SEHEMU YA 37
Siku hiyohiyo Keith akawasiliana na Dk. Fabby wa Hospitali ya New Lucas Medical Center ambaye alikuwa mtaalamu wa upasuaji kwa watu waliokuwa wakihitaji kuwekewa muonekano wa jinsi nyingine. Wakakubaliana na hivyo kitu cha kwanza kabisa alichokitaka ni kuonana na huyo mtu.
Fareed akapelekwa hospitalini hapo. Dk. Fabby alipomuona, hakuamini kama mtu huyo alikuwa mwanaume, alimwangalia kwa makini, alionekana kama mwanamke kwa jinsi alivyokuwa akijiweka.
Akamuita ofisini kwake na kukaa kisha kuzungumza naye. Fareed aliulizwa maswali kadhaa ambayo aliyajibu bila kuwa na hofu yoyote ile kitu kilichomfurahisha daktari huyo.
“Na huyu ni bwana wako?” aliuliza Dk. Fabby!
“Hapana! Ni rafiki yangu!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Unajua wewe ni mzuri sana!” alisema Dk. Fabby huku akimsogelea Fareed pale alipokaa, akamshika mkono, kijana huyo akashtuka kwani hakutegemea kumuona dakatri huyo akiwa amebadilika ghafla kama alivyokuwa.
“Unataka kufanya nini?” aliuliza Fareed, alijua kile alichokitaka kukifanya daktari huyo ila alimua kumuuliza kama kumtega.
“Dhambi iliyofanya Sodoma na Gomora kuteketezwa kwa moto,” alisema Dk. Fabby huku akimvua shati laini alilolivaa Fareed ambaye naye bila kipingamizi akamsaidia dokta huyo kuliondoa kabisa mwilini mwake.
“Mh! Leo kazi ipo! Kama hii hospitali haitopaa leo kwa ufirauni ninaotaka kuufanya, basi nitakuwa na bahati,” alijisemea daktari huyo huku akimwangalia Fareed, tena wakati mwingine alitoa pumzi nzitonzito.
Je, nini kitaendelea?