Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

Mwanaume ni kuishi nao kwa akili tu
Hao waliolaaniwa ndiyo mafirauni siyo wote!!
Naona Nyemi kaamua kuhamasisha ushoga maana mwanzo mwisho watu wanazibua vyoo vya wenzao
 
SEHEMU YA 41

“Haina shida.”
Akakaa na kumsubiria mzee huyo. Alimwambia kwamba angefika nyumbani hapo muda si mrefu. Akajiachia kochini huku moyo wake ukiwa na amani kwamba alifanikiwa kulala na Dk. Fabby, hata kama hakumtaka tena kwake wala hakulijali sana.

Baada ya saa moja, Keith akafika nyumbani hapo. Alipomuona Fareed, akamfuata na kumkumbatia. Alimkumbuka na muda wote alikuwa akimuwaza yeye tu. Walikaa na kuzungumza, Keith hakutaka kumwambia ukweli Fareed jinsi alivyokuwa akijisikia ila alijua kwamba mwanaume tata huyo alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

“Umefanikiwa?” aliuliza Keith.
“Ndiyo!”
“Safi sana, hebu nione,” alisema mwanaume huyo na kutaka kuonyeshewa.
Hilo halikuwa tatizo kwa Fareed, akavua nguo zake na kisha kumwangalia. Mapigo ya moyo wa Keith yalikuwa yakienda kasi, hakuamini kama alikuwa akimwangalia mwanaume huyo.

Mwili wake ukamsisimka, hakutaka kukubali, akamchukua Fareed na kwenda naye kitandani, hapo, akaanza kumwambia maneno mengi ya mahaba, jinsi alivyokuwa akimpenda, hakuacha kumsifia kwa kila kitu kiasi kwamba Faredd akajiona kuwa mzuri kuliko watu wote duniani.

“Kweli?”
“Ndiyo! Wewe ni malaika wangu, ni mrembo kuliko warembo wote waliowahi kutokea katika hii dunia!” alisema Keith maneno ambayo alikuwa na uhakika kwamba hayakuwa kweli bali alitaka kukamilisha kile alichokitaka.

Fareed akaachia tabasamu pana, akajiangalia, akahisi kwamba kweli alikuwa mrembo kuliko warembo wote waliowahi kutokea katika dunia hii. Akashikwa mkono, akaacha, akashikwa bega, akaacha, kila alipokuwa akishikwa huku na kule, aliacha na mwisho wa siku, baada ya saa moja wote kujikuta wakiwa hoi kitandani.

“Ahsante,” alisema Fareed huku akimwangalia Keith kwa uso uliokuwa na tabasamu pana.
“Umeridhika?”
“Sana mpenzi! Kumbe nilikuwa najichelewesha tu!” alisema Fareed huku akimwangalia mwanaume huyo.

Penzi jipya likaanzishwa, kila mmoja alikuwa bize na mwenzake, japokuwa Keith alikuwa na familia yake jijini New York lakini hakutaka kurudi huko, alitekwa na biashara zake zote alizihamishia huko, mahesabu akawa anapelekewa hukohuko alipokuwa.
 
SEHEMU YA 42

Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, mapenzi ya jinsi moja yalimpeleka puta na hakukumbuka kitu chochote kile. Siku wiki moja baadaye akaamua kumfanyia sapraizi Fareed, alitaka kumnunulia gari jipya kwani hakutaka kuona akipata tabu yoyote ile.

Siku hiyo akakaa na kuzungumza naye mengi, ilipofika saa sita mchana, akamchukua na kisha kuondoka nyumbani hapo. Wakati wametoka ndani ya jumba hilo kubwa na kushika barabara, ghafla akaliona gari moja likiwafuata kwa nyuma.

Wakawa na hofu kwa kuhisi kwamba inawezekana watu waliokuwa humo walikuwa majambazi waliotaka kuwaua au kuwaibia hivyo. Kila Keith alipokuwa iongeza mwendo, gari la nyuma likawa linaongeza kasi kiasi kwamba wakaona huo ndiyo ungekuwa mwisho wao.

Walichokifanya ni kuingia kwenye barabara kubwa ambapo walikwenda mpaka sehemu iliyokuwa na watu wengi, akalisimamisha gari hilo kwa kuamini kwamba hata kama watu hao wangeteremka kwenye gari na kuwafuata, wasingeweza kuwaua kutokana na wingi wa watu mahali hapo.

Gari lile la nyuma likasimama na mwanaume mmoja kuteremka. Hawakuzungumza kitu, walibaki wakimwangalia mwanaume huyo ambaye alionekana kuwa na hasira kubwa.
Fareed hakumtambua mpaka alipofika karibu, Keith akateremsha kioo, macho ya Fareed yakatua kwa mwanaume aliyekuwa akimfahamu, alikuwa Godfrey aliyeonekana kuwa mwenye hasira kupita kawaida.

Akaanza kuwaangalia wote wawili kwa macho yaliyokuwa na shari, kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa tayari kufanya jambo lolote lile kwani hata mwili wake ulianza kutetemeka kwa hasira kali.

Je, nini kitaendelea?
 
Nataka nione jinsi ayakavyoanza kuwashughulikia mamilionea
 
Back
Top Bottom