SEHEMU YA 141
Zoezi hilo liliambatanisha na kushikana hapa na pale. Wakati yote yakiendelea, akili ya De Leux ilikuwa kwenye kadi aliyokuwa nayo msichana huyo, hakutaka kupoteza lengo lake kwani aliamini kwamba kama asingefanikisha suala hilo muda huo basi kazi waliyokuwa wakiitaka isingeweza kufanyika.
Wakapelekana mpaka kitandani, wakavuana nguo na kuendelea na zoezi lao. Miguno ya kimahaba ilikuwa ikisikika kila kona na baada ya muda fulani, sauti zile ziliongezeka zaidi.
Kulikuwa na mwanga hafifu, Natalie alichanganyikiwa, muda wote wakati mwanaume huyo alipokuwa juu yake, aliyafumba macho yake, hisia za raha zilikwenda mpaka kwenye ubongo wake, zikamchanganya kiasi kwamba akaona hakukuwa na kitu kilichokuwa na raha duniani kama hicho kilichokuwa kikiendelea kitandani hapo.
De Leux akachukua nafasi hiyohiyo kupekua katika mifuko ya msichana huyo, alichokuwa akikitaka ni kadi iliyokuwa na uwezo wa kufungua milango yote, hilo wala halikuwa zoezi gumu kwani ndani ya sekunde chache, tayari alikuwa na kadi hiyo mkononi mwake.
Akaificha kwenye mfuko wa suruali yake, alipomaliza kufanya mapenzi na msichana huyo, wakabaki wamelala huku wakivuta raundi ya pili iendelee.
Muda wote Natalie alikuwa akifikiria ngono, kilipita kipindi kirefu pasipo kufanya mchezo huo na ndiyo maana alipoambiwa aende chumbani kwa mwanaume huyo, hakutaka kujiuliza, haraka sana akaenda tena huku akiwa amejiandaa kikamilifu.
“Una pumzi sana,” alisema natalie huku akiupeleka mkono wake chini ya kiuno cha De Leux.
“Kweli?”
“Yeah! Sijawahi kukutana na mwanaume mwenye pumzi kama wewe. Halafu unajua, kuna wakati nilihisi kama unataka kunivunja kwa jinsi ulivyokuwa ukinikunja,” alisema msichana huyo huku mkono ule ukiwa kulekule.
“Pole sana jamani! Ila nataka tuendelee!”
“Wewe tu! Mimi nipo tayari!” alisema De Leux.
Hata kabla hawajaendelea, De Leux akasimama na kumwambia Natalie kwamba alitaka kwenda kumuona rafiki yake kwamba ikiwezekana asimpigie simu asubuhi sana kwani ilikuwa ni lazima alale na msichana huyo ambaye kwa siku inayofuatia ilikuwa ni ya mapumziko kwake.