Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 50

Keith hakutaka kubaki nchini Marekani, aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima Fareed afe kama alivyokuwa amepanga hivyo ilikuwa ni lazima aondoke na kuelekea Dubai.
Njiani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo, aliuumiza moyo wake vilivyo, alitumia kiasi kikubwa cha fedha kumlea lakini kama kunguru vile alishindwa kufugika kabisa.

Aliamua kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuua ili kuupa furaha moyo wake. Wakati mwingine aliiona ndege ikienda taratibu sana, alitamani hata kuiongezea kasi kwani ilikuwa ni lazima afike mapema, amuue Fareed na kurudi zake nchini MArekani.

Baada ya saa zaidi ya ishirini, ndege ikatua uwanja wa ndege ambapo moja kwa moja akaondoka na kuelekea hotelini. Akawasiliana na Mickey, kijana wake aliyempa kazi ya kufanya mauaji na kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima waonane hotelini na vijana wenzake kwa ajili ya kupanga ni kwa namba gani wangeweza kufanya mauaji hayo.

Ndani ya dakika ishirini, vijana wote walikuwa hotelini humo. Akazungumza nao na kuwaambia mipango iliyokuwepo, wakajadili ni kifo cha namna gani mwanaume tata huyo alitakiwa kufa, wakakubaliana kwamba ilikuwa ni lazima abakwe, aingizwe kwenye boti, iende katikati ya bahari huku akiwa amefungwa miguu kwa jiwe kubwa kisha kufa hukohuko.

“Sawa. Wewe endelea kuwasiliana naye,” alisema Keith.
Hapo akawa na amani moyoni mwake, Mickey hakuwa na hofu alijua kwamba Fareed hawezi kutoka mikononi mwake hivyo ilikuwa ni lazima kufanya kama alichoambiwa.

Ili kumtia mshawasha Fareed, siku hiyo alizima simu siku nzima kitu kilichomnyima raha Fareed na kumpigia kila wakati lakini simu haikuweza kupatikana.

Ilipofika saa moja usiku na Fareed kupiga simu, ikawa inaita, mapigo yake ya moyo yakawa juu, hakuamini kama kweli simu hiyo ilikuwa hewani. Alikumbuka Mickey, hakujua kama mwanaume huyo alikuwa mtu mbaya aliyetaka kumuua baada ya kumbaka yeye na wenzake.
 
SEHEMU YA 51

Kitendo cha Mickey kupokea simu, Fareed akaanza kuongea kwa sauti ya kulialia kwani alitaka abembelezwe sana, apozwe kama mwanamke aliyekuwa akihitaji faraja kutoka kwa mwanaume aliyekuwa akimpenda kwa dhati.

“Nisamehe mpenzi! Nilikuwa sehemu fulani hivi,” alisikika Mickey kwenye simu.
“Nimekukumbuka jamani! Mpaka nikataka nijiue kwa ajili yako,” alisema Fareed kwa sauti yake ya kuwapagawisha wanaume.

Wakazungumza mengi na mwisho wa siku wakakubaliana kwamba lingekuwa jambo jema kama wangekutaka katika Klabu ya Dubai Night kwa ajili ya kuburudika na kuzungumza mengi. Hiyo ilikuwa furaha kwa Fareed kwani kitu pekee alichokuwa akikitaka kwa kipindi hicho ni kuonana na mwanaume huyo tu.

“Nakuja bebi!” “Sawa.”
Akakata simu. Akaelekea bafuni na kujiandaa. Siku hiyo alijiapiza kwamba ni lazima alale na Mickey kwani kama asingefanya hivyo basi kungekuwa na watu ambao wangemfuata na kulala naye kisha kumsahau yeye.

HAkutaka kuona hilo likitokea. Alichukua dakika kumi kuoga, akatoka bafuni na kisha kuanza kujipaka losheni na kujipulizia marashi yake ya Kizenji, alipomaliza, akavaa taiti iliyombana hasa iliyokuwa na rangi nyeusi, akakibusti kifua chake na kisha kupaka wanja sehemu nyusi zake alizokuwa amezinyoa na kumalizia na kujipata lipstiki mdomoni.

Alipojiangalia kwenye kioo, yeye mwenyewe akajitamani, siku hiyo alitoka chicha, alikuwa akivutia na aliamini kwa kila mwanaume ambaye angemuona, kusingekuwa hata na mtu mmoja ambaye angegundua kwamba alikuwa mwanaume kwani alikuwa na muionekano wa kike kwa asilimia mia moja.

Akatoka mpaka nje ya hoteli ambapo ndani ya dakika chache, Mickey akafika mahali hapo na kumchukua. Ndani ya gari kila mmoja alionekana kuwa na furaha tele. Ilikuwa vigumu kumgundua Mickey kwamba alikuwa na mpango mchafu kwani kwa jinsi alivyokuwa akitabasamu, ilionekana kabisa hakukuwa na tatizo lolote lile.
 
SEHEMU YA 52

Hawakuchukua muda mrefu wakafika klabu ambapo wakateremka na kuelekea ndani. Humo, Fareed alionekana kama kuchanganyikiwa, alikuwa akicheza kila wimbo uliokuwa ukipigwa na kila alipotaka kunywa, alikwenda sehemu ya kununulia vinywaji na kunywa kwani alikuwa na mtu mwenye pesa.

Wakati hayo yote yakiendelea, vijana wa Keith walikuwa humo ndani, walikuwa wakifuatilia kila kitu, walimwangalia, wao wenyewe walihisi kwamba alikuwa mwanamke kwa jinsi alivyokuwa amejiremba na kuonekana mrembo kupita kawaida.

Muziki uliendelea mpaka iipofika saa tisa ambapo wakatoka huku Fareed akiwa amechoka kupita kawaida. Wakaingia ndani ya gari na kuondoka mahali hapo.
Wala hawakuchukua mwendo mrefu, Mickey akasimamisha gari pembezoni mwa barabara ambapo hakukuwa na mwanga mkali na kisha kuteremka, Fareed alishangaa, naye akateremka kwa kuhisi kulikuwa na kitu lakini hata kabla hajafanya kitu chochote kile, gari moja likasimama, wanaume wawili waliokuwa na miili mikubwa wakateremka, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumfuata, wakamkamata na kumziba mdomo kisha kumuingiza ndani ya gari lao na kuondoka.

Fareed aliogopa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendela, hakujua wale watu walikuwa wakina nani na kwa sababu gani walikuwa wamemteka kama walivyofanya.
Wakati akijiuliza hilo, mwanaume aliyekaa pembeni ya dereva akageukia kule nyuma na kumwangalia Fareed, walipogonganisha macho, akashtuka baada ya kugundua kwamba alikuwa Keith.

“Keith…” aliita Fareed.
“Yes my love!” (ndiyo mpenzi wangu) alisema Keith huku akitoa tabasamu.
“What are you doing?” (unafanya nini?)
“I just want to play a game! A nice one, it is Flecks of Blood,” (ninataka tucheze mchezo! Mchezo mzuri, unaitwa Michirizi ya Damu) alijibu Keith huku akiwa kwenye tabasamu pana.

Safari iliendelea, Fareed alikuwa na hofu kubwa moyoni mwake, alijua kabisa kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake, hakutegemea kuona mwanaume huyo akimfuatilia mpaka huko.

Akaanza kuomba msamaha kwa kuamini kwamba angesamehewa lakini hicho hakikuwa kipindi cha kusamehewa bali kilikuwa kipindi cha kuuawa kwa kile alichokuwa amekifanya.
 
SEHEMU YA 53

Gari likaondoka na kuelekea katika ufukwe wa Kite, huko, tayari kulikuwa na boti waliyokuwa wameiandaa ambayo ingewapeleka mpaka mbali kabisa kwa ajili ya kumtosa baharini, na hawakutaka kabisa mwili wake uonekane, hivyo walikuwa na jiwe ndani ya boti ile kubwa.

Wakateremka na kuingia ndani ya boti na safari ya kuelekea katikati ya bahati kuanza. Njiani, kila mtu alikuwa akimwangalia Fareed kwa macho yaliyojaa tamaa, kwani kwa jinsi alivyokuwa, ilikuwa vigumu sana kumuacha hivihivi.

Hapo ndipo walipoanza kumbaka kama walivyokubaliana. Fareed alisikia maumivu makali, alikuwa akilia huku akitaka kuachwa lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa radhi kumuachia.

Aliendelea kubakwa mpaka akahisi mwili ukikosa nguvu, macho yake yakaanza kujaa giza, na hakujua ni kitu gani kiliendelea baada ya hapo.
“Tayari! Mfungeni jiwe,” aliagiza Keith, Fareed akafungwa jiwe kubwa na kisha kutupwa baharini. Akaanza kuzama huku akiwa amepoteza fahamu.

Walichokifanya wanaue hao, kwa haraka sana wakaondoka mahali hapo huku kila mmoja akiwa na furaha kwani waliamini kwamba kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angeuona mwili wa Fareed.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 54

Asteria alichanganyikiwa, hakujua mahali alipokuwa Fareed, alijaribu kumtafuta katika simu yake kwa kuona kwamba angempata na kuwasiliana naye kwa ajili ya biashara lakini mwanaume huyo hakupatikana.

Hakujua alikuwa wapi, aliangalia kwenye WhatsApp yake, ilionyesha kwamba mara ya mwisho kwa mwanaume huyo kuwa katika mtandao huo ilikuwa ni wiki moja iliyopita.

Hakujua ni kwa jinsi gani angempata, akajaribu kuwasiliana na Keith na kumuuliza kuhusu Fareed lakini bilionea huyo alimwambia kwamba yeye mwenyewe alikuwa akimtafuta kwani alimuaga kwamba anakwenda Dubai, baada ya hapo hakumuona tena.

Hakumwambia ukweli kwamba alimuua Fareed, alimficha kwa kuhisi kwamba siri hiyo ingedumu milele. Moyoni mwake hakuwa na huruma, kwa kile alichokifanya kwake kilionekana kuwa sahihi kwani kama kuumizwa moyo wake na mwanaume huyo, aliumizwa sana na hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya kumuua bila huruma.

Asteria hakutaka kukubali kuendelea kubaki nchini Tanzania, Fareed ndiye alikuwa biashara yake kubwa, japokuwa alikuwa na wanawake wengine waliokuwa wakijiuza lakini kwa mwanaume huyo ndiye alikuwa soko, aliyempa pesa na kuishi katika maisha ya raha kupita kawaida.

“Nakwenda Dubai!” alisema Asteria.
“Kufanya nini?”
“Kumtafuta Fareed.”
“Kwani bado hujampata?”
“Ndiyo! Wewe umempata?”
“Hapana!”

Alikuwa akizungumza na mmoja wa wasichana waliokuwa wakimfanyia kazi. SIku iliyofuata, hakutaka kubaki nchini Tanzania, akapanga safari na kupaa kuelekea Dubai kwa kuamini kwamba angeweza kumuona huko.

Moyo wake ukaanza kuingiwa na hofu, akahisi kwamba mwanaume huyo alikuwa amekufa na mwili wake kutupwa kwani kwa mtu kama Fareed, jinsi alivyokuwa akipenda mitandao ya kijamii lingekuwa suala gumu sana kukaa hata saa moja pasipo kuingia Facebook, WhatsApp, Beashare au mtandao mwingine wowote ule.
 
SEHEMU YA 55

Alipofika Dubai, akaelekea hotelini. Siiku hiyo hakuwa sawa, alipanga kuonana na wanawake wengine ambao walikuwa chini yake, akaonana nao na kuzungumza nao pamoja na kuwauliza kuhusu Fareed lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akifahamu mahali alipokuwa, kila mmoja alisema kwamba mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni kabla hajakwenda Ubelgiji, baada ya hapo hawakujua alikuwa wapi.

Alikaa Dubai kwa mwezi mzima, hakumuona Fareed na wala hakujua mahali alipokuwa. Akakata tamaa na kuona kwamba tayari mwanaume huyo alikuwa marehemu hivyo kitu pekee alichokuwa akikitaka ni kuiona maiti yake ili ajiridhishe tu.

“Hata nikiiona maiti yake nitashukuru Mungu! Yaani Fareed amekufa? Amekufaje? Mbona hata taarifa sikupewa?” alijiuliza huku akiwa amechanganyikiwa, hakujua kabisa mahali alipokuwa mtu huyo.

Alichokifanya ni kuwasiliana na marafiki zake wengine waliokuwa wakiishi nchini humo na kuwaambia kile kilichokuwa kikiendelea kwamba kulikuwa na ndugu yake ambaye hakujua mahali alipokuwa mpaka muda huo, hao ndiyo waliomshauri kwamba alitakiwa kutembelea katika hospitali mbalimbali kwa ajili ya kumtafuta kwani inawezekana alikuwa amekufa ila mwili wake ulihifadhiwa mochwari.

Hilo lilikuwa wazo zuri, alichokifanya siku iliyofuata ni kwenda katika hospitali mbalimbali lakini kote huko hakuweza kuukuta mwili wa Fareed kitu kilichomfanya kumalizia katika hospitali ya mwisho ya Sultan Idris Medical Center iliyokuwa pembezoni mwa Dubai ambapo haikuwa mbali kutoka baharini.

Alipofika huko akajitambulisha na kitu kilichomfanya kufika mahali hapo. Kwa jinsi alivyokuwa akijielezea, kila mmoja alimuonea huruma hivyo kumchukua na kuondoka naye kuelekea mochwari kwa ajili ya kuitambua maiti ya ndugu yake aliyokuwa akiitafuta.

“Ni tangu lini?” aliuliza daktari.
“Mwezi mmoja sasa umepita sijaweza kumuona.”
“Una uhakika kwamba alikuja Dubai?”
“Ndiyo! Mara ya mwisho kuwasiliana naye alikuja huku,” alijibu Asteria.
 
Back
Top Bottom