Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 131

Lilikuwa tukio kubwa lililoishtua dunia, hakukuwa na mtu aliyeamini kama kweli Marekani ingeweza kulipuliwa kama ilivyotokea.

Kila mtu alishangaa kwani kwa jinsi nchi hiyo ilivyokuwa imejiwekea ulinzi tangu kulipuliwa kwa maghorofa ya biashara ya WTC, hakukuwa na aliyeamini kwamba kweli magaidi wangeweza kuilipua nchi hiyo kwa mara nyingine.

Watu zaidi ya elfu moja mia tano wakasadikiwa kufa katika tuki hilo huku maelfu wakijeruhiwa vibaya. Ndani ya dakika chache tangu tukio hilo litokee, magari ya zimamoto yakafika mahali hapo yakiongozana na magari kadhaa ya wagonjwa.

Polisi wakaweka kamba ya nyano iliyoandikwa ‘Do not cross’ yaani Usivuke huku ni polisi tu na watu wa afya ndiyo walioruhusiwa kwenda ndani ya kituo kile kulipotapakaa miili mingi ya watu.
Mambo yote hayo yalikuwa yakiendelea huku Fareed akiwa chini, hakujitambua, pale alipokuwa, kwa jinsi alivyokuwa amerushwa, ilikuwa vigumu kuamini kama mtu huyo alikuwa mzima.

Yeye na majeruhi wengine wakachukuliwa na kukimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu huku nyuma waandishi wa habri wakiendelea kukusanyika katika eneo hilo la tukio kwa ajili ya kuripoti kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

Gari halikuchukua muda mrefu likafika katika Hospitali ya St. Joseph Medical Centre iliyokuwa hapohapo Pennsylvania ambapo mara baada ya magari kuingizwa ndani, machela zikaletwa, majeruhi wakapandishwa kwenye machela hizo kisha kupelekwa ndani.

Hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kwanza kwa Fareed kukaa ndani ya hospitali hiyo. Matibabu yalikuwa yakiendelea kama kawaida. Baada ya saa kumi na mbili, akarudiwa na fahamu, akayafumbua macho yake na kuanza kuangalia huku na kule.

Mahali pale palikuwa ni hospitali, hakujua alikuwa amefikaje, aliangalia huku na kule, kwa juu, dripu ilikuwa ikining’inia huku mwili wake ukiwa na maumivu makali kiasi kwamba alishindwa hata kugeuka.
 
SEHEMU YA 132

Mbali na yeye, ndani ya wodi ile kulikuwa na wagonjwa wengine ambao hawakuonekana kuwa na nafuu kama alivyokuwa.

Huo haukuwa mwisho wa safari yake, ilikuwa ni lazima aondoke mahali hapo, alitaka kwenda sehemu kwa ajili ya kukaa kisha kumtafuta Bilionea Belleck ambaye aliamini kwamba bado alikuwa hapohapo Marekani.

“Ni lazima niondoke hapa,” alisema Fareed.
Kuondoka mahali hapo haikuwa kazi nyepesi, mara kwa mara madaktari na manesi walikuwa wakifika kwa ajili ya kuangalia maendeleo yao. Hakutaka kabisa kuendelea kubaki kwani bado maisha yake aliyaona kuwa na hatari kubwa.

Kwa kuwa kulikuwa na ugumu wa kufanya hivyo, kitu chepesi alichokifanya ni kusubiri mpaka usiku ambapo akaomba nafasi ya kwenda chooni kwa lengo la kufika huko na kukimbia zake.

Akasimama na kutembea kwa mwendo wa taratibu, mwendo ulioonyesha kwamba hakuwa mzima kiafya, alipofika chooni, akajisaidia haja ndogo na kuangalia ni kwa namna gani angeweza kutoroka hospitali hapo pasipo kuonekana.

** Bado watu waliendelea kushangaa juu ya tukio la kigaidi lililokuwa limetokea nchini Marekani.

Shirika la kipelelezi la FBI lilikuwa kwenye wakati mgumu, hawakujua ni kwa jinsi gani wangeweza kuwapata wahusika wakuu wa tukio hilo ingawa Al Qaida walijitokeza hadharani na kusema kwamba wao walihusika kwa kila kitu.

Walichokuwa wakikihitaji FBI ni picha zilizokuwa zimepigwa dakika kadhaa kabla ya tukio kutokea. Ilikuwa ni lazima waangalie kwenye kamera za CCTV kuona kila kitu kilichokuwa kimetokea humo.

Wakaelekea katika chumba kilichokuwa na kompyuta nyingi, zilikuwa zimeunguzwa vibaya lakini walichoshukuru Mungu ni kwamba memory cards zote ambazo zilikuwa zimechukua picha kutoka ndani ya kituo hicho kabla ya tukio la kmlipuko kutokea, zilikuwa salama kabisa.

Wakazichukua na kuelekea katika kompyuta zao na kuangalia kuona kama wangeweza kuwaona wahusika wa mlipuko ule. Walifanikiwa kumuona Fareed na wenzake, waliwahisi kwamba hawakuwa na nia nzuri kutokana na mabegi ya kufanana waliyokuwa nayo. Baada ya dakika kadhaa, wakamuona Fareed akiondoka.
 
HV haiwezekani mods mkaweka story yote kwenye page ya 1 na kila inapoongezwa mkafanya iwe inaendelea hapo hapo? Maana naona km ni kero unakuta Uzi umejaa story za majibizano ya watu wa3 tu na wanachojibizana wanaweza kuambiana kwenye simu zao binafsi sasa kwa sisi tunaotafuta story tu inatupa kero kuitafuta.
Wapiga soga ni kero sana.
 
Back
Top Bottom