sasa kama ulianza na 400k ikawa aitoshi,ikapanda mpaka 1,2m aitoshi tu hata ukipata 10m aitotosha.
unadai hujui pesa yako inaenda wapi,unadai huwa unafanya bata mara moja moja na huwa hutumii si zaidi ya 30k.
hapo shida tu ni matumizi ya pesa,maana mshaara wako upo sawa hata ukitaka kujiendeleza ila nidhamu tu ya matumizi ndo imekukosa.
fanya zoezi hili ili ujue hela yako inaenda wapi,nunua notebook ya 1,500tsh hii ni ile dizaini ya kuweka mfukoni,huitaji kununua kalamu maana huwa zinakuja na kalamu yake ndogo na inatosha kwa matumizi.
anza kuandika kila kitu unachotolea pesa mfukoni mwako,pesa yoyote unayoitoa mfukoni kwa matumizi yoyote.
andika kila kitu,hapa usijiambie kuwa:haaa na mia nayo ya pipi niandike!!! rafiki yangu andika kila kitu,hata hile mia tano utakayo mpatia omba omba pale kamanga ferry wewe andika.hela ya sadaka kanisani andika.mpaka hile ya michango ya kijamii yote andika.
nachokuambia ni kuandika kila pesa inayotoka mfukoni mwako.
fanya zoezi hili kwa mwezi mmoja,alafu rejelea matumuzi yako,angalia matumizi yapi yaliyochukua hela yako,kisha ujue kama ni ya lazima au si ya lazima.
hapo utafanya kuwa na bajeti,itakuepusha kutumia hela hovyo kwa kuwa tu unayo,kama ni hela ya pipi utapangilia kabla ya kuitoa