SEHEMU YA 142
Hilo halikuwa na tatizo, akaruhusiwa na kuondoka huku akiwa na kadi ile mkononi. Alipofika katika chumba cha rafiki yake, akagonga mlango, ulipofunguliwa, akampa kadi na kumwambia ampe Fareed ambaye alitakiwa kukamilisha kazi ya mauaji na kuondoka hotelini hapo.
Hilo halikuwa tatizo, kadi ikachukuliwa, De Leux akarudi chumbani kwake kuendelea kufanya mapenzi na msichana huyo. Huku nyuma, rafiki yake akampelekea kadi ile Fareed ambaye aliichukua na kuufuata mlango wa chumba kile.
Fareed hakuwa mikono mitupu, alikuwa na kisu pamoja na dawa kali ya usingizi ya Microphenon ambayo ilikuwa ikitumika sana katika vyumba vya upasuaji.
Alipoulikia mlango ule, akaingiza kadi, mlango ukafunguka, akaingia ndani.
Belleck na mpenzi wake walikuwa wamelala, kabla ya kufanya chochote, akaanza kupulizia dawa ile ya usingizi ambapo baada ya kuwaingia wote wawili, wakapitiwa na usingizi mzito, tofauti na ule waliokuwa nao.
Kwa haraka sana Fareed akamfuata Belleck pale alipokuwa, akamshusha na kumuweka sakafuni, akanza kumchomachoma visu vya tumbo. Damu zilitoka lakini hakujali, alichoma mara kadhaa, akauacha mwili wa mwanaume huyo chini na kuuburuza kidogo hali iliyoifanya damu ile kutengeneza michizrizi sakafuni pale.
Hakutaka kuondoka hivihivi, akachukua kalamu na karatasi kisha kuandika maneno mafupi yaliyosomeka C'est fait yakiwa na maana ya kukamilika kwa jambo au ‘done’ kwa Lugha ya Kiingereza.
Fareed hakutaka kubaki ndani ya chumba hicho, kwa haraka sana akatoka na kuelekea chumbani kwa rafiki yake, De Leux ambapo akampa ile kadi na yeye kuichukua na kumpeleka mwanaume huyo ambaye bado alikuwa akiserebuka na msichana yule chumbani kwake.
Alipopiga hodi tu, De Leux akafungua mlango, akapewa kadi ile na kisha kurudi kitandani. Mpaka mambo hayo yote yanafanyika, Natalie hakujua kitu chochote kile, alichukulia kawaida, hakujua kama mwanaume huyo alichukua kadi na kwenda kufanya mauaji ndani ya chumba kimoja humo.