Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 145

“Let’s jump,” (turuke) alisema De Leux huku akimwangalia mwenzake, tayari maparachuti yalikuwa migongoni mwao.
“What about me?” (na mimi je?) aliuliza Fareed.

Hawakumjibu kitu chochote zaidi ya kumwangalia. Wakaufungua mlango wa ndege na kutokana na upepo mkali uliokuwa ukiendelea kuvuma, hali ikawa mbaya zaidi, ndege ikayumbishwa kupita kawaida, De Leux na mwenzake wakaruka na maparachuti yale kuelekea chini huku wakimwacha Fareed akiwa na rubani wa ndege ile.

Alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, alitamani kuruka lakini alishindwa kufanya hivyo. Haraka sana akamfuata rubani na kuanza kuzungumza naye, alimwambia kwamba lengo lake lilikuwa ni kuruka kwani vinginevyo ndege ile ingepata ajali na kufa humo.

Akamtaka kushusha ndege, kutoka kwenye umbali wa mita mia moja mpaka hamsini ili aweze kujirusha baharini. Kwanza rubani akaogopa, aliijua bahari hiyo, ilikuwa hatari kuliko bahari nyingine kwani baridi lililokuwa likipiga humo, lilikuwa kubwa na ndiyo bahari ileile iliyoua watu katika meli ya Titanic miaka hiyo ya nyuma.

“It’s impossible! You can’t jump,” (haiwezekani! Huwezi kuruka) alisema rubani yule huku akimwangalia Fareed.

Fareed hakutaka kuelewa, alichokitaka kilikuwa ni kuyaokoa maisha yake kutoka katika ndege ile. Alimwangalia rubani, aliangalia mbele ya ndege ile, ni kweli kulikuwa na upepo mkali na mawingu mazito yalitanda kiasi kwamba ilikuwa vigumu sana kuona mbele.

Aliendelea kumwambia rubani yule ashushe ndege kwa kiasi fulani ili aweze kuruka. Baada ya kubembelezwa sana hatimaye rubani huyo akaishusha ndege hiyo kwa umbali wa mita hamsini kisha kumruhusu Fraeed kuruka.

“Una parachuti?” aliuliza rubani.
“Hapana!”
“Boya!”
“Hapana!”

“Hebu subiri!” alisema rubani huyo.
Akaangalia chini ya kiti chake, akaona boya la kuvaa na kumwambia Fareed alivae kwani hapo alipokuwa akirukia palionekana kuwa sehemu ya hatri sana.

Hilo halikuwa tatizo, akalichukua boya hiyo, akalivaa, akaufungua mlango na kisha kuruka baharini.
 
SEHEMU YA 146

Alikuwa kwenye hali mbaya, wakati mwingine alishindwa kuhema vizuri kutokana na upepo mkali uliokuwa ukiendelea kuvuma. Baada ya sekunde chache akatumbukia ndani ya maji.

Bahari ilichafuka, kulikuwa na mawimbi makubwa yaliyopiga huku na kule. Fareed alipelekwa huku na kule, hakutulia baharini pale, kitu kilichokuwa kikimsaidia kilikuwa ni lile boya tu alilokuwa amelivaa.

Ilikuwa ni mchana lakini kitu cha ajabu, kulionekana kama jioni, hakuweza kuona hata mita kumi na tano kutoka pale alipokuwa.

Alikiona kifo, mawimbi makubwa yaliendelea kumpiga na kumpeleka huku na kule mpaka kuona kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wake.

“Mungu nisaidie,” alisema Fareed huku mawimbi yakiendelea kumpeleka huku na kule.

**** Bilionea Belleck alikuwa kwenye kiti chake ofisini kwake, masikio yake yalikuwa kwenye simu yake iliyokuwa mezani. Alikuwa na presha kubwa, alitaka kuona simu kutoka kwa De Leux ikiingia na kumpa taarifa kwamba tayari walifanya mauaji ya Fareed ili moyo wake uridhike.

Muda ulizidi kusonga mbele, dakika ziliendelea kukatika lakini hakukuwa na taarifa yoyote ile. Moyoni mwake akawa na hofu, akahisi kabisa kwamba watu hao walishindwa kumuua au kulikuwa na tatizo jingine ambalo lilitokea.

Aliwaambia kwamba walitakiwa kufanya mauaji hayo haraka sana baada ya ndege kupaa lakini kitu cha ajabu kabisa hakukuwa na simu iliyoingia kumpa taarifa hiyo ambayo aliamini kwamba ingeufanya moyo wake kumtukuza Mungu kwa hicho kilichotokea.sheangelus_Kwani belleck si alishakufa???
 
SEHEMU YA 147

Baada ya kupita saa mbili, akaamua kumpigia mwanaume huyo ili kujua ni kitu gani kiliendelea. Simu haikuwa ikipatikana, ilionekana kuzimwa kitu kilichomuudhi sana Belleck kwa kuona kwamba amedharauliwa.

Alichokifanya ni kumtumia ujumbe wa sauti (voice mail) ili atakapoiwasha simu yake aweze kuipata sauti hiyo na kumwambia kitu kilichokuwa kimeendelea.

“Kitu gani kinaendelea? Kwa nini umekuwa kimya sana? Mmekamisha au bado hamjakamilisha? Hebu ukifungua simu nitafute nijue manake nilishatuma pesa, kama amekufa niambie nizitoe pesa kabla hajathibitisha kuzipata,” alisema Belleck huku simu ikiwa sikioni mwake.

Moyo wake haukuwa na amani hata kidogo, bado aliendelea kuwa na hofu kwamba inawezekana kulikuwa na jambo lililokuwa limetokea huko.

Hakutulia, moyo wake ulikuwa na shaka tele kwa kuona kwamba kama Fareed hakuuawa basi kile kiasi alichokuwa amemtumia, kingeweza kuondoka mikononi mwake jumla kama tu mwanaume huyo angethibitisha kukipokea ndani ya siku saba.

Alitaka afe haraka iwezekanavyo! Alifanya kazi aliyoitaka, mtu aliyetakiwa kuuawa aliuawa hivyo alichokuwa akikiangalia kwa sasa ni kupewa taarifa kwamba kazi ile ilifanyika.

Siku ya kwanza ikapita, ukimya ukatawala, siku ya pili nayo ikapita, ukimya ukatawala, siku ya tatu na nne nazo zikaingia lakini hakukuwa na taarifa yotoye ile kama Fareed aliuawa au la, mbaya zaidi hata alipokuwa akimpigia simu rubani, naye hakuwa akipatikana.

Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom