Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 36

Alipambana lakini kila alipotaka kujivika ujasiri aliisikia sauti ikimwambia moyoni mwake kwamba kwa nini asimwambie ukweli Fareed na kumpa kile alichokitaka? Lakini wakati akifikiria hivyo, pia upande mwingine, sauti nyingine ikamwambia kwamba hakutakiwa kufanya hicho alichokuwa akikifikiria kwani lilikuwa chukizo mbele za Mungu wa mbinguni.

“Nitaweza kweli kumshinda shetani? Mungu! Sina nguvu zako moyoni mwangu! Kweli nitaweza kumshinda shetani?” aliuliza Keith huku akimwangalia Fareed ambaye hakuuonekana kuwa na wasiwasi pale kwenye kitanda alipokuwa amekaa, ndiyo kwanza akazidi kuvianika vipaja vyake vilivyopakwa losheni na kukolea hasa.

“Haya niambie sasa…” alisema Fareed.
“Umenikumbusha! Kuna kitu nilitaka kukwambia,” alisema Keith huku akimsogelea Fareed kitandani pale.
“Kitu gani?”
“Ninahitaji ukafanyiwe upasuaji!”
“Upasuaji! Wa nini?”
“Uwekewe makalio makubwa na hata kifua chako kitunishwe, kiwe kama cha mwanamke,” alisema Keith huku akimwangalia Fareed.

Hilo ndilo alilokuwa akilitaka, alitamani kuonekana kama mwanamke. Alitamani kubadilisha jinsia yake na kuwa mwanamke lakini alishindwa, aliogopa kwa kuhisi kwamba angeweza kupata matatizo makubwa.

Akakubaliana na Keith kwamba akafanyiwe upasuaji na kuwekewa muonekano wa kike. Fareed akafurahi sana kiasi kwamba akasimama pale alipokuwa na kumfuata Keith kisha kumkumbatia kwa furaha kubwa.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
 
SEHEMU YA 37

Siku hiyohiyo Keith akawasiliana na Dk. Fabby wa Hospitali ya New Lucas Medical Center ambaye alikuwa mtaalamu wa upasuaji kwa watu waliokuwa wakihitaji kuwekewa muonekano wa jinsi nyingine. Wakakubaliana na hivyo kitu cha kwanza kabisa alichokitaka ni kuonana na huyo mtu.

Fareed akapelekwa hospitalini hapo. Dk. Fabby alipomuona, hakuamini kama mtu huyo alikuwa mwanaume, alimwangalia kwa makini, alionekana kama mwanamke kwa jinsi alivyokuwa akijiweka.

Akamuita ofisini kwake na kukaa kisha kuzungumza naye. Fareed aliulizwa maswali kadhaa ambayo aliyajibu bila kuwa na hofu yoyote ile kitu kilichomfurahisha daktari huyo.
“Na huyu ni bwana wako?” aliuliza Dk. Fabby!
“Hapana! Ni rafiki yangu!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”

“Unajua wewe ni mzuri sana!” alisema Dk. Fabby huku akimsogelea Fareed pale alipokaa, akamshika mkono, kijana huyo akashtuka kwani hakutegemea kumuona dakatri huyo akiwa amebadilika ghafla kama alivyokuwa.

“Unataka kufanya nini?” aliuliza Fareed, alijua kile alichokitaka kukifanya daktari huyo ila alimua kumuuliza kama kumtega.
“Dhambi iliyofanya Sodoma na Gomora kuteketezwa kwa moto,” alisema Dk. Fabby huku akimvua shati laini alilolivaa Fareed ambaye naye bila kipingamizi akamsaidia dokta huyo kuliondoa kabisa mwilini mwake.

“Mh! Leo kazi ipo! Kama hii hospitali haitopaa leo kwa ufirauni ninaotaka kuufanya, basi nitakuwa na bahati,” alijisemea daktari huyo huku akimwangalia Fareed, tena wakati mwingine alitoa pumzi nzitonzito.

Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom