Miaka 5 kazini mshahara haujawahi kutana

Miaka 5 kazini mshahara haujawahi kutana

DAVID PALMER

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2020
Posts
323
Reaction score
1,625
Wakuu, hii ni nini?

Nilipomaliza chuo, 2014 nikapata shule fulani ya kujishikiza huku nikisubiri ajira ya fani yangu. Mshahara ulikua 400k kwa mwezi. Nilikuwa naishi fresh, natuma kwa maza home, namlipia dogo tution mapambako akija likizo na pesa ikawa inakutana na mshahara ujao. Nilifundisha kwa mwaka mmoja na sijawahi ishiwa.

Mwaka 2015 nikapata ajira yangu sasa. Mshahara take home ikawa ni around 900k. Lakini pesa haijawahi kutana. Sinywi pombe, naendaga club na matamasha ya muziki mara moja moja lkn sijawahi tumia zaidi ya 30. Na kwa mwezi labda ktk bata naenza enda mara 2 au 3.

Mwaka 2018 nikapata kazi ingine, take home ikawa zaid ya 1.2m. Nilkuwa nishaoa. Wife nikawa nampa 300k matumizi, inabaki 900k. Wazazi na nini labda inabaki 700k. Lkn haijawahi wekeka bank ikutane na mshahara ujao na sioni nimefanyia nini.

Nikaona siwezi weka pesa nikaamua kuchukua mkopo 8m nikajenga nyumba nimehamia home. Makato 410k. So nikikatwa mkopo nabaki na hela lakini same story, hazikutani a mshahara ujao.

Kuna mtu anapitia situation kama hii isiyo na majibu? Tukutane hapa.

Uzi tayari
 
Tabia ya pesa ipo hivi, unatumia kadri unavyokuwa nayo karibu au mfukoni.

Kwa mfano ukiwa na laki moja mfukoni huoni tatizo kujiunga kifurushi cha sh 2000, 3000, 4000 n.k lakini ukiwa na na elfu mbili mfukoni utatafuta kifurushi cha mia tatu.

Moja ya njia za kuji control ni pamoja na hivyo kama kukopa kufanyia jambo alafu wawe wanakata chao na kukubakizia cha kwako.
 
Mpe mke wako akuwekee, kama umeshindwa kuzigusanisha JAN na FEB.
Umemalizaa Mkuu...!!


Japo ni risk lakini kama una mwanamke anaejielewaa mpe akushikiee baki na kiasi kidogo cha matumizi na mkeo awe mbinde sanaa yani kila ukitaka hela sio anakupa tuu bora akupe ya kutumia siku hiyo tu maana umeshindwa kujiendeshaa mkuu japo haya mambo acha tu Pesa ya mshaara ina mapepo sijui
 
Katika mazingira yako, hapa ndipo ulicheza pele. Jitahidi umalize mkopo wako. Nyumba yako itakuwepo siku zote.
Nikaona siwezi weka pesa nikaamua kuchukua mkopo 8m nikajenga nyumba nimehamia home. Makato 410k. So nikikatwa mkopo nabaki na hela lkn same story, hazikutani a mshahara ujao.
 
Back
Top Bottom