Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 38

Godfrey alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, moyo wake ulimuuma sana kwani kwa jinsi mambo yalivyokuwa yakiendelea, alihisi kabisa kuna jambo baya nyuma yake.

Alijaribu kumtafuta Fareed kwenye simu, hakuwa akipatikana, alimtumia meseji nyingi sana WhatsApp lakini mwanaume huyo hakujibu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, akili yake ilimwambia kwamba wakati huo alikuwa na mwanaume mwingine kitandani kitu kilichouchoma moyo wake vilivyo.

Hakutaka kukata tamaa, aliendelea kumtafuta zaidi na zaidi lakini hakufanikiwa hata kumpata. Kwa kuwa aliwafahamu baadhi ya marafiki zake, akaanza kuuliza huko lakini hakupata majibu, kila aliyemuuliza alisema kwamba hakumuona kitu kilichomuuma sana.

Akakosa furaha, hata kula hakuwa akila, mkewe alimshangaa, alihisi kwamba mume wake alikuwa mgonjwa hivyo kumuuliza mara kadhaa juu ya kilichokuwa kikimsumbua lakini hakuwa radhi kukisema.

“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Theresa huku akimwangalia mume wake usoni.
“Moyo unauma sana!” alijibu huku akishika upande wa moyo wake.
“Kwa nini unauma? Umeanza lini kuuma? Twende hospitali,” alisema Theresa huku akimwangalia mume wake ambaye hakuzungumza kitu zaidi ya kukaa kimya tu.

Aliwahi kuumia maishani mwake lakini maumivu aliyoyapata siku hiyo yalikuwa ni zaidi ya maumivu. Hakukuwa na kitu kilichokwenda sawa, muda mwingi alikuwa akihuzunika, alipokuwa akilala, alimuona Fareed akiwa na mwanaume chumbani kitu kilichouchoma moyo wake vilivyo.
“Haiwezekani! Nitamtafuta mpaka nimpate!” alijisemea.

Alichokifanya siku iliyofuata ni kumtafuta kijana mkali wa kompyuta na kuanza kuzungumza naye. Alimwambia dhumuni lake kwamba ni kumtafuta mtu ambaye alikuwa akitumia simu aliyompa namba zake. Mwanaume huyo akachukua na kuziingiza kwenye kompyuta yake.
Ilikuwa kazi kubwa lakini aliona ilikuwa ni lazima kumsaidia mwanaume huyo kwani kwa jinsi alivyoonekana, alihitaji msaada wake kuliko kitu chochote kile.

Alichokifanya jamaa ni kuiweka programu moja iitwayo Hack My Phone kisha kuziweka namba zile. Hilo wala halikuwa tatizo kwani baada ya nusu sana, GPRS ilionyesha mahali alipokuwa Fareed, alikuwa Los Angeles nchini Marekani.
 
SEHEMU YA 39

“Nimempata!” alimwambia Godfrey ambaye alimsogelea.
“Yupo wapi?”
“Los Angeles!”
“Sehemu gani?”
Akamwambia sehemu alipokuwa, hilo halikuwa tatizo alichokifanya ni kuchukua maelezo yote na kuiscreen shot eneo alilokuwa Fareed na hivyo kupanga siku ya kwenda Marekani.

“Unakwenda Marekani? Mbona ghafla hivyo?” aliuliza Theresa huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Kuna kitu nakwenda kufanya.”
“Kitu gani?”
“Nimesema kuna kitu nakwenda kufanya!” alisema Godfrey kwa sauti kubwa yenye ukali.

Theresa akahisi kwamba kulikuwa na tatizo kubwa hivyo akamuacha mumewe, kitendo cha kumjibu namna ile kilimaanisha kulikuwa na jambo kubwa nyuma yake.

Hakutaka kuzungumza sana, aliogopa kumkorofisha hivyo kumuacha afanye alichotaka kukifanya. Usiku mzima Godfrey hakulala, alichanganyikiwa na kichwa chake alikiona kuwa kizito sana.
Alipokamilisha taratibu zote za safari, hakutaka kuendelea kubaki nyumbani, akaondoka zake kuelekea Marekani.

Ndani ya ndege, alikuwa kimya kabisa, alikuwa na mawazo mengi, hata mtu aliyekaa pembeni yake hakutaka kumuongelesha kwani kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa mtu wa mawazo tele.
Ndege ilichukua saa ishirini na mbili mpaka kufika nchini Marekani, katika Jiji la New York ambapo akateremka na kuunganisha ndege mpaka jijini Los Angeles katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa LAX na kuteremka.

Akaichukua simu yake, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuiangalia ile picha aliyokuwa ameiscreen shot, picha iliyomuonyesha sehemu ambapo mpenzi wake alipokuwepo. Alipopaangalia vizuri, akaelekea hotelini.

Hakuacha kumtafuta Fareed, aliendelea kumtafuta zaidi lakini hali haikubadilika, ilikuwa vilevile kwamba hakumpata na hata alipomtumia meseji, hazikujibiwa kitu kilichomchanganya zaidi.

“Huyu atakuwa na mwanaume tu! Yaani wewe subiri! Nitaua mtu,” alijisemea. Japokuwa alikuwa amechoka, hata kulala hakuweza kulala, kichwa chake kilivurugwa na ilikuwa ni lazima ajue kitu gani kilikuwa kikiendelea.
 
SEHEMU YA 40

Baada ya dakika arobaini na tano, kila mmoja alikuwa hoi. Dk. Fabby alimwangalia Fareed, moyo wake ukajisikia hukumu nzito na kulaumiwa kwa kile alichokuwa amekifanya. Hakujua ni shetani gani alimuingia mpaka kumpelekesha namna ile na kuamua kufanya ushenzi mkubwa kama ule.

Alijuta moyoni mwake, alishindwa kumwangalia Fareed, akaelekea choooni. Huko, alibaki akilia kwa maumivu mazito, huzuni kubwa ilimuingia na hakuamini kama ingetokea siku ambayo angefana ushenzi mkubwa kama huo.

Alimlaumu shetani, alimpa tamaa mbaya ambayo ilimfanya kuusaliti moyo wake na Mungu wake. Kule chooni hakutoka haraka, alikuwa akilia kwa majuto makubwa.

Fareed alipoona Dk. Fabby anachelewa kutoka, akausogelea mlango na kuugonga. Daktari huyo alishtuka na kukumbuka kwamba kulikuwa na kazi aliyotakiwa kufaya, hivyo harakaharaka akanawa uso na kutoka nje.

Hakutaka kumchangamkia Fareed, alichokifanya ni kumpeleka kitandani, akamlaza na kisha kumchoma sindano iliyokuwa na dawa ya kuyaongeza makalio yake kidogo na kifua chake, awe na muonekano kama mwanamke mbichi.
“Tayari!” alisema Dk. Fabby huku akimwangalia Fareed.

“Nashukuru mpenzi!” alisema Fareed huku akimshika kidevu Dk. Fabby lakini akajikwepesha.
“Eeh! Jamani una nini?” aliuliza Fareed.
“Nenda nyumbani!”
“Sawa. Lakini usikose kunipigia.

Nitakumiss sana,” alisema Fareed, Dk. Fabby hakuzungumza kitu chochote kile, akamuondoa Fareed chumbani humo.
Hilo hakutaka kulijali sana, Fareed ni akaondoka hospitalini hapo. Moyo wake uliridhika kwani hicho ndicho kitu alichokifanya kila siku. Aliuchukia muonekano wake na alipogundua kwamba baada ya siku chache angekuwa na muonekano wa kike, akafurahi zaidi.

Alipofika nyumbani, akaelekea chumbani na kutulia kitandani. Akachukua simu yake na kuanza kumpigia Dk. Fabby lakini mwanaume huyo hakuhitaji mazoea tana.
“Lakini mbona unanikataa?” aliuliza Fareed.

“Naomba uniache!”
“Nikuache upumzike?”
“Yaani uniache moja kwa moja. Usinijuejue,” alisema Dk. Fabby na kukata simu.

Fareed alihuzunika lakini hakuwa na jinsi, hakutaka kuwasiliana na Dk. Fabby kwani hakumpenda kama alivyompenda Keith ambaye alikuwa tayari kumpa kiasi chochote cha fedha japokuwa hakutaka kumwambia ukweli.
 
Back
Top Bottom