya kama alichoambiwa.
Ili kumtia mshawasha Fareed, siku hiyo alizima simu siku nzima kitu kilichomnyima raha Fareed na kumpigia kila wakati lakini simu haikuweza kupatikana.
Ilipofika saa moja usiku na Fareed kupiga simu, ikawa inaita, mapigo yake ya moyo yakawa juu, hakuamini kama kweli simu hiyo ilikuwa hewani. Alikumbuka Mickey, hakujua kama mwanaume huyo alikuwa mtu mbaya aliyetaka kumuua baada ya kumbaka yeye na wenzake.

