Mianaume ndo tulivyo......hovyoooo!

Mianaume ndo tulivyo......hovyoooo!

B' basi ninakukaribisha bana... Uzi wenyewe wababa wameiniga wengi kuliko hata wadada...
alafu hapo kwenye mabano ITS ALL ABOUT FRICTION....
uuuuuuuuuuwwwwiiiiiiii nimecheeeeeeeeeeeeeka mpaka basi,haya bana nimeelewa.
na log off (source:washawasha).
 
we acha tu nna dozi,niweke tu kiporo,ila hoi nimechoka maana leo nimevurumishiwa mi maneno na kina baba humu mmu mpaka basi,kumbe kusemwa kunauma aisee.

Pole sana, bora hata leo umekuwa mtetezi wa akina mama jamani. Hao hawapendi kusemwa wala huwa hawakosei madai yao wao ni vichwa vya nyumba l.o.l
 
Mungu alimuumba mwanaume kwa kusudio maalum, ambalo halijulikani kwa wengi zaidi ya kujua kusudio la Eva pekee ambalo ni kumsaidia Adamu. A stronger gender needs be stronger in all aspects of life.......................!
 
We bishanga next time tutakuendea makorora weye ili utembee na ule 'mzigo' kwa muda ili utie akili, ebooooooooooo!
 
Mimi niliulizwa jinsia yangu, we nadhani utaulizwa kama 'jongoo anapanda mtungi au laah', we subiri tu utaniambia.
 
We bishanga next time tutakuendea makorora weye ili utembee na ule 'mzigo' kwa muda ili utie akili, ebooooooooooo!
Mkuu yaani umekasirika mpaka unataka unishushe mshipa? kwi kwi kwi kwi....mbavu sina!
 
Namba 9 nimeipenda, kumbe mwaturuhusu tucheze mechi za nje ila tusizae huko eeh? Na tukizaa tusizae zaidi ya mmoja! Hapa ndio ninapowapendea wanawake hamna wivu kabisa!!!

Nimekaa na jiuliza kwanini una furahia possibility ya kuweza kutoka nje ya ndoa na kuzaa. Why would u do that? Why did u get married in the first place? Ndo maana magonjwa hayaishi. Haupendi maisha yako nini? Kwani mke wako akizaa watoto wengine utapata kichaa? acheni kuwa na akili finyu.
 
Wewe kweli ni tata. Unatoka povu kwanini sasa ukweli unauma eeh??

Sitoki povu najaribu tu kuweka rekodi sawasawa. Huyu Bishanga anaongea utadhani ametembea dunia nzima na kuangalia wanachofanya hao anaowaita Mianaume na anataka kuaminisha watu hapa kuwa wote ndivyo tulivyo. Huku ni kugeneralize ambako hakuitendei haki hata hiyo thread yake ambayo mimi naiona imekaa kishabiki zaidi.
 
kwani amesema ni wanaume wote twenye hizi tabia mkuu?
Ni kwa baadhi, na ametaja vijitabia vingi tu.

Labda kama tunasome thread tofauti. Labda unieleze wewe umeelewa nini aliposema MIANAUME NDO TULIVYO --- HOVYOOOO! Hii dhana yako kwamba ni kwa baadhi sijaiona kwenye thread labda kama unataka ku-edit thread.
 
Ndio nimeibuka toka mafichoni nakutana na huu uzi! aisee bishanga hapa amegusa kila idara...sidhani kama kuna kidume ambaye hajaguswa kwa namna moja au nyingine hapo! mi hapo kuna vitu ka 10 hivi vimenilenga!

Yaleyale. Kwa sababu umeguswa na vitu kumi basi unadhani kila mtu ameguswa.
 
Mie namtafuta mmoja ambaye hana kati ya hayo yalioorodheshwa................tunaruhusiwa kuongeza mengine.
Usihangaike Chauro nipo hapa. Kwa ushahidi zaidi itabidi ukawasiliane na mtani wa wangu wa jadi.
 
Wapo wengi na wapo ambao ni wanaume na wanajua nini maana ya ndoa zao na wanaheshimu ndoa zao
Ni baba wa familia na mume kwa mke wake
Wanajua muda wa kukaa na familia na muda wa kukaa na marafiki
Muda wa kukaa na watoto na uhuru wanaopaswa kupewa watoto
Wanaoheshimu hisia za wake zao na wanaoheshimu pia hisia za watoto wao na wanaojua watoto wao au wake zao kwa muda huo wanataka nini na wanahitaji nini kutoka kwa baba au mume

Tatizo kubwa hapa ni maudhui ya hii thread ya Bishanga kuwa kila mwanaume ni mlevi, kila mwanaume ni mshabiki wa mpira wa miguu hasa ligi ya uingereza, kila mwanaume ni fuska na ana nyumba ndogo au anatembea na house girl, kila mwanaume hana muda na familia yake na amewatelekeza watoto. Hii siyo sahihi hata kidogo na mtu responsible hawezi akaiacha mada kama hii ipite bila kurekebishwa. Nimefuatilia thread za akina mama inaonekana wengi wanakubaliana na huo mtazamo wa Bishanga na wengine wanahamu ujumbe uwafikie waume zao. Wasichotaka kukiri ni kuwa wapo wanaume wengi ambao hawaingii kwenye hii "stereotying" ya Bishanga kuhusu wanaume. Hii thread haiwatendei haki wanaume ambao:
  • siyo walevi kwa hiyo hawakai bar muda huo anaosema Bishanga,
  • siyo washabiki wa mpira wa miguu kiasi cha kukesha wanaangalia mpira,
  • wanahudumia familia zao kwa hali na mali,
  • wake zao wanafanya kazi na bado wanawapa huduma zote kama wanawake ndani ya nyumba,
  • hawadeki wanapougua kama anavyotaka kutuaminisha,
  • hawana muda wa kunyang'anyana remote na watoto - Mfano kwangu watoto hawaruhusiwi kuangalia TV muda wote na vipindi wanavyoangalia vinadhibitiwa: siyo kila kipindi watoto wanaruhusiwa kuangalia; Huo ni utaratibu wa taasisi ya familia yetu ya Tata & family.
  • hawaongei habari za wake zao nje - hili hata mila na desturi zetu wengine haziruhusu na sijawahi kukaa chini na rafiki au hata ndugu zangu kujadili matatizo ya familia yangu. Siamini kama hii ni njia sahihi ya kutatua matatizo kama yapo.
  • Hawatembei nje na vimada/malaya
Hoja yangu ya msingi ni kuwa siyo sahihi kuchukua tabia mbovu za wanaume wachache ukadhani ndio tabia za kila mwanaume. Sipingi kimsingi kuwa kuna baadhi ya wanaume wana hizo tabia kama ambavyo tumeshapata ushuhuda wa baadhi ya wachangiaji wanawake humu ndani - Japo siamini kuwa wote waliochangia wanakutana na matatizo hayo. Ni muhimu kuwaeleza hata hao kina mama wenye wanaume wasiowajibika "irresponsible" kama hawa wa Bishanga kuwa siyo kila mwanamke aliyeolewa anakutana na matatizo kama hayo.
 
Sitoki povu najaribu tu kuweka rekodi sawasawa. Huyu Bishanga anaongea utadhani ametembea dunia nzima na kuangalia wanachofanya hao anaowaita Mianaume na anataka kuaminisha watu hapa kuwa wote ndivyo tulivyo. Huku ni kugeneralize ambako hakuitendei haki hata hiyo thread yake ambayo mimi naiona imekaa kishabiki zaidi.
we ukoje Mkuu?
 
Usihangaike Chauro nipo hapa. Kwa ushahidi zaidi itabidi ukawasiliane na mtani wa wangu wa jadi.

mmmmmmmhhhh i wish ningeongea na mkeo halafu ambayo angenipasha ningekuja nikueleze,ungeshangaa,labda ni mama mkimya na hiyo haimaanishi you are perfect,ni uvumilivu wake tu.Umesoma thread aliyorusha Mtambuzi leo? Itafute uisome pliz.
 
Tatizo kubwa hapa ni maudhui ya hii thread ya Bishanga kuwa kila mwanaume ni mlevi, kila mwanaume ni mshabiki wa mpira wa miguu hasa ligi ya uingereza, kila mwanaume ni fuska na ana nyumba ndogo au anatembea na house girl, kila mwanaume hana muda na familia yake na amewatelekeza watoto. Hii siyo sahihi hata kidogo na mtu responsible hawezi akaiacha mada kama hii ipite bila kurekebishwa. Nimefuatilia thread za akina mama inaonekana wengi wanakubaliana na huo mtazamo wa Bishanga na wengine wanahamu ujumbe uwafikie waume zao. Wasichotaka kukiri ni kuwa wapo wanaume wengi ambao hawaingii kwenye hii "stereotying" ya Bishanga kuhusu wanaume. Hii thread haiwatendei haki wanaume ambao:
  • siyo walevi kwa hiyo hawakai bar muda huo anaosema Bishanga,
  • siyo washabiki wa mpira wa miguu kiasi cha kukesha wanaangalia mpira,
  • wanahudumia familia zao kwa hali na mali,
  • wake zao wanafanya kazi na bado wanawapa huduma zote kama wanawake ndani ya nyumba,
  • hawadeki wanapougua kama anavyotaka kutuaminisha,
  • hawana muda wa kunyang'anyana remote na watoto - Mfano kwangu watoto hawaruhusiwi kuangalia TV muda wote na vipindi wanavyoangalia vinadhibitiwa: siyo kila kipindi watoto wanaruhusiwa kuangalia; Huo ni utaratibu wa taasisi ya familia yetu ya Tata & family.
  • hawaongei habari za wake zao nje - hili hata mila na desturi zetu wengine haziruhusu na sijawahi kukaa chini na rafiki au hata ndugu zangu kujadili matatizo ya familia yangu. Siamini kama hii ni njia sahihi ya kutatua matatizo kama yapo.
  • Hawatembei nje na vimada/malaya
Hoja yangu ya msingi ni kuwa siyo sahihi kuchukua tabia mbovu za wanaume wachache ukadhani ndio tabia za kila mwanaume. Sipingi kimsingi kuwa kuna baadhi ya wanaume wana hizo tabia kama ambavyo tumeshapata ushuhuda wa baadhi ya wachangiaji wanawake humu ndani - Japo siamini kuwa wote waliochangia wanakutana na matatizo hayo. Ni muhimu kuwaeleza hata hao kina mama wenye wanaume wasiowajibika "irresponsible" kama hawa wa Bishanga kuwa siyo kila mwanamke aliyeolewa anakutana na matatizo kama hayo.
Tata,mimi nashauri tukubaliane kutokukubaliana,it appears wewe umejiweka a class above all men on this planet,hongera zako.Usichokijua ni usiku wa giza,kama una uhakika huwa humkeri mkeo kwa lolote lile potelea mbali haya machache niliyoorodhesha hapa basi nakuvulia kofia.
Na kama hivyo ndivyo basi UMEBARIKIWA KULIKO WANAUME WOTE DUNIANI!
Nalog off (source:Washawasha)
 
Sorry sana ndugu yangu Bishanga, utanisamehe kwa comment yangu. Yaani ni muda mrefu sana huwa nakuhisi kuwa wewe ni mmoja wa wanaJF wanao fake gender... sijui kwa nini, lakini niwie radhi.
 
Back
Top Bottom