Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

**Akaanza kuwaangalia wote wawili kwa macho yaliyokuwa na Shari, kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa tayari kufanya jambi lolote lile kwani hata mwili wake ulianza kutetemeka kwa hasira kali**

 
SEHEMU YA 43

“What can I help you, sir?” (nikusaidie nini bwana mkubwa?) aliuliza Keith huku akimwangalia Godfrey aliyekuwa na hasira kali.
“I want my bae,” (namtaka mpenzi wangu)
“Your bae? Who the hell is she?” (mpenzi wako? Ndiye nani huyo?) aliuliza Keith huku akimwangalia mwanaume huyo machoni.

Godfrey akayahamisha macho yake na kumwangalia Fareed ambaye alikuwa akitetemeka tu. Kwa kitendo kile cha kumwangalia Fareed, Keith akajua mtu aliyekuwa akizungumziwa na hivyo kumuuliza Fareed kama alikuwa akimfahamu mwanaume huyo.

“I don’t know him,” (wala simfahamu) alisema Fareed huku akimwangalia Godfrey kwa macho yaliyojaa mshangao, alionekana kama kweli hamfahamu mwanaume huyo.

“Fareed, look at my eyes! Don’t you know me? Look at my eyes bastard,” Fareed, yaangalie macho yangu! Hunifahamu? Yaangalia macho yangu mwanaharamu weee) alisema Godfrey huku akionekana kuwa na hasira kali zaidi.

Bado Fareed aling’ang’ania kwamba hakuwa akimfahamu mwanaume huyo na hiyo ndiyo siku ya kwanza kumuona machoni mwake. Keith hakutaka maswali zaidi, alichokifanya ni kumwambia dereva wake aliondoe gari mahali hapo na kufanya hivyo.

Godfrey alibaki akiwa amelowa, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea, kukataliwa na Fareed mchana kweupe namna ile kulimuumiza mno moyoni mwake. Watu wote walikuwa wakimwangalia, wengine walimpigia honi kumaanisha kwamba walimtaka aondoke mahali pale ili waendelee na safari yao.

Akarudi ndani ya gari, akaingia na kutulia kwenye usukuni, alikuwa na wazo tele na muda mwingine alikuwa akitokwa na machozi, kwa kile kilichokuwa kimetokea kwake kilionekana kuwa kama ndoto ya mchana. Hakukaa sana mahali hapo, akaondoka zake huku akiwa na hasira kifuani.

Moyo wake ukajaa ghadhabu, hakufikiria kitu kingine kama kumuua Fareed. Aliutesa moyo wake, hakuwa radhi kumuona mwanaume tata huyo akiendelea kuishi na wakati aliuumiza moyo wake kupita kawaida.

“Ni lazima nimuue, nitatumia gharama zangu zote kumuua huyu mpumbavu,” alisema Godfrey huku akionekana kuwa na hasira sana. Moyo wake ukapanga kumuua Fareed kama kumlipizia kisasi kwa kile alichokifanya.
 
SEHEMU YA 44

Wanaume wote waliokuwa wakitembea na Fareed walichanganyikiwa, hawakuamini kama alikuwa akijua sana kitandani. Mioyo yao iliuchanganyikiwa, walipokutana naye, hawakutaka kumuacha, waliendelea kumtafuta zaidi na zaidi.

Kitendo cha kuwa na Keith kwake yalikuwa mateso makubwa, alibanwa sana kwani mwanaume huyo hakutaka kumuona akiondoka kuelekea sehemu yoyote ile.
Alipokea simu kutoka kwa matajiri wengi ambao walimuahidi kumpa kiasi kikubwa cha fedha lakini kuonana nao suala hilo lilikuwa gumu sana. Aliwasiliana nao kwenye simu, aliwatumia picha zilizokuwa zikionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa mzuri.

Hakuzoea kuwa na mwanaume mmoja, tangu alipompata wakala wake, Asteria, alikuwa akitoka na wanaume mbalimbali, hayo ndiyo yalikuwa maisha yake na hata alipoambiwa na Keith kwamba hakutakiwa kutoka, kwake yalikuwa mateso makubwa.

“Haiwezekani! Siwezi kukaa na mwanaume mmoja, kwani kanioa? Yeye mbona ana familia yake, lazima nitoke,” alisema Fareed huku akionekana kutokukubaliana na kile kilichokuwa kikiendelea.

Ndivyo alivyofanya, baada ya wiki moja huku akiwa amempa Godfrey mahaba mazito akaamua kuondoka na kuelekea Dubai. Hakuwa ameaga, alimtoroka kwani kitu alichokuwa akikiangalia ni kwa namna gani angeweza kuifurahisha roho yake.

Huko Dubai alikwenda kuonana na bilionea mwingine, Saed ambaye alikuwa akimsumbua sana kwenye simu. Walipoonana kwa mara nyingine, wakaelekea kitandani ambapo huko wakafanya mambo yote na kukumbushiana siku ya kwanza walipokuwa wameonana.

Hakutaka kuwasiliana na Keith, mwanaume huyo alimpigia sana simu kutaka kuzungumza naye lakini hakupokea, alinyamaza kimya na hata zile meseji alizokuwa akitumiwa, nazo hakuzijibu japokuwa aliziona na kuzisoma.

Akili na mawazo yake yalikuwa kwa Bilionea Saed tu ambaye hakuwa msiri, alimchukua Fareed na kumtamulisha kwa baadhi ya marafiki zake na kuwaambia kwamba alikuwa mpenzi wake wa kufa na kuzikana. Hilo lilimpa furaha Fareed kwa kuamini kwamba angeishi milele na mwanaume huyo.
 
SEHEMU YA 45

Marafiki wa Saed nao hawakutaka kukubali, kwa kuwa Fareed alionekana kuwavutia tena huku kwa nyuma akianza kutuna na kifua kuonekana, hawakutaka kumuacha, walichokifanya ni kuanza kummendea kitu ambacho kilimfurahisha kwani akili yake ilifikiria fedha kuliko mapenzi.

Alipokea meseji nyingi kutoka kwa wanaume mbalimbali, wote walimtaka kimapenzi. Hakuwa mchoyo, alikubali kufanya nao na hivyo kukutana nao sehemu yoyote waliyotaka na kuwaridhisha.

Ndani ya mwezi mmoja akatembea na marafiki kumi wa Saed, hakuwa akijua, alipokuwa naye alikuwa akimsifia kwa marafiki zake kumbe ndiyo haohao waliokuwa wakimbadilikia kila alipowapa kisogo.

Wakati mwezi wa pili ulipokatika, ndipo akaingia kwenye umbo rasmi la kike, alikuwa na muonekano kama wa wanawake wengine, alikuwa na kifua kikubwa, wowowo, mavazi ya kile, alijitahidi kuibadilisha sura yake kwa kuipaka sana poda, akaseti nywele zake, kwa kifupi alikuwa mwanamke kamili isipokuwa sehemu za siri ambapo alishindwa kuibadilisha.

“Hivi huyu mpumbavu Keith anaendelea kunisubiri au? Asahau! Mimi siwezi kuwa na bwana mmoja. Kwanza ukila ugali kila siku utachoka, siku nyingine kula wali, ukiuchoka, kula pilau, nalo ukilichoka, nyonya koni,” alijisemea huku akiirambaramba midomo yake kama mwanamke aliyepewa ahadi ya kukutana na mwanaume kwenye nyumba ya wageni.

Wakati yeye akifikiria hayo yote, upande wa pili Keith alikuwa na hasira kali, hakuamini kama kweli Fareed alikuwa amemtenda kiasi hicho na wakati alikuwa ametumia kiasi kikubwa cha fedha kumgharamia.

Hakukubali, moyo wake ulijaza ghadhabu nzito na alikuwa tayari kufanya lolote lile kumshughulikia mwanaume huyo.
Alimtafuta, aliwaagiza vijana wake kila kona hapo Los Angeles kumtafuta na kumleta kwake. Vijana hao wakafanya kazi usiku na mchana, wakazunguka katika Cassino mbalimbali lakini hawakuweza kumuona.

Hawakuishia hapo, wakazunguka kwenye miji mingine lakini napo hawakuweza kumuona kitu kilichowapa maswali mtu huyo alikuwa wapi.
“Tumemtafuta sana! Hatujamuona!” alisema kijana mmoja.
 
SEHEMU YA 46

“Sawa. Ngoja nimpigie wakala wake,” alisema Keith na kumpigia simu Asteria, alitaka kufahamu mahali alipokuwa Fareed ili amuue, hata mapenzi aliyokuwa akiyataka, yakamtoka, hakuwa radhi kuona mtu aliyemgharamia akimchukua mwanaume mwingine.

“Na akisema yupo Tanzania tu, namfuata na kumuua hukohuko!” alisema Keith na kumpigia simu mwanamke huyo. Kwa kuwa Fareed hakumwambia kuhusu kumtoroka Keith, wala kumwambia kwamba alikuwa bwana wake mpya, mwanamke huyo akamwambia kwamba alikuwa Dubai akila maisha na bilionea Saed, maneno yaliyomchoma mno Keith.

“Yaani anakula maisha na mwanaume mwingine. Sasa atanitambua,” alisema Keith! Hapohapo akawapigia simu vijana wake. Alitaka kuzungumza nao, mezani kulikuwa na jambo moja tu. Kumteka Fareed na kumuua.

***
Huko Dubai maisha yalikuwa ni ya raha kabisa, Fareed hakuishia kwa wanaume hao tu, alichokuwa akikiangalia kilikuwa pesa tu. Siku zikakatika huku akiendelea kupata fedha, alilala katika mahoteli makubwa na ya kifahari ambayo alipangiwa na mabwana zake.

Alisahau kabisa kama kulikuwa na shida katika dunia hii, alifurahia kwa kuwa aliona kwamba hakukuwa na kitu alichoshindwa kukifanya kwa sababu alikuwa na pesa ya kufanya kitu chochote kile.

Baada ya wiki mbili akapigiwa simu na mwanaume mmoja, alikuwa mwanaume wa Kizungu aliyemwambia kwamba alitaka kuonana naye, mwanaume huyo alijitambulisha kwa jina la Mickey Downford.

Kwanza Fareed hakutaka kukubali, lilikuwa jambo gumu kukutana na mwanaume huyo, alihisi kwamba hakuwa na fedha za kumpa kwani yeye aliwazoea mabwana wa Kiarabu ambao walikuwa radhi kutoa kiasi chochote cha pesa ili kupata wanachokihitaji.

Kwa kipindi cha wiki nzima Mickey alikuwa akiomba kuonana na Fareed lakini alikuwa akikataa na wakati mwingine alimwambia kwamba hakuzoea kutembea na Wazungu, yeye aliwapenda Waarabu tu.

“Lakini nina pesa!” alisema Mickey kwenye simu.
“Nitaamini vipi?”
“Subiri! Nipe namba yako ya benki,” alisema Mickey na hivyo kupewa namba hiyo.
 
Wee Shunie mbona umeweka fupi? Afu mbona Hii script ya huyu Bwabwa ndefu sana? Anyway weka nyingine sa hivi ni saa nane usiku usinishangae mi huwa silalagi
 
Wee Shunie mbona umeweka fupi? Afu mbona Hii script ya huyu Bwabwa ndefu sana? Anyway weka nyingine sa hivi ni saa nane usiku usinishangae mi huwa silalagi
Hata sijui kama haulali me huwa sikeshi jf
 
SEHEMU YA 47

Ndani ya dakika kumi, simu ya Fareed ikalia kuonyesha kwamba kulikuwa na ujumbe, haraka sana akaichukua na kuangalia, ilikuwa ni meseji kutoka katika huduma ya kibenki ambayo ilimwambia kwamba alikuwa amepokea kiasi cha dola elfu hamsini, zaidi ya milioni mia moja na nusu kwa fedha za Kitanzania.

Akakaa chini, hakuamini kile alichokuwa amekiona, hakujua kama alitumiwa na mwanaume ambaye alimpuuzia kila alipomwambia kwamba walitakiwa kuonana. Kiasi hicho kilikuwa kikubwa sana kwake, kwa kawaida aliwatoza wanaume kiasi cha dola elfu moja mpaka elfu mbili, kitendo cha kupewa kiasi kikubwa cha fedha kilimchanganya.

Wakati akiwa kwenye hali ya furaha, Mickey akampigia simu.
“Nadhani umeona mabadiliko kwenye akaunti yako!” alisema Mickey.
“Nimeona mpenzi!”
“Huo ni mwanzo. Na nimekupa kiasi kidogo kwa sababu tu huniamini!” alisema Mickey.

Kichwa cha Fareed kilichanganyikiwa, hakuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa amemtumia kiasi kikubwa cha fedha. Hapo ni kwamba hawakuwa wamekutana na kuzungumza, hawakulala kitandani alimgawia kiasi hicho cha fedha, kama angemfanyia kama wengine angepata kiasi gani?

Alipojiuliza, akajikuta akianza kuvutiwa na Mickey. Hakutaka kubaki hotelini, haraka sana anawasiliana na mwanaume huyo kwa miadi ya kuonana na kumwambia kwamba walitakiwa kuonana sehemu tulivu, katika ufukwe wa Kite uliokuwa Magharibi mwa mji huo.
Ndani ya saa moja, tayari Fareed alifika mahali hapo. Alikuwa akiangalia huku na kule akimtafuta mwanaume aliyekuwa amepanga naye miadi ya kuonana.

Baada ya dakika kadhaa, akaliona gari la kifahari, Bugatti la watu wawili likifika mahali hapo. Alilikodolea macho, lilikuwa gari la gharama kubwa na ilionyesha kwamba mtu aliyekuwa humo ndani hakuwa wa mchezomchezo kuhusu masuala ya pesa.

Mlango ukafunguliwa, ukafunguka kwa kwenda juu na mwanaume mmoja aliyevalia suti kuteremka. Watu wote waliokuwa katika ufukwe huo walikuwa wakimwangalia, hawakuamini kama kijana mdogo aliyeteremka ndiye aliyekuwa akiendesha gari hilo la kifahari.

“Mmh! Kuna watu wana hela bwana!” alijisemea Fareed, hakuwa amejua kwamba mwanaume huyo ndiye alikuwa Mickey aliyekuwa akimsubiri.
 
SEHEMU YA 48

Moja kwa moja Mickey akaifuata meza ya chakula iliyokuwa katika eneo la kulia chakula, akachukua simu yake na kumpigia Fareed kwa ajili ya kumpa taarifa kwamba alikuwa amefika.
“Mbona sikuoni?” aliuliza Fareed.
“Unaliona hilo gari lililosimama hapo ufukweni?”

“Ndiyo! Hili la kifahari?”
“Yaap!”
“Sasa wewe upo wapi?”
“Umemuona dereva aliyeteremka?”
“Ndiyo!”
“Huyo ndiye mimi!”
“Ndiye wewe? Unaendesha Bugatti?”
“Yeah! Naomba unifuate! Bila shaka unajua hapa nilipokuja kukaa,” alisema Mickey na kisha kukata simu.

Fareed hakuamini, alimdharau mwanaume huyo lakini kumbe alikuwa bilionea mkubwa tu. Wakati anapiga hatua kuelekea kule kulipokuwa na meza ile, macho yake hayakuacha kuliangalia gari lile, lilimpagawisha na kujiona kama yeye ndiye mmiliki halali.

Alipofika katika meza hiyo, kitu cha kwanza Mickey akasimama na kumkumbatia. Ilikuwa vigumu kuamini kama mtu huyo alikuwa mwanaume kwani alivalia gauni refu, kilemba na nyuma alijazia kwani zile sindano alizokuwa amechomwa zilifanya kazi vizuri na hata kifua chake kilijaa.

“U mzuri sana,” alisema Mickey huku akimkumbatia Fareed.
“Nashukuru sana mpenzi!” alisema Fareed, akatoa tabasamu la kike na kutulia kwenye kiti.

Walizungumza mambo mengi huku Mickey akimwambia kwamba alikuwa bilionea kutoka nchini Australia na alifika hapo kwa ajili ya mambo yake ya biashara ila alipomuona klabu siku za nyuma ndizo zilimpagawisha na kuitafuta namba yake ambayo kwa maelezo yake alimwambia kwamba aliinunua kutoka kwa mtu kwa dola elfu mbili.

“Jamaniiiii!”
“Ndiyo ukweli!”
Walizungumza mambo mengi mno huku muda wote Mickey akizungumza kama bilionea mkubwa. Walichukua saa moja, walipomaliza, wakaelekea katika Bugatti ile, wakaingia na kuondoka mahali hapo.

Njiani, Fareed alipagawa mno, moyo wake ulijuta kutofahamiana na mwanaume huyo tangu kitambo kwani alikuwa mzuri wa sura na kubwa zaidi ni kwamba alikuwa na pesa kitu kilichokuwa ugonjwa wake mkubwa kama mtu aliyezaliwa benki.
 
Back
Top Bottom