Mianaume ndo tulivyo......hovyoooo!

Mianaume ndo tulivyo......hovyoooo!

Mkuu bishanga mie kuna waheshimiwa flan sijaona michango yao hapa nataman sn kusoma coment zao kwenye huu uzi,
Nao ni my dia wangu Klorokwin,mwanasheria wetu wa jf na shem wangu Uporoto,my broda Fidel80,my broda Igwe,Bujibuji,katavi,rejao,mzizi mkavu,mzee wa rula,SMU,Pakajimmy mko wapi jaman?
Semen chochote basi kwa huu uzi wa ukweli!
Ndio nimeibuka toka mafichoni nakutana na huu uzi! aisee bishanga hapa amegusa kila idara...sidhani kama kuna kidume ambaye hajaguswa kwa namna moja au nyingine hapo! mi hapo kuna vitu ka 10 hivi vimenilenga!
 
Kwa mwanaume rijali aliyo andika Bishanga hapo juu hawezi fanya upumbavu kama huo.
Yawezekana yeye Bishanga anafanya kiaina.
Haaa haaa haaa,that is my broda!
Unataka kunambia hakuna hata moja linakugusa hapo?
 
Ndio nimeibuka toka mafichoni nakutana na huu uzi! aisee bishanga hapa amegusa kila idara...sidhani kama kuna kidume ambaye hajaguswa kwa namna moja au nyingine hapo! mi hapo kuna vitu ka 10 hivi vimenilenga!


Mkuu wacha ni balaa
huu uzi umeleta aibu kwa wanaume mbaya
yaani ni kama anaonyesha kuwa wewe unafanya nini ukiwa home au ukiwa bar au ukiwa popote pale ulipo
 
Ndio nimeibuka toka mafichoni nakutana na huu uzi! aisee bishanga hapa amegusa kila idara...sidhani kama kuna kidume ambaye hajaguswa kwa namna moja au nyingine hapo! mi hapo kuna vitu ka 10 hivi vimenilenga!
Afadhali umetokea broda,
Yani bora hata ww umeuona ukweli jamaa leo kapita mlemle kwenye ishu zenu!
Niliamua kupiga mbiu coz nimeona wengi wenu wanaingia km guest wakichungulia wanasepa!
Leo nasi tumepumua lol!
 
Mkuu wacha ni balaa
huu uzi umeleta aibu kwa wanaume mbaya
yaani ni kama anaonyesha kuwa wewe unafanya nini ukiwa home au ukiwa bar au ukiwa popote pale ulipo
dah..aise kaexpose maujanja yetu yote!
kunasiku mshkaji wangu alishtumia hiyo technique ya kurudi asubuhi na difenda ya polisi hom..but bado ilikuwa ni mshike mshike!
 
Hebu fikiria:
1.Uko ndani ya ndoa,mwaka wa kumi sasa na hamjapata mtoto,mkeo hospitali zote kamaliza na anaambiwa hana tatizo,kila akikwambia na wewe ukapimwe hutaki unajidai huna tatizo,ndo nini sasa hiyo? Kwa nini usipimwe mkajaribu IVF?
2.Ukienda Rose Garden we ndo Reginald Mengi kazi kuzungusha raundi huku ukijidai kusema...'uza nyumba utunze heshima bar'....asubuhi mwanao akikwambia 'baba shati la shule limechanika'..unakuwa mkaaaaaali,hovyooooo!
3.Umetoka zako kwenye mipombe,ni saa saba za usiku ,mama siku nzima mihangaiko kachoka we ukifika kitandani na ny....zako unamrukia tu bila hata maandalizi....ku ku...ku .....aaaaaaaagh....halafu huyo unakoroma,yaani mpaka mkeo anaona ka alikuwa anaota hivi,jamani hiyo sio baiskeli ya gym huyo ni binadamu ati.
4. Mnawaita beki tatu ma haus geli hao,juu ya nini unajipoza kwa mtumishi wa ndani? huoni unamdhalilisha mwenzio? Hivi ukibambwa utasema nini?
5.Ulipompenda ulimkuta ana kakazi kake,we na miwivu yako hutaki afanye kazi unamwachisha,hivi una uwezo wa kumpatia mahitaji yake yote yakiwemo matunzo ya wazazi na ndugu zake? Halafu kwa nini utake mwenzio kazi yake iwe kusafisha makochi na kuangalia plasma wakati wewe uko bize unachangamsha mwili na akili? Kufanya kazi au biashara is more than kuingiza kipato ,na ku interract na watu pia is healthy.
6.Mkeo akikusoea unaanza kumtangaza kwa watu...'mkeo wangu sijui yukoje....mara hivi mara vile.....huoni unajiaibisha mwenyewe?
7.Na hizo nyumba ndogo hizo,ukienda huko kazi kumsimanga mkeo,matokeo yake siku mkeo akigombana na hawara yako anashangaa matusi anayovurumishiwa...we nae mwanamke wewe...si kikojozi wewe....du toba yarabi!
8.Ukiumwa kidogo tu full madeko yaani unajitia hata kidole huwezi kukisogeza,mwenzio serious tumbo linamsumbua,hata kusema ngoja nikae ndani nimuuguze mwenzangu ndo kwaaaanza unawahi kaunta Jackies,sana sana unampigia simu dada yako akamwangalie wifi,inahuu kwani yeye ndo kamwoa,akilalamika mkeo unamsimanga eti anadeka.
9.Nje utembee sasa ndo hata kuzaa uzae kabisa huko? maduka zinakouzwa condoms huyajui? au utasingizia ilikupasukia,na wa pili nayo ilipasuka? acheni hizo!
10.Huko kwenye mabaa na huo upuuzi unaoongelewa huko ....eh chapati shurti ikaangwe pande zote...sijui nini sijui nini...unarudi nyumbani na mipombe yako unataka ujaribu upuuzi wako kwa mkeo,peleka huko ujinga wako.
11.Umelala nje asubuhi unajitia kurudi nyumbani umefungwa pingu ili mke aone ulilala kituoni,mambo ya 1947 hayo,kinamama hawadanyiki na hizo siku hizi!
12.Mpira ..mpira...mpira....hamchoki? wikiendi nzima uko bar unaangalia mpira ,jumamosi man siti vs man yu,jumapili aseno vs chelz, weekdays kazi,hivi lini unakaa na kukagua kazi za watoto za shule? lini unakaa na mke na wanao na ku chat nao? mpira ndo utakaokuzika?
13. Ubinafsi wako huo,ukikaa sebuleni remote control haiko mbali na wewe unabadilisha tu chanel,si umuulize mkeo au wanao kama nao kuna kitu wanataka kuangalia? kuna mtu aliwahi kusema eti wanaume huona remote control kama ni extension ya mb....zao.
14.Sijui ndo umepiga wapi kabomu kako cha kwanza unamnunulia hawara yako ka vitz wakati mkeo anapanda daladala,kha!
15.Mke akilalamika mitabia yako mibovu unaanza..'kwani unataka nini..gari nimekupa..zaabu nakununulia...frigi imejaa chakula...kelele za nini? kwani kwao hakuacha chakula? yeye alikufuata wewe ati na sio plasma yako.
.......itaendelea....leo wababa wa humu ndani nakula nao sahani moja!

What a gentleman! Umewasanua mbayaa! Wapi Mtambuzi leo?
 
Mimi mwanaume rijali sipo kundi lolote hapo na siamini kama kuna mwanaume mwenye akili zake timamu anayafanya hayo

Mkuu yapo sana
Ni vile kila nyumba ina siri zake ila wanawake zetu wangeamua kufunguka wakasema kinachoendelea ndani ya nyumba zao mkuu tungeficha sura zetu
haya yanatokea sana miongoni mwetu sisi wanaume na tunayafanya mengi
Kama ni mpenzi wa mpira kuko tayari kukaa bar mpaka saa saba za usiku kisa kuna mechi ya Man U na Man City au mechi ya kirafiki kati ya Hispania na Uholanzi
Mkuu haya yanatokea sana
Wengine wamadiriki hata kuleta hawara yake nyumbani anakokaa na familia yake kisa amelewa huko hajui hata anafanya nini
Au amewekeza sana kwa hawara hata familia haikumbuki
 
Hao ni wanaume mifuko sio wanaume rijali
Haaaa haaaa,my broda hii ya wote tu!
Raha ni kwamba mkuu bishanga kagusa kila engo hakuna pa kutokea hapo!
Hasa hasa ni kujastifai tu,ila mambo hazarani broda!
 
dah..aise kaexpose maujanja yetu yote!
kunasiku mshkaji wangu alishtumia hiyo technique ya kurudi asubuhi na difenda ya polisi hom..but bado ilikuwa ni mshike mshike!

Yote yaani
Kila kitu kakiweka wazi aise
Yaani mkuu ni njia zile zile tunazopita ndo ameweka hapa
 
Afadhali umetokea broda,
Yani bora hata ww umeuona ukweli jamaa leo kapita mlemle kwenye ishu zenu!
Niliamua kupiga mbiu coz nimeona wengi wenu wanaingia km guest wakichungulia wanasepa!
Leo nasi tumepumua lol!
Yaani kama kuna mwanaume rijali anasema hajaguswa hapa atakuwa na matatizo. Hata number 12 ya kuangalia mpira??
 
Yaani kama kuna mwanaume rijali anasema hajaguswa hapa atakuwa na matatizo. Hata number 12 ya kuangalia mpira??
Hata mie namshangaa kaka yangu Fidel ina maana hata ile ya no 8,ya kudeka akiwa anaumwa!
Naamin anajastifai tu ukweli anao moyon!
 
mhhhh. haya mkuu
umesomeka. mwenye masikio ya kusikia na kuelewa amesikia na kuelewa pia.
thanks
 
Back
Top Bottom