Ukweli mchungu. Ukiwa na pesa zinakuwa kama zinakuwasha hivi. Zinakutaka uzitumie tu. Usipokuwa na nidhamu ya matumizi utachanganyikiwa.
Mi naona njia nzuri ni kuweka limit ya matumizi kwa mwezi. Binafsi hio hela naona ni nyingi mno kwa mtu ambaye hana familia kubwa.
Mf. Budget ya chakula:
Sukari
Mchele
Unga
Mafuta
Tambi
Chumvi
Nyama
Samaki
Kuku
Miscellaneous:
Dawa za mswaki
Pampers
Vifurushi vya Tv na simu
Luku
Bill ya maji
Toilet papers
Napkins
Wipes
Nauli
Petrol/Diesel (kama ana gari)
Gas ya kupikia
Vehicle maintance (kama ana gari)
Gambe weekends
Aanze na kuangalia hivyo vyote na kulimit matumizi na ili ku save anunue jumla kwa suppliers. Kununua hayo mahitaji kwa rejareja inaumiza sana ila hatujui tu.
Kwa mfano mwezi kwa average family hata vikabaki sio kesi.
Sukari 5kgz, kwa jumla 15k
Unga Fika mashineni nunua mahindi kwa sado au debe saga mwenyewe. Haitazidi 12k ila utapata unga wa kutosha!
Mchele fanya kama unga tu, fika mashineni nunua. 25kg itakuwa kati ya 50k-55k
Chumvi nunua carton kabisa ile yenye vifuko vingi utasahau. Haitazidi 15k
Mafuta dumu la litre 5 almost ni 20-22k kulingana na ulipo.
Tambi, sio lazima ila kama utapenda nunua hata nusu dozen kwa bei yake jumla sidhani kama zitazidi 10k
Nyama, nenda machinjioni kule weekend moja damka ukanunue kilo za jumla kule. Kwa 10kg cost hazitazidi 70k .
Samaki, hawa sina uzoefu nao sana maana naonunua wanatoka nyumba ya Mungu, huku niliko nikiwa na 30k nawajaza frijini 🤣🤣🤣🤣🤣 nakula mpaka nachoka. Naweza nikawala mwezi mzima size tofauti tofauti bila kubadili mboga. Ila wale sato, sangara, kibua naona wapo expensive. Kukadiria labda anunue wa 30k tu kwa aina anayopenda.
Kuku, jumla ni buku 5500 kwa order kubwa ila roughly kwa 6k hawezi kuku wake hata 7 wanatosha kwa mwezi. Hii ni optional akitaka punguza anaweza pia ila 7 ni around 42k inatosha.
Hizi ni estimates tu ila anaweza limit budget akapunguza mpaka around 200k kwa matumizi ya kula kwa mwezi akawa anaongezea vinavyopungua tu akifika mwishoni.
Miscellaneous:
Nako akilimit kwa 250k inatosha na hii itafika kama akiwa na gari! Bila gari anaweza save 100k au zaidi.
NB: Gari aweke full tank inasadia zaidi kuliko mafuta ya kujaza kwa kibaba. Yanakula hela nyingi zaidi.
Akiweza tumia mfumo huu kadri siku zinavyoenda gharama itakuwa inapungua na ataweza ku save mpaka laki 5 kwa mwezi.
Mke ampe laki na nusu tu. Hela zote hizo za nini? Hana kazi